Sunday, August 4, 2024

WMA WATAKA WAKULIMA KUZINGATIA VIPIMO KWENYE UJAZO WA MAZAO.

 

Wakala wa Vipimo (WMA) umewataka wakulima kuzingatie sheria ya vipimo inayotaka ujazo wa mazao yao kwenye gunia yasizidi kilo 100.


Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa WMA, Albogast Kajungu amefafanua sheria hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika manda la WMA kwenye maonesho la wakulima nane nane.


Amesema moja ya mambo wanayowaeleza wakulima ni namna ya kuweka ujazo wa mazao yao na kuzingatia vipimo vilivyowekwa na Serikali.


Amesema katika kutafsiri neno lumbesa kwenye ujazo wa gunia sheria inasema lumbesa ni kile kilichozidi juu ya ujazo wa kilo 100.


Ameongeza kwa kusema kuwa wakulima wanapaswa kuzingatia sheria ya ujazo wa mazao kwenye gunia nayo ni kuhakikisha ujazo huo usizidi kilo 100.


Amesema sheria inataka mazao yote yanapaswa yafungashwe kwenye ujazo wa kilo 100 na si vinginevyo.


Katika kuhakikisha sheria hiyo inatekelezwa ili kulinda haki ya mkulima na mnunuzi, inashauriwa kuwe na vituo vya kuuzia mazao ambapo mizani itawekwa hapo ili kuhakiki ujazo mazao husika


No comments:

Post a Comment