Wednesday, April 13, 2022

MAGAZETI YA LEO JUMATANO 13 APRIL 2022.

 No description available.

No description available.

No description available.No description available.

No description available.No description available.No description available.No description available.No description available.No description available.No description available.No description available.

No description available.No description available.

SERIKALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA CDC KUDHIBITI MAGONJWA

 No description available.

Na WAF- DOM

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu leo amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa Kituo cha Udhibiti wa Magonjwa nchini Tanzania (Centre of Diseases Control – CDC) Dkt. Mahesh Swaminathan katika Ofisi za Wizara Jijini Dodoma.

Waziri Ummy Mwalimu ameishukuru CDC kwa kuendelea kuwa mshirika wa Karibu wa Serikali na Wizara ya Afya kwa kutoa ushirikiano na msaada katika mapambano dhidi ya Magonjwa mbalimbali ikiwemo Ugonjwa wa Virusi Vya Ukimwi, Kifua Kikuu, Malaria pamoja na UVIKO-19.

“CDC amekuwa mshirika wetu wa karibu katika mapambano dhidi ya magonjwa mbalimbali na katika kutekeleza afua za kuboresha ubora wa huduma za afya nchini Tanzania.” Amesema Mhe. Ummy Mwalimu.

Waziri Ummy Mwalimu ametaka ushirikiano zaidi katika kuboresha na kuongeza huduma za maabara za afya ya jamii pamoja na kuboresha mifumo ya ufuatiliaji wa magonjwa ili kuwezesha Serikali kuchukua hatua stahiki mapema zaidi na kuokoa maisha ya wananchi.

Waziri Ummy Mwalimu ameishukuru Serikali ya Marekani kupitia miradi na programu zinatokelezwa hapa nchini kwa kutoa msaada wa USD Milioni 22 kwa jili ya kusaidia Serikali katika mapambano dhidi ya UVIKO-19 na kuhamasisha wananchi kuchanja zaidi chanjo ya UVIKO-19.

Aidha Waziri Ummy Mwalimu ameiomba CDC kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kusaidia kupunguza uhaba wa rasilimali watu katika Kada za Afya kwa kutoa ajira za mikataba kwa Watanzania ili kuweza kupunguza pengo la ajira za Kada ya afya ambalo kwa sasa kuna uhaba wa asilimia 53.

Kwa upande wake Mkuregenzi Mkazi wa CDC nchini Dkt. Swaminathan ameishukuruku Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya kwa kuendelea kuwapa mazingira rafiki na ushirikiano zaidi katika kupambana na kdhibiti magonjwa.

“Tunaamini tupo hapa sio kwajili ya kuzuia magonjwa kuingia marekani, ugonjwa ukitokea hapa Tanzania unaathari moja kwa moja kabla ya kwenda kwingine na ndio lengo letu kuu kushirikana kwa pamoja katika mapambano dhidi ya magonjwa mbalimbali.” Amesema Dkt. Swaminathan

Dkt. Swaminathan amesema kuwa CDC imekuwa ikifanya kazi kwa ukaribu na Wizara ya Afya nchini katika mapambano dhidi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) kwa kutoa msaada wa dawa za kupunguza makali ya VVU, kushiriki katika tafiti mbalimbali zenye kulenga kupata tiba dhidi ya magonjwa mbalimbali pamoja na mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu, Malaria pamoja na ugonjwa wa UVIKO-19 nchini.

Dkt. Swaminathan amesema kuwa milango ya CDC iko wazi muda wote kwa kutoa ushauri wa kitaalam pamoja na rasilimali katika kusaidia Serikali kuweza kutoa huduma bora za tiba kwa wananchi.

No description available.

Saturday, February 26, 2022

ULEGA ATAKA VIKUNDI VYA BAGAMOYO VIKOPESHWE FEDHA ZA HALMASHAURI, KWA KUTUMIA VIZURI FURSA YA UCHUMI WA BLUU.

 No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akizungumza na wana kikundi cha ufugaji wa Majongoo Bahari kilichopo Kaole kata ya Dunda Halmashauri ya Bagamoyo, kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge.

................................................ 

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo, kuvipatia fedha vikundi viwili vilivyopo Bagamoyo ambavyo vinajishughulisha na ufugaji wa Majongoo Bahari na kilimo cha Mwani.

Ulega ametoa agizo hilo Tarehe 25 Februari 2022 alipotembelea vikundi hivyo ili kujionea shughuli zinazofanywa na vikundi hivyo.

Naibu waziri huyo alifika Bagamoyo kufungua  kikao kazi cha mkakati na kampeni ya kuhamasisha shughuli za ukuzaji viumbe Bahari ambacho kilijumuisha wataalamu kutoka mikoa ya Dar es salaam na Pwani lengo likiwa ni kutoa elimu juu ya fursa zilizopo kwenye uchumi wa bluu ambao unjumuisha mazao ya Bahari ikiwemo ufugaji wa Majongoo Bahari, Ufugaji wa Kaa, ukuzaji wa Kamba kochi na kilimo cha mwani.

Kikao kazi hicho kilijumuisha kutembelea vikundi vilivyopo Kaole na Mlingotini ambavyo tayari vinatumia fursa ya uchumi wa bluu kwa kutekeleza ufugaji wa majongoo Bahari na kilimo cha mwani.

Kufuatia kazi nzuri alizoziona Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo, kuwapatia fedha za Halmashauri zilizotengwa kwaajili ya vikundi ili waweze kuzitumia kuendesha miradi yao.

Alisema serikali inapotoa fedha inapenda kujiridhisha juu ya utendaji kazi wa hicho kikundi ambapo kwa kikundi cha ufugaji Majongoo Bahari cha Kaole tayari kimeonyesha juhudi kwa kufanya kazi inyoonekana pamoja na kikundi cha Msichoke cha Mlingotini kinachojishughulisha na kilimo cha mwani pamoja na utengezaji wa bidhaa mbalimbali.

Wakati huo huo amemuomba mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Muharami Mkenge kuwasaidia kufuatilia upatikanaji wa nembo ya tbs kwaajili ya bidhaa wanazozalisha ili waweze kutafuta masoko nchi nzima na nje ya nchi.

Pia amemuagiza Mkurugenzi wa Benki ya Kilimo kurudi Bagamoyo baada ya wiki moja ili kuwasikiliza wana vikundi hao na kuwapa ushauri wa kitaalamu na baadae kuwakopesha fedha ambazo zitatua changamoto zao.

Awali kikundi cha ufugaji majongoo bahari cha kaole kimesema kinabiliwa na changamoto ya wizi wa majongoo hivyo wanaomba kupatiwa Boti itakayowasaidia kufanya doria eneo la mradi, huku kikundi cha Msichoke cha Mlingotini nacho kimesema wanahitaji fedha zitakazowaongezea kupata mashine ya kukaushia Mwani na kusindika, pamoja na boti itakayowasidia katika shughuli za ulimaji wa mwani hasa pale maji yanapojaa.

Vikundi vyote hivyo vimeishukuru serikali ya wilaya kwa kuwapa ushirikiano wa karibu ili kufanikisha kazi zao.

No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akiwa ameshika jongoo bahari wanaofugwa na kikundi cha ufugaji wa majongoo bahari kilichopo Kaole kata ya Dunda Halmashauri ya Bagamoyo.

No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akisikilza taarifa ya kikundi cha ufugaji wa majongoo bahari kilichopo Kaole kata ya Dunda Halmashauri ya Bagamoyo.

No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akiwa anakunywa juisi ya Mwani iliyotengenezwa na kikundi cha Msichoke kilichopo kijiji cha Mlingotini kata ya Zinga Halmashauri ya Bagamoyo, Kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, na kulia ni Katibu mwenezi wa CCM wilaya ya Bagamoyo, John Francis (Bolizozo)

No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akizungumza na wana kikundi cha Msichoke ambacho kinaajishughulisha na kilimo cha Mwani na utengenezaji wa bidhaa zinazotokana na zao la Mwani.

No description available.No description available.

Hizi ni baadhi ya bidhaa zinazotokana na zao Mwani, ambazo zinatenezwa na kikundi cha Msichoke kilichopo kijiji cha Mlingotini kata ya Zinga Halmashauri ya Bagamoyo.