Thursday, September 26, 2019

ZIMZMOTO YAPOKEA BOTI YA MAOKOZI.

Kamishna wa Operesheni wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, (CF) Billy Mwakatage, akizungumza na Waandishi wa habari wakati wa kupokea msaada wa boti ya maokozi uliotolewa na Serikali ya Ujerumani kupitia Mji wa Hamburg.

 Kiongozi wa Kikosi cha Wazamiaji majini wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Stesheni Sajini  Saidi Sekibojo, akitoa maelezo jinsi vifaa mbalimbali vinavyotumiwa na wazamiaji wanapotekeleza majukumu yao katika uokoaji majini, wakati wa kupokea msaada wa boti ya maokozi uliotolewa na Serikali ya Ujerumani kupitia Mjini wa Hamburg.

 Kamishna wa Operesheni wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, (CF) Billy Mwakatage, akiwa kwenye picha ya pamoja na askari wa kikosi cha uzamiaji majini cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kinachoongozwa na Stesheni Sajini  Saidi Sekibojo, wakati wa kupokea msaada wa boti ya maokozi uliotolewa na Serikali ya Ujerumani kupitia Mjini wa Hamburg.
 

 Boti ya maokozi iliyotolewa msaada na Nchi ya Ujerumani kupitia Mji wa Hamberg kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji itakayo saidia katika shughuli ya uokoaji majini. Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.

KIKWETE ASEMA SERIKALI IMETEKELEZA AHADI KWA ASILIMIA 93 JIMBONI KWAKE.

 
wa Jimbo la chalinze, Ridhiwa Kikwete, akizungumza na viongozi wa CCM kutoka kata mbalimbali za Halmashauri ya Chalinze.
....................................
Na Shushu Joel

MBUNGE wa Jimbo la chalinze, Ridhiwa Kikwete amewataka wana CCM jimboni humo, kutembea kifua mbele akisema ahadi nyingi zimetekelezwa na kwamba hayo ni matokeo ya kuichagua CCM.

Akizungumza katika kikao cha maelekezo ya uchaguzi kwa viongozi wa kata zote 15 za jimbo la chalinze Kikwete alisema kuwa, serikali imefanya mambo makubwa kwa wananchi na hivyo kufanikisha utekelezaji wa ilani kwa asilimia 93.


Chama cha mapinduzi (CCM) kimefanya mengi katika jimbo la chalinze na wilaya ya Bagamoyo kwa ujumla ikiwemo ujenzi wa vituo vya afya, mradi wa maji, kujengwa kwa daraja kubwa la Wami, ujenzi wa vyumba vya madarasa, miundombinu ya barabara na mengine Mengi.

"Kwa Utendaji huu wa serikali ni lazima kila kiongozi na mwanaccm atembee kifua mbele kwa kufanikisha kutatua changamoto za wananchi" Alisema Kikwete.

Aidha Mbunge huyo ametumia kikao hicho Cha viongozi wa matawi na Wana CCM kuwataka wakatoe Elimu kwa wananchi kulinda miundombinu ya miradi hiyo ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

Kwa upande wake katibu wa tawi la Magogoni kata ya kiwangwa Msisi Safisha amempongeza mbunge kwa kuwakumbusha viongozi wa matawi juu ya kuyatangaza mazuri yaliyofanywa na chama hicho.

"Sisi tulikuwa tukijua kuwa kazi ya kukisemea chama juu ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inafanywa na viongozi wa ngazi za juu tu kumbe hata sisi wa chini tunatakiwa kusema "Alisema Safisha.

Aidha amempongeza mbunge kwa kuwafumbua macho na hivyo amewataka viongozi wenzake kutumia elimu hiyo ili wananchi wengine waweze kutambua kilichotekelezwa na serikali ya awamu ya tano.

Naye katibu wa CCM, Mkoa wa Pwani, Ally Makoa, amemsifu mbunge wa Chalinze kwa usimamizi na utekelezaji wa ilani katika Jimbo lake kwani kazi anazozifanya zinaonekana.

Aidha amewataka viongozi wa matawi na kata kuwapelekea wananchi viongozi wanaowataka wananchi na si yule asiyetakiwa.

Pia aliongeza kuwa kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa wanatakiwa kujipanga ili kisipotee hata kitongoji kimoja.
 

Viongozi wa CCM kutoka kata mbalimbali za Halmashauri ya Chalinze, wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo hilo alipokutana nao kupeana maelekezo mbalimbali kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa, Picha zote na Shushu Joel