Friday, May 10, 2019

NAIBU WAZIRI MAVUNDE AKUTANA NA MWAKILISHI WA UNICEF NCHINI

 Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde (kulia) akizungumza na Mwakilishi wa

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto
(UNICEF) Tanzania, Bi. Maniza Zaman (kushoto) alipokwenda kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi nchini Mei 10, 2019 Jijini Dodoma, katikati ni Bi. Khadija Othman mwakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
 
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) Tanzania, Bi. Maniza Zaman, (kushoto) akimweleza jambo Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe. Anthony Mavunde alipomtembelea Ofisini kwake Jijini Dodoma. Kulia ni Bi. Khadija Othman mwakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Mkuu wa Ushauri na Sera za Kijamii Bw. Paul Van Lifford (kushoto), akieleza jambo kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe. Anthony Mavunde (kulia) kuhusu ushirikiano baina ya UNICEF na Serikali katika utekelezaji wa Sera ya Hifadhi ya Jamii (Social Security Policy).

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde (kulia) akionyeshwa picha ya Watoto na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) Tanzania, Bi. Maniza Zaman, mara baada ya mazungumzo yao, Jijini Dodoma.

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde akijadili jambo Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) Tanzania, Bi. Maniza Zaman, mara baada ya mazungumzo yao, Jijini Dodoma.

MCHEZA POOL TABLE ASHIKILIWA NA POLISI LINDI.

NA HADIJA HASSAN, LINDI.

Mkuu wa mkoa wa Lindi Godfrey zambi ameliagiza jeshi la Polisi Wilaya ya Lindi kumkamata Mkazi wa kata ya Chikonji Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mkoani humo ISMAIL HASSAN kwa kosa la kukutwa anacheza pooll table nyakati za Asubuhi pamoja na kuwasaka wamiliki wa pool Table hiyo Abdallah Ally Jadu. 


hayo yametokea mai 9 mwaka huu majira ya saa nne Asubuhi ambapo mkuu huyo wa Mkoa alikuwa katika ziara yake ya kutembelea Miradi ya TASSAF katika mtaa wa Nanyanje na Jangwani Halmashauri ya manispaa ya Lindi. 


Akiwa anaelekea katika mradi huo ndipo alikuta baadhi ya Vijana wa kata hiyo wakicheza mchezo huo wa Pooll Table nyakati za Asubuhi hali ya kuwa Serikali ilishapiga marufuku michezo hiyo kuchezwa nyakati za Asuhuhi hasa katika siku za kazi. 


Zambi alionyesha kuchukizwa na kitendo hicho huku akisema kuwa kijana huyo ataendelea kushikiliwa na Jeshi la polisi kuwataja wenzake aliokuwa akicheza nao mchezo huo pia liwe fundisho kwa vijana wengine wenye tabia kama yake. 


Aidha, Zambi pia pamoja na mambo mengine aliamuru jeshi hilo la polisi kuharibu meza hiyo ya pooll kwakuzivunja vunja. 


“tumekuwa tukisema mara kwa mara sio ruhusa kucheza pooll table nyakati za asubuhi lakini kunawatu wanajaribu kukaidi maagizo yanayotolewa na Serikali sasa nyinyi mnachukuliwa ili iwe fundisho kwa wengine maana hatuwezi kuendelea kuishi kwa namna hii , haiwezekani tuseme kila siku yale yale sasa kwa sababu huku kuna watu wananchi yao basi wanaishi wanavyotaka wao kucheza pooll asubuhi maana yake mnaendekeza uvivu” alisisitiza zambi.


 Akihojiwa na BAGAMOYO KWANZA. Ismail Hassan ambae ameshikiliwa na jeshi la polisi alisema kuwa amesikitishwa na kitendo cha Mkuu huyo wa Mkoa kuagiza ashikiliwe na jeshi hilo badala ya viongozi wa serikali ya mtaa ambao ndio walikuwa na wajibu wa kusimamia michezo hiyo isifanyike. 


“Mimi nimeshikwa tuu ndugu muandishi lakini kwanza mimi ni mgeni katika maeneo hayo nimekuja tuu kwa muda lakini toka nimefika hapo miezi miwili iliyopita nimekuwa nikishuhudia mchezo huu ukiendelea nikajua huu ndio utaratibu wao waliojiwekea, kama viongozi wa mtaa wangefanya majukumu yao kwa ufasaha hata mkuu wa mkoa asingeweza kukuta mchezo huu unachezwakwa wakati huu hivyo mimi sina kosa katika hili” alisema Hassan.