Wednesday, February 15, 2023

KAMATI YA UELIMISHAJI JAMII YATAMBULISHWA BAGAMOYO.

 No description available.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo, Shauri Selenda, akizungumza wakati wa kuwatambulisha wajumbe wa Kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji jamii, kuhusu magonjwa ya mlipuko uliofanyika leo Februari 15, 2023.  katika Ukumbi wa Chuo cha unesi Bagamoyo.

No description available. 

Afisa Mipango wa huduma za Afya ngazi ya Jamii kutoka Wizara ya afya, Bahati Mwailafu, akizungumza na washiriki wakati wa Mkutano wa kuwatambulisha wajumbe wa Kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji jamii, kuhusu magonjwa ya mlipuko uliofanyika leo Februari 15, 2023. katika Ukumbi wa Chuo cha unesi Bagamoyo.

No description available.  

Washiriki wa Mkutano wa kuwatambulisha wajumbe wa Kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji jamii, kuhusu magonjwa ya mlipuko uliofanyika leo Februari 15, 2023. katika Ukumbi wa Chuo cha unesi Bagamoyo.

No description available. 

Mratibu wa Elimu ya Afya kwa uma wilaya ya Bagamoyo, Jeni Mcharo, akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi mara baada ya kumalizika kwa   Mkutano wa kuwatambulisha wajumbe wa Kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji jamii, kuhusu magonjwa ya mlipuko uliofanyika leo Februari 15, 2023. katika Ukumbi wa Chuo cha unesi Bagamoyo.

No description available. 

No description available. 

Washiriki wa Mkutano wa kuwatambulisha wajumbe wa Kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji jamii, kuhusu magonjwa ya mlipuko uliofanyika leo Februari 15, 2023. katika Ukumbi wa Chuo cha unesi Bagamoyo. 

........................................................................

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo, Shauri Selenda, amesema mafanikio ya utekelezaji wa Mipango na mikakati mbalimbali ya serikali inatokana na jamaii kuelewa, kuhamasika na kushirikishwa katika utekelezaji wa mikakati hiyo.

Mkurugenzi huyo wa Halmashauri ya Bagamoyo, ameyasema hayo wakati wa kufunga Mkutano wa kuwatambulisha wajumbe wa Kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji jamii, kuhusu magonjwa ya mlipuko uliofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha unesi Bagamoyo.

Alisema jamii inahitaji kupata elimu juu ya jambo husika ili waweze kushiriki kikamilifu katka mambo mbalimbali yanayoandaliwa na serikali na kwa kutambua hilo serikali imeweza kuandaa namna ya kuwashirikisha, kuwaelimisha na kuwahamasisha kupitia kamati hiyo.

Ameitaka Kamati hiyo itakapopata elimu juu ya kile wanachotakiwa kwenda kukifanya wakafanye kwa utaalamu waa hali ya juu kwa kuwafikia makundi mbalimbaali katika jamii.

Aliwakumbusha kuwa, kazi yao kubwa ni kwenda akutoa elimu, kuhamasisha na kuwashirikisha kuhusu magonjwa ya mlipuko ili kila mmoja awe na uelewa ulio sahihi hali itakayosaidia kwa serikali kutotumia nguvu katika kuhamasisha chanjo zaa magonjwa ya mlipuko.

Kwa upande wake Afisa Mipango wa huduma za Afya ngazi ya Jamii kutoka Wizara ya afya, Bahati Mwailafu,  amesema kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji jamii, imeundwa ili kukabiliana na magonjwa ya mlipuko ambapo wananchi wanapaswa kupata elimu sahihi kuhusu magonjwa hayo ili waweze kujilinda na kujitibu.

Alisema lengo la mkutano huo ni kutambulisha kamati ambayo itashiriki katika kutoa elimu, kuhamasisha, na kushirikisha jamii ili waweze kuelewa madhara ya magonjwa ya mlipuko.

Nae Mratibu wa Elimu ya Afya kwa uma wilaya ya Bagamoyo, Jeni Mcharo amesema wanatarajia kupata mafanikio katika Kamati hiyo iliyotambulishwa kwakuwa imeshirikisha makundi mbalimbali ya kijamii.

Alisema mara kadhaa serikali inapotaka jambo la kijamii liwafikie wananchi hutumia makundi mbalimbali ya kijamii ili kurahisisha ufikishaji wa taarifa kutokana na kamati husika kukubalika katika jamii kwani miongoni mwao wapo viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwemo wa viongozi wa dini, serikali na asasi za kiraia.

Aliongeza kwa kusema kuwa, mafanikio katika kutoa elimu kuhusu magonjwa ya mlipuko ni jambo kwakuwa tutakuwa tumemsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambae amekuwa akihakikisha wananchi wake wanakuwa salama dhidi ya magonjwa mbalimbali.

Alisema Rais Samia ni mpenda maendeleo hivyo anapenda wananchi wake wawe na afya njema ili waweze kushiriki katika kujiletea maendeleo wenyewe na taifa kwa ujumla.

Aidha, amewashukuru Wizara ya Afya kitengo cha Elimu ya afya kwa uma kwa kuona umuhimu wa jambo hilo na kuchagua mkoa wa Pwani kuwa miongoni mwa mikoa inayostahili kupata kamati hiyo ili kuweza kupambana na magonjwa ya mlipuko.

Mkutano huo wa kutambulisha wajumbe wa Kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji jamii, umeandaliwaa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI na Shirika la Afya duniani W.H.O. 

 

KERO YA UPUNGUFU WA MAJI NA KUKATIKAKATIKA KWA UMEME,YAWACHOMA MADIWANI KIBAHA MJINI

 No description available.

Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha

Upungufu wa Maji na kukatikakatika kwa Nishati ya Umeme ,imekuwa gumzo na kilio kwa Madiwani wa Kibaha Mjini katika baraza la madiwani ,na kudai ni kero ya muda mrefu iliyo na ukakasi kwenye ufumbuzi wake.

Agustino Mdachi diwani wa Kata ya Pangani na Mohamedi Chamba diwani wa kata ya Viziwaziwa walisema kero ya Maji na Nishati ya Umeme imekuwa kero kubwa kwa wananchi hali inayoathiri utendaji kazi ,;muda mrefu wanatumia kutafuta Maji sanjali na kukatika  Umeme kukiathiri uzalishaji mali kwa wajasiliamali.

Hoja hiyo imekuwa msumali wa moto baada ya kuungwa mkono na Madiwani wote na kuziaguza taasisi husika kushughulikia huduma hizo .

Awali akiwasilisha hoja ya ziara ya Madiwani wa Viti maalum,Katibu wa Kamati hiyo Shufaa Mshana alisema ziara yao imebaini  vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia,Kero za miundombinu ya Barabara na Mikopo ya asilimia 10 ikishindwa kurudishwa kwa wakati na vikundi nufaika ambapo takribani kiasi cha Shilingi Bilioni moja kipo mikononi mwa wakopaji.

Vilevile madiwani wamekuwa wachungu kwa wakala wa Barabara nchini TANROAD kutokana na ucheleweshaji wa fidia kwa wananchi wanapofanya utekelezaji wa ujenzi wa Barabara.

Kitengo cha kujenga Barabara kwa muda mrefu ilielezwa kuwa hakiwafurahishi Madiwani  hao kutokana na kuwa kero kwa wananchi wanapotekelezaji shughuli zao za Wananchi.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha ,Selina Wilson alisema wananchi wameoneshwa kutofurahishwa na kitendo hicho kwani wanahitaji Maendeleo.

Nae Diwani wa Kata ya Visiga Kambi Legeza alishauri matengenezo ya Barabara ya zamani ya Morogoro ipewe kipaumbele cha matengenezo kwani imekuwa mbadala kwa Barabara ya Sasa inapokuwa na foleni.

 No description available.

 

WAZIRI DKT.KIJAJI AWATAKA WAFANYABIASHARA KUENDELEA KUZINGATIA MISINGI YA USHINDANI

 No description available.

Waziri wa Uwekezaji,Viwanda na Biashara Dkt.Ashatu Kijaji akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo Februari 15,2023 katika Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Jijini Dar es Salaam kuhusu mwenendo wa bei za bidhaa muhimu nchini kwa mwezi Februari 2023.

No description available.

Waziri wa Uwekezaji,Viwanda na Biashara Dkt.Ashatu Kijaji akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 15,2023 katika Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Jijini Dar es Salaam kuhusu mwenendo wa bei za bidhaa muhimu nchini kwa mwezi Februari 2023.

 ............................................................................................

 

NA EMMANUELMBATILO, DAR ES SALAAM

Waziri wa Uwekezaji,Viwanda na Biashara Dkt.Ashatu Kijaji amewahimiza Wafanyabiashara nchini kuendelea kuzingatia misingi ya ushindani wa haki katika kufanya biashara ili kuunga mkono jitihada za Serikali za kukuza uchumi kwa manufaa ya Wananchi wote. 

 

Wito huo  ameutoa leo Februari 15,2023 katika Ofisi za Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) Jijini Dar es Salaam wakati  akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa bei za bidhaa muhimu nchini kwa mwezi Februari 2023.

Amesema kutokana na mabadiliko ya tabia nchi na athari zake kwenye kiasi cha mavuno ya mazao muhimu ya chakula kama mchele, mahindi, maharage na viazi mviringo, mahitaji ya bidhaa hizo kwenye nchi jirani yamekuwa makubwa kuliko uzalishaji hivyo, kuchangia kupanda kwa bei za bidhaa za vyakula nchini na nchi jirani.    

Aidha amesema Mfumuko wa bei nchini Tanzania ni wa kiwango cha chini zaidi ikilinganishwa na nchi jirani ambapo kwa Tanzania kiwango cha mfumuko wa bei ni asilimia 4.9 kwa mwezi Januari 2023 ikilinganishwa na asilimia 9.1 ya Kiwango cha mfumuko wa bei nchini Kenya , asilimia 10.4 nchini Uganda na asilimia 21.7 nchini Rwanda kwa mwezi Januari, 2023.

Dkt.Kijaji amesema Wizara inaendelea kuratibu ukusanyaji wa takwimu za bei za mazao na bidhaa muhimu kama vile vyakula na vifaa vya ujenzi kutoka kwenye masoko yaliyopo katika Mikoa yote ya Tanzania Bara kupitia Wakusanya Taarifa za Masoko (Market Monitors) na Maafisa Biashara wa Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa. 

“Takwimu hizi husaidia Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) katika ukokotoaji wa kiwango cha mfumuko wa bei kila mwezi na kuweza kufanya tathmini ya upatikanaji wa mazao na bidhaa mbalimbali nchini”.  Amesema 

 

Hata hivyo amesema mwenendo wa bei za bidhaa za vyakula kama  mahindi kwa mwezi Februari ni kati ya Shilingi 750 na 1,750 kwa kilo. Bei ya chini haijaonyesha mabadiliko wakati bei ya juu imepanda ikilinganishwa na bei ya mwezi Januari, 2023 ambayo ilikuwa kati ya Shilingi 750 na 1600 kwa kilo, na bei ya bidhaa ya Unga wa mahindi kwa mwezi Februari ni kati ya Shilingi 1,500 na 2,100 kwa kilo. Bei ya unga wa mahindi haijabadilika ikilinganishwa na bei ya mwezi Januari 2023. Bei ya chini ipo katika Mikoa ya Geita na Manyara na bei ya juu ipo katika Mikoa ya Kigoma na Mara.

Pamoja  na haayo amesema Serikali inaendelea kufuatilia na kufanya tathmini ya bei za bidhaa muhimu ili kulinda maslahi ya wadau wote ikiwa ni pamoja na wazalishaji, wafanyabiashara na watumiaji wa bidhaa husika.