Friday, August 16, 2024

MPANGO WA IMASA WATUA LINDI, BILIONI 3.6 ZATENGWA.

 


LICHA ya zoezi la utoaji wa MIKOPO kwa wanawake, vijana na Watu wenye mahitaji maalumu kusitishwa kwa muda kwa ajili ya uboreshaji, Mkoa wa Lindi imeendelea kutenga fedha hizo ambapo mpaka sasa zimeshatengwa Jumla ya shilingi Bilioni 3.6

Hayo yameelezwa na mkuu wa wilaya ya Lindi kwa niamba ya mkuu wa Mkoa huo wakati wa mafunzo ya uwasilishaji wa program ya uwezeshaji wananchi kiuchumi iliyofanyika huko Manispaaa ya Lindi 


Program hiyo ya uwezeshaji wananchi kiuchumi imepewa jina la Imarisha uchumi na Mama Samia (IMASA)



Ndemanga Amesema Fedha hizo zimetengwa kutoka kila Halmashauri ambazo zinatolewa kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu .


Amesema kuwa kutokana na dhamira ya serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha inaendelea kuwawezesha wananchi kiuchumi katika makundi husika imekuja na mpango wa Imarisha uchumi na Mama Samia (IMASA) ambao katika hatua ya awali imejikita katika kukusanya maoni ya walengwa kuhusu vipaumbele vya mkoa na kuwasajili.


Kwa upande wake katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la uwezeshaji wananchi kiuchumi Bi. Beng'i M. Issa amesema kuwa madhumuni ya programu hiyo katika hatua ya awali ni kupata takwimu za wananchi kwenye maeneo yao husika na shughuli zao katika maeneo hayo.

 Malengo mengine ni kupata Mahitaji ya kiuchumi kwenye maeneo husika kwa kushirikiana na viongozi wa Mikoa na Wilaya, kujenga uwezo wa wananchi wote wenye uhitaji kwenye maeneo husika, kutekeleza programu ya kuwezesha wananchi kwenye Mikoa na maeneo yao.



Wakizungumza mara baada ya semina hiyo wajasiriamali kutoka wilaya za Mkoa wa Lindi wameshukuru kwa programu hiyo ambayo inakwenda kuwainua kiuchumi









No comments:

Post a Comment