Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekufungua mkutano wa 9 wa CDF na Makamanda uliofanyika katika Shule ya Kijeshi ya Ulinzi wa Anga (SKUA) mkoani Tanga leo tarehe 15 Desemba 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekufungua mkutano wa 9 wa CDF na Makamanda uliofanyika katika Shule ya Kijeshi ya Ulinzi wa Anga (SKUA) mkoani Tanga leo tarehe 15 Desemba 2025.
Mhe. Nchimbi ametoa kauli hiyo Disemba 15, 2025 Mkoani Kagera baada ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Kampasi ya Kagera ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kutokana na mchango huo, Serikali imejizatiti kuleta mageuzi ya elimu katika ngazi zote, ili kuhakikisha kuwa wahitimu wanapata ujuzi, stadi na maarifa yanayoendana na soko la ajira.
‘’ Rai yangu kwa UDSM, hakikisheni Kampasi hii mpya inakuwa kitovu cha uvumbuzi na ubunifu; kuwawezesha vijana wetu kuibua mawazo mapya, kufanya ubunifu, na kutumia fursa za soko la pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki’’ Ameseama Mhe. Nchimbi.
Mhe. Nchimbi ameipongeza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kuratibu mradi mkubwa wa HEET kwa kuhakikisha matumizi adili ya fedha na kwa kuzingatia thamani ya fedha. Ameitaka Wizara kushirikiana na wadau kuandaa mapema mahitaji kama vile ithibati, vifaa na rasilimaliwatu, ili kuwezesha shughuli za mafunzo katika Kampasi hiyo kuanza kama ilivyopangwa bila kuchelewa
Pia ameipongeza UDSM, kwa kusimamia mchakato wa ujenzi wa Kampasi hiyo, ameitaka kuendelea kuwa mfano wa kuigwa katika matumizi bora ya rasilimali na utoaji wa elimu yenye tija kwa kizazi cha leo na kesho.
" hapa niwatake wasimamizi mkabdarasi na wote wanauhusika kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa wakati uliopangwa hatutavumilia ucheleqaji wowote" anesema Mhe. Nchinbi
Ameishukuru Benki ya Dunia kwa kushikiriana na Serikali kufadhili utekelezaji wa mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) , ambao umewezesha ujenzi wa Kampasi ya Kagera hukua akiahidi uwekezaji katika kukamilisha jengo la abweni la wanafunzi wa kiume na miundombinu mingine muhimu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameshiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Utatu wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC Organ Troika) uliofanyika kwa njia ya mtandao akiwa Bukoba mkoani Kagera leo tarehe 15 Desemba 2025.
Mkutano huo umejadiili hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika kurejesha amani na usalama katika Jamhuri ya Madagascar.
Mkutano huo pia umehudhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe.
"Tanzania continues to stand as a reference point for peace and social cohesion in Africa and the world."
These were the words of the United Nations Secretary-General, H.E. AntΓ³nio Guterres, today upon receiving a Special Envoy carrying a message from the President of the United Republic of Tanzania, H.E. Dr. Samia Suluhu Hassan.
The message was delivered by the Special Envoy, H.E. Ambassador Mahmoud Kombo, the Minister of Foreign Affairs and East African Cooperation, who led the Tanzanian delegation to the United Nations Headquarters in New York.
Secretary-General Guterres noted that Tanzania’s reputation as an icon of peace was tested during the General Elections held on 29 October 2025, and acknowledged the country’s resilience in maintaining national unity and stability.
He expressed the United Nations’ strong interest in seeing Tanzania continue to remain united and serve as a positive example.
The UN Secretary-General emphasized the importance of a meaningful and inclusive national dialogue aimed at addressing the root causes of the violent incidents that occurred on 29 October 2025, and at putting in place measures to prevent their recurrence.
He also reaffirmed the United Nations’ full support to Tanzania’s ongoing efforts, including support during and after the completion of the mandate of the Commission of Inquiry established in the United Republic of Tanzania.
Leo Desemba 9, tunapoadhimisha miaka 64 tangu Taifa letu lipate Uhuru, Tanzania Bloggers Network (TBN) inawapongeza Watanzania wote kwa kufikia hatua hii muhimu katika historia ya Taifa letu. Hii ni siku ya kutafakari safari tuliyotoka, mahali tulipo, na mwelekeo tunaoujenga kwa pamoja.
Waasisi wetu walituwachia zawadi kubwa—Uhuru. Lakini walituonya kuwa Uhuru hauwezi kuwa kamili bila kujitegemea. Leo tunakumbusha maneno ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliyewahi kusisitiza:
"Uhuru hauwezi kukamilika pasipo kujitegemea. Hatuwezi kuitwa huru kama tunategemea wengine kutupatia mahitaji yetu ya kimsingi."
Tujenge Taifa Letu – Tusiibomoe Tanzania
Kama mtandao wa habari za kidijitali, TBN inasisitiza kuwa mafanikio yetu kama Taifa yametokana na utulivu, umoja na mshikamano. Ili kuendelea mbele, tunahitaji kudumisha amani na maridhiano—nguzo muhimu za maendeleo.
Rais mstaafu Benjamin William Mkapa alituasa kwa busara:
"Amani si kitu cha asili; tunahitaji kuilinda na kuitunza kila siku. Bila amani, hakuna maendeleo ya kweli."
Tukikubali kuongozwa na chuki, uchochezi na vurugu, juhudi za waasisi wetu za kupambana na ujinga, umaskini na maradhi zitapotea. Tusiitumie mitandao au uhuru wa maoni kuharibu Taifa letu; tuitumie kulijenga.
Kila Zama na Kiongozi Wake – Tuunge Mkono Mageuzi
Kila kizazi kina wajibu wake. Kama alivyoeleza Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi:
"Kila utawala na zama zake. Kila kiongozi na mchango wake katika ujenzi wa Taifa hili."
Katika awamu ya sasa chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Tanzania inaendelea na mwelekeo wa 4R: Reconciliation, Resilience, Reforms, and Rebuilding. Huu ni mwaliko kwa Watanzania wote kushiriki katika kujenga Taifa lenye maridhiano, mageuzi chanya na uimara wa kiuchumi na kijamii.
Tuna nafasi ya kuzungumza—basi tuseme kwa njia inayojenga, si inayobomoa. Kuthamini Uhuru ni kufanya kazi kwa bidii, kulinda amani, na kuacha kutumiwa kuharibu misingi ya Taifa letu.
TBN Inawatakia Maadhimisho Mema ya Miaka 64 ya Uhuru!
Tanzania Kwanza — Kazi, Utu na Mshikamano. Tusonge Mbele!
Beda Msimbe
Mwenyekiti, Tanzania Bloggers Network (TBN)
Mkuu wa Wilaya ya Oloililai, Rift Valley nchini Kenya Mhe. Andrew Mwiti Mathew amesema serikali ya Kenya haiungi Mkono wachochezi wa vurugu, ghasia na maandamano nchini Tanzania, akiahidi kuzuia Wakenya kuchochea na kushiriki kwenye vurugu na maandamano haramu.
Mhe. Mwiti amebainisha hayo leo Disemba 08, 2025 mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla, wakati wa Kikao cha ujirani mwema kilichofanyika Wilayani Longido, ikihusisha Kamati za Ulinzi za Mkoa wa Rift Valley na Mkoa wa Arusha, kama sehemu ya kuimarisha usalama na biashara kwenye eneo la mpaka wa Namanga.
"Sisi tuwahakikishie kuwa tumejipanga vizuri kuzuia wachochezi na mtu yeyote ambaye anaweza kuwa na nia ya kuja kujiunga na wale watakaokuwa wanapanga kufanya maandamano ambayo tayari tumehakikishiwa kuwa ni haramu kwani hayajaruhusiwa kisheria." Amesisitiza Mhe. Mwiti.
Awali katika maelezo yake, Mhe. Makalla ameihakikishia Kenya kuwa serikali ya Tanzania imejipanga kikamilifu kuhakikisha hakuna vurugu wala matukio ya uvunjifu wa amani yatakayojitokeza kesho Jumanne Disemba 09, 2025, akiwataka wananchi kuendelea na shughuli zao za kiuchumi na kijamii bila ya kuwa na wasiwasi wowote.
Mhe. Makalla kadhalika katika kikao hicho ameahidi kuwa serikali ya Tanzania itaendelea kuhakikisha mpaka wa Namanga unaendelea kuwa salama pamoja na kuheshimu mipaka iliyopo na kuimarisha ufanyaji wa biashara kupitia mpaka huo ili kuleta tija kwa wananchi wa nchi hizo mbili.
Na Albert Kawogo
MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ( TPA) imesaini hati ya Makubaliano ( MoU) na Kampuni ya Africa Global Logistics ( AGL) Tanzania Ltd yenye Makao Makuu yake Nchini Ufaransa ambayo ni kampuni tanzu ya MSC, kwa ajili ya usanifu, Ujenzi na uendeshaji wa gati mpya tatu katika Bandari ya Bagamoyo.
Hati hii ya makubaliano ( MoU) imesainiwa tarehe 6 Disemba,2025 Makao Makuu ya TPA Jijini Dar es Salaam kati ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA Bw. Plasduce Mbossa na Rais wa AGL Philippe Labonne.
Bw. Mbossa amesema, kusainiwa kwa hati ya Makubaliano ni ishara ya utayari wa kuanza kwa mradi wa Bandari mpya ya Bagamoyo ambapo kwa kuanzia AGL itaanza usanifu na Ujenzi wa gati tatu mpya za Kisasa kati ya 28 zinazotatajiwa kujengwa katika Bandari hiyo pamoja na gati mbili mpya za Kisasa katika Bandari ya Dar es Salaam.
“Tunategemea kuanza Ujenzi wa gati mpya tatu katika Bandari ya Bagamoyo mapema mwezi Januari na pia tunawakaribisha Wawekezaji wengine wa ndani na wa nje katika Mradi huo ambapo lengo ni kuleta mapinduzi makubwa katika Shughuli za Kibandari Nchini” Amesema Bw. Mbossa.
Kwa upande wake Rais wa AGL Bw. Philippe Labonne anasema wameamua kuingia makubaliano na TPA na kuwekeza Tanzania kutokana na kuwa nchi yenye Amani, Usalama na mazingira bora na tulivu ya uwekezaji iliyosehemu sahihi kijiografia kwa Sekta ya Uchukuzi na kuwa lango la Biashara Kitaifa na kimataifa.
“ Ninaamini Tanzania ni nchi inayokuwa kwa kasi kimaendeleo ikiwa na mtaji Mkubwa wa watu wakatimu na mtazamo Chanya na pia ni lango la kuingilia nchi nyingi barani Afrika na kuyafikia masoko ya kimataifa, Naamini ushirikiano huu utafungua mambo mengi ikiwemo kutengeneza Ajira ambazo ni muhimu sana kwa maendeleo ya Mtu mmoja mmoja na Taifa kwa Ujumla” Amesema Bw. Labonne.
Mradi wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo kwa gati mpya tatu utajengwa kwa miezi 36 ( miaka mitatu) na Kampuni ya AGL imepata nafasi hii ya kushirikiana na TPA katika Ujenzi huo kutokana na uzoefu wao kama kampuni kubwa ya huduma za usafirishaji na logistiki, inayotoa huduma kamili za usafirishaji, usimamizi wa mizigo, usafirishaji wa kimataifa na huduma za forodha, ikihudumia sekta mbalimbali kama uchimbaji, mafuta, chakula, na misaada ya kibinadamu, ikiwa sehemu ya kundi la kimataifa la AGL (zamani BollorΓ© T&L) na sasa wakiwa chini ya MSC.