Sunday, December 18, 2022

HAKUNA MAENDELEO WALA AMANI BILA YA UHURU WA HABARI.-NAPE.

 No description available.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Mnauye, amesema hakuna Maendeleo, hakuna amani na hakuna furaha katika jamii ikiwa hakuna uhuru wa habari katika jamii hiyo.

Waziri Nape amebainisha hayo wakati akifungua Kongamano la kwanza la Maendeleo ya Sekta ya Habari nchini lililofanyika ukumbi wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam ambalo limehudhuriwa na washiriki wasiopungua 1000 wa ndani na nje ya nchi.

Alisema uhuru wa habari ni muhimu katika maendeleo ya nchi kwani jamii inapaswa kupata habari za mambo mbalimbali ambazo serikali inatekeleza.

Alifafanua kuwa, ikiwa wananchi hawatapata habari ni wazi kuwa watakuwa hawaelewi mambo mengi yanayotekelezwa na serikali yao na hivyo kuwafanya kuwa na manung’uniko ambayo yataondoa furaha yao na kuwakosesha amani.

Aidha, Waziri Nape aliwapongeza wanahabari kwa kufanya kazi yao kwa weledi, juhudi na moyo wa kujituma kuhakikisha wananchi wanapata taarifa zilizo sahihi na kwa wakati.

Alisema serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan inathamini uhuru wa habari hali iliyopelekea Rais Dkt. Samia kuiagiza wizara ya habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, kuandaa mkutano mkubwa wa wanahabari ili kuangalia mambo mbalimbali yanahusu habari hapa nchini.

Waziri huyo wa habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, amesema kwa umuhimu huo, serikali imeandaa kongamano hilo ambalo lengo ni kujadili namna ya kuboresha sekta ya habari ambapo majadiliano yanatakiwa kutoka na maazimio yatakayotekelezwa.

Aliendelea kusema kuwa, uhuru wa habari unapaswa kulindwa na sheria na wala sio utashi wa mtu ili kuufanya uhuru wa habari uwe ni endelevu kwa kiongozi yeyote atakaekuwepo madarakani.

Aliwahakikishai wanahabari kuwa ifikapo januari 2023 muswada wa marekebisho ya sheria ya habari utawasilishwa bungeni ili kupitisha baadhi ya vingele vya sheria kwa lengo la kutoa uhuru wa habari.

No description available.

 

Saturday, December 17, 2022

BALILE ATAKA UHURU WA HABARI NCHINI ULINDWE KISHERIA

 No description available.

Deodatus Balile, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) amesema, licha ya kuwepo kwa uhuru wa habari nchini, ameomba uhuru huo ulindwe kisheria.

Akizungumza katika Kongamano la Kwanza la Maendeleo ya Sekta ya Habari 2022 leo tarehe 17 Desemba 2023 amesema, wadau wa habari nchini wanafurahia uhuru uliopo lakini haujalindwa kisheria.

“Wadau wa habari nchini wanafurahia uhuru wa habari uliopo nchini, tunaamini serikali italinda uhuru huu kisheria katika Mabadiliko ya Sheria ya Habari yajayo.

Kwenye mkutano huo Balile amesema, mapendekezo ya mabadiliko ya sheria ya habari yatafikishwa bungeni Januari 2022.

“Nimezungumza na Waziri Nape (Nape Nnauye, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari) kuhusu mjadala wa Sheria ya Huduma za Habari, amesema Januari (2022) mapendekezo yatafikishwa bungeni,” amesema.

Akizungumzia madeni ya vyombo vya habari katika serikali na taasisi zake, Balile amesema licha ya juhudi kufanywa, bado taasisi za serikali ikiwemo halmashauri hasijalipa madeni yao kwa vyombo vya habari.

“Mpaka mwishoni mwa mwaka jana, madeni ambayo vyombo vya habari vinadai kwa serikali na taasisi zake ni Tsh. 7 bilioni.

“Ukijumuisha na deni la Gazeti la Daily News la serikali (Tsh. 11 Bilioni), jumla ya deni ni Tsh. 18 Bilioni na zaidi,” amesema.

“Halmashauri wana roho ngumu, hawajalipa mpaka leo licha ya kuandikiwa barua na TAMISEMI. Tunaomba mheshimiwa waziri (Nape) liwekee mguu chini, utusaidie,” amesema Balile.

Katika mapendekezo ya mabadiliko ya sheria, miongoni mwa mapendekezo ya wadau wa habari, ni kuweka sheria itakayowalazimisha watangazaji kwenye vyombo vya habari kulipa fedha ndani ya miezi sita baada ya matangazo yao kuchapishwa.

Miongoni mwa adhabu iliyopendekezwa iwapo mtangazaji atashindwa kulipa, walau kifungo cha miezi Sita.

 No description available.

WADAU WA BIASHARA WATAKIWA KUJISAJILI UPYA OFISI YA MAKAMU WA RAIS

 No description available.

Serikali imetoa rai kwa wadau wa biashara ya kaboni wahuishe miradi yao na kujisajili upya kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais na Kituo cha Ufuatiliaji wa Kaboni kilichopo Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Morogoro ili iendane na matakwa ya Kanuni na Mwongozo wa Biashara ya Kaboni.    

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo Dkt. Jafo amesema hayo wakati akitoa taarifa ya uzingatiaji na utekelezaji wa Kanuni na Mwongozo wa Biashara ya Kaboni leo Desemba 16, 2022 jijini Dodoma.

 

Amebainisha kuwa uzingatiaji na utekelezaji wa kanuni na mwongozo huo utasaidia kuboresha usimamizi mzuri wa miradi ya biashara ya kaboni inayotekelezwa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika sekta zote. Hivyo, amesema utekelezaji wa biashara ya kaboni utachangia kupunguza gesijoto zinazosababisha ongezeko la joto duniani na hatimae kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi, kuchangia katika utunzaji endelevu ya mazingira na kuleta maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi.

 

Waziri Jafo amesisitiza kuwa uzingatiaji na utekelezaji wa Kanuni na Mwongozo wa Usimamizi wa Biashara ya Kaboni ni jukumu la wadau wote, ikiwemo Wawekezaji wa Kimataifa na wanaotoka ndani ya nchi, Wizara za Kisekta, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa.  

 

“Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazoathiriwa na athari za mabadiliko ya tabianchi na hali ya hewa isiyotabirika na hali hii inajidhihirisha kupitia matukio ya mvua zisizotabirika, ongezeko la joto, ukame na mafuriko.  

 

“Athari hizi za mabadiliko ya tabianchi zimeathiri sekta za kijamii na kiuchumi na maendeleo kama vile kilimo, utalii, nishati, maji, afya, mifugo na mifumo ikolojia ya bahari na ardhi, hivyo kuathiri ongezeko la pato la taifa.

 

Aidha, ukame wa muda mrefu na mafuriko yamechangia gharama kubwa za kiuchumi, kuathiri maendeleo na maisha ya jamii za vijijini na mijini,” alisema Dkt. Jafo.  

 

Aidha, amesema kanuni na mwongozo huo vimejikita katika kuimarisha mchango wa nchi katika jitihada za kupunguza uzalishaji wa gesijoto na hivyo kupunguza athari za mazingir