Sunday, December 2, 2018

RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI MKUBWA WA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA KATIKA JIJI LA ARUSHA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia maji yanayotoka katika moja ya visima virefu vilivyopo katika mradi huo mkubwa wa maji safi na usafi wa mazingira katika jiji la Arusha. Mradi huo utakapokamilika utaweza kuzalisha lita za ujazo milioni 200  kwa siku tofauti na sasa ambapo lita za ujazo ni 45 milioni wakati mahitaji ya jiji la Arusha ni lita za ujazo milioni 90.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akivuta utepe pamoja na Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa Maji safi na usafi wa Mazingira katika jiji la Arusha. Wengine katika picha ni Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Isaack Kamwelwe pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB Alex Mubiru.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi wa mradi mkubwa wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira utakaosaidia jiji la Arusha katika sherehe zilizofanyika katika kijiji cha Kimyaki Arumeru mkoani Arusha.
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB Alex Mubiru wakati wa mkutano na wananchi wa Arumeru jijini Arusha mara baada ya kuzindua mradi huo wa maji.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Arumeru mara baada ya kuweka  jiwe la msingi mradi wa Maji safi na usafi wa Mazingira katika jiji la Arusha.

Wananchi wa Arumeru wakishangilia wakati wa hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika kijiji cha Kimnyaki Arumeru.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wananchi wakati akiondoka katika eneo la mkutano.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Meya wa jiji la Arusha Calist Lazaro mara baada ya kuwahutubia wananchi wa Arumeru. PICHA NA IKULU.

CCM PWANI YATOA AGIZO ZITO KWA WATENDAJI WAKE.

MNEC wa mkoa wa pwani (kushoto) akimsikiliza mwenyekiti wake katika kikao na watendaji wa CCM wilaya zote za mkoa wa Pwani.
......................................................

Na Shushu Joel, Kibaha.
MWENYEKITI wa ccm mkoa wa Pwani Ramadhani Maneno amewaagiza watendaji wa chama hicho kuacha kufanya kazi kwa mazoe kama walivyokuwa wamezoea miaka ya nyuma.

Watendaji wa Ccm walio wengi wameshindwa kuendana na kasi ya awamu ya tano chini ya mwenyekiti wa taifa Dkt John Pombe Magufuli ambaye pia ni Rais wa Tanzania kwa watendaji wengi kufanya kazi za chama kipindi cjha chaguzi tu.

Akizungumza na watendaji wa mkoa huo mwenyekiti huyo aliwataka watendaji wote kuwajibika kwa wanachama wa chini katika kuwasaidia kutambua sitahiki zao kwani wanachama wa chini wamekuwa wakinyanyaswa na matajili huku viongozi wa chama wakiangalia tu na kushindwa kuwajibika katika kuwasaidia ili waweze kupata haki zao.

 “Watendaji wa chama wamekuwa wajijisahau katika uwajibika wao na kibaya zaidi wamekuwa ni watu wa kuagiza tu huku wakiwa wamekaa ofisini”Alisema

Aliongeza kuwa watendaji wa chama ndio mhimiri mkubwa katika chama hivyo ni lazima watendaji wote katika mkoa wahakikishe wanakuwa ni kiungo kikubwa kati ya uongozi na wanachama wea chini.

 Aidha amewataka watendaji kuwa wabunifu katika kipindi hiki kutokana na kuwa kipindi cha sasa ni kipindi cha siasa ni uchumi kwa kuwaelimisha wanachama juu ya umuhimu wa kuwa na vikundi vilivyosajiliwa katika vyombo husika ili waweze kukopesheka na kujijengea uchumi wao ambao utawatoa katika kipindi cha kuwa omba omba kwa watu.

Kwa upande wake mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa kupitia mkoa wa Pwani (NEC)Haji Jumaa amempongeza mwenyekiti huyo kwa kuona umuhimu wa kukutana na makatibu wote wa mkoa wa Pwani na kuwakumbusha wajibu wao katika utendaji.

Aliongeza kuwa watendaji wakisimama imara katika usimamizi wa mali za chama hali ya ccm itakuwa zaidi ya hapo ilipo sasa.

“Makatibu wanapaswa kuwajibika kwa bidii ili kuhakikisha chama chetu kinazidi kuwa bora kuanzia ngazi za mashina mpaka taifa na hii inawezekana pale kila mmoja atahakikisha anakuwa mkali kwa yule mwenye nia mbaya na chama katika kutumia mali za chama ovyo”Alisema Jumaa.

Aliongeza kuwa zoezi la kuwasajili wanachama wa ccm kwa njia ya kielectronic ni jema kwani liwaongeza mapato ya chama na kukifanya chama kuwa juu zaidi ya hapo kilipo sasa.

Naye katibu wa ccm wilaya ya Kibaha vijijini Janeth Mnyaga ameupongeza uongozi wa ccm mkoa kwa kuwakutanisha na kuwataka kuwajibika katika shughuli zao za usimamizi wa chama katika ngazi za wilaya.

Hivyo aliongeza kuwa elimu iliyotolewa leo kwa watendaji wote iwe endelevu kwani inawapatia motisha katika uwajibikaji na usimamizi wa chama katika ngazi za wilaya.

Makatibu wa CCM mkoa wa Pwani wakimsikiliza mwenyekiti wa mkoa huo akitoa maelezo juu yao.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Pwani Ramadhani Maneno aliyesimama akitoa maelekezo kwa watendaji wa chama hicho.

DC BAGAMOYO AAGIZA KUKAMATWA MHASIBU MKUU NA WASAIDIZI WAKE WATATU HALMASHAURI YA CHALINZE KWA UBADHILIFU WA FEDHA.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Bi Zainabu Kawawa ameagiza watumishi wa idara ya fedha katika halmashauri ya wilaya ya Chalinze wanaoshughulika na ukusanyaji mapato wakamatwe na kupisha uchunguzi kufuatia hali ya ukusanyaji mapato katika halmashauri hiyo kuwa chini ya kiwango tarajiwa, agizo hili amelitoa leo katika kikao alipokuwa akizungumza na watumishi wa halmashauri hiyo.

Watumishi alioagiza wapishe uchunguzi ni Mweka Hazina wa halmashauri Bwana David Rubibira, na wahasibu watatu ambao ni Waziri Ally, Jumanne Sanga na Maneno Kwambwa

Mheshimiwa Kawawa alisikitishwa na ukusanyaji mapato katika halmashauri ya Chalinze kuwa chini ya malengo na kudai kuwa kuna mianya ya ubadhirifu wa mapato kwani mapato ya halmashauri yakikusanywa kwa umakini yanafikia milioni 920 kwa mwezi kwa chanzo cha madini ya kokoto nje ya vyanzo vingine kwa maana ya milioni 33 kwa siku.

Hivyo kutokana na makisio hayo Mkuu wa wilaya hana imani na mapato yanayokusanywa katika halmashauri hiyo ambayo ni wastani wa milioni 550 hadi 659 kwa mwezi.

Aidha baada ya kikao hicho Mheshimiwa kawawa alimtaka Mkuu wa polisi Chalinze kuwaweka chini ya ulinzi na kuwachukua kwa ajili ya uchunguzi na baada ya uchunguzi kukamilika hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao kwa kusababisha upotevu wa mapato.

"Nimekuwa nikifuatilia ukusanyaji mapato kuna mianya mingi ya utoroshaji mapato, tusitafutane wala kujaribiana kwa kuvujisha mapato tumepoteza Mapato sana kwenye makrasha kwa siku tuna uwezo wa kukusanya milioni 33 ,kwa mwezi tuna uwezo wa kukusanya zaidi ya milioni 900, badala ya kufuatilia na kukagua mnakaa tu ofisini katika hili hatuwezi kuvumiliana hata kidogo,Mkurugenzi nakuagiza watumishi wanaohusika na mapato wakae pembeni kwa hatua zaidi kuanzia leo na vyombo vya usalama vifanye kazi katika kuchunguza haya." Mheshimiwa Kawawa aliagiza.


Saturday, December 1, 2018

RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI PAMOJA NA RAIS WA KENYA UHURU KENYATTA WAFUNGUA KITUO CHA KUTOA HUDUMA KWA PAMOJA MPAKANI NAMANGA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipongezana na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta mara baada ya kufungua Kituo cha Kutoa huduma kwa pamoja mpakani Namanga One Stop Border Post (OSBP) upande wa Tanzania.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakimwagia maji mti mara baada ya kuupanda wakati wa hafla ya ufunguzi wa Kituo cha Kutoa huduma kwa pamoja mpakani Namanga One Stop Border Post (OSBP) upande wa Tanzania.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipongezana na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta mara baada ya kufungua Kituo cha Kutoa huduma kwa pamoja mpakani Namanga One Stop Border Post (OSBP) upande wa Kenya.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakiwa wameshikana mkono wakati  wakimwagia maji mti mara baada ya kuupanda wakati wa hafla ya ufunguzi wa Kituo cha Kutoa huduma kwa pamoja mpakani Namanga One Stop Border Post (OSBP) upande wa Kenya.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakipanda mti mara baada ya mara baada ya kufungua Kituo cha Kutoa huduma kwa pamoja mpakani Namanga One Stop Border Post (OSBP) upande wa Kenya.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakipata maelezo ya kituo hicho cha Kutoa huduma kwa pamoja mpakani Namanga One Stop Border Post (OSBP) upande wa Kenya.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na  Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakati wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa Kituo cha Kutoa huduma kwa pamoja mpakani Namanga One Stop Border Post (OSBP) upande wa Tanzania.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na   Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakipungia wananchi mara baada ya kuwasili katika eneo la mkutano pembezoni mwa Kituo cha Kutoa huduma kwa pamoja mpakani Namanga One Stop Border Post (OSBP) upande wa Tanzania.
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na   Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakifurahi nyimbo zilizokuwa zikipigwa na bendi ya polisi katika hafla ya ufunguzi wa vituo hivyo vya mpakani.
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi funguo Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta mara baada ya kufungua Kituo cha Kutoa huduma kwa pamoja mpakani Namanga One Stop Border Post (OSBP) upande wa Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea funguo kutoka kwa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta mara baada ya kufungua Kituo cha Kutoa huduma kwa pamoja mpakani Namanga One Stop Border Post (OSBP) upande wa Kenya.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na  Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa Kituo cha Kutoa huduma kwa pamoja mpakani Namanga One Stop Border Post (OSBP) upande wa Kenya.

ZIJUE STESHENI ZA RELI YA KISASA-SGR

Jumla ya Stesheni za reli ya kisasa-SGR 14 zinajengwa katika awamu mbili za Ujenzi wa Reli ya Kisasa – SGR kuanzia Dar es Salaam hadi Makutupora ambapo Stesheni kubwa ni Dar es Salaam, Morogoro na Dodoma. Usanifu wa Stesheni hizi umesadifu mazingira halisi ya kitanzania, Tamaduni, madini pamoja na maliasili zinazopatikana nchini.

 Stesheni ya Dar es Salaam kwa Kipande cha Dar es Salaam hadi Morogoro umesadifu Madini ya Tanzanite yanayopatikana mkoani Arusha Tanzania, vituo vidogo vya Pugu, Soga, Ruvu na Ngerengere vikisadifu aina ya nyumba zinazopatikana maeneo ya Morogoro na Dodoma huku Kituo cha Morogoro kikisanifiwa kuakisi Milima ya Uruguru inayopatikana mkoani Morogoro. 

Ujenzi wa Vituo hivi vyote unazingatia mahitaji muhimu ya kibinadamu kwa kuwa vitakuwa na Migahawa, Huduma za Kibenki, Maegesho ya Magari, Maduka ya Kisasa pamoja na sehemu za kupumzikia.
Stesheni ya Morogoro
Picha zikionesha Muonekano wa kituo cha Reli ya Kisasa – SGR cha Soga  kinachojengwa  Soga mkoani Pwani 
Stesheni ya Morogoro
Picha zikionesha Muonekano wa kituo cha Reli ya Kisasa – SGR cha Morogoro kinachojengwa mkoani Morogoro. Kituo hiki kitakuwa na Huduma muhimu kama Huduma za kifedha, Mgahawa, Sehemu za Kuegesha Magari na Maduka. Kituo hiki kimesanifiwa kuakisi Milima ya Uruguru inayopatikana Mkoani Morogoro