Monday, December 15, 2025

𝗦𝗘𝗞𝗧𝗔 𝗬𝗔 𝗘𝗟𝗜𝗠𝗨 𝗜𝗡𝗔 𝗠𝗖𝗛𝗔𝗡𝗚𝗢 𝗠𝗞𝗨𝗕𝗪𝗔 𝗞𝗔𝗧𝗜𝗞𝗔 𝗨𝗖𝗛𝗨𝗠𝗜 𝗪𝗔 𝗧𝗔𝗜𝗙𝗔 - 𝗠𝗛𝗘. 𝗡𝗖𝗛𝗜𝗠𝗕𝗜


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema kuwa sekta ya Elimu, hususan elimu ya Juu ina mchango mkubwa  katika uchumi wa Taifa, kutokana na kuzalisha nguvukazi inayoshiriki kutoa huduma katika sekta mbalimbali.  

Mhe. Nchimbi ametoa kauli hiyo Disemba 15, 2025 Mkoani Kagera baada ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Kampasi ya Kagera ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kutokana na mchango huo, Serikali imejizatiti kuleta mageuzi ya elimu katika ngazi zote, ili kuhakikisha kuwa wahitimu wanapata ujuzi, stadi na maarifa yanayoendana na soko la ajira. 


‘’ Rai yangu kwa UDSM, hakikisheni Kampasi hii mpya inakuwa kitovu cha uvumbuzi na ubunifu; kuwawezesha vijana wetu kuibua mawazo mapya, kufanya ubunifu, na kutumia fursa za soko la pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki’’ Ameseama Mhe. Nchimbi.


Mhe. Nchimbi ameipongeza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kuratibu mradi mkubwa wa HEET kwa kuhakikisha matumizi adili ya  fedha na kwa kuzingatia thamani ya fedha. Ameitaka Wizara kushirikiana na wadau kuandaa mapema mahitaji kama vile ithibati, vifaa na rasilimaliwatu, ili kuwezesha shughuli za mafunzo katika Kampasi hiyo kuanza kama ilivyopangwa bila kuchelewa 


Pia ameipongeza UDSM, kwa kusimamia mchakato wa ujenzi wa Kampasi hiyo, ameitaka kuendelea kuwa mfano wa kuigwa katika matumizi bora ya rasilimali na utoaji wa elimu yenye tija kwa kizazi cha leo na kesho. 


" hapa niwatake wasimamizi mkabdarasi na wote wanauhusika kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa wakati uliopangwa hatutavumilia ucheleqaji wowote" anesema Mhe. Nchinbi

 

Ameishukuru Benki ya Dunia kwa kushikiriana na Serikali kufadhili utekelezaji wa mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) , ambao umewezesha ujenzi wa Kampasi ya Kagera hukua akiahidi uwekezaji katika kukamilisha jengo la abweni la wanafunzi wa kiume na miundombinu mingine muhimu.









No comments:

Post a Comment