Thursday, July 28, 2016

MBUNGE WA CHALINE APOKEA MADAWATI YENYE THAMANI MILIONI 80, KUTOKA SAYONA FRUIT YA SHUBASHI PATELI.




Halmashauri ya Chalinze mkoani pwani, imepokea Madawati ya  Sekondari yenye thamani ya shilingi milioni 80, kutoka kwa  Kampuni ya Sayona Fruit chini ya mkurugenzi wake Shubashi Pateli.

Akipokea msaada huo wa meza na viti, Mbunge  wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete,  alimshukuru Mkurugenzi wa Kampuni ya Sayona Furt Shubashi Pateli kwa kusaidia madawati hayo ambayo yatagaiwa katika shule tano na kwamba baada ya hapo hakutakuwa na upungufu wa madawati katika Halmashauri ya Chalinze.

Aidha, aliwatakawadau mbalimbali katika Halmashauri ya Chalinze kuunga mkono Mkakati wa Rais Magufuli wa kuhakikisha kila mtoto wa kitanzania anapata elimu bure na kwamba ili kuonesha kumuunga mkono Rais kila mdau  anapaswa kuchangia maendeleoya shule ikiwa ni pamoja na ujenzi wa vyumba vya kusoimea.

Alisema kwa sasa Halmashauri  Ya Chalinze tayari imekamilisha madawati na kwamba haina upungufu wa  madawati ispokuwa ni uhaba wa vyumba vya madarasa.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo, Mkurugenzi msaidizi wa kampuniya  Sayona Fruit, Aboubakari  Mlawa, amesema mbali na msaada  huo kampuni yake imepanga kutoa  madawati ya  shule zamsingi yapatayo  1200 yenye thamani ya milioni 90, kwa Halmashauri ya  Chalinze na Bagamoyo.

Nae  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chalinze Edes  Lukoa, amesema kufuatia msaada  huo Halmashauri ya Chalinze imekamilisha utengenezaji wa madawati na kwamba  kilichobaki kuyasambaza  kwenye  shule zenye mahitaji hayo.


Mbunge wa jimbo la Chalinze, Ridhiwani  Kikwete, akizungumza wakati wa kupokea madawati hayo katika shule ya sekondari Lugoba, nyuma yake ni mkurugenzi  msaidizi wa Sayona Fruit Abouubakari Mlawa, anaefuata mwenye suti rangi ya udongo ni mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze, Saidi Zikatimu, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa mtendaji wa Halmashauri  ya Chalinze, Edes Lukoa, wa  pili kulia ni makamo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze,
Waliokaa  kwenye Dawati kushoto ni Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete, kulia ni Mkurugenzi msadizi wa kampuni ya Sayona Fruit bwana Aboubakari Mlawa wakijaribu kukalia moja kati ya madawati yaliyotelewa, waliosimama kutoka kushoto ni Mkuu wa shule ya Sekondari ya  Lugoba, Abdallaah  Sakasa, wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze, Saidi Zikatimu, aliyesimama kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chalinze, Edes Lukoa.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya  Chalinze Saidi Zikatimu, (katikati) akifurahia jambo pamoja na makamo mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kulia, kushoto ni mkuu wa shuleya sekondari ya  Lugoba  wakati  wa kupokea  madawati yaliyotolewa na Sayona  Fruit.

Mkuu wa shule ya sekondari  Lugoba  Abdallaah Sakasa kushoto akimkabidhi kiloba cha Chooko Mkurugenzi msaidizi ikiwa ni zawadi  kwa mkurugenzi mkuu wa kampuni ya Sayona Group, Shubash Pateli ambae hakuwepo wakati  wa tukio.
Baadhi  ya madawati yaliyotolewa

Tuesday, July 26, 2016

SERIKALI YATENGA BILIONI 1.6 KUANZISHA MFUMO WA KIELETRONIKI WA KUSAJILI MAKAZI.



Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – TAMISEMI Injinia Mussa Iyombe akiongea na wanahabari wakati wa kupokea maendeleo ya mfumo wa kuboresha upatikanaji wa taarifa sahihi katika serikali za mitaa, hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam.
 

Diwani wa Kata ya Mapinga Wilaya ya Bagamoyo Ibrahimu Mbonde akiongea jambo wakati wa kupokea maendeleo ya mfumo wa kuboresha upatikanaji wa taarifa sahihi katika serikali za mitaa, hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam.
 

Kamishna wa Sensa ya Watu na Mkazi Hajjat Amina Mrisho Said akiongea jambo wakati wa kupokea maendeleo ya mfumo wa kuboresha upatikanaji wa taarifa sahihi katika serikali za mitaa, hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam.




Serikali imetenga Jumla ya shilingi bilioni 1.6 kupitia ofisi ya Taifa ya Takwimu huku wafadhili wakitoa shilingi bilioni 1.4 kwa ajili ya uanzishwaji wa mfumo wa kieletroniki wa kusajili wakazi Tanzania .

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- TAMISEMI Injinia Mussa Iyombe wakati wa kupokea maendeleo ya mfumo wa kuboresha upatikanaji wa taarifa sahihi katika serikali za mitaa.

Injinia Iyombe alisema mfumo huo unalenga kuwa na kanzi data ya watu wote nchini kiumri, uraia, jinsia, hali ya ulemavu, hali ya elimu, shughuli za kiuchumi, uhamaji na uhamiaji ikiwa ni pamoja ikiwa na vizazi na vifo.

“Taarifa hizi zitaisaidia serikali na wadau wengine kujibu maswali ambayo wengine tumekuwa tukijiuliza kila siku”.Alsema Injini Iyombe. 

Alisema katika kutekeleza malengo Endelevu ya Maendeleo ya Mwaka 2030 serikali haina budi kuhakikisha wananchi wanaandikishwa katika rejesta ya wakazi ili iweze kuwafahamu mahitaji yake.

Aliongezea kuwa mfumo huo utasaidia upatikanaji wa idadi kamili ya wanafunzi waliopo mashuleni na kiasi gani cha fedha kinachotitajika kupelekwa shuleni, upatikanaji wa hali halisi ya uandikishaji wa watoto katika shule za msingi, mahudhurio shuleni na idadi ya walimu na taarifa nyingine.

Alisema kwa upande wa TAMISEMI mfumo huo utasaidia kuwagundua wazazi ambao hawana nia nzuri ya kuwapeleka watoto kuandikishwa kupitia katika kata zao kwa kutumia Global Positioning System za kaya zao katika ramani.

Akielezea faida za mfumo huo Injinia Iyombe alisema utaiwezesha serikali kufahamu idadi kamili ya watu wake kiumri na kijinsia kwa kuwa kazi hiyo itakuwa endelevu na itafanyiwa kazi kila siku na maafisa watendaji wa vijiji na mitaa kwa Tanzania nzima kwa kutumia teknolojia ya simu.

Aidha mfumo huo utaipa fursa Ofisi ya Takwimu ya kuwa na takwimu bora ambazo zitaipunguzia gharama ya kufanya tafiti za kila baada ya miaka mitatu, mitano hata kumi ikiwa ni pamoja na kupunguza maswali mengi ambayo huulizwa wakati wa sensa wa watu na makazi ambayo itafanyika tena hapa nchini mwaka 2022.