Saturday, October 14, 2023
Friday, October 13, 2023
Thursday, October 12, 2023
HAKUNA HUDUMA YA UMEME WALA MAJI GAZA.
Waziri wa Nishati wa Israel, Israel Katz anasema Israeli haitaacha kuizingira Gaza hadi mateka wa Israel waachiliwe.
Katika chapisho la mitandao ya kijami Katz alisema hakuna "swichi ya umeme itawashwa, hakuna bomba la maji litakalofunguliwa na hakuna lori la mafuta litakaloingia" hadi "mateka" wawe huru.
Israel ilisimamisha usambazaji wa bidhaa kwa Ukanda wa Gaza baada ya mashambulizi ya Hamas siku ya Jumamosi.
BBC SWAHILI
Wednesday, October 11, 2023
KIKWETE AMPONGEZA BITEKO, KERO ZA UMEME KUSHUGHULIKIWA HARAKA.
Chalinze imetekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020- 2025 kwa mafanikiopp
Chalinze - Pwani
Serikali imeahidi kushughulikia changamoto ya umeme iliyopo nchini kwa kasi kubwa ili tatizo hilo liweze kuisha katika kipindi kifupi kuanzia sasa.
Hayo yameelezwa leo Oktoba 11, 2023 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko katika Mkutano Mkuu Maalum wa Jimbo la Chalinze wa kupokea taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2020-2025) wilaya ya Chalinze mkoa wa Pwani.
Dkt. Biteko amesema kuwa, katika kipindi cha miezi sita inayokuja ukosefu wa umeme nchini utaisha baada ya Serikali kuweka mikakati madhubuti ya kumaliza tatizo hilo nchini. Amesema Watendaji wanafanya kazi ili watanzania wapate umeme wa kutosha.
Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko ameiagiza TANESCO kupeleka umeme katika shule ya Sekondari ya Moreto ili shule hiyo iunganishwe na umeme mapema. Aidha amechangia kompyuta 10 kwenye shule hiyo maalum kwa matumizi ya TEHAMA kuwasaidia wanafunzi.
Kuhusu Halmashauri ya wilaya ya Chalinze Dkt. Biteko ametumia nafasi hiyo kupongeza juhudi zinazofanywa katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kijamii ikiwemo ujenzi wa madarasa, zahanati na miundombinu muhimu na pia kufanya vizuri katika makusanyo ya mwaka ambapo wilaya hiyo imekusanya shilingi bilioni 15.
Kwa upande wake, Rais wa Awamu ya Nne Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anatoa msukumo mkubwa kwenye maendeleo ya nchi yetu na fedha hizo zinaelekezwa katika miradi mbalimbali ili kukuza uchumi wa nchi.
Vile vile, Mhe. Dkt. Kikwete amempongeza Mhe. Dkt. Biteko kwa kuteuliwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati hapa nchini na kumsisitiza awe msaada mkubwa katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya Serikali na kufanya kazi kwa bidii.
Akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa mkoa wa Pwani unaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa shule, madaraja, vituo vya afya ili mkoa huo ukue kiuchumi na hatimaye kuboresha maisha ya wananchi wake.
Aidha, Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema, katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa Rais Dkt. Samia, halmashauri ya wilaya ya Chalinze imefanikiwa kutekeleza kwa kiwango kikubwa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020/25.
"Wananchi wamewezeshwa kiuchumi, hali ya uzalishaji katika Kilimo, uvuvi, umwagiliaji, viwanda na biashara imeongezeka, miundombinu ya shule, zahanati, vituo vya afya na hospitali ya wilaya imekamilika kwa asilimia kubwa na kwenye baadhi ya vijiji na kata ujenzi unaendelea," amesema Mhe. Ridhiwani.
Naye, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Halima Okash amesema, katika uongozi wa miaka wa Rais Samia wameshuhudia mabadiliko makubwa kimaendeleo ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze. Amesema Mbunge anaonesha ushirikiano
Wilaya ya Bagamoyo ni miongoni mwa wilaya Saba zinazounda mkoa wa Pwani. Wilaya hiyo ina halmashauri Kuu mbili ambazo ni Halmashauri ya wilaya ya Chalinze na Halmashauri ya Bagamoyo.
Mkutano huo umehudhuriwa na Viongozi Mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wanachama zaidi ya 1000 walioshiriki katika uwasilishwaji wa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi CCM 2020/25
Saturday, October 7, 2023
WAWEKEZAJI WAKARIBISHA SOKO LA UTALII NCHINI
Na Andrew Chale, Dar es Salaam.
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki amesema Serikali ya Tanzania inafanya maboresho makubwa kwenye miundombinu sekta ya utalii na amewakaribisha wawekezaji kutoka sehemu mbalimbali duniani kuja kuwekeza nchini kwa kuwa Tanzania imejaaliwa kuwa na maliasili za kipekee, vivutio vya kitamaduni na maeneo marefu ya fukwe za Tanzania Bara na Zanzibar.
Mhe. Kairuki ametoa kauli hiyo katika siku ya pili ya Maonesho ya Saba ya Swahili International Tourism Expo – S!TE, 2023 leo Oktoba 7,2023 wakati akifungua Jukwaa la Uwekezaji jijini Dar es Salaam linalojulikana kama “Uwekezaji Endelevu kwa Maendeleo Jumuishi ya Kijamii na Kiuchumi”.
Mhe. Kairuki amesema pamoja na kazi kubwa ya kuboresha miundombinu iliyofanywa na kusaidia kuleta watalii pia amefafanua kuwa ongezeko kubwa la watalii limetokana na kazi nzuri iliyofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia filamu ya “The Royal Tour”. Filamu hii ilionyeshwa katika vituo vingi vya televisheni vinavyotambulika nchini Marekani na kwingineko duniani ili kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania.
Amesema The Royal Tour na juhudi nyingine za masoko umesababisha kuongezeka kwa idadi ya watalii waliofika kutoka nje ya nchi imeongezeka kutoka watalii 922,692 mwaka 2021 hadi watalii 1,454,920 mwaka 2022, sawa na ongezeko la asilimia 57.7. Aidha, idadi ya watalii wa ndani imeongezeka kutoka watalii 788,933 mwaka 2021 hadi 2,363,260 mwaka 2022, sawa na ongezeko la asilimia 199.5.
Aidha amesema utalii umeendelea kuwa msingi wa ukuaji wa uchumi wa nchi ambapo amefafanua kuwa sekta, inachangia hadi 17.2% ya jumla ya Pato la Taifa na 25% ya mapato yote ya mauzo ya nje ambapo amesema kuna sekta inaweza kuchangia zaidi kwenye uchumi zaidi pia baada ya kupatikana kwa bidhaa mpya za utalii kama utalii wa mikutano na utalii wa meli ambazo kwa sasa Serikali inafanya kazi.
Akitoa mada kwenye Jukwaa la Uwekezaji Naibu Kamishna wa Uhifadhi kutoka Hifadhi ya Ngorongoro Imani Richard Nkuwi amefafanua kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii na Menejimenti ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), imepokea andiko la mradi (project proposal) unaotambulika kama “Development of Water Front and Cruising Ship Terminal” kutoka kwa Mkandarasi tarajiwa. Mradi husika unatarajiwa kugharimu takribani kiasi cha USD 300 milioni na utahusisha ujenzi wa gati la mizigo ya mwambao na ujenzi wa gati la meli za kitalii pamoja na uendelezaji wa ufukwe wa Bahari ya Hindi jirani na gati la meli za kitalii. Ujenzi wa miundombinu husika unategemewa kuanza kabla ya mwaka wa fedha 2023/24.
Mhe. Waziri amezitaja baadhi ya juhudi zinazochukuliwa na Serikali katika kuboresha miundombinu kuwa ni pamoja na Reli ya Standard Gauge (SGR) ambayo iko katika hatua za mwisho kukamilika inalenga kuunganisha Jiji la Dar es Salaam kama lango kuu la watalii wanaofika njia ya kati na Kusini, kuimarisha Shirika la Ndege la Taifa kwa kuongeza idadi ya safari za ndege ili kuimarisha utalii kuunganishwa kwa kanda mbalimbali za kitalii za Tanzania.
Pia ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal 3 na ukarabati wa Viwanja vya Ndege vya Mikoani.

































































