Tuesday, February 22, 2022

MILIONI 600 KUJENGA SEKONDARI MAKURUNGE BAGAMOYO.

 No description available. 

Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Bagamoyo, Aloisi Damian Kaziyareli, (kushoto) na Mtendaji kata Makurunge, Chumi Joel (kulia) wakishiriki katika zoezi la kuchimba msingi kwaajili ya ujenzzi wa shule mpya ya Sekondari inayojengwa kitongoji cha Gezaulole kata ya Mkurunge, Halmashauri ya Bagamoyo, fedha hizo za ujenzi zimetolewa na Rais Samia Suluhu Hassan katika mpango wa kuhakikisha hakuna mtoto aneshindwa kwenda kidato cha kwanza kwa kukosa shule.

...................................

Na Athumani Shomari, Bagamoyo.

Wanachi wa kata ya Makurunge Halmashauri ya Bagamoyo wamejitokeza kuchimba msingi kwaajili ya ujenzi wa shule mpya ya sekondari inayojengwa kwa fedha zilizotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan.

 

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo, Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Bagamoyo, Aloisi Damian Kaziyareli, amesema ujenzi wa shule hiyo mpya utasaidia kuondoa adha kwa wanafunzi wanaoishi kata ya Makurunge ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakitembea umbali wa kilomita zaidi ya kumi kufuata shule ya sekondari.

 

Ameongeza kuwa, kata hiyo ya Makurunge haikuwahi kuwa na shule ya Sekondari na kwamba ametumia nafasi hiyo kumshukuru Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kutenga milioni mia sita kwaajili ya ujenzi wa shule hiyo ya sekondari.

 

Amesema tayari milioni 470 zimeshaingizwa kwaajili ya kazi hiyo ambapo zitatumika kujenga jengo la utawala, vyumba vya madarasa nane, Maabara za sayansi tatu, Maktaba, Vyoo pamoja na nyumba za walimu huku milioni 130 iliyobaki itatolewa baadae.

 

Afisa elimu huyo amesema kutokana na mpangilio wa majengo hayo, mara tu baada ya kukamilika ujenzi wa shule hiyo itakuwa imejitosheleza na kwamba itakuwa na ubora wa unaotakiwa kwaajili watoto kupata elimu.

 

Aidha, ametoa wito kwa wazazi kujipanga kusomesha watoto katika shule hiyo ambayo januari 2023 itapokea watoto wa kuanza kidato cha kwanza.

 

Nae Diwani wa kata ya Makurunge, Hamisi Mohamed, amesema wananchi wa kata hiyo wamefurahishwa sana na ujenzi wa shule ya sekondaari katika kata  hiyo na wapo tayari kutoa ushirikiaano wao pindi watakapohitajika kufanya hivyo.

 

Amesema ili kuthibisha kuwa wananchi hao wamefurahishwa na ujenzi huo, wamejitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa ujenzi huo katika haatua ya awali ya kuchimba msingi wa madarasa.

 

Kwa upande wake Mtendaji kata Makurunge Chumi Joel amesema amefanikiwa kuunganisha nguvu za wananchi wa kata yote kupitia wenyeviti wa vitongoji ndani ya kata hiyo ambapo kila mwenyekiti wa kitongoji amfika na wananchi wake na kushiriki kazi kikamilifu.

 

 Aidha, amewataka wananchi wa kata hiyo kuwa tayari kujitolea katika kazi za maendeleo ili kufanikisha malengo yao ndani ya kata.

 

 Nao wazazi wa kata ya Makurunge wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuwatengea fedha hizo za ujenzi wa shule ya sekondari ili watoto wao sasa wapate kusoma shule iliyo karibu nao.

No description available.No description available.

Wahandisi kutoka idara ya ujenzi Halmashauri ya Bagamoyo wakihakiki vipimo vilivyopo kwenye michoro katika zoezi la uchimbaji msingi wa shule mpya ya sekondari inayojengwa katika Kitongoji cha Geza ulole Kata ya Makurunge.

No description available.No description available.

Wananchi wa kata ya Makurunge Halmashauri ya Bagamoyo, wakishiriki zoezi la uchimbaji msingi katika ujenzi wa shule mpya ya sekondari inayojengwa katika Kitongoji cha Geza ulole kata ya Makurunge.

No description available.No description available.

Wananchi wa kata ya Makurunge Halmashauri ya Bagamoyo, wakishiriki zoezi la uchimbaji msingi katika ujenzi wa shule mpya ya sekondari inayojengwa katika Kitongoji cha Geza ulole kata ya Makurunge.

No description available.No description available.

Mtendaji kata Makurunge, Chumi Joel akishirikiana na Wananchi wa kata hiyo iliyopo Halmashauri ya Bagamoyo, katika zoezi la uchimbaji msingi wa ujenzi wa shule mpya ya sekondari inayojengwa katika Kitongoji cha Geza ulole kata ya Makurunge.

No description available.No description available.

Mtendaji kata Makurunge, Chumi Joel akishirikiana na Wananchi wa kata hiyo iliyopo Halmashauri ya Bagamoyo, katika zoezi la uchimbaji msingi wa ujenzi wa shule mpya ya sekondari inayojengwa katika Kitongoji cha Geza ulole kata ya Makurunge.

No description available.

Wananchi wa kata ya Makurunge Halmashauri ya Bagamoyo, wakiwa na nyuso za furaha wakati wa wakishiriki zoezi la uchimbaji msingi katika ujenzi wa shule mpya ya sekondari inayojengwa katika Kitongoji cha Geza ulole kata ya Makurunge. 

VITAMBULISHO VYA WAJASIRIAMALI MILIONI 1.6 VIMETOLEWA NCHINI.

 No description available.

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Zainab Chaula,akizungumza wakati akifungua  kikao na  viongozi wa  Shirikisho la Umoja wa Wamachinga nchini na viongozi wa Wamachinga  kutoka Mikoa 26 nchini kilichofanyika leo Februari 22,2022 jijini Dodoma.

....................................

Na.Alex Sonna, DODOMA

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk. Zainabu Chaula amesema mpaka sasa vitambulisho vya wajasiriamali milioni  1.6 vimetolewa nchini  kati ya vitambulisho  milioni 3.7.

Pia amesema mikakati iliyopo kwa sasa ni jinsi ya kuwapatia vitambulisho vyao  wajasiriamali milioni  2.1 waliobaki.

Hayo ameyasema leo Februari 22,2022 Jijini Dodoma wakati akifungua  kikao na  viongozi wa  Shirikisho la Umoja wa Wamachinga nchini na viongozi wa Wamachinga  kutoka Mikoa 26 nchini, Dk. Chaula amesema kuwa Januari 25 mwaka huu Rais Samia Suluhu Hassan alikutana na viongozi wa  Wamachinga Mkoa wa Dar es salaam ambapo alipokea changamoto na mafanikio wanayokutana nayo.

Amesema kupitia kikao hicho Rais Samia  aliagiza kwamba wamachinga   ni kundi maalum na sasa liwe chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.

Amesema  taarifa aliyonayo ni kuwa  mpaka sasa vimetolewa vitambulisho milioni  1.6 vya wajasiriamali  kati ya vitambulisho  milioni 3.7 huku  mikakati iliyopo kwa sasa ni jinsi ya kuwapatia vitambulisho vyao  wajasiriamali milioni  2.1 waliobaki.

“Lakini taarifa niliyonayo  tunawamachinga milioni  3.7 sasa tunataka hawa waliobaki  milioni 2.1 tunawapaje vitambulisho sasa ndio maana tunatembea na wenzetu wa TAMISEMI watuambie mchakato unaendaje.Kitambulisho ni jambo jema hata sisi ofisini tuna vitambulisho kwahiyo kitambulisho kinakutambua wewe ni nani na upo wapi lile tutaliboresha,”amesema.

Kuhusiana na kuwatambua wamachinga amesema : “Uzuri mifumo  ya Serikali ni endelevu kwahiyo  suala la kutambuliwa sio kwamba walikuwa hawatambuliwi,walitambuliwa na walipata usaidizi wote unaostahili isipokuwa kwa sababu imeanzishwa Wizara mpya yenye mambo mahsusi”

Amesema mgawanyo wa shilingi bilioni 5 zilizotolewa na Rais Samia suala hilo Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) linaendelea kulishughulikia

“Ule mgawanyo uliishatolewa kwa ajili ya kuonesha miundombinu na mchakato unaendelea nina imani tukimaliza haya tutajua tunatokaje Tamisemi wataendelea na uratibu,”amesema.

Kwa upande wake,Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,Amon Mpanju amesema lengo la kikao hicho cha siku mbili  ni kulipokea hilo kundi kutoka Tamisemi walikokuwa wakiwahudumiwa mara baada ya Rais kuagiza liwe chini ya Wizara hiyo.

Amesema ndani ya siku mbili watapitishwa katika masuala ya uongozi,taratibu za kiuongozi na namna wanavyoweza kujiongoza kuanzia katika masoko mpaka Taifa,mifumo na mbinu mbalimbali za mawasiliano,pamoja na sheria,taratibu na kanuni za kuongoza umoja wao.

Naye,Mwenyekiti wa Jumuiya ya Machinga nchini Ernest Matondo, amesema kuwa  wanakabiliwa na changamoto ya miundombinu katika masoko kutokuwa rafiki ambapo ameomba fedha walizopewa zaidi ya shilingi bilioni 5 ziende kukarabati miundombinu hiyo ili waweze kufanya biashara katika mazingira mazuri.

“Nimpongeze Mheshimniwa Rais kwa kulitambua kundi hili maalum na kutupatia Wizara hili ni jambo la kumshukuru sana Mheshimiwa Rais,”amesema.

No description available.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Amon Mpanju, akitoa salamu wakati wa kikao na  viongozi wa  Shirikisho la Umoja wa Wamachinga nchini na viongozi wa Wamachinga  kutoka Mikoa 26 nchini kilichofanyika leo Februari 22,2022 jijini Dodoma.

No description available.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Onesmo Lyanga,akizungumza wakati wa kikao na  viongozi wa  Shirikisho la Umoja wa Wamachinga nchini na viongozi wa Wamachinga  kutoka Mikoa 26 nchini pamoja na Wizara  ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum kilichofanyika leo Februari 22,2022 jijini Dodoma.

No description available.

Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara ya ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Patrick Golwike,akizungumza wakati wa kikao na  viongozi wa  Shirikisho la Umoja wa Wamachinga nchini na viongozi wa Wamachinga  kutoka Mikoa 26 nchini kilichofanyika leo Februari 22,2022 jijini Dodoma.

No description available.No description available.

Washiriki wa kikao wakifatilia hotuba ya Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Zainab Chaula (hayupo pichani) wakati wa kikao na  viongozi wa  Shirikisho la Umoja wa Wamachinga nchini na viongozi wa Wamachinga  kutoka Mikoa 26 nchini kilichofanyika leo Februari 22,2022 jijini Dodoma.

No description available.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Machinga nchini Ernest Matondo,akitoa neno la shukrani kwa Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Zainab Chaula (hayupo pichani) mara baada ya kufungua  kikao na  viongozi wa  Shirikisho la Umoja wa Wamachinga nchini na viongozi wa Wamachinga  kutoka Mikoa 26 nchini kilichofanyika leo Februari 22,2022 jijini Dodoma.

No description available.

No description available.

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Zainab Chaula akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua kikao na  viongozi wa  Shirikisho la Umoja wa Wamachinga nchini na viongozi wa Wamachinga  kutoka Mikoa 26 nchini kilichofanyika leo Februari 22,2022 jijini Dodoma.