Wednesday, October 26, 2016

UBORESHAJI WA TAARIFA ZA WANAKAYA WAINGIA MAKURUNGE WILAYANI BAGAMOYO.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Mh. Majid Mwanga akiangalia namna taarifa za wana kaya zinavyoingizwa kwenye mtandao kupitia simu, wanaoshuhudia wengine kutoka kushoto ni Diwani wa kata ya Makurunge, Paulo Kabile, na wa pili kushoto ni Mtendaji kata ya Makurunge, Yoel Chumi.
............................................
 
Zoezi la kuboresha taarifa za wana kaya hapa nchini zimeanza katika wilaya ya Bagamoyo ambapo mpaka sasa tayari kata tatu zimerosha taarifa zake, ub oreshaji wa taarifa za makazi wilaya ya Bagamoyo umeanza kata ya Mapinga, Fukayosi na Makurunge na kuendelea na katza zilizobaki.

Taarifa za wanakaya zinaboreshwa kutoka kuhifadhi taarifa kwenye vitabu vya usajili wa makazi vilivyopo kwa wenyeviti wa vitongoji na sasa taarifa hizo zinaingizwa kwenye mtandao ambapo mwenyekiti ataweza kuwasiliana na watu wake kupitia simu ya mkononi muda wote.

Uboreshaji huu wa Taarifa utasaidia hata pale mwenyekiti anapohitaji kufanya mkutano na wananchi wake ujumbe atakaoandika na kuutuma utawafikia wananchi wake wote kwa wakati mmoja.



Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Mh. Majidi Mwanga akipata maelezo ya namna taarifa za wanakaya zitakavyokuwa kutoka kwa mtaalamu wa takwimu kutoka chuo cha takwimu Dar es Salaam.


Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majidi Mwanga akimueleza jambo Diwani wa kata ya Makurunge, Paulo Kabile



Safari ya kutembelea kaya katika kitongojicha Gezaulole kata ya Makurunge, Kkushoto ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Mh. Majid Mwanga, akiwana mwenyekiti wa kitongoji cha Gezaulole, Tabu luaga na kulia ni Diwani wa kata ya Makurunge, Mh. Paulo Kabile.

Safari ya kutembelea kaya katika kitongojicha Gezaulole kata ya Makurunge, Kkushoto ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Mh. Majid Mwanga, akiwana mwenyekiti wa kitongoji cha Gezaulole, Tabu luaga na kulia ni Diwani wa kata ya Makurunge, Mh. Paulo Kabile.

Monday, October 24, 2016

RAIS DK. MAGUFULI AMPOKEA MFALME VI WA MOROCCO IKULU, ZAIDI YA MIKATABA 20 YA KIBIASHARA YASAINIWA

1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakielekea kusalimiana na viongozi mbalimbali wakati Mfalme huyo alipowasili kwenye viwanja vya Ikulu.
 jc1

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakipita katika gadi ya mapokezi iliyoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Ikulu jijini Dar es Salaam.
 jc2

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakilakiwa na wafanyakazi pamoja na wageni mbalimbali katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasili.2

Mfalme wa Morocco Mohamed VIakisalimiana na viongozi wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama wakati alipowasili kwenye  viwanja vya Ikulu ambapo amepokelewa na Mwenyeji wake Rais Dk. John Pombe Maguful.