Saturday, July 15, 2017

DC. BAGAMOYO AZINDUA MAZINGIRA CUP MWANAKALENGE.

Katikati ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga, akijiandaa kuingia uwanjani hii leo Julai 15, 2017 kuchezesha mechi kati ya Madiwani wa Wialya ya Bagamoyo na wakuu wa idara ikiwa ni uzinduzi wa kombe la Mazingira  litakalojumuisha timu 28 ikiwa ni 26 kutoka kata zote za Wilaya ya Bagamoyo na 2 ni makundi maalum, pembeni yake ni washika vibendera ambao kulia ni Mkuu wa Polisi wilaya ya kipolisi Bagamoyo, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP- Adam Maro, kushoto ni Mkuu wa Gereza la Kigongoni, Mrakibu wa Magereza, SP-Muyengi Bulilo, wakipena maelekezo kabla ya kuanza kwa mechi ufunguzi katika Uwanja wa Mwanakalenge mjini Bagamoyo.
  
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga,wa pili kulia, ambae ndiye aliyekuwa mwamuzi wa pambano la mechi kati ya Madiwani na Wakuu wa idara, akitoa maelekezo kwa washika vibendera wake, kulia ni Mkuu wa Polisi wilaya ya kipolisi Bagamoyo, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP- Adam Maro, kushoto ni Mkuu wa Gereza la Kigongoni, Mrakibu wa Magereza, SP-Muyengi Bulilo, wakipena maelekezo kabla ya kuanza kwa mechi ufunguzi katika Uwanja wa Mwanakalenge mjini Bagamoyo.
 
Timu ya Madiwani wa Halmashauri ya Chalinze na Bagamoyo wakiwa  tayari kuingia uwanjani kupambana na wakuu wa idara za halmashauri za Chalinze na Bagamoyo katika mechi ya ufunguzi uwnja wa Mwanankalenge hii leo tarehe 15 julai 2017.
 
Timu ya wakuu wa idara za Halmashauri ya Chalinze na Bagamoyo wakiwa  tayari kuingia uwanjani kupambana na madiwani wa Halmashauri za Chalinze na Bagamoyo katika mechi ya ufunguzi uwnja wa Mwanankalenge hii leo tarehe 15 julai 2017.
Mshika kibendera katika mchezo huo, Mkuu wa Polisi wilaya ya kipolisi Bagamoyo Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP- Adam Maro,akiendelea na majukumu yake katika uwanja wa Mwanakalenge Bagamoyo mjini.

 Mshambuliaji wa timu ya wakuu wa idara akijaribu kuwatoka madiwani katika mechi ya ufunguzi iliyochezwa leo Tarehe 15 Julai 2017 katika uwanja wa Mwanakalenge ambapo katika mechi hiyo wakuu wa idara walitok na ushindi wa mabao 2 -1 dhidi ya madiwani.
 Mwamuzi wa Mechi ya ufunguzi kati ya Madiwani na Wakuu wa idara, ambae ni mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga (aliyeshika mpira) akitoa timu uwanjani baada ya kumalizika ambapo Wakuu wa idara walitoka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Madiwani.
 
Watizamaji wakifuatilia mchuano katika uwanja wa Mwanakalenge mjini Bagamoyo.
Katikati ni Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Happyness William Seneda wakifurahia jambo na Mwenyeji wake kushoto,  Mkuu wa Wilya ya Bagamoyo, Majid Mwanga, katika uwanja wa Mwanakalenge Bagamoyo mjini,  kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo, Fatuma Omari Latu.

MAKAMU WA RAIS AMJULIA HALI MTOTO WA KIKWETE MUHIMBILI.

salm2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  amemjulia hali mtoto wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Khalfan Kikwete ambaye amelazwa katika wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam. ( Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 salm1

BODI MPYA TaSUBa YATAMBULISHWA NA WAZIRI MWAKYEMBE.

Pix 1
Waziri wa Habari Sanaa Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akimkabidhi Mwenyekiti mpya  wa Bodi ya Ushauri ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa)  Bw. George Daniel Yambesi (kulia)  alipoitambulisha rasmi bodi  hiyo jana Jijini Dar es Salaam.
 Pix 2
Wajumbe wakimsikiliza Waziri wa Habari Sanaa Utamaduni na Michezo Mhe.Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo katika picha) jana Jijini Dar es Salaam alipokuwa akiwatambulisha wajumbe wapya wa  bodi ya ushauri waTaasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).
Pix 3
Wajumbe wakimsikiliza Waziri wa Habari Sanaa Utamaduni na Michezo Mhe.Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo katika picha) jana Jijini Dar es Salaam alipokuwa akiwatambulisha wajumbe wapya wa  bodi ya ushauri waTaasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).
 Pix 4
Waziri wa Habari Sanaa Utamaduni na Michezo Mhe.Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wapya wa wa  bodi ya ushauri waTaasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa). (Picha na Lorietha Laurence-WHUSM).