Saturday, May 5, 2018
Friday, May 4, 2018
NAIBU WAZIRI WA NISHATI AWASHA UMEME VIJIJI VYA CHALINZE,

Naibu
waziri wa Nishati, Mh. Subira Mgalu amesema Serikali ya awamu ya tano chini ya
uongozi wa Dkt. John Magufuli imedhamiria kufikisha umeme kila kijiji ili
kuwaondolea adha wananchi walikosa huduma ya umeme kwa muda mrefu.
Naibu
waziri huyo wa Nishati ambae pia ni Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Pwani
aliyasema hayo katika ziara yake Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo
ambapo aliweza kuzindua miradi ya umeme vijijini REA kwa kuwasha umeme katika
vijiji kadhaa vya Halmashauri hiyo.
Aidha,
alisema ni fusa kwa wananchi sasa kujitokeza kuchukua fomu na kulipa gharama ya
shilimngi 27,000 kwaajili ya kuunganishiwa.
Alisema
uzinduzi wa miradi hiyo ya umeme ni utekelezaji wa ahadi zilizotolewa na
serikali ya awamu ya tano katika kampeni za uchaguzi na kwamba kilichobaki sasa
ni utekelezaji tu.
katika
hatua nyingine Naibu waziri huyo amewashukuru wadau wa Elimu katika Halmashauri
hiyo wakiongozwa na Mrs Barbara na Wentworth Africa Foundation kwa msaada wao
walotoa katika Sekondari ya wasichana Mandela ambapo waliweza kukabidhi taulo
maalum kwaijili ya matumizi ya wasichana na kila msichana amepata Taulo Za
kutumia Mwaka Mzima Kwa Wasichana Mia Tano Hamsini.
Wakati
huo huo Naibu waziri huyo wa Nishati aligawa Taa za sola kwa Zahanati ambazo
hazijafikiwa na umeme ili kuwarahishia kina mama wakati wa kujifungua.

Naibu waziri wa Nishati Mh. Subira Hamisi Mgalu akiwa ziara katika vijiji vya Chalinze ambapo aliweza kuwasha umeme katika vijiji vya Hondogo na Saleni pmoa na kugawa Taa za sola katika Zahanati ya Mihuga.

Naibu
waziri wa Nishati Mh. Subira Hamisi Mgalu ambae pia ni Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Pwani akikabidhi Taulo maalum kwaijili ya matumizi ya wasichana Kwa Shule ya
Sekondari ya Wasichana Mandela ambapo kila msichana amepata Taulo Za kutumia
Mwaka Mzima Kwa Wasichana Mia Tano Hamsini, Msaada
huo umetolewa na Mrs Barbara na Wentworth Africa Foundation, Wadau hao wa Elimu Pia wameahidi kufadhili
ujenzi wa Maktaba.
Mh. Subira Mgalu amekabidhi, Mabox ya Vitabu Kwa Maendeleo ya Shule.

Naibu
waziri wa Nishati, Subira Mgalu akiwa katika zoezi la kugawa Taa za solar Kwa
ajili ya Wadi za kuzalishia Kina Mama Kwa ajili ya Zahanati za Mihuga ,
Masimbani na Kweikonje Maeneo ambayo hayana MiundoMbinu ya Umeme.
Naibu waziri wa Nishati, Subira Mgalu akiwa kijiji cha Hondogo kata ya Miono Halamshauri ya Chalinze ambapo aliweza kuzindua mradi wa umeme viijini REA ambapo kijiji hicho sasa kimepata umeme.
Wednesday, May 2, 2018
DKT. ABBAS AKUTANA NA WAANDISHI, WASOMI WA MAWASILIANO YA UMMA MKOANI MWANZA

Mkurugenzi Mtendaji wa Muungano
wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania Abubakar Karsan akimuonesha
Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan
Abbasi bango lenye kuonesha majukumu ya klabu za waandishi wa habari nchini,Jana
1/05/2018 mkoani Mwanza.

Mkurugenzi Mtendaji wa Muungano
wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania Abubakar Karsan
akikabishi Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa
Serikali Dkt. Hassan Abbasi kalenda ya chama hicho,Jana 1/05/2018 mkoani
Mwanza.
Mkurugenzi wa Idara ya
Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akiongea na
wasomi wa Mawasiliano ya Umma wa Chuo cha Mtakatifu Agustino (SAUT) Mwanza
kuhusu Maadili ya Uandishi wa Habari na umuhimu wa uandishi katika kufuata weledi,
Jana 1/05/2018 mkoani Mwanza.
Mkurugenzi wa Idara ya
Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akishiriki
kipindi cha TUJADILIANE kinachoendeshwa na Doto Bullendu chenye lengo la
kuhamasisha maendeleo katika nchi kwa kutumia vyombo vya Habari, Jana 1/05/2018
mkoani Mwanza

Mkurugenzi Mtendaji wa Muungano
wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania Abubakar Karsan akiongea wakati wa
kumkaribisha Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO Dkt. Hassan Abbasi kabla
hajashiriki kipindi cha TUJADILIANE kilicho hudhuriwa na waandishi mbalimbali
wa vyombo vya habari vya kanda ya Ziwa, Jana 1/05/2018 mkoani Mwanza.
Tuesday, May 1, 2018
MAADHIMISHO YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI KUFANYIKA DODOMA KITAIFA.

WAZIRI wa Habari, Utamaduni,
sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe anatarajiwa kuwa mgeni rasmi
katika Kilele cha Maadhimisho ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini .
Akizungumza
na Waandishi wa Habari Jijini Dodoma , Katibu wa Jukwaa la Wahariri
Tanzania (TEF) Nevile Meena alisema mada mbalimbali zitakazojadiliwa ni pamoja
na changamoto zinazovikumba vyombo vya habari katika kipindi cha miaka 27
tangu Azimio la Windhoek, Namibia, lilipopitishwa linalohusu uhuru wa vyombo
vya habari.
Akieleza
zaidi alisema, Kilele cha Maadhimisho hayo kitafikiwa
kesho, Mei 3, mwaka huu, mkoani Dodoma, ambapo siku moja kabla kutakuwa
na majadiliano kuhusu hali ya vyombo vya habari nchini ambayo yatafunguliwa na
Spika wa Bunge, Job Ndugai.
“Tutapata
Wakati muafaka wa kujadili mada kuu ya changamoto zetu, pia kutakuwa na mada
nyingine zitakuwa zinaendelea katika vikundi, ikiwemo inayohusu mitandao ya
kijamii kama inatakiwa kudhibitiwa au watumiaji ndio wajidhibiti wenyewe,”
alisema Meena.
Pamoja
na hayo alisema kutakuwa na mada kuhusu unyanyasaji wa kingono ndani ya vyombo
vya habari, na kuona kama suala hilo bado ni kikwazo hasa kwa waandishi
wanawake kupata nafasi za juu kwenye vyombo vya habari.
Aidha
Katibu huyo wa TEF alisema, kutakuwa na mada kuhusu usalama wa waandishi wa
habari, ni kiasi gani waandishi wanakuwa salama wanapofanya kazi zao katika
maeneo mbalimbali.
“Suala
la haki za kupata habari, japo limeingizwa kwenye sheria tangu mwaka 2016 na
kanuni zake Februari mwaka huu, na namna gani mwandishi anaweza kudai haki
hiyo,” alisema.
Naye
Makamu Mwenyekiti wa Klabu za Waandishi Tanzania (UTPC), Jane Mihanzi aliyataja
maadhimisho hayo kuwa ni fursa kwa wadau wa habari kujadili namna vyombo vya
habari vilikotoka, vilipo na wapi vinaelekea.
” Sisi
kama wadau wa habari tunaotambua na kuwajali wananchi kupata habari, tumekuwa
tukisaidia waandishi kuwapamafunzo na vifaa vya kazi,”alisema.
Kwa
upande wake mwakilishi wa Mfuko wa Habari Tanzania (TMF), Razia Mwawanga
alisema kupitia maadhimisho hayo wanahabari na jamii kwa ujumla wataelewa
umuhimu na wajibu wa kuwajibika.
Alisema,japo
kuwa taaluma hii ina vikwazo vingi kuna ,waandishi watapaswakuwajibika kwa
kujitolea ikiwa ni pamoja na kuhamasika kuacha kuandika habari kwa mazoea
na bafala yake wajikite katika kuandika habari zenye maslahi za kueleza wajibu
wa serikali kwa umma na umma kwa serikali yao.
Hata hivyo alisema fani ya uandishi habari inapaswa kujikita katika maadili ya
uandishi bora kwa kuzingatia vigezo weledi na si vinginevyo kwani hii
itasaidia ukuwaji wa fani hiyo hapa nchini na kuondokana na uandishi wa
kimazoea katika kutekeleza majukumu ya wanahabari ya kila siku.
Monday, April 30, 2018
BAGAMOYO YAZINDUA CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga akiandaa sindano kwaajili ya uzinduzi wa chanjo ya Saratani ya Mlango wa kizazi kwa wasichana wenye umri wa miaka 14.
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga akizungumza kabla ya kuzindua chanjo ya Saratani ya Mlango wa kizazi kwa wasichana wenye umri wa miaka 14.
.......................................
Mkuu
wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga amesema mtu atakaekwamisha zoezi la chanjo
ya Saratani ya shingo ya Kizazi atachukuliwa hatua za kisheria.
Mkuu
huyo wa wilaya ametoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti katika Halmashauri za
Bagamoyo na Chalinze wakati wa uzinduzi wa chanjo ya Saratani ya mlango wa
kizazi.
Alisema
serikali inapanga mikakti ya kuboresha Afya za wananchi wake ili waweze
kutumikia taifa pamoja na kuihudumia wenyewe na familia zao.
Aliongeza
kuwa, Bagamoyo ina mikakati ya kukuza uchumi kwa kujenga viwanda hivyo ni wazi
kuwa wanaotakiwa kufanya kazi katika viwanda hivyo ni watu wenye afya nzuri isoyokuwa
na mgogoro.
Serikali
kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imekuwa ikitoa chanjo za magonjwa
mbalimbali lengo likiwa ni kuhakikisha afya za wananchi zinakuwa salama.
Katika
hatua nyingine mkuu huyo wa wilaya ameigiza Halmashauri ya Chalinze kuangalia
madeni ya madaktari na kuwalipa ili kuwaondolea manung'uniko ambayo yanaweza
kuzorotesha utendaji kazi wao.
Alisema yapo malalamiko kwa madaktari ambao hawalipwi fedha za kuitwa kazini kwa matukio ya dharula nje ya muda wa kazi (On-call Allowance) ambayo ni haki yao kimsingi.
Ameitaka Halmshauri ya Chalinze kufanya haraka kuwalipa madaktari On-call Allowance ili waweze kuwa na moyo wa kufanya kazi muda wowote wanapohitajika.
Alisema Serikali imetenga bajeti kubwa katika wizara ya Afya ili kuboresha huduma za afya hivyo Halmashauri nazo zinapaswa kuongeza bajeti zake katika sekta ya afya ili kuwajengea mazingira rafiki madaktari na watumishi wa afya kwa ujumla.
Alisema yapo malalamiko kwa madaktari ambao hawalipwi fedha za kuitwa kazini kwa matukio ya dharula nje ya muda wa kazi (On-call Allowance) ambayo ni haki yao kimsingi.
Ameitaka Halmshauri ya Chalinze kufanya haraka kuwalipa madaktari On-call Allowance ili waweze kuwa na moyo wa kufanya kazi muda wowote wanapohitajika.
Alisema Serikali imetenga bajeti kubwa katika wizara ya Afya ili kuboresha huduma za afya hivyo Halmashauri nazo zinapaswa kuongeza bajeti zake katika sekta ya afya ili kuwajengea mazingira rafiki madaktari na watumishi wa afya kwa ujumla.
Aidha,
alimtaka Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Chalinze Dkt. Rahim Hangai kuchukua hatua za dhati
kuhakikisha zahanati ambazo hazina madaktari anapeleka madaktari ili kuwasogezea
wananchi huduma za afya ambazo kwa sasa wanatembea umbali mrefu licha ya kuwepo
zahanati kwenye maeneo yao.
Awali
wakichangia mada katika semina elekezi iliyofanyika shule ya Kikaro Halmashauri
ya Chalinze washiriki wa semina hiyo walisema wananchi wanakabiliwa na
changamoto ya kufuata huduma za afya mbali na maeneo yao hali inayopelekea kushindwa kuwapatia
watoto wao chanjo.
Walisema vipo baadhi ya vijiji mwananchi analazimika kutumia shilingi elfu nane ili kumpeleka mtoto akapate chanjo.
Walisema vipo baadhi ya vijiji mwananchi analazimika kutumia shilingi elfu nane ili kumpeleka mtoto akapate chanjo.
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Chalinze Dkt. Rahim Hangai alisema atahakikisha anayafanyia
kazi maelekezo ya Mkuu wa wilaya ili kukidhi mahitaji ya wananchi katika maeneo
ambayo tayari kuna Zahanati lakini hakuna Daktari.
Alisema
tatizo la upungufu wa madaktari katika Halmashauri hiyo limetokana na watumishi
walioondolewa kutokana na kuwa na vyeti feki hivyo idara ya afya katika
Halmashauri hiyo ni miongoni mwa wathirika ambapo mpaka sasa wanasubiri
watumishi wengine watakaopangiwa na wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa. (TAMISEMI) ili kuziba mapengo hayo.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa Halmashuri ya Chalinze Saidi Zikatimu alisema
ataiongoza Halmashauri hiyo katika kuhakikisha inatekeleza majukumu yake kwa
watumishi ili nao wafanye kazi kwa moyo na bidii.
Alisema ni kweli serikali imetenga fedha kwaajili kuboresha sekta ya afya ambapo Halmashauri ya Chalinze imepoke zaidi ya shilingi milioni 440 kwaajili ya kuboresha huduma katika vituo vya afya na Zahanati na milioni 400 kwaajili ya kituo cha afya ambapo ujenzi wake unaendelea.
Alisema ni kweli serikali imetenga fedha kwaajili kuboresha sekta ya afya ambapo Halmashauri ya Chalinze imepoke zaidi ya shilingi milioni 440 kwaajili ya kuboresha huduma katika vituo vya afya na Zahanati na milioni 400 kwaajili ya kituo cha afya ambapo ujenzi wake unaendelea.
Chanjo
ya Saratani ya mlango wa kizazi imezinduliwa rasmi hii leo jumatatu ya tarehe
30 Aprili katika Halmashauri za Bagamoyo na Chalinze ambapo walengwa ni
wasichana wenye umri wa miaka 14.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga akivaa koti la udaktari ikiwa ni maandalizi ya kuzindua chanjo ya Saratani ya Mlango wa kizazi kwa wasichana wenye umri wa miaka 14.


Watumishi
wa halmashuri ya Chalinze wakifutilia kinachoendelea kwenye semina elekezi
kuhusu chnjo ya mlango wa kizazi kwa wasichana iliyofanyika shule ya Kikaro
kata ya Miono.
Mwenyekiti wa Halmashuri ya Chalinze Saidi Zikatimu akizungumza katika semina hiyo.


Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Chalinze Dkt. Rahim Hangai akitoa maelekezo kwa washiriki.



Washiriki
wa semina hiyo wakifuatilia maelezo yanayotolewa.
Muwezeshaji
akitoa semina kwa washiriki.


Mkuu
wa wilaya ya Bagamoyo Alhaj, Majid Mwanga akiwa na viongozi wa dini katika
picha ya pamoja.
Mkuu
wa wilaya ya Bagamoyo Alhaj, Majid Mwanga akiwa na maafisa tarafa pamoa na viongozi wengine waandamizi katika
picha ya pamoja.
WATATU WAFA NA 530 WAKUTWA NA DALILI ZA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI PWANI

Mganga mkuu wa Mkoa wa Pwani
,Yudas Ndungile akitoa chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi kwa mmoja
wa wanafunzi, wakati wa uzinduzi wa zoezi ya chanjo hiyo kwa watoto wenye umri
wa miaka 14 ,kimkoa yaliyofanyika kituo cha afya mkoani,Kibaha.
..........................
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
JUMLA ya akinamama 20,815 waliofanyiwa uchunguzi wa
saratani ya mlango wa shingo ya kizazi mkoani Pwani katika kipindi cha miaka
mitatu kati yao
530 walikutwa na dalili za awali za saratani hiyo,ambapo watatu walifariki.
Aidha kati ya akinamama hao waliofanyiwa uchunguzi
akinamama 412 walitibiwa matibabu na 115 walipata rufaa ya kwenda
Oceanroad na hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Akitoa takwimu hizo ,wakati wa uzinduzi wa zoezi la
chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa shingo ya kizazi kwa watoto wenye umri
wa miaka 14 ,kimkoa yaliyofanyika kituo cha afya mkoani,Kibaha,mganga mkuu wa
Mkoa wa Pwani ,Yudas Ndungile alisema , ipo changamoto ya kutojua idadi ya vifo
kamili kwa kuwa wengi hupata rufaa.
Pamoja na hayo ,alisema ipo haja ya kuona ukubwa wa
tatizo hilo kwa
kuangalia afya mapema na watoto wa mashuleni kupata chanjo.
Ndungile alisema jumla ya watoto wa kike 18,823
waliopo shule na nje ya shule mkoani hapo watapatiwa chanjo ya kukinga saratani
ya mlango wa kizazi mwaka huu.
Alielezea, tayari wameshapokea chanjo na wataanza
kuzitoa katika vituo mbalimbali vya huduma.
Ndungile aliitoa shaka jamii kuwa chanjo ya kukinga
saratani ya mlango wa kizazi ni salama ,haina madhara na haiathiri uwezo wa
binti kupata watoto hapo baadae
” Serikali imethibitisha usalama wa umadhubuti wa
chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi ndiyo maana imeiongeza kwenye
mpango wa Taifa wa chanjo ili iweze kusaidia kudhibiti tatizo hilo kwa akinamama”:!
Ndungile alieleza mwaka 2018 chanjo itatolewa kwa
wasichana waliofikisha umri wa miaka 14 na ili kupata kinga kamili walengwa
watahitaji kupatiwa dozi mbili.
Alisisitiza chanjo hiyo huwakinga wasichana wasipate
saratani ya mlango wa kizazi pindi wawapo watu wazima wakiwa na familia zao.
“Nchini Tanzania saratani ya mlango wa
kizazi ni ya kwanza kwa vifo ikifuatiwa na saratani ya matiti ” Saratani hizi
mbili kwa pamoja husababisha zaidi ya asilimia 50 ya vifo vyote vya wakinamama
vitokanavyo na saratani”alibainisha Ndungile.
Kwa upande wake ,Mganga mkuu wa halmashauri ya Mji
wa Kibaha ,Dkt.Tulitweni Mwinuka alisema ,wamezindua chanjo hiyo kwa wasichana
wenye umri wa miaka 14.
Alielezea ,kiwilaya wamezindua chanjo hiyo kwa
wasichana 100 kituoni hapo na wanatarajia kufanikisha na kuleta matokeo
kutokana na chanjo hiyo .
Akizindua zoezi hilo ,kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa
Pwani,mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama aliwataka wanafunzi wa kike
kuacha kujiiingiza kwenye vitendo vya ngono mapema ili kujiepusha kuingia
kwenye hatari ya kupata magonjwa ya zinaa,ukimwi na hata saratani ya mlango wa
kizazi.
Alisema moja ya sababu zinazosababisha saratani hiyo
ni kuwa na wanaume wengi ,kuvuta sigara ,wenye mitala, na kuanza mapema kufanya
ngono.
“Acheni kujiingiza kwenye mapenzi mapema ni hatari
katika maisha yenu, ukivua sketi ,na mwanaume akavua suruali jua kuna hatari ya
kuhatarisha maisha yako kwa magonjwa yanayosababishwa kutokana na ngono”
“Jizuieni hadi hapo mtakapoolewa ,msikimbilie ngono
za haraka,mtapata saratani”: alisisitiza Mshama.
Mshama aliwahimiza wazazi na walezi kuwapeleka
watoto wao wa kike wenye umri wa miaka 14 kupata chanjo hiyo kwani haina
madhara.
Subscribe to:
Comments (Atom)