Tuesday, October 19, 2021

DC KIBAHA AAGIZA KUONDOLEWA MARA MOJA WAFANYABIASHARA PICHANDEGE ,AELEKEZA ENEO KUBAKI WAZI NA SAFI

No description available.

 Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha

MKUU Wa Wilaya ya Kibaha, Mkoani Pwani, Sara Msafiri amewaagiza Maafisa mazingira, biashara na afya kusimamia agizo la kuwaondoa wafanyabiashara wa eneo  la Pichandege na kuhakikisha wanahamia  Msufini River Road kupisha upanuzi wa barabara.

 

Aidha amepiga marufuku wenye maduka kuuza bidhaa za sokoni na mbogamboga na kuwaasa kulinda miundombinu ya barabara iwe safi.

 

Ameeleza ni mara ya nne uongozi wa wilaya umekwenda kuongea na kutoa onyo kwa wafanyabiashara hao lakini wanaonekana kukaidi agizo la serikali.

 

Msafiri aliyaeleza hayo, wakati alipofika kwa mara ya mwisho eneo hilo na kutoa amri ya kuondolewa kwa nguvu oktoba 19 mwaka huu ili kuacha eneo hilo wazi.

 

Alisema , wafanyabiashara baadhi yao wamekuwa wakipenda kuhamishwa  kwa nguvu badala ya kutii kwa hiari Jambo ambalo sio zuri.

Alisema mwisho ilikuwa tarehe moja Oktoba mwaka huu ,ambapo ni muda wa kutosha.

 

“Shirika la elimu limeshatoa eneo na miundombinu yote ya maji, umeme, barabara, vyoo vipo, sasa tumekuja kuwaondoa wote.

 

“Kama una bidhaa za sokoni nendeni sokoni, huwezi ukawa na leseni ya maduka ukauza  mchicha mbogamboga,matunda,nyanya mbele ya duka lako, Ni ukiukwaji wa leseni yako uliyopewa,'”;!

 

maeneo ya kutosha yameshatengwa, limeongezwa na eneo la mnada, hivyo Ni makosa kufanya biashara maeneo yasiyo rasmi”:alifafanua Msafiri.

 

Msafiri alieleza kwamba, maeneo ya Pichandege yaachwe wazi, na ihakikishwe yanakuwa safi.

 

Nae Ofisa Mazingira Mji wa Kibaha, Mkana Mkana alisema kwa mujibu wa sheria ndogo ya mazingira Kibaha mwaka 2012 vipengele vyote hadi 32 inamtaka mwananchi afanye usafi maeneo ya biashara yake na kutofanya biashara nyingine nje ya leseni yake.

 

Mkana alieleza, endapo mtu akienda kinyume na takwa hilo, atakuwa ametenda kosa kifungu 33  hivyo basi atatakiwa kulipa faini 50,000 ama kifungo cha miezi sita au vyote kwa pamoja.

 

“Wanakiuka taratibu hivyo sheria kali ya kifungo cha miezi sita ama faini 50,000 itatolewa ama vyote kwa pamoja, Na wafanyabiashara hawa walishapewa taarifa na onyo mara kadhaa lakini bado wanakiuka.”alisisitiza Mkana.

 

Ofisa biashara Mji wa Kibaha, Adolf Msangi, alibainisha wafanyabiashara hao wanapaswa waondoke na pia maeneo bado yapo kama wapo ambao hawataki kuhamia Msufini basi waende loliondo Kama sio loliondo waende Lulanzi.

 

Kwa upande wake,Mwenyekiti wa wafanyabiashara, Daniel singa alisema maeneo yapo ya wafanyabiashara wote waende wakagawiwe maeneo na kuacha kukaidi.

No description available. No description available.

 

DC TEMEKE AIPONGEZA SHULE YA YEMEN DYCCC.

 No description available.

Mkuu wa wilaya ya Temeke Jokate Mwegelo amepongeza uongozi wa shule za Yemen DYCCC kwakusimamia utoaji wa elimu bora katika shule zake na kuipa sifa wilaya hiyo.

Katika hutuba iliyosomwa kwa niaba yake na Kaimu Afisa Elimu Msingi, Rashid Ally, amesema elimu bora ndio inayomjenga mtoto katika maisha yake ya baadae, kwa familia yake, jamii inayomzunguuka na Taifa kwa ujumla.

Rashid alisema anamuwakilisha Mkuu wa wilaya ya Temeke na kwamba salamu za Mkuu wa wilaya hiyo ni kuupongeza uongozi wa Yemen DYCCC kutokana na kusimamia utoaji wa elimu bora katika shule zake.

Alisema kitendo cha kutoa elimu ni kuunga mkono juhudi za serikali, hivyo uongozi wa wilaya utakuwa pamoja na uongozi wa Yemen DYCCC katika kuhakikisha shule hiyo inaendelea kutoa elimu bora.

Aidha, katika kuhakikisha elimu bora inapatikana shuleni hapo amewataka wazazi kulipa ada kwa wakati ili kuiwezesha shule kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi katika kufundisha watoto.

Nae Mwenyekiti wa Bodi ya Elimu ya DYCCC, Hassan Akrabi amesema kazi kubwa waliyonayo ni kuhakikisha mtoto anakuwa na maadili mema katika kipindi chote anapokuwa shuleni ambapo hali hiyo itamjenga kuishi katika maadili mema pia hata akiwa nje ya shule.

Aidha, aliwataka wahitimu hao kuendeleza maadili mema waliyoyapata wakiwa shuleni hapo ili waweze kuendelea kutafuta elimu huku wakiwa na maadili mema.

Aliwataka wazazi kuendelea kuwaamini na kuwaomba watoto wanaoanza kidato cha kwanza wapelekwe katika shule ya Sekondari ya Yemen DYCCC ili wakaendelezwe katika malezi yenye maadili.

Awali akisoma risala mbele ya mgeni rasmi, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Yemen DYCCC, Rahim Burhan, alisema shule hiyo imepata mafanikio mbalimbali toka kuanzishwa kwake mwaka 2003 ambapo kwa sasa shule inamiliki jengo la kisasa la ghorofa tatu ambalo linajumuisha madarasa 36, ofisi 18, vyoo 52, stoo 02, maktaba 01, chumba cha maabara 01, maabara ya Computer 01, na ukumbi ambao hutumika kwaajili ya ibada ya swala.

 No description available. 

Kaimu Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Temeke, Rashid Ally, akizungumza katika mahafali ya Darasa la saba 2021 katika shule ya Msingi Yemen DYCCC iliyopo Chang'ombe jijini Dar es salaam.


No description available.No description available.

Wahitimu wa darasa la saba, Shule ya Msingi Yemen DYCCC iliyopo Chang'ombe jijini Dar es salaam wakifuatilia kwa umakini kinchaoendelea katika mahafali yao yaliyofanyika shuleni hapo.


No description available.

  

MAGAZETI YA LEO TAREHE 19 OKTOBA 2021

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

No description available.

Monday, October 18, 2021

KARIBUNI KWENYE TAMASHA LA SANAA BAGAMOYO-DC. ZAINAB.

 No description available. 

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallaah (katikati) akizungumza na waandishi wahabari (hawapo pichani) kuhusu Tamashala la 40 Kimataifa la Sanaa na Utamaduni litakalofunguliwa rasmi siku ya Alhamisi tarehe 28 oktoba 2021, wa tatu kushoto ni
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, Dkt. Herbert Francis Makoye.

...................................................................

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallaah, amewakaribisha wananchi ndani na nje ya Bagamoyo kuhudhuria Tamasha la 40 la kimataifa la sanaa na Utamaduni litakalofanyika katika  viwanja vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) siku ya tarehe 28 Oktoba 2021 hadi 30 Oktoba 2021.

Akizungumza na waandishi wa Habari katika Mkutano uliofanyika ukumbi wa TaSUBa, Mkuu huyo wa wilaya ya Bagamoyo amesema Tamasha hilo la kimataifa la sanaa na utamaduni ni fursa ya kipekee kwa wasanii kuonyesha kazi zao mbele ya wageni watakaohudhuria hilo.

Alisema katika Tamasha hilo zipo fursa nyingi kwa wasanii, wananchi wa kawaida pamoja na serikali kwa ujumla.

Akifafanua zaidi DC. Zainab alisema kwa wasanii ni fursa ya kuonyesha kazi zao kwa waliohudhuria wakiwemo wageni kutoka nje ya nchi na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wadau wa sanaa na utamaduni.

Aidha alisema wananchi wanaweza kutumia fursa hiyo ya Tamasha kujifunza namna sanaa inayoweza kumuinua kijana wa kitanzania na kumfanya sio tu mtoa burudani kwa jamii lakini pia ikampatia kipato kwaajili ya kuendesha maisha yake.

Aliongeza kwa kusema kuwa, Serikali pia itatumia fursa hiyo ya Tamasha la sanaa kutangaza vivutio vilivyopo Bagamoyo ambapo wageni watweza kujionea maeneo mbalimbali ya kihistoria yaliyopo ndani ya Bagamoyo na hivyo watakapoweza kutembelea vivutio hivyo serikali itaingiza mapato kupitia watalii hao.

Alisema kutokana na umuhimu wa Tamasha hilo kwa wageni kutoka nje ya Bagamoyo na nje ya Tanzania kutakuwa na punguzo maalum la bei katika hoteli zote za Bagamoyo ili kuwarahisishia wageni kupata sehemu za kulala kwa gharama nafuu.

Mkuu huyo wa wilaya amesema kutokana na mapambano dhidi ya ugonjwa Corona, kama wilaya itatumika nafasi hiyo kuweka banda maalum lakupata chanjo ya uviko19, kwa wale ambao bado hawajapa chanjo hiyo ili iwe rahisi kwao kuchanja huku wakiendelea na burudani kwa siku zote tatu za Tamasha hilo.

Wakati huohuo, Mkuu huyo wa wilaya ambae pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya, amewahakikishia wageni wote wilayani humo kuwa, wilaya ya Bagamoyo ipo salama na kwamba wataweza kutembea maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo bila ya bghudha ya aina yoyote.

Alisema wilaya ya Bagamoyo ni tulivu na haina vitendo vyovyote vya uhalifu na kwamba ulinzi utaimarishwa zaidi siku za Tamasha.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, Dkt. Herbert Francis Makoye, alisema wanajinia kuendelea kuandaa matamasha kila mwaka ndani ya chuo hicho tamasha la mwaka huu ni la 40.

Alisema yapo matamasha mengi yanaanzishwa hapa nchini lakini hayana muendelezo kwa TaSUBa kuendelea kuandaa Tamasha kila mwaka ni mafanikio makubwa ya kujivunia ndani ya chuo, kwa viongozi wa wilaya, wizara na Taifa kwa ujumla.

Dkt. Makoye alisema Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo hufanyika kila mwaka na huandaliwa na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) chini ya Wizara ya Sanaa Utamaduni na Michezo likiwa na malengo ya

·       Kutunza na kuenzi sanaa na utamaduni wa mtanzania.

·       Kutengeneza jukwaa ambalo wanafunzi wa TaSUBa wanalitumia kupima viwango vyao vya umahiri katika sanaa kwa mwaka katikia fani za sanaa za maonyesho na zile za ufundi.

·       Kukutanisha watu wa tamaduni mbalimbali kutoka sehemu mbalimbali za dunia ili kuonyesha utajiri wao wa sanaa na utamaduni.

·       Kutenegeneza jukwaa ambalo ni kiungo cha kujenga mahusiano ya wasanii wa ndani na nje ya nchi kupitia maonyesho ya sanaa.

·       Kubadilishana uzoefu na mawazo katika kuendeleza tasnia ya sanaa.

·       Kutoa burudani kwa watanzania na wageni kutoka nchi mbalimbali.

Tamasha la mwaka huu litapambwa na ngoma za asili, muziki wa kizazi kipya, singeli, sarakasi, mazingaombwe, maigizo pamoja na maonyesho na biashara ya sanaa na ufund.

Aidha, Dkt. Makoye aliongeza kuwa, katika Tamasha hilo kutakuwa na warsha na semina zitakazohusu mambo mbalimbali katika Nyanja za sanaa na utamaduni.

Alisema jumla ya vikundi ambavyo vimethibitisha kushiriki ni 70 ambapo vikundi vya ndani ya nchi ni 60 na vikundi 10 kutoka nje ya nchi.

Tamasha litafunguliwa rasmi siku ya Alhamisi Tarehe 28 Oktoba 2021 likitanguliwa na mkesha siku ya Jumatano tarehe 27 Oktoba 2021 ambapo kila siku kutakuwa na mgeni mashuhuri na litafungwa rasmi siku ya jumamosi tarehe 30 Oktoba 2021.

No description available. 

Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, Dkt. Herbert Francis Makoye, (aliyesimama) akizungumza wakati wa kumkaribisha Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Bi Zainab Abdallaah (wa tatu kulia).

No description available. 

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallaah (wa nne kushoto) amkiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wakufunzi na wageni waalikwa.