Friday, October 29, 2021

TaSUBa KUWA CHUO CHA KIMATAIFA CHA SANAA NA UTAMADUNI.

No description available.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Innocent Bashungwa akifungua Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Tamaduni Bagamoyo lililofanyika Usiku wa kuamkia  Oktoba 28 hadi 30, 2021 katika viwanja vya Chuo cha Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo(TASUBA) mjini Bagamoyo.

.........................................

 

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa amesema wizara yake imekusudia kukibadilisha chuo cha TaSUBa kilichopo Bagamoyo kuwa ni chuo cha Sanaa na Utamaduni cha kimataifa, ili kwenda sambamba na dhamira ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kukuza na kuendeleza Sanaa na Utamaduni hapa nchini.

 

Waziri Bashungwa ameyasema hayo mjini Bagamoyo katika viwanja vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni (TaSUBa) wakati wa kuzindua rasmi Tamasha la 40 la kimataifa la sanaa na utamaduni ambalo limeanza Tarehe 28 Oktoba 2021 litakalodumu kwa muda wa siku tatu hadi 30 Oktoba 2021.

 

Alisema kutakuwa na maboresho makubwa yatakayofanyika katika chuo cha TaSUBa ili kukidhi viwango na vigezo vya kimataifa katika maswala Sanaa na Utamaduni.

 

Aidha, alisema kuwa, maboresho hayo pia yatahusisha taasisi zinazowasaidia wasanii hapa nchini kama vile Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) na Chama cha hakimiliki Tanzania (COSOTA) ambapo utendaji kazi wa taasisi hizo unapaswa kuwa wa kiwango cha juu ili wasanii waweze kunufaika kupitia kazi zao.

 

Aliongeza kuwa, Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo itaendelea kushirikiana na wasanii hapa nchini ili kuhakikisha wasanii wanaboreshewa mazingira yao ya kazi pamoja na kulinda haki zao za msingi katika kazi zao.

 

Alifafanua kuwa, ushirikiano baina wizara na wasanii utasaidia kulinda ajira za wasanii na kazi zao ili waweze kufanya vizuri zaidi na hatimae wao iwe ni chachu ya kuenea ajira kwa vijana wengi walioingia kwenye tasnia ya sanaa.

 

Akizungumzia Tamasha hilo la 40 la kimataifa la sanaa na utamaduni Bagamoyo, Bashungwa alisema ni Tamasha kubwa na la aina yake kuwahi kutokea na kwamba wizara itaendelea kuboresha mazingira ya maandalizi ili kila mwaka Tamasha liongezeke ubora katika macho ya kitaifa.

 

Alitumia nafasi hiyo kuwapongeza viongozi mbalimbali ambao wamfanikisha maandalizi ya Tamasha hilo akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge, Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallaah, Katibu Mkuu wa wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbas pamoja Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUB) Dkt. Harbert Makoye.

 

Aidha, alisema kuwa kukamilika kwa Tamasha hilo la 40 ndio mwanzo wa maandalizi ya Tamasha ka 41 na kwamba amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abasi kuanza maandalizi ya Tamasha 41 hapo mwakani.

 

Aliwapongeza pia viongozi wa nchi mbalimbali waliohudhuria Tamasha hilo na kusema kuwa hiyo ndio maana ya kuita Tamasha la kimataifa kwa kukusanya kwake wageni kutoka nchi mbalimbali wakiwemo viongozi na vikundi vya sanaa kutoka katika nchi hizo.

 

Tamasha la 40 la kimataifa la Sanaa na Utamaduni limezinduliwa rasmi Tarehe 28 Oktoba 2021 na linatarajiwa kufungwa tarehe 30 Oktoba 2021 katika viwanja vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni (TaSUBa) ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni Sanaa ni Ajira.

Thursday, October 28, 2021

BENKI KUU YAONYA MATUMIZI MABAYA YA NOTI.

 No description available.

Hivi karibuni kuimeibuka wimbi la vitendo vya matumizi mabaya ya noti katika shughuli mbalimbali  za kijamii hususan kwenye sherehe za harusi ambapo watu wamekuwa na tabia ya kutunza wahusika  wa matukio kwa kuwarushia noti zinazoanguka sakafuni na muda mwingine kukanyagwa, kuziviringisha katika maumbo mbalimbali na kutumia kama mapambo, kuweka kwenye mwili wa  mtu ulio loa jasho na matukio yote yanayofanana na hayo.  

Matendo haya yanatweza fedha ya Tanzania ambayo ni moja ya tunu za taifa letu.Vitendo hivyo  vinaendelea kutokea licha ya Benki Kuu ya Tanzania na viongozi mbalimbali wa Serikali kwa nyakati  tofauti kuvikemea. 

Hivyo basi, Benki Kuu ya Tanzania inatoa onyo kwa wananchi ambao bado wanakaidi onyo hili  ambalo limetolewa mara kadhaa kuhusu namna sahihi ya kutunza noti za Tanzania zinazokuwa  mikononi mwao kwa kuzitumia kinyume na maadili pamoja na matakwa ya kisheria. 

Kwa taarifa hii, Benki Kuu ya Tanzania itaanza kuchukua hatua dhidi ya wale wote watakaohusika  na vitendo vya matumizi mabaya ya noti za Tanzania kwa njia yoyote ile ikiwamo kuweka pesa  sakafuni au sehemu yoyote ambayo siyo nadhifu. Vitendo hivyo vinachangia kutweza fedha zetu na kusababisha uchakavu hivyo kuiongezea Serikali gharama kubwa za kuchapisha fedha zingine. 

Aidha, Benki Kuu inawashauri washiriki katika matukio yote ambayo yanahusisha matumizi ya fedha  kuandaa vyombo maalum vya kuweka fedha hizo badala ya kufanya vitendo ambavyo havikubaliki. 

Wananchi wote mnahamasishwa kutoa taarifa mara moja kwa Benki Kuu au Vyombo vya Usalama  pale mnapobaini matumizi yasiyo sahihi ya fedha zetu ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi  ya wahusika. 

Tukitunza fedha zetu tunachangia kuzifanya zitumike kwa muda mrefu na hivyo kuipunguzia  Serikali

 

MAGAZETI YA LEO TAREHE 28 OKTOBA 2021.

 No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

Wednesday, October 27, 2021

KILOSA KUTUMIA BILIONI 4 ZA IMF KUIMARISHA AFYA NA ELIMU

 No description available.

No description available.

Na Mwandishi Wetu

WILAYA ya Kilosa mkoani Morogoro imepata mgao wa Sh bilioni 4.33 kutoka kwenye fedha zilitolewa na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), kwa Serikali ya Tanzania.

Mgao huo wa Sh bilioni 4.33 uliopelekwa Kilosa na Serikali ni kati ya Sh, trilioni 1.3 ambayo imetangazwa na Rais Samia Suluhu Hassan hivi karibuni kuwa zitatumika kwenye kutekeleza miradi mbalimbali kwenye sekta ya afya, elimu, maji, viwanda na nyingine.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Alhaj Majid Mwanga amesema fedha hizo zitatumika kutekeleza miradi mipya kupitia mpango wa maendeleo  kwa usatawi wa taifa na mapambano dhidi ya Uviko-19 ambapo wilaya hiyo imepata fedha kwenye sekta ya elimu na afya.

Alhaj Mwanga amesema Sh bilioni 2.94 zitatumika kujenga vyumba 147 vya madarasa ya shule za sekondari na Sh milioni 780 zitajenga vyumba vya madarasa 39 ya vituo shikizi 13.

“Shilingi milioni 420 zitatunua mashine za mionzi katika Hospitali ya Mikumi, Sh milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya wagonjwa mahututi na Sh milioni 90 zitajenga nyumba za watumishi,” alisema.

Mkuu huyo amesema wamejipanga kusimamia vizuri mchakato mzima wa ujenzi wa miradi hiyo na kutoa angalizo kwa watu ambao wanatarajia kutumia miradi hiyo kwa manufaa binafsi.

Mwanga amewataka watendaji wote kuanzia ngazi ya kitongoji hadi wilayani ambao wanahusika na utekelezaji wa miradi hiyo kujituma ili miradi ikamilike kwa wakati.

“Kwa niaba ya wananchi na viongozi wa Kilosa, napenda kumshukuru Rais Samia na Serikali yake kutupatia kiasi hiki cha fedha ambacho kinaenda kufanya mapinduzi katika sekta husika. Ninapenda kumhakikishia kuwa tupo pamoja na yeye na hatutavumilia mtu yoyote ambaye atajaribu kuenda kinyume na malengo,” alisema.

Alhaj Mwanga amesema iwapo kila mmoja atatimiza malengo yake kwa weledi ni wazi kuwa Kilosa itabadilika na kupata maendeleo kwa haraka.