Friday, December 2, 2016

DC BAGAMOYO AMPA SIKU MOJA OCD CHALINZE KUMUHAMISHA MKUU WAKITUO CHA WAMI KWA KUTOSHUGHULIKIA MATATIZO YA WAFUGAJI NA WAKULIMA.

Mkuu  wa wilaya ya Bagamoyo, Majid  Mwanga  amempa siku moja kamanda wa polisi wilaya ya  Kipolisi Chalinze SSP Janeth Magomi, kumuondoa mkuu wa kituo cha  polisi cha Wami kufuatia tuhuma za  kuwapendelea wafugaji na kuwanyanyasa  wakulima na  kupelekea  kushindwa kuwachukulia hatua wafugaji wanaoingiza mifugo yao kwenye mashamba ya wakulima.

Agiza hilo  amelitoa kwenye  Mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha  Mandela kata ya Mandela ambapo awali wananchi  walipata nafasi ya kutoa  malalamiko yao  mbele ya mkuu wa wilaya na kufanya kero  kubwa iliyotawala katika mkutano huo ni kuhusu wafugaji  kuingiza mifugo  kwenye  mazao ya  wakulima na kwamba polisi waliopo kituo cha  polisi Wami wameshindwa kuwasimamia ili kudhibiti hali hiyo.
Akizungumza mbele ya  mkuu  wa wilaya mzee mmoja  alisema aliwahi kufika kituo cha    PolisiWami kutoa Taarifa ya kuliwa mazao yake,  lakini hatua  waliyochukua  Polisi ni  kumwambia huyo mzee akatafute mgambo ili  amkamate mfugaji aliyeingiza mifugo kwenye shamba  lake jambo  limemsikitisha mzee huyo.

Aidha, wananchi mbalimbali walizungumza  katika mkutano huo, wamelalamikia kitendo cha wafugajikuwa na uwezo wa kuharibu mazao ya wakulima bila ya kuchukuliwahatua yoyote.

Kero hizo za wafugaji kwa wakulima ni pamoja na mifugo kula mazao  ya wakulima na hata wanapotakiwa kutoa fidia ya mazao hayo  wamekuwa hawatimizi  kwa kile kinachodaiwa kulindwa na  Polisi, mkuu wa wilaya   anachukua jukumu  la kuomba namba za simu za wafugaji wanaodaiwa na wakulima na kuwapigia simu ili walipe fidia za wakulima.
Mkuu wa Polisi wilaya ya Kipolisi Chalinze. Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP Janeth Magomi akimsikiliza  mkuu  wa wilaya wakati wa mkutano  uliofanyika  kijiji cha Mandela  kata ya Mandela Halmashauri ya Chalinze,  kulia ni mkuu  wa kituo cha Polisi  Wami ambae mkuu  wa wilaya ameagiza ahamishwe.
Wazee wa Kijiji cha  Mandela  wakipiga makofi mara baada ya  mkuu  wa wilaya kutoamaamuzi ya kuhamishwa kwa mkuu wa kituo cha  polisi Wami.
Wananchi wa kijiji cha Mandela wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga alipofanya mkutano wa hadhara na kusikiliza kero mbalimbali za wananchi  wa  kata ya Mandela, Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo.

Wednesday, November 30, 2016

MAADHIMISHO YA SIKU YA WALEMAVU KITAIFA YAFUTWA

index
Maadhimisho ya siku ya watu wenye ulemavu duniani, ambayo kitaifa yalitarajiwa kufanyika jijini Dar es salaam,Desemba 3, mwaka huu yameahirishwa na badala yake kila mkoa utaadhimisha kivyake.

Akitoa tamko la kuharishwa kwa maadhimisho hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), George Simbachawene amesema maadhimisho hayo yalilenga kila halmashauri isafirishe wanachama wa vyama vya watu wenye ulemavu ili washiriki maadhimisho hayo jijini humo.

Amesema kwa mujibu wa maelekezo aliyopewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa wakuu wa mikoa kuwa badala ya maadhimisho hayo ya kitaifa kukusanya walemavu wote kwenye mikoa kwenda Dar es salaam yafanyike kwenye mikoa yao.

Tuesday, November 29, 2016

HALMASHAURI ZAONGOZA KWA RUSHWA ZIKIFUATIWA NA POLISI.

mlowolapicha
 Halmashauri nyingi hapa nchini zinaongoza kwa kupokea rushwa kubwa kubwa huku jeshi la polisi likiongoza kwa kupokea rushwa ndogo ndogo suala ambalo limepelekea mapambano dhidi ya rushwa kuwa magumu.

Hayo yameelezwa jana na Mkurugenzi wa Takukuru Valentino Mlowola wakati wa mkutano wa mkuu mwaka wa siku 2 wa Shirikisho la mamlaka za kuzuia na kupambana na rushwa nchi za Afrika Mashariki(EAAACA) unaofanyika jijini Arusha ambapo unawashiriki kutoka mataifa 8 barani Afrika.

Mlowola alisema kuwa Hadi sasa katika kipindi cha mwaka mmoja wa wameweza kuokoa zaidi ya billion 45 za miradi mbalimbali zilizokuwa ziangukie mikononi mwa watu wachache ambapo aliitaka jamii kutoa ushirikiano dhidi ya mapambano ya kuzuia rushwa.

Alisema kuwa miradi mingi inayopitia katika halmashauri nyingi hapa nchini imekuwa ikigubikwa na rushwa na kuifanya miradi hiyo kujengwa chini ya viwango hali inayopelekea matumizi mabaya ya fedha za umma.

Aidha katika jeshi la Polisi alitanabaisha kuwa kumekuwa na ongezeko la kuomba na kupokea rushwa ndogo kutoka kwa jamii hali inayosababisha wananchi kukosa imani na kupelekea malalamiko kwa jeshi hilo.

“Waandishi wa habari iwapo mtaona mradi wowote hauendi kwa viwango vilivyokusudiwa mtoe taarifa kwani hivi sasa tuna maofisa wetu katika kila wilaya ambao wataweza kufanya uchunguzi na kubaini mianya ya rushwa”alisema Mlowola.

Kwa upande wake waziri wa nchi ofisi ya Raisi Utumishi na Utawala Bora  Angela Kairuki alisema kuwa serikali imeanzisha mahakama ya mafisadi ambapo kesi kadhaa zimeanza kusikilizwa hali itakayopelekeakupunguza kuomba na kupokea rushwa hapa nchini.

Alisema kuwa kesi nyingi zimepelekwa katika mahakama hiyo na siku si nyingi mafanikio ya vita dhidi ya ubadhirifu wa mali za umma utapungua kama sio kwisha kabisa

Waziri huyo alitoa wito kwa taasisi mbalimbali za serikali kushirikiana na sekta binafsi katika kuhakikisha mapambano dhidi ya rushwa katika nchi za ukanda wa afrika mashariki zinakoma.

ASKARI POLISI AFARIKI DUNIA KIBAHA KWA KUJIPIGA RISASI BILA YA KUKUSUDIA.

Askari  Polisi  mwenye namba H.3348 PC  Armand  Evarist  Furaha mwenye umri wa miaka 33 amefariki dunia baada ya kujipiga risasi kwa bahati mbaya.

Taarifa iliyotolewa na  Kaimu kamanda wa  Polisi  Mkoa wa  Pwani, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP- Blasius Chatanda imesema tukio hilo  limetokea Tarehe 22 Novemba 2016 majira ya saa moja usiku katika eneo  la maili moja sokoni, kata ya maili moja Tarafa ya Kibaha Wilaya ya Kibaha  mkoani  Pwani.

Kaimu Kamanda Chatanda alisema Marehemu alikuwa amepangiwa lindo kwa mkuu wa wilaya ya Kibaha ambapo baada ya kushuka  kwenye Gari  Bunduki ilfyatuka  na  kumjeruhi na  kwamba alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya rufaa ya Tumbi.

SSP Chatanda alisema marehemu alikuwa mbele katika Gari namba PT 1732  lililokuwa likiendeshwa na Askari mwenye namba F. 3064 CPL Grayson na kutaja Bunduki aliyokuwa nayo marehemu aina ya SMG ambayo ilimpiga kifuani upande wa kushoto.