Tuesday, August 6, 2024

WATANZANIA WAHIMIZWA KULA NA KUNYWA BIDHAA ZA KOROSHO

 

NA HADIJA OMARY , LINDI.


Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Ikulu (kazi maalum)  George Mkuchika Amewahimiza watanzania kupenda Kula na kunywa bidhaa za korosho kwani zinavirutubisho vingi vya kupambana na magonjwa pamoja na kufanya uhamasishaji wa  uongezaji wa thamani ya zao hilo.



Mkuchika ametoa Rai hiyo alipokuwa akizungumza na wananchi, Wadau na wakulima wa mikoa ya Lindi na Mtwara wakati wa maadhimisho ya siku ya Kula na Kula korosho ambayo ni mahusisi kwa ajili ya uhamasishaji wa ulaji na unywaji korosho.


Katika maadhimisho hayo Wananchi Wadau na wakulima wa korosho walijionea bidhaa mbalimbali zitokanazo na korosho kama vile chapati, maandazi, kashata , maziwa ya korosho pamoja na mvinyo.


Amesema ulaji wa  korosho licha ya kumlinda Mlaji na magonjwa lakini pia ni husaidia kukuza uchumi kwa mtu mmoja Mmoja na Soko la ndani .


" Kwa upande wa afya ya Binadamu ukila korosho zilizobanguliwa unakuwa na faida ya kuzuia ugonjwa wa moyo kwa kuzuia shindikizo la damu, ukila korosho unaongeza viini lishe vinavyozuia hatari ya kupata ugonjwa wa kansa pamoja na kuzuia Hatari ya kupata ugonjwa wa kisukari"




Kaimu mkurugenzi wa Taasisi ya utafiti wa kilimo TARI Naliendele, Dr. Rashid Kidunda  amesema licha ya Mikoa hiyo ya Lindi na Mtwara kuwa  ni wazalishaji wakubwa wa zao la korosho lakini ni asilimia 10 pekee ya kile kinachozalishwa ndicho kinachotumika kama chakula kwa wakazi wa mikoa hiyo


"Unaweza kuona ni kwa namna gani tupo chini Katika ulaji na unywaji wa korosho kwa hivyo ili kukuza Soko la ndani tuliamua  kuzifanya siku ya tarehe 5 August kila mwaka tuadhimishe siku hii" Amesema Kidunda 


Amesema Nchini Tanzania korosho imeendelea kuwa zao kubwa la kibiashara  Katika kuchangia kipato cha wakulima hasa Katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Pwani na Ruvuma 


" Kwa sasa tumeona Mikoa mingine 17 ikiingia Katika kilimo cha zao hilo na sisi kama TARI Naliendele tumepewa jukumu la  kufanya utafiti na kutatua changamoto za wakulima wa zao Hilo" alifafanua 


Kaimu mkurugenzi wa Bodi ya korosho Reveliani  Ngaiza amesema zao la korosho ni zao la kipekee tofauti na mazao mengine kwa kuwa Lina matumizi mengi kuanzia kwenye Majani, Mbegu,  Tawi , shina na hata mzizi wake


" Ukiacha ulaji wa korosho zao la korosho kwa upande wa Majani yanatumika kama Dawa kutibu minyoo tumboni, kuzuwia kuhara , kutoa Gesi tumboni pamoja na kutibu vidonda vya tumbo"


"Lakini ukichukia Jana ukachanganya na gome la mkorosho unapata Dawa ya kutibu ugonjwa wa meno, maganda ya korosho baada ya kubangua yakikamuliwa upatikana kimiminika chakutengeneza wino wa kuandikia kupitia kalamu"







No comments:

Post a Comment