Friday, October 22, 2021

MAJALIWA AFUNGUA MKUTANO WA TANO WA TEHAMA

 No description available.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipokea kwa Tuzo kutoka kwa Waziri wa  Habari, Mawasiliano na Tekinolojia ya Habari, Dkt. Ashatu Kijaji  kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ya kutambua mchango wake katika kukuza sekta ya TEHAMA Nchini.  katika Mkutano wa Tano wa Mwaka wa Tehama Tanzania uliofanyika kwenye ukumbi wa  Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) jijini Arusha.

No description available.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akionyesha nakala za mwongozo wa usajili wa  watalaamu wa Tehama baada ya kuuzindua,  katika Mkutano wa Tano wa Mwaka wa Tehama Tanzania uliofanyika kwenye ukumbi wa  Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) jijini Arusha, Oktoba 22, 2021. Kushoto ni Waziri wa  Habari, Mawasiliano na Tekinolojia ya Habari, Dkt. Ashatu Kijaji.

 No description available.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Wadau wa Sekta ya TEHAMA wakati alipofungua Mkutano wa Tano wa Mwaka wa TEHAMA Tanzania uliofanyika kwenye ukumbi wa  Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) jijini Arusha.

No description available.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akimsikiliza, Mkurugenzi wa Masuala ya Sekta kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Emmanuel Manasseh  (kushoto) wakati alipotembelea banda la TCRA katika Mkutano wa Tano wa Mwaka wa TEHAMA Tanzania uliofanyika kwenye ukumbi wa  Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) jijini Arusha, Oktoba 22, 2021.  Wa pili kushoto ni Waziri wa  Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Ashatu Kijaji, kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Zainab Chaula na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongella.

No description available.

Wadau wa Sekta ya TEHAMA wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Mkutano wa Tano wa Mwaka wa TEHAMA Tanzania uliofanyika kwenye ukumbi wa  Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) jijini Arusha, Oktoba 22, 2021. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI MAKAMBA AKUTANA NA VIONGOZI EQUINOR

 May be an image of 2 people, people sitting, people standing and indoor

Waziri wa Nishati Mh. January Yusuf Makamba amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa kampuni ya utafutaji na uzalishaji wa mafuta na gesi asilia ya Equinor (Afrika) Bw. Paul McCafferty.

 

Viongozi hao wamekutana, Oktoba 21, 2021 katika ofisi ndogo za Wizara ya Nishati zilizopo jijini Dar es Salaam.

 

Mazungumzo hayo yamehudhuriwa pia na viongozi wengine wa Equinor na Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC).

 

Imeelezwa kuwa mazungumzo hayo ni sehemu ya maandalizi ya majadiliano ya Mkataba wa Nchi Hodhi (HGA) wa Mradi wa Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia (LNG) yanayotarajiwa kuanza rasmi Novemba 8, 2021.

 

Kwenye kikao hicho, Bw. McCafferty amempongeza Waziri Makamba kwa niaba ya serikali kwa hatua hiyo ya kuanza tena kwa majadiliano ya mkataba huo wa HGA kwani yatafungua njia kwaajili ya kuanza kwa utekelezaji wa mradi huo wa LNG.

 

Bw. McCafferty ameeleza kuwa Equinor iko tayari kwa majadiliano hayo na kuongeza kwamba mradi huo ni moja ya miradi yenye uwekezaji mkubwa inayotekelezwa na Equinor duniani, hivyo ni majadiliano muhimu katika kuweka msingi mzuri wa utekelezaji wake.

 

Equinor ni moja ya wabia wakuu wa utekelezaji wa mradi huu wa LNG ambao utasimamiwa na Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA). Wabia wengine ni pamoja na kampuni ya Shell na TPDC kwa niaba ya serikali.

Mradi wa LNG unakadiriwa kuwa wa thamani ya takriban Dola za Marekani bilioni 30 huku ukitarajiwa kutengeneza nafasi za ajira za moja kwa moja 6,000 na zisizo za moja kwa moja zaidi ya 15,000 kwa Watanzania.

May be an image of 3 people, people sitting and indoor

May be an image of 2 people, people sitting and indoor