Wednesday, February 2, 2022

MBARONI KWA KUUZA JEZI BANDIA ZA YANGA

 No description available.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam ACP  Muliro Muliro akiwaonyesha waandishi wa habari jezi bandia za timu ya Yanga Afrika 1208 ambazo wamezibaini zinazotengenezwa na kusambazwa na kampuni ya GSM.

……………………

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam limewakamata watu 17 kwa tuhuma za kuuza jezi bandia za timu ya Yanga Afrika 1208 zinazotengenezwa na kusambazwa na kampuni ya GSM.

Kazi hiyo ilifanyika katika maeneo mbali mbali ya Jiji Dar es salaam,lakini pia kwa kushirikiana na baadhi ya mikoa nchini kwa kipindi cha kuanzia tarehe 02.01.2022 hadi tarehe 28.01.2022.

Katika Jiji la Dar es salaam Jeshi la Polisi limewakamata watuhumiwa watano, akiwemo Zahiri Hassan (17) Mmwera aliyekutwa huko Uwanja Benjamin William Mkapa akiwa na Jezi bandia za Timu ya Yanga 52, Kariakoo mtaa wa Agrey alikamatwa Majiba Ndahya (50) Msukuma akiwa na Jezi 124, Mohamed Ramadhani (26) Mchaga alikutwa na Jezi 86, John Staslaus (19) Mchaga alikamatwa na Jezi 39 Watuhumiwa hao waliwataja wenzao wa Zanzibar, ambapo Uwanja wa Amani watuhumiwa watatu walikutwa na Jezi bandia 36.

Jezi zingine bandia 134 zilipatikana kwa kushirikiana na Polisi Mkoa wa Tanga na Mwanza ambapo watuhumiwa tisa walikutwa na Jezi 811.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam linawatahadharishawananchi wote wanaojihusisha na vitendo vya kutengeneza, kuuza na kusambaza, bidhaa kwa kuiga au kufananisha nembo za biashara au huduma za watu wengine iliyosajiliwa kisheria, kufanya hivyo ni kosa nakinyume na sheria za nchi.

Jeshi la Polisi litashirikiana na mamlaka nyingine za kisheria ili kuona watuhumiwa wamechukuliwa hatua kali za kisheria

MULIRO J. MULIRO– ACP

KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM

DAR ES SALAM.

 

Saturday, December 11, 2021

SUBIRA MGALU AKABIDHI MATOFALI NIANJEMA NA MAPINGA

 No description available. 

MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa pwani, Subira Hamisi Mgalu (kulia) akimkabidhi Diwani wa kata ya Nianjema, Abdul Mzee Pyalla matofali kwaajili ya ujenzi wa choo katika shule ya mpya ya sekondari inayojengwa katika kata ya Nianjema Halamshauri ya Bagamoyo.

.........................................................

 

MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa pwani, Subira Hamisi Mgalu, ametoa Tofali 350 kusaidia ujenzi wa vyoo katika shule mpya za kata zinazojengwa Kata ya Nianjema na Mapinga zilizopo Halmashauri ya Bagamoyo  Mkoani humo.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi Tofali hizo akiwa kata ya Nianjema Halmashauri ya Bagamoyo, Mgalu alisema anamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassani kwa kutenga fedha kwa kila Halimashauri ili zitumike kujenga vyumba vya madarasa ambapo kwa kata za Nianjema na Napinga zimetumika kujenga shule mpya za kata ambazo hapo awali hazikuwepo.

Aliongeza kwa kusema kuwa licha ya fedha hizo zilizotolewa kwaajili ya ujenzi wa shule hiyo ya sekondari, bado baadhi ya kazi zinahitaaji kutekelezwa na Halmashauri,  wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo ili kufanikisha malengo hayo ambapo yeye Mbunge wa viti maalum, mkoa wa Pwani ambae pia ni mdau wa maendeleo alitoa ahadi ya kuchangia tofali na sasa ametekeleza.

Akielezea baadhi ya kazi ambazo zinahitaji kutekelezwa na Halmashauri,  wananchi na wadau mbalimbali ni pamoja ujenzi wa vyoo,

‘’ Nilipokuja Tarehe 21 mwezi wa 11 nilitoa ahadi ya kuchangia tofali 250 katika shule hii mpya ya Nianjema na Mwenyezimungu amenijaalia leo kutekeleza ahadi yangu’’ Alisema Mgalu.

Alisema mpaka sasa ameshatembelea shule 25 katika Halmashauri za Bagamoyo, Chalinze, Kibaha Mji, Kibaha Vijijini, Kisarawe, na Mkuranga ili kukagua miradi ya maendeleo na kuchangia kwa nafasi yake kama Mbunge anewakilisha Mkoa wa Pwani.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Nianjema Abdul Pyalla, amemshukuru Mbunge huyo kwa namna anavyoonyesha ushirikiano wa karibu katika mambo mbalimbali ya maendeleo.

Alisema Mh. Subira Mgalu ni mfano wa kuigwa kwani kwa hatua hii ya ujenzi ilipofikia tayari ameshatembelea mara tatu na hasa ikizingatiwa kuwa ana majukumu ya kutembea mkoa wote wa Pwani na hilo analifanya bila ya kuchoka.

 

Aidha, amewapongeza wananchi wa kata ya Nianjema kwa kujitolea mambo mbalimbali yanayohusu ujenzi huo wa shule mpya ya sekondari katika kata hiyo.

Alisema wananchi wa kata ya Nianjema ni waelewa na wpo tayari kwa kila wanachoshirikishwa kuhusu maendeleo ya kata yao.

Wakati huohuo amewashukuru wadau mbalimbali ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa ni wenye kujitolea hali na mali katika kufanikisha ujenzi huo

Ujenzi huo wa shule Kata za Nianjema na Mapinga unatekelezwa kupitia fedha zilizotolewa na Shirika la fedha la Kimataifa (IMF) kwaajili ya mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19, ambapo Halmashauri ya Bagamoyo imepokea shilingi Bilioni 1.4

No description available. 

MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa pwani, Subira Hamisi Mgalu akizungumza mara baada ya kukabidhi matofali kwaajili ya ujenzi wa choo  katika shule ya mpya ya sekondari inayojengwa katika kata ya Nianjema Halamshauri ya Bagamoyo.

No description available. 

MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa pwani, Subira Hamisi Mgalu, (kushoto) akipita eneo la ujenzi wa shule ya sekondari Nianjema kukagua kazi inavyoendelea, kulia ni Diwani wa kata ya Nianjema, Abdul Pyalla pamoja na Diwani wa kata ya Kisutu, Awesu Ramadhani.

No description available. No description available. 

MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa pwani, Subira Hamisi Mgalu, (kushoto) akipita eneo la ujenzi wa shule ya sekondari Nianjema kukagua kazi inavyoendelea, nyuma yake ni Diwani wa kata ya Nianjema, Abdul Pyalla pamoja na Diwani wa kata ya Kisutu, Awesu Ramadhani.

No description available.No description available.

MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa pwani, Subira Hamisi Mgalu, akiwa anachapia udongo kwenye moja ya chumba cha darasa katika ujenzi wa shule ya sekondari unaojengwa kata ya Nianjema Halmashauri ya Bagamoyo, Mgalu alifika eneo hilo la ujenzi kukaabidhi matofali yatakayotumika kujenga choo.

Friday, November 26, 2021

WAZIRI AWESO NA DC ZAINAB WAHITIMU SHAHADA ZA UZAMILI.

 No description available. 

Waziri wa maji Mh.Jumaa Aweso na mke wake Mh. Bi Zainabu Abdallah ambaye ni mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, wakiwa katika picha ya pamoja katika sherehe za kuhitimu shahada zao za uzamili chuo kikuu huria Tanzania, sherehe zilizofanyika jana Kikwajuni Zanzibar.

........................................................

Waziri wa maji Mh.Jumaa Aweso na mke wake Mh. Bi Zainabu Abdallah ambaye ni mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, wahitimu shahada zao za uzamili (masters) .

 

Wana ndoa hao walikuwa wakisoma masuala ya uongozi na utawala (masters of arts in governance and leadership) toka chuo kikuu huria Tanzania, Mh. Jumaa Aweso ambaye ni mbunge wa Pangani, tayari ana bachelor of science in chemistry toka chuo kikuu cha Dar es salaam. 

 

Kwa upande wa Mh. Bi Zainabu Abdallah yeye tayari alikuwa na Diploma in Customs & Tax Management (DCTM), Bachelor of Business Administration in Accounting (BBA - Accounts)  Postgraduate Diploma in Economic Diplomacy (PGD - ED) Wanandoa hao wamjaaliwa kuwa na watoto watatu.

No description available. 

 Waziri wa maji Mh.Jumaa Aweso na mke wake Mh. Bi Zainabu Abdallah ambaye ni mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, wakiwa katika picha ya pamoja katika sherehe za kuhitimu shahada zao za uzamili chuo kikuu huria Tanzania, sherehe zilizofanyika jana Kikwajuni Zanzibar.

No description available. 

Waziri wa maji Mh.Jumaa Aweso na mke wake Mh. Bi Zainabu Abdallah ambaye ni mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, wakiwa katika picha ya pamoja katika sherehe za kuhitimu shahada zao za uzamili chuo kikuu huria Tanzania, sherehe zilizofanyika jana Kikwajuni Zanzibar.

No description available.  

Waziri wa maji Mh.Jumaa Aweso na mke wake Mh. Bi Zainabu Abdallah ambaye ni mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, wakiwa katika picha ya pamoja na watoto wao, katika sherehe za kuhitimu shahada zao za uzamili chuo kikuu huria Tanzania, sherehe zilizofanyika jana Kikwajuni Zanzibar.