Saturday, October 20, 2018

RC SHINYANGA AKAGUA MRADI WA UPANUZI KITUO CHA AFYA.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack akikagua ubora wa matofali yalitengendezwa kwa ajili ya kujenga majejngo ya kituo cha afya Kishapu kinachofanyiwa upanuzi.
..........................

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack amekagua mradi wa upanuzi wa kituo cha afya Kishapu ulioanza kutekelezwa katika Wilaya ya Kishapu.

Akiwa katika mradi huo kituoni hapo wenye thamani ya sh. milioni 400 Mhe. Telack alitaka nguvu za wananchi zishirikishwe katika ujenzi wa vituo vya afya.

Sanjari na hilo aliwataka wataalamu waziache kamati za ujenzi zifanye kazi ya kusimamia miradi hiyo ya ujenzi wa vituo vya afya.

“Wataalamu msiingilie hizo kamati na tunachotaka ni majengo imara, tofali imara, simenti iwe haijaexpire (haijakwisha muda wake), agizeni kwa bei ya jumla na nafuu itatusaidie kujenga kituo,” alisisitiza.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa alikutana na Kamati ya Lishe Wilaya ya Kishapu na kuwataka wataalamu hao kutoa elimu ya lishe kwa wananchi ili kuondoa udumavu.

Aliagiza fedha zinazotengwa kwenye bajeti kwa ajili ya masuala ya lishe zisimamiwe vizuri ili kuhakikisha zinafanya kazi hiyo lishe.

“Kila mtu kwa nafasi yake akifanya kile kinachotakiwa kufanyika mkoa wetu  utasimama vizuri ka hiyo kila mmoja kwa jukumu lake,” alisisitiza Mhe Telack.


MOHAMMED DEWJI APATIKANA AKIWA HAI.

Hatimae Mfanyabiashara Bilionea Mohamed Dewji maarufu kwa jina la Mo Dewji amepatikana na amerejea nyumbani kwake kuungana na familia yake akiwa salama. Kwa mujibu wa mtandao wa Makampuni ya Mohamed Enterprises ya MeTL Group, Mo amerejea nyumba ikiwa ni siku ya tisa baada ya kutekwa na watu wasiojulikana Alhamis Oktoba 11 katika Hoteli ya Colessium iliyopo Masaki jijini Dar es salaam.

Akitoa taarifa hizo kuptia mtandao wa Twitter unaomilikiwa na Kampuni yake ya Mohamed Enterprises Ltd, Mo ameandika: “Namshukuru Mwenyezi Mungu nimerudi salama nyumbani. Nawashukuru Watanzania wenzangu na watu wote kote duniani kwa dua na sala zao. Nashukuru mamlaka zote, ikiwemo Jeshi la Polisi, zilizofanya kazi ya kuhakikisha narudi salama.” — Mohammed Dewji na , taarifa ambayo aliipost Saa 9:15 alfajiri, saa za Tanzania.

Aidha, Waziri wa Mazingira, Mhe. Januari Makamba, nae kupitia mtandao wake wa Twitter, amethibitisha kupatikana kwa Mo na kusema kuwa Mfanyabiashara huyo alitupwa maeneo ya Gymkhana huku akiwa na alama za kufungwa kamba mikononi.

“Nimemuona na kuongea kwa kirefu na Mohammed Dewji. Ni mzima wa afya isipokuwa ana alama za kufungwa kamba mikononi na miguuni. Mnamo saa nane usiku, watekaji waliamua kumtupa kwenye maeneo ya viwanja vya Gymkana. Naamini Polisi watatoa taarifa za ziada kuhusu kilichojiri.,” ameandika Makamba.


Friday, October 19, 2018

RC. NDIKILO AZINDUA KAMPENI YA FURAHA YANGU KUPAMBANA NA VVU

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo akiwaonyesha wananchi  kadi mara baada ya kumaliza zoezi la kupima virisi vya ukimwi ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa kampeni ya furaha yangu yenye lengo la kupambana na maambukizi ya VVU, pamoja na kuwahimiza watu kupima afya zao.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
................................

VICTOR MASANGU, PWANI 

KATIKA kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano katika kukabiliana na kupambana na  maambukizi mapya ya virusi vya vya ukimwi hatimaye Mkoa wa Pwani umezindua rasmi kampeni ijulikanayo  kwa jina la  furaha yangu kwa lengo la kuwahimiza wananchi wake kwenda kupima mapema ili kujua afya zao na kuanza kupatiwa matibabu endapo watabainika kuwa  na maambukizi.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo akizungumza katika halfa hiyo ya  uzinduzi ambapo alikuwa mgeni rasmi  amebainisha kuwa lengo la serikali ya awamu ya tano ni kuweka mipango ya kupambana na maambukizi mapya ya VVU  ambapo kwa sasa kiwango cha maambukizi  katika ngazi ya Mkoa kimepungua kutoka asilimia 7.1 kwa mwaka 2003 hadi kufikia asilimia 5.5 kwa mwaka wa 2017.

“Kampeni hii inawalenga watanzania wote watambue hali zao za maaambukizi ya VVU.hususan kwa wanaume na makundi mengine ambayo ni wasichana walio katika umri wa balehe, wanawake na vijana wenye umri wa miakaa 15-24 akinammama wajawazito na wanaonyonyesha  sambamba na watoto wao,”alisema Ndikilo.

Aidha Ndikilo alibainisha kuwa hali ya wananchi kutokujua hali zao za maambukizi ya virusi vya ukimwi katika Mkoa wa Pwani inaweza kuleta atharu kubwa kwa wenza na familio zao na pia inadhoofisha mapambano dhidi ya ukimwi hivyo amewaasa wananachi wote kujenga tabia ya kupima  kwa lengo la kuweza kujua afya zao. 

Kwa upande wake Kaimu mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani Hussein Athumani alisema  kwamba lengo lao ni kuhakikisha wanaweka mipango ya kuwaelimisha wananchi katika maeneo mbali mbali ili kuweza kupunguza kasi ya maambukizi mapya  ya virusi vya ukimwi pamoja na kuongeza vituo vingine  kwa ajili ya utoaji wa dawa za kufubaza.

Nao baadhi ya wananchi wa Mkoa wa Pwani ambao wamehudhuria katika uzinduzi huo wanaoishi na na maambukizi ya VVU akiwemo Bahatisha Hemed na Ibrahimu Venasi hawakusita kutoa ushuhuda wao huku wakiitaka jamii kuachana na vitendo vya kuwanyanyapaa  na badala yake wawashirikishe kikamilifu  katika shuguli mbali mbali za kimaendeleo.

UZINDUZI wa kampeni ya furaha yangu katika Mkoa wa Pwani utaweza kuleta mkombozi mkubwa kwa wananchi kutokana na  mikakati ambayo imepangwa kwa ajili ya kutoa mafunzo na elimu ambayo itawasaidia na kujikinga na maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi huku kauli  mbiu  yake ikisema kwamba Pima ,jitambue, na Ishi