Monday, April 30, 2018

TEDDY MALKIA WA NGUVU 2018.

Malkia wa nguvu 2018 Teddy Davis kutoka Bagamoyo akionyesha tuzo yake ya Malkia wa nguvu katika Ukumbi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, TaSUBa.
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga akizungumza wakati wa hafla za kumtangaza Malkia wa nguvu 2018 iliyofanyika Ukumbi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, TaSUBa.
........................................
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga amewataka wanawake kushirikiana ili kujiletea maendeleo kupitia vikundi vya ujasiliamali.

Majid aliyasema hayo wakati wa sherehe za kumtangaza Malkia wa Nguvu 2018 Teddy Davis  ambae ametoka wilayani Bagamoyo.

Alisema ushindi  wa Teddy kuwa Malkia wa nguvu ni wazi kuwa wanawake wakifanya juhudi wananweza kufanikiwa hivyo ni vyema wakawa na ushirikiano ili kuonyeshana njia.

Aliongeza kwa kusema kuwa, Halmashauri za Bagamoyo na Chalinze zinatenga asilimia tano kwa wanawake na vijana ili waweze kujikwamua kiuchumi kupitia vikundi vyao.

Aidha, Mkuu huyo wa wilaya alisema Serikali ya wilaya Bagamoyo itashirikiana na wanawake wote wilayani humo wenye kuonyesha nia ya kujikwamua kiuchumi kwa kujishughulisha na mambo mbalimbali ya uzalishai mali kupitia vikundi vyao.

Nae katibu Mwenezi wa CCM wilaya ya Bagamoyo, John Francis (Bolizozo) alisema wanawake wanapaswa kuiwekea malengo ya maendeleo kwakuwa wao ndio dira ya familia.

Alisema kuna baadhi ya wanawake waba tabia ya kujiuza miili yao hivyo aliwataka kuacha tabia hiyo na badala yake wafanye shughuli zitakazowaingizia kipato kwa njia ya halali.

Aliongeza kwa kusema kuwa ili mwanamke awe na thamani katika jamii na kuweza kupata msaada wa kitaalamu anapaswa kwanza kujiheshimu yeye mwenyewe na kujitambua thamani yake.

Bolizozo alikemea tabia ya wanawake wanaovaa mavazi ya kujidhalilisha pamoja vijana wakiume ambao huiga tamaduni zisizo na maadili.

Alimpongeza Teddy pamoa na ukwaa zima la uwezeshai wanawake Bagamoyo kwa kuikita katika shughuli za kujiletea maendeleo na kuongeza kuwa hayo ndio matunda ya CCM.

Kwa upande wake Mshindi wa Malkia wa Nguvu 2018 Teddy Davis alisema anaishukuru serikali ya wilaya ya Bagamoyo kwa kumuunga mkono yeye na wanawake wenzie katika shughuli za uasiliamali.

Teddy ambae ni Mwenyekiti wa Jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi wilayani Bagamoyo aliwashukuru watu wote waliompigia kura ili kupata nafasi hiyo ambayo hakuitarajia.

Jukwaa analoliongoza la uwezeshaji wanawake kiuchumi ni agizo la makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la kuundwa kwa Majukwaa hayo nchi nzima ili wanawake wapate fursa za kujiajiri na kujiwezesha kiuchumi.

Teddy ni mjasiliamali anaejishghulisha na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zitokanazo na Lozela huku akiwaonyesha wanawake wenzie fursa za kujikwamua kiuchumi kupitia bidhaa za kutengeneza kwa mikono na ubunifu wa aina mbalimbali.

Akizungumzia namna ya mchakato wa kumpata Malkia wa nguvu, Muwakilishi kutoka Clouds Media Group, Amani Maltin ambao ndio waandaai wa shindano la Malkia wa nguvu alisema kura zimepigwa kutoka kwa wasikilizaji wa Clouds fm na Clouds tv ambapo majina ya washiriki yalitoka nchi nzima.

Maltin Alisema miongoni mwa sifa za kumpata Malkia wa nguvu ni pamoja na kujishughulisha kwake na mambo ya kimaendeleo yeye wenyewe pamoja na kushirikiana na wanawake wenzie sehemu anayoishi na ni kwa jinsi gani anakubalika katika jamii.
 
 Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga pamoa na kamati ya ulinzi na Usalama wakipiga makofi kumkaribisha Malkia wa nguvu wakati akiingia ukumbini.

 Mshindi wa Malkia wa Nguvu 2018 Teddy Davis akiingia Ukumbini.
 

 Mshindi wa Malkia wa Nguvu 2018 Teddy Davis akizungumza katika sherehe hizo.
 
Diwani wa Kata ya Dunda, Dckson Makamba akimkaribisha Mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo ili kuzungumza katika sherehe hiyo.

 Katibu Mwenezi wa CCM wilaya ya Bagamoyo, John Francis (Bolizozo) akizungumza katika sherehe hiyo.
 Mshindi wa Malkia wa Nguvu 2018 Teddy Davis akikata keki katika sherehe hizo.
 Mshindi wa Malkia wa Nguvu 2018 Teddy Davis akimlisha keki mama yake mzazi, kulia na kushoto ni watoto wake.
 Katibu Mwenezi wa CCM wilaya ya Bagamoyo, John Francis (Bolizozo)kimlisha keki Malkia wa nguvu 2018, Teddy Davis.
 
 
Malkia wa nguvu 2018, Teddy Davis, akimkabidhi zawadi ya kanzu kofia na tasbih Mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga.
 
Picha ya pamoja Mgeni rasmi, Malkia wanguvu, Kamati ya ulinzi na usalama na viongozi wengine waandamizi pamoja na watoto wa Malkia wa nguvu waliochuchumaa chini na Katibu mwenezi wa CCM wilaya Bolizozo.

MAGAZETI YA LEO 30 APRIL 2018.

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AFUNGUA BARABARA YA IRINGA-DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mwakilishi wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB Jeremy Aguma wa pili kutoka kulia  wakivuta utepe kwenye jiwe la msingi kuashiria ufunguzi wa Barabara ya Iringa-Dodoma katika sehemu ya Iringa-Migori-Fufu Km 189 iliyokamilika kujengwa katika kiwango cha lami. Sherehe hizo za ufunguzi zilifanyika katika kijiji cha Ndolela kilichopo Isimani nje kidogo ya mji wa Iringa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mwakilishi wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB Jeremy Aguma, Balozi wa Japan Masaharu Yoshida wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa Barabara ya Iringa-Dodoma katika sehemu ya Iringa-Migori-Fufu Km 189 iliyokamilika kujengwa katika kiwango cha lami. Wengine katika picha ni Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli, Waziri wa Ujenzi Profesa Makame Mbarawa , Spika wa Bunge Job Ndugai pamoja na viongozi wengine wa Serikali na wageni kutoka nje ya nchi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi katika sherehe za ufunguzi wa Barabara ya Iringa-Dodoma katika sehemu ya Iringa-Migori-Fufu Km 189 iliyokamilika kujengwa katika kiwango cha lami.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Isimani Mkoani Iringa.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa jukwaa kuu pamoja na Balozi wa Japan Masaharu Yoshida, Waziri wa Ardhi Wiliam Lukuvi, pamoja na Waziri wa Mambo ya nje Balozi Dkt. Augustine Mahiga wakifatilia sherehe za ufunguzi wa barabara ya ya Iringa-Dodoma katika sehemu ya Iringa-Migori-Fufu Km 189 iliyokamilika kujengwa katika kiwango cha lami.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Iringa mjini waliofika kumpokea mara baada ya kuwasili akitokea Isimani mkoani Iringa.


PICHA NA IKULU

Monday, April 23, 2018

TAKUKURU BAGAMOYO YATOA SOMO SHULE ZA SEKONDARI.

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Pwani, Suzana Raimond kulia akizungumza katika Tamasha la klabu za wapinga rushwa shuleni, kushoto ni Mkuu wa TAKUKURU wilaya ya Bagamoyo, Raimond Katima.
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Alhaj, Majid Mwanga akifungua Tamasha la klabu za wapinga rushwa shuleni. 
.................................
Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wilaya ya Bagamoyo imeandaa Tamasha la klabu za kupinga rushwa katika shule za sekondari.

Katika Tamasha hilo lililofanyika Shule ya Sekondari ya Baobab iliyopo Mapinga wilayani Bagamoyo, Mgeni Rasmi alikuwa Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga ambapo aliwataka wanafunzi kujifunza kuchukia rushwa ili kuwa raia wenye uzalendo na nchi yao.

Alisema vijana ni kundi muhimu linalopaswa kutambua ubaya wa rushwa kwakuwa hao ndio wanaondaliwa kuwa viongozi wa baadae hivyo kutambua ubaya wa rushwa kwao kutapelekea nchi kupata viongozi wenye uzalendo watakaoiletea nchi yao maendeleo.

Aidha, ameipongeza TAKUKURU wilaya ya Bagamoyo kwa kufanya kazi vizuri na kupelekea vitendo vya rushwa kupungua wilayani humo na kulinda haki za watu katika idara mbalimbali.

Aliwapongeza TAKUKURU kwa utaratibu wao wa kutoa elimu katika kila idara ili kuelezea ubaya wa rushwa na namna ya kuiepuka.

Kwa upande wake Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Pwani, Suzana Raimond alisema klabu za wapinga rushwa shuleni zimesaidia kwa kiasi kikubwa kazi kupambana na rushwa kwakuwa wananfunzi wamekuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu kwa njia ya maigizo na kutambua ubaya wa rushwa.

Alisema TAKUKURU mkoa wa Pwani imefanikiwa kukamata watu kupitia taarifa zinazotolewa na klabu za wapinga rushwa shuleni na kwamba hiyo imesaidia kupunguza kwa kiasi kikubwa vitendo vya rushwa shuleni.

Nae Mkuu wa TAKUKURU wilaya ya Bagamoyo Raimond katima ambao ndio waandaaji wa Tamasha hilo alisema vitendo vya rushwa vinasababishwa na mmomonyoko wa maadili katika jamii kuanzia ngazi ya chini.

Alisema maadili yanapaswa kujengwa kwenye familia, mashuleni na katika kila maeneo yanayohusiana na malezi ili kuwajenga watoto na vijana kutambua umuhimu wa kuwa na maadili mema ikiwa ni pamoja na kutambua ubaya wa rushwa.

Aliongeza kwa kusema kuwa kiongozi au mtumishi wa uma anapokuwa na vitendo vya rushwa ni wazi kuwa vitendo hivyo vimeanzia chini.

Alisema nchi inakabiliwa na rushwa hivyo ni vyema wananchi wakatambua kuwa rushwa inasababisha kurudisha nyuma maendeleo

Aliwataka wananchi kushirikiana na TAKUKURU ili kubaini wale wote wanaojihusisha na vitendo vya rushwa ili hatua za kisheria zichkue mkondo wake.

Wanfunzi wa klabu za wapinga rushwa shuleni walisema wamefaidika na elimu wanayopata kupitia klabu hizo ambapo kwa sasa wamefahamu vyema madhara yatokanayo na kupokea na kutoa rushwa.

Walisema taasisi nyingi hapa nchini kuna vijna hivyo kuwajengea uelewa vijana wakiwa shuleni ni jambo la msingi na kwamba wakitoka watatoa elimu hiyo katika jamii.
Wanfunzi wa klabu za wapinga rushwa shuleni kutoka shule za sekondari sita wilayani Bagamoyo wakifuatilia Tamasha hilo.