Tuesday, December 11, 2018

TIMU YA MICHEZO YA BUNGE MSHINDI WA JUMLA WA MEDALI KATIKA MICHEZO YA MABUNGE YA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI YALIYOFANYIKA BUJUMBURA NCHINI BURUNDI

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia) akipokea cheti cha ushiriki wa michezo ya Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoka kwa Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson ambae ni kiongozi wa msafara wa wanamichezo wa timu ya michezo ya Bunge katika michezo ya Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliyofanyika Bujumbura, Burundi katika tukio lililofanyika tarehe 10 Desemba, 2018 katika uwanja wa ndege Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kushoto) akimpongeza Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson alipowasili katika uwanja wa ndege wa Mjini Dodoma akitokea Bujumbura, Burundi katika michezo ya Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Naibu Spika aliongoza msafara wa timu ya michezo ya Bunge. Kushoto ni katibu wa Bunge, Mhe. Stephen kagaigai.
Wanamichezo wa timu ya michezo ya Bunge wakipokelewa na uongozi wa Bunge, watumishi wa Bunge wakiongozwa na Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai walipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma wakitokea katika michezo ya Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliyofanyika Bujumbura, Burundi.
 
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (mwenye koti nyeusi) akiwa katika picha ya pamoja na wanamichezo wa timu ya michezo ya Bunge walioongozwa na Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson (mwenye tisheti nyeusi) baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mjini Dodoma wakitokea Bujumbura, Burundi katika michezo ya Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson (katikati) akizungumza na wanamichezo wa timu ya michezo ya Bunge na watumishi wa Ofisi ya Bunge leo tarehe 10 Desemba, 2018 katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma, wakati timu hiyo ilipowasili kutoka Bujumbura, Burundi katika michezo ya Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Ikiwa ni kuwaeleza kwa ufupi mafanikio waliyoyapata katika mashindano hayo na ushirikiano ulioonyeshwa na watumishi wa ofisi ya Bunge kabla na baada ya mashindano

RAIS DKT. MAGUFULI AGAWA VITAMBULISHO 670,000 KWA WAKUU WA MIKOA KWA AJILI YA MATUMIZI YA WAJASIRIAMALI WADOGO WADOGO (MACHINGA) KATIKA MIKOA YOTE YA TANZANIA BARA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia wakati Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila alipokuwa akisaini hati ya makabidhiano ya vitambulisho vya wajasiriamali wadogo wadogo machinga kwa ajili ya mkoa wa Mbeya.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia wakati Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira alipokuwa akisaini hati ya makabidhiano ya vitambulisho vya wajasiriamali wadogo wadogo machinga kwa ajili ya mkoa huo wa Kiliamnjaro.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia wakati mkuu wa mkoa wa Njombe Cristopher Ole Sendeka alipokuwa akisaini hati ya makabidhiano ya vitambulisho vya wajasiriamali wadogo wadogo machinga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia wakati mkuu wa mkoa wa Simiyu Antony Mtaka alipokuwa akisaini hati ya makabidhiano ya vitambulisho vya wajasiriamali wadogo wadogo machinga .
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Agrey Mwandri kabla ya kusaini hati ya makabidhiano ya vitambulisho vya wajasiriamali wadogo wadogo machinga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia wakati mkuu wa mkoa wa Tabora Agrey Mwandri alipokuwa akisaini hati ya makabidhiano ya vitambulisho vya wajasiriamali.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizingumza na Wakuu wa Mikoa, Mawaziri na Makatibu Wakuu wa baadhi ya Wizara, Mameneja wa Mikoa wa Mamlaka ya Mapato nchini TRA, Wawakilishi wa Machinga kabla ya kutoa Vitambulisho kwa ajili ya Wafanyabiashara wadogo wadogo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. Vitambulisho hivyo vitagharimu kiasi cha Shilingi 20,000/ kwa kila kimoja. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizingumza na Wakuu wa Mikoa, Mawaziri na Makatibu Wakuu wa baadhi ya Wizara, Mameneja wa Mikoa wa Mamlaka ya Mapato nchini TRA, Wawakilishi wa Machinga kabla ya kutoa Vitambulisho kwa ajili ya Wafanyabiashara wadogo wadogo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. Vitambulisho hivyo vitagharimu kiasi cha Shilingi 20,000/ kwa kila kimoja.
Baadhi ya Wakuu wa Mikoa wakisikiliza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyokuwa akiitoa katika ukumbi wa katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Meneja wa Mamlaka ya Mapato TRA kwa mkoa wa Kilimanjaro Msafiri Mbibo ambaye alikataa rushwa ya Dola za kimarekani $2000. Rais Dkt. Magufuli ameagiza kuandikiwa barua ya kupongezwa kwa Meneja huyo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri wa Ardhi Wiliam Lukuvi wakati akiondoka kwenye ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipungia mkono wakati akiondoka kwenye ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, PICHA NA IKULU.

NAIBU WAZIRI ATEMBELEA ENEO LITAKALOTUMIWA KUBANGUA KOROSHO YA SERIKALI

 Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya, akiwaonyesha mtambo maalum wa kuchemsha korosho wataalamu kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele. Wataalam hao wametembelea eneo la SIDO kujiridhisha kama linafaa kwa ajili ya kuanza kubangua korosho iliyonunuliwa na serikali.
 Kaimu Meneja wa SIDO mkoa wa Mtwara, Zamla Dongwala, akimuonyesha mashine ya kukausha korosho Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji (hayupo pichani) wakati alipotembelea eneo la SIDO, mkoani Mtwara leo. Eneo hilo ni moja ya maeneo yaliyochaguliwa kuanza kutumiwa wa wabanguaji wa korosho wadogo kubangua korosho zilizonunuliwa na serikali.
 
Fundi umeme akiwa kwenye hatua za mwisho kukamilisha matengenezo ya mashine ya kuchambua korosho kama alivyokutwa na mpiga picha wetu eneo la SIDO mjini Mtwara  (Picha na Idara ya Habari-MAELEZO)

RAIS DKT. MAGUFULI ATOA VITAMBULISHO KWA WAJASIRIAMALI NCHI NZIMA

Na. Immaculate  Makilika – MAELEZO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amegawa vitambulisho kwa wajasiriamali nchi nzima wenye mitaji isiyozidi shilingi milioni nne kwa lengo la kuwasaidia kufanya biashara zao kwa uhakika sambamba na kutambulika katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Akizungumza mapema leo jijini Dar es salaam, katika  kikao kazi na viongozi wa TRA, Rais Magufuli aligawa jumla ya vitambulisho 25,000 kwa kila Mkuu wa Mkoa, na kusema kuwa vitambulisho hivyo vimelengwa kutolewa kwa wajasiriamali wote nchi nzima wenye mitaji isiyozidi shilingi milioni nne ili viwasaidie kufanya shughuli zao mahali popote nchini, ikiwa ni pamoja na kutambulika TRA.

Ambapo Rais Magufuli alisema kuwa vitambulisho hivyo vinagawiwa bure, isipokuwa  kila mjasiriamali atatozwa gharama ya shilingi 20,000/= ikiwa ni sehemu ya gharama ya uandaaji wa kitambulisho husika.

“Kitambulisho hiki nimetoa mimi bure, sioni kama kuna mtu atakayekuja kuwasumbua, na kila Mkuu wa Mkoa atapata vitambulisho 25,000, ambapo atashirikiana na Wakuu wa wilaya ili kugawa vitambulisho hivyo kwa wajasiriamali walioko katika mkoa wake”

Halikadhalika, Rais Magufuli aliwataka wajasiriamali hao kuwa waaminifu, na kutokubali kufanya biashara za wafanyabiashara wakubwa wenye mitaji yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni nne.

Sambamba na hilo, Rais Magufuli alisisitiza watanzania kulipa kodi kwa kuwa kodi ndio msingi wa maendeleo kwa taifa lolote lile duniani, huku akiwataka TRA kupunguza viwango vikubwa vya kodi ambavyo wananchi wamekuwa wakivilalamikia.

Kwa upande wake, Gavana wa Benki Kuu, Profesa Florence Luoga alisema kuwa Benki hiyo imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali ikiwemo kudhibiti matumizi haramu ya fedha,  kuhakikisha kuwa thamani ya fedha haiyumbi na kudhibiti matumizi ya dola kwa kufungia maduka ya kubadilishia fedha ambayo hayakuwa na leseni.

Profesa Luoga alisema  kuwa BOT iligunduwa kuwepo kwa maduka ya kubadilishia fedha 1,000 badala ya maduka 300 yaliyokuwepo awali na ambayo hayakuwa na leseni.

“Tunajadiliana na Waziri wa Fedha ili kuwezesha wananchi au wafanyabiashara kulipia bidhaa  kwa kutumia benki” alisema Profesa Luoga

Profesa Luoga  aliongeza kuwa kwa sasa hivi hali ya fedha ni nzuri na hivyo Serikali ina fedha za kutosha kufanya matumizi mbalimbali kwa kipindi cha miezi mitano ijayo na kuwataka wananchi wasiwe na hofu.

Aidha, aliongeza kuwa kabla ya mwezi Desemba kuisha , BOT itakuwa imeshatengeneza kanuni za kuwalinda watumiaji wa mabenki.

Naye, Kamishna wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Charles Kichere, alisema kuwa katika kipindi cha miaka ya Serikali ya Awamu ya Tano, TRA imefanikiwa kukusanya mapato ya jumla ya shilingi trilioni 42.9
Ambapo, katika kipindi cha robo mwaka wa fedha 2018/2019, Serikali kupitia TRA imekusanya kodi jumla ya shilingi trilioni 3.8.

Aidha, Kichere alisema kuwa licha ya changamoto mbalimbali zinazoikabili Mamlaka hiyo, wameweza kusajili jumla ya wafanyabiashara wadogo yaani wamachinga 97,256 huku takribani  asilimia 80 ya wafanyabiashara wanatumia mashine za EFD

Sunday, December 9, 2018

WAZIRI MKUU AFURAHISHWA NA UWEKEZAJI WA VIWANDA CHALINZE


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa afurahishwa na uwekezaji wa viwanda katika halmashauri ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, kwa kutembelea na kukagua viwanda vikubwa viwili katika ziara aliyoifanya Jana katika halmashauri hiyo.

Mheshimiwa Majaliwa ametembelea kiwanda cha kuzalisha vigae cha Twyford kilichoko katika kitongoji cha Pingo katika mamlaka ya mji mdogo wa Chalinze na kujionea shughuli za uzalishaji katika kiwanda hicho,ambacho ni kiwanda kinachozalisha vigae bora katika afrika mashariki na kinauza ndani na nje ya nchi.

Aidha Waziri Mkuu alitembelea pia kiwanda cha kutengeneza bidhaa zinazotokana na matunda cha Sayona Fruits Ltd kilichopo katika kijiji cha Mboga, kiwanda ambacho kinamilikiwa na mwenyekiti wa wamiliki wa viwanda Tanzania Subashi Patel, ni kiwanda kikubwa katika afrika mashariki chenye mitambo ya kisasa na kinachonunua matunda kwa wingi kama malighafi ya kuendesha kiwanda hicho.

Mheshimiwa Majaliwa alikagua na kuona uzalishaji wa vinywaji mbalimbali na kuona jinsi watanzania wanavyonufaika na ajira kiwandani hapo.

Mheshimiwa Majaliwa katika hotuba yake kiwandani hapo alimpongeza mwekezaji wa kiwanda hicho Subashi Pateli kwa uwekezaji wenye tija unaotoa huduma za jamii, kuzalisha ajira kwa watanzania lakini pia kutoa kodi ya serikali kuu na halmashauri ya wilaya kwa maendeleo ya nchi na kuwataka wawekezaji wengine wawekeze kwa tija ili kutekeleza kwa vitendo Ilani ya Chama cha Mapinduzi kama ilivyonadiwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.

" Katika kipengele cha viwanda kama kilivyotajwa kwenye Ilani kazi yetu ni kuweka vema kwani kimetekelezwa na muda wa uchaguzi utakapofika ni kuwauliza watanzania mnataka tufanye kitu gani kingine ." Waziri Mkuu alisema.

Majaliwa aliendelea kutoa wito kwa wanachalinze kulima matunda ambayo soko lake sasa linapatikana hapa kiwandani na kuwahamasisha kuleta matunda hayo kwani soko ni la uhakika na pasipo matunda uzalishaji haupo, akawataka wananchi kwa ujumla kuwalinda wawekezaji kwa udi na uvumba ili waweze kuzalisha kwa tija na kwa amani na utulivu kwani pasipo amani hakuna uzalishaji utakaofanyika hivyo aliwataka wananchi kwa ujumla kuwalinda wawekezaji popote pale nchini Tanzania ili uzalishaji ukafanyike kwa amani na wawekezaji wasikate tamaa kwa kutokuwa na amani katika maeneo waliyowekeza

Naye Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo kwa niaba ya wananchi wa mkoa wa Pwani alitoa wito kwa wawekezaji wanaotaka kuja kuwekeza mkoani Pwani wanakaribishwa Pwani ni salama,mazingira ni rafiki kwa uwekezaji na amani ni ya kutosha," Tunayo ardhi ya kutosha kwa uwekezaji wa aina yoyote karibuni Pwani ya Viwanda." Ndikilo alisema.