Wednesday, March 21, 2018

SERIKALI YATENGA BILIONI TANO KUNUNUA MASHINE YA KUPIMA VIPIMO VYA TB.


Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na baadhi ya wadau wa Sekta ya afya hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa dawa ya kutibu kifua kikuu kwa watoto wadogo kueleka maadhimisho ya siku ya Kifua Kikuu tarehe 24 Machi 2019.
...................................

NA WAMJW-DAR ES SALAAM.

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imetenga shilingi bilioni 5 kwa ajili ya kununua mashine za kupima vipimo vya ugonjwa wa kifua kikuu katika zahanati na vituo vya afya nchini. 

Hayo yamezungumzwa jijini Dar es salaam na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa dawa za kutibu ugonjwa wa Kifua Kikuu kwa watoto kuanzia umri wa miaka 14 kushuka chini.

“Serikali imadhamiria kupambana na ugonjwa wa Kifua Kikuu hivyo tumetenga shilingi bilioni 5 kwa ajili ya kuongeza mashine nyingine za kufanya uchunguzi kwa haraka ugonjwa wa Kifua Kikuu zinazoitwa Genexpert ” alisema Waziri Ummy. 

Aidha Waziri Ummy alisema kuwa marufuku kwa watoa huduma kutoa matibabu ya Kifua Kikuu kwa gharama yoyote kwani huduma hiyo ni bure. 

Kwa mujibu wa Waziri Ummy alisema kuwa marufuku kwa waganga wa kienyeji kuwashikilia wagonjwa wa Kifua kikuu na badala yake wawaruhusu waende hospitali kwa ajili ya msaada wa haraka. 

Aidha, Waziri Ummy alisema kuwa takribani  watu laki moja na 60 wana maambukizi ya ugonjwa wa kifua kikuu kwa makadirio ya mwaka 2016. 
Sambamba na uzinduzi wa dawa hizo Waziri Ummy amegawa mashine nyingne za Genexpert kwa ajili ya kufanyia uchunguzi wa makohozi ili kugundua kuna maambukizi au hapana kwa hospitali za  ,Kairuki, Agakhan,  Regency , TMJ na Indumandal ambazo kila mashine moja inagharimu shilingi milioni 34 .

Aidha Waziri Ummy ametoa rai kwa wazazi na walezi wa watoto kwenda hospitali mara wanapoona dalili moja wapo ya TB ikiwemo kuumwa mara kwa mara kwa muda wa wiki mbili, kukosa furaha, mtoto kulia mara kwa mara, kupungua uzito , kuchelewa kukua na kikohozi cha mara kwa mara. 
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akimuangalia mtoto Salome katikati akinywa dawa ya Kifua Kikuu wakati wa uzinduzi wa dawa ya kutibu kifua Kikuu kwa watoto wadogo leo jijini Dar es salaam, kutoka kulia ni Mratibu wa Kupambana na Magonjwa ya Kifua Kikuu na Ukoma Dkt. Beatrice  Mutayoba, anayefuata aliyevaa kitenge ni mzazi wa Salome Bi. Upendo Jeremiah.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akionyesha dawa kutibu Kifua Kikuu kwa watoto wadogo wakati wa uzinduzi wa dawa hiyo leo jijini Dar es salaam kueleka maadhimisho ya siku ya Kifua Kikuu tarehe 24 Machi 2018.
Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Bakari Kambi baadhi ya wadau wa Sekta ya afya hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa dawa ya kutibu kifua kikuu kwa watoto wadogo kueleka maadhimisho ya siku ya Kifua Kikuu tarehe 24 Machi 2018.
Baadhi ya wadau wa Sekta ya afya wakifuatilia kwa makini Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu hayupo pichani wakati wa uzinduzi wa dawa ya kutibu kifua kikuu kwa watoto wadogo kueleka maadhimisho ya siku ya Kifua Kikuu tarehe 24 Machi 2018.

MAGAZETI YA LEO TAREHE 21 MACHI 2018.

Tuesday, March 20, 2018

MAKAMU WA RAIS ATEMBELEA HOSPITALI YA ABDALLA MZEE PEMBA.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimjulia hali mtoto Rayna Abdala mwenye umri wa mwaka mmoja aliyelazwa kutokana na kuungua moto katika hospitali ya Abdala Mzee, mkoa wa Kusini Pemba.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimjulia hali mtoto Hafidh Jabir Ali mwenye umri wa miaka 3 aliyelazwa kutokana na kuungua na chai katika hospitali ya Abdala Mzee, mkoa wa Kusini Pemba.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Dkt. Wuxiao Shu juu ya matibabu ya mguu wa mtoto AzarAli mwenye umri wa miaka aliyelazwa  katika hospitali ya Abdala Mzee, mkoa wa Kusini Pemba.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi nje ya majengo ya hospitali ya Abdala Mzee, mkoa wa Kusini Pemba mara baada ya kukagua maendeleo ya hospitali hiyo. 

Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais

MSITU WA ZIGUA SASA UMEREJEA KATIKA HALI YAKE YA KAWAIDA.


Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mh. Alhaj, Majid Hemedi Mwanga akionyesha sehemu ya makazi ya watu waliokuwa wamevamia msitu wa Zigua hivi karibuni katika Doria maalu ya kukagua msitu huo iliyowashirikisha watendaji kutoka TFS wilaya ya Bagamoyo na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ambapo kwa pamoja wamejiridhisha kwamba hakuna mvamizi aliykuwemo ndani ya msitu huo kwa sasa.
........................................

Hifadhi ya msitu wa zigua imerejea katika hali yake ya kawaida baada ya kuwaondoa wavamizi ndani ya msitu huo.

Akizungumza na bagamoyokwanza blog amara bada ya kufanya doria maalum katika msitu huo, Kaimu Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu nchini (TFS) Halmashauri ya Chalinze David George Ntemi, alisema hali ya msitu huo kwa sasa inaridhisha kutokana na miti kushamiri na baadhi ya wanyama kuonekana kurejea ndani ya msitu huo ambao awali walianza kutoweka.

Alisema  hifadhi hiyo ya msitu wa Zigua, ulikuwa umeharibiwa na wananchi ambao walivamia kwa kufanya shughuli za kibinadamu ikiwemo kulima, kukata miti na kuchungia mifugo hali iliyopelekea msitu kuharibika asili yake na wanyama kukimbia.

Aliongeza kwa kusema kuwa, mara baada ya kuwatoa wavamizi katika zoezi lililoshirikisha wilaya tatu za Bagamoyo, Handeni na Kilindi kwa sasa Hifadhi ya msitu wa Zigua kwa upande wa Bagamoyo uko vizuri baada ya kujihakikishia kuwa hakuna mtu hata mmoja ndani ya msitu huo kwa sasa.

Alisema Doria hiyo maalum imefanywa katika kipindi hiki ambacho tayari wakulima huandaa mashamba kwaajili kilimo cha mwaka hivyo lengo lilikuwa ni kujiridhisha endapo wakulima hao wamerudi au wameondoka moja kwa moja.

Aidha, alisema baada ya kuzunguuka eneo lote wapo watu wawili ambao waliozidisha mipaka yao na kuingilia sehemu ya msitu na kwamba tayari wameshapewa taarifa ya kuacha kupanda sehemu ya msitu ili kuepuka kuharibiwa mazao yao.

Akizungumzia umuhimu wa msitu huo Ntemi alisema msitu huo ni mapitio ya wanyama kutoka hifadhi ya taifa ya Saadani na kuelekea Mikumi.

Ntemi aliongeza kuwa, msitu huo pia ni chanzo cha maji cha mito ya saja na kigulu inayopeleka maji katika mto wami ambao unahudumia miji ya Chalinze na Bgamoyo.

Alisema msitu huo pia ni sehemu ya kuzalia wanyama ambapo kuharibika kwa msitu huo kutapelekea wanya hao kutoweka na hivyo kupoteza rasilimali za taifa.

Ntemi alisema kutunzwa kwa msitu huo kunapelekea kupatikana kwa mvua kwa wakati ambapo ukiharibiwa ni sababbu ya kutoweka kwa mvua hali itakayosababisha ukame katika ukanda huo.

Nae aliyekuwa akiongoza vikosi katika kuwatoa wavamizi Mkuu wa polisi wilaya ya Kipolisi Chalinze Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Janeth Magomi aliwataka wananchi wanaozunguuka msitu huo kutii sheria bila ya shuruti ili kuepuka usumbufu ambao wanaweza kuupata pindi wanapokaidi sheria.

Alisema viongozi wa Mkoa na wilaya kupitia mikutano mbalimbali na wananchi walishatoa maelekezo namna ya kuulinda msitu huo hivyo kila mwananchi akazingatia maelekezo ya viongozi na kuacha kuvunja sheria kwa makusudi.

Alisema kwa sasa hali ya msitu huo tulivu kwakuwa tayari wananchi wanaonekana kutii sheria bila ya shuruti.

Wananchi wa kata ya Kibindu waliozungumza na bagamoyokwanza blog walisema faida walizopata katika kuhamishwa kutoka kwenye msitu ni pamoa na kupata huduma za Afya, Barabara na Elimu.

Walisema katika maeneo ya msitu ilikuwa vigumu watoto kwenda shule na matibabu pale mtu anapoumwa lakini kwa sasa wanapata huduma zote kwa urahisi kwakuwa wapo katika makazi ya watu.
 Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mh. Alhaj, Majid Hemedi Mwanga akiwa na watendaji kutoka TFS wilaya ya Bagamoyo wakitabasamu baada ya kuona hali ya msitu wa mzigua imeanza kuridhisha.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya ya Bagamoyo, ambae ni Mkuu wa Wilaya ya hiyo Mh. Alhaj, Majid Hemedi Mwanga (aliyeshika fimbo) akiongoza Doria maalum ya kukagua msitu wa Zigua.

 Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mh. Alhaj, Majid Hemedi Mwanga (kushoto) akifurahia jambo na wanakijiji waliotolewa ndani ya msitu wa Zigua kata ya Kibindu hivi karibuni wakati wa Doria maalum ya kukagua Msitu huo.

VIJANA 20 WAOZESHWA SIKU MOJA MOROGORO.


Taasisi ya The Islamic Foundation kwa kushirikiana na Taasisi ya Sharjah Charity International katika falme za kiarabu UAE pamoja na Mabwana harusi 20 wamefanikiwa kwa pamoja kukamilisha zoezi la ibada ya ndoa ya kiihistoria nchini Tanzania kwa vijana wa kislamu 20.

Ndoa hiyo imefanyika katika makao makuu ya #Taasisi ya the Islamic foundation mjini Morogoro na kuhudhuriwa na watu mbalimbali kutoka katika mkoa wa Morogoro na maeneo ya jirani huku taasisi ya TIF ikiweza kuratibu shughuli hiyo na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Akizungumza katika Ndoa hiyo ya kihistoria mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya barabara na usafirishaji Dubai UAE Dkt. Yusuph Mohamed Abdalla Hassan AL-ALI ambaye ndiye mgeni Rasmi katika ibada hiyo ya ndoa amewataka vijana kuoa kwa kufuata mafundisho ya Mtume Mohammad (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aaalihi Wa Sallam)

Naye Mwenyekiti wa Taasisi ya The Islamic Foundation Aref Nahdi amesema kuwa TIF itaendelea kusimamia na kudhamini vijana mbalimbali wa kiislamu ili kuweza kufikia malengo yao ya kutekeleza ibada ya ndoa.

Hata hivyo MAMLAKA ya barabara na usafirishaji Dubai RTA Dubai UAE imeikikabidhi kituo cha yatima cha Darul Imaan kinachomilikiwa na taasisi ya The Islamic Foundation Basi la Abiria aina ya Ashok Leyland lenye uwezo wa kubeba abiria 50.

Hayo yamebainishwa na mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya barabara na usafirishaji Dubai UAE Dakta Yusuph Mohamed Abdalla Hassan AL-ALI katika ziara yake kwa taasisi ya the Islamic foundation mkoani Morogoro na kusema kuwa mamlaka hiyo imeikabidhi kituo hicho ili kuweza kurahisisha huduma za usafiri kwa watoto ya tima wanaolelewa na TIF.

Aidha mamlaka hiyo imekabidhi mabegi 200 kwa watatoto yatima wanaolelewa katika kituo cha taasisi ya the Islamic foundation cha Darul Imaan na kusema kuwa mabegi hayo yatawasaidia watoto hao kwa kiasi kikubwa.

Katika hatua nyingine mamlaka ya barabara na usafirishaji Dubai UAE imetoa baiskeli 25 kwa watoto hao yatima.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa taasisi ya the Islamic foundation Aref Nahdi ameishukuru mamlaka hiyo kwa kuona umuhimu wa kuisaidia tif katika kitengo cha Yatima na kusema kuwa tif imefarijika na msaada huo.
Mwenyekiti wa Taasisi ya The Islamic Foundation Aref Nahdi akizungumza wakati wa hfla hiyo ya kuwaozesha vijana 20 wa kiislamu mjini Morogoro.

Mkurugenzi Mtendaji wa mamlaka ya barabara na usafirishaji nchini Dubai UAE, Dakta Yusuph Mohamed Abdalla Hassan AL-ALI akizungumza katika hafla hiyo ya kuwaozesha vijana 20 wa kiislamu iliyofanyika Mjini Morogoro nchini Tanzania.

Katibu Mkuu wa Taasisi ya The Islamic Foundation, Sheikh Ibrahim Twaha (kulia) na Mkurugenzi wa vyombo vya Habari vya Imaan, Ahmed Bawaziri (kushoto) wakiwaongoza vijana 20 wa kiislamu katika zoezi la kuwafungisha ndoa wote kwa siku moja zoezi ambalo limesimamiwa na Taasisi ya 
The Islamic Foundation kwa kushirikiana na Taasisi ya Sharjah Charity International kutoka falme za kiarabu UAE. 
Upande wa chakula mambo yalikuwa hivi.
Sehemu ya umati wa watu waliofika kushuhudia ndoa hiyo ya kihistoria hapa nchini.