Monday, November 6, 2023

DKT. BITEKO ASHIRIKI MAZISHI YA KAKA WA WAZIRI MKUU MAJALIWA

 

Asisitiza Watanzania wanaupendo wa dhati kwake


Waziri Mkuu Majaliwa awashukuru Watanzania kwa kumfariji


Ruangwa - Lindi


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameungana na Viongozi mbalimbali wa kitaifa na Watanzania kwa kutoa salamu za pole kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa kufuatia kifo cha Kaka yake, marehemu Issa Juma, aliyezikwa leo.


Akizungumza leo Novemba 6, 2023 wilayani Ruangwa Mkoa wa Lindi wakati akitoa salamu hizo kwa niaba ya waheshimiwa Mawaziri, Dkt. Biteko amesema watanzania wanaupendo wa dhati kwa Waziri Mkuu Majaliwa ambao wameuonesha pia katika kipindi hichi cha kumpoteza marehemu kaka yake.


"Sisi ni kielelezo kuwa Watanzania wanaupendo nawe ndio maana tumekuja kuungana pamoja na wewe, kulia pamoja na wewe lakini kukutia moyo kwamba sisi tuliofika hapa na wengine tunakupa pole kwa msiba wa kumpoteza kaka," ameeleza Dkt. Biteko.


Amesema kuwa, jambo lolote linalotokea ni mipango ya Mwenyezi Mungu hivyo ni muhimu kuombeana heri ili tuwe na mwisho mwema duniani. 


Kwa upande wake, Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa amewashukuru Watanzania kwa kumfariji katika kipindi hichi cha msiba wa kaka yake. Amesema amepokea salamu za pole kutoka kwa Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zanzibar, Dkt.Hussein Mwinyi na watanzania wote wanaompa pole na kumfariji.


Naye, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson akiwasilisha salamu kwa niaba ya Wabunge, ametoa pole kwa Waziri Mkuu Majaliwa na familia yote kwa kuondokewa na mpendwa wao na kusisitiza kuendelea kushirikiana na kutenda mazuri yanayompendeza Mungu.


Wengine walioshiriki kumpa pole Mhe. Waziri Mkuu ni Viongozi mbalimbali wa Serikali wakiwemo Mawaziri, Wakuu wa Mikoa ya Lindi na Mtwara, Wakuu wa Wilaya, vyama vya siasa na wananchi wa mkoa huo. 











JWT YAANZA ZIARA PWANI,KUTATUA KERO KWA WAFANYABIASHARA

 

Na Mwandishi Wetu, Pwani.


JUMUIYA ya Wafanyabiasha nchini (JWT) imeanza ziara ya kikazi ya kusikiliza kero za Wafanyabishara katika Wilaya zote za Mkoa wa Pwani.


Lengo la ziara hiyo ni kusikiliza kero za wafanyabishara, wenye viwanda na kampuni ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu na kuepuka changamoto ikiwamo migomo ya mara kwa mara.


Mwenyekiti wa JWT, Hamis Livembe, akiongozana na viongozi wengine mapema leo, wamewasili ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani na kufanya mazunguzo na Katibu Tawala, Rashid Mchatta kabla ya mikutano yao.


Livembe amesema Rais Samia anawapenda wafanyabishara ndio sababu amewaagiza wasikilize kero zao ili kupatiwa ufumbuzi wa kudumu.


Amesema wafanyabishara wakiungana wanaweza kujisemea na kumaliza kero zao bila kufunga biashara wala kufanya vurugu hivyo ni muhimu kujitokeza kwenye mikutano hiyo.


Naye Mchatta ameipongeza jumuiya hiyo kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuisaidia serikali kusikiliza kero hizo nchi nzima na kuzifikisha kwenye mamlaka husika.


"Niwasihi tu viongozi wa JWT msiache kuwaelimisha wafanyabishara umuhimu wa kulipa kodi pamoja na hayo wazingatie tahadhari za mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini," amesema.





VIJANA 24 KUTOKA TULIA TRUST WAMEHITIMU TaSUBa, BAGAMOYO.

 

Na Athimani Shomari

Vijana 24 kutoka Taasisi ya Tulia Trust ya Mkoani Mbeya wamehitimu mafunzo yao ya mwezi mmoja ya Sanaa na Utamaduni leo Tarehe 06 Novemba 2023, katika chuo cha TaSUBa Wilayani Bagamoyo na kufanikiwa kuongeza elimu yao ya Sanaa na Utamaduni,
ambapo sasa wanaweza kufanya shughuli zao  kwa ufanisi zaidi ukilinganisha na awali.

Mgeni Rasmi katika Mahafali ya kumaliza mafunzo hayo, Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt. Herbert Makoye, ametoa wito kwa vikundi mbalimbali nchini vinavyofanya shughuli za Sanaa na Utamaduni kufika chuoni hapo ili kupata elimu itakayowaongoza katika kazi za Sanaa na Utamaduni.

Dkt. Makoye alisema TaSUBa ni sehemu ya kulea wasanii wa aina mbalimbali ikiwemo wale wa ngoma za asili hivyo watanzania wasione uvivu kujiunga na chuo hicho kwa kukuza Taaluma zao ili waweze kufikisha kwenye jamii ujumbe unaolingana na maadili ya kitanzania kwa weledi uliotukuka.

Wakati huohuo Dkt. Makoye ameishukuru Taasisi ya Tulia Trust ya Mkoani Mbeya kwa kugharamia mafunzo ya vijana hao ili wapate mafunzo sahihi ya Sanaa na utamaduni kwa lengo la kukuza vipaji vyao, kuongeza vipato vyao na kufikisha ujumbe kwa jamii kwa njia ya Sanaa na Utamaduni.

Alisema Tulia Trust, imekuwa msatari wa mbele katika kuwafadhili vijana mbalimbali kuendeleza vipaji vyao vya Sanaa na Utamaduni katika chuo hicho kinachotoa mafunzo ya Sanaa na Utamaduni kilichopo chini ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambpo miongoni mwao
wapo wanaopata kozi fupi, ngazi ya cheti na Astashahada.

Awali wakisoma risala mbele ya mgeni rasmi, wahitimu hao walismea wanaishukuru Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kwa
kuwapokea na kuwapa mafunzo bora yatakayowawezesha kufanya shughuli
zao kwa ufanisi zaidi ukilinganisha na awali kabla ya kupata mafunzo hayo.

Walisema uwepo wa TaSUBa na vijana kupata fursa ya mafunzo chuoni hapo
kumewafanya vijana wengi hapa nchini kuiona thamani ya vipaji walivyonavyo kwani vinaendelezwa na hatimae wananufaika kupitia vipaji hivyo.

Waliongeza kwa kusema kuwa katika mafunzo hayo waliyopata wamefanikiwa
kujifunza ngoma mpya ambazo walikuwa hawazijui, lakini pia wameweza kujifunza namna ya kufanya maboresho ya ngoma zao za asili za mkoa wa Mbeya.

Aidha, sambamba na hayo, vijana hao pia walisema wameweza kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu Sanaa na Utamaduni wa Mwafrika kupitia Tamasha la 42 la kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo ambalo lilifanyika chuoni hapo (TaSUBa) mwezi Oktoba 2023.

Kupitia risala yao, vijana hao wamemshukuru Mbunge wa Mbeya Mjini na
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, pamoja na Taasisi ya Tulia Trust, kwa kutambua uwepo wa vijana na kuwashika mkono kwa kuwawezesha kutoka kwenye hatua moja kwenda hatua nyingine na kunufaika kupitia vipaji walivyonavyo.

Taasisi ya Tulia Trust ya Mkoani Mbeya imeasisiwa na na Mbunge wa jimbo la Mbeya mjini, ambae pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, lengo likiwa ni kuwasaidia
vijana na wakazi wa mkoa huo kwa ujumla kutatua changamoto mbalimbali
zinazowakabili.











Picha zote Na Herry Pesa

Sunday, November 5, 2023

RAIS, SAMIA AMKABIDHI NYUMBA MAMA JANETH MAGUFULI.


Rais Samia Suluhu Hassan amemkabidhi Nyumba Mjane wa Rais wa awamu ya Tano Dkt John Magufuli, Mama Janeth Magufuli jijini Dar es Salaam, leo Tarehe 05 Nobemba 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi mfano wa ufunguo mjane wa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli aliyekuwa Rais wa awamu ya tano, Mama Janeth Magufuli ikiwa ni ishara ya kukabidhi nyumba mpya ya kuishi kwa familia ya Dkt. John Pombe Magufuli iliyopo wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam ambayo amejengewa na Serikali kwa mujibu wa sheria, Jijini Dar es Salaam tarehe 5 Novemba, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa nyumba mpya ya Hayati Dkt. John Pombe Magufuli aliyekuwa Rais wa awamu ya tano, na kuikabidhi kwa Mama Janeth Magufuli, nyumba hiyo imejengwa na Serikali kwa mujibu wa sheria, Jijini Dar es Salaam tarehe 5 Novemba, 2023.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na mjane wa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli aliyekuwa Rais wa awamu ya tano, Mama Janeth Magufuli wakati wa hafla fupi ya kukabidhi nyumba ya kuishi iliyopo wilaya ya Kinondoni ambayo imejengwa na Serikali kwa mujibu wa sheria, Jijini Dar es Salaam tarehe 5 Novemba, 2023.




TAREHE 5 GOLI 5 YANGA, SIMBA 1.

 







MAGAZETI YA TANZANIA LEO TAREHE 05 NOVEMBA 2023.

 












Saturday, November 4, 2023

DKT. ABBAS AONGOZA MAPOKEZI YA WAWEKEZAJI ZAIDI YA 150 KUTOKA MAREKANI

 

Na. Edmund Salaho- Kilimanjaro


Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbas ameongoza mapokezi ya wawekezaji zaidi ya 150 kutoka Taifa la Marekani ambao wamewasili katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA) majira ya saa moja na nusu kwa ndege ya Shirika la Oman.


Wawekezaji hao wanatarajia kutembelea vivutio mbalimbali nchini ikiwemo Hifadhi bora Afrika kwa mara tano mfulululizo Serengeti pamoja na kivutio bora Afrika kwa mwaka 2023 ‘Ngorongoro’ lengo likiwa ni kujionea fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana katika vivutio hivyo ambapo wanatarajia kutumia zaidi ya siku 10 katika vivutio hivyo.


Aidha Dkt. Abbas, aliongozana na viongozi mbalimbali wa Taasisi za Uhifadhi kutoka TANAPA na Ngorongoro. 








Friday, November 3, 2023

MZEE MBAGALA, MDAU WA MAENDELEO BAGAMOYO ATUA BUNGENI.

 

Mzee, Rajabu Selemani Mbagala (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha nje ya ukumbi wa Bunge, Jijini Dodoma leo tarehe 03 Novemba 2023, katikati ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson na kulia ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Mh. Muharami Mkenge, kitoka kushoto ni Mwenyekiti wa CCM kata ya Nianjema ndugu Omar Makamba na katibu mwenezi CCM Kata, Mzee Marijani (Minjori.)


Mzee, Rajabu Selemani Mbagala (kushoto) akiwa katika picha nje ya ukumbi wa Bunge Jijini Dodoma leo tarehe 03 Novemba 2023, kutoka kulia ni Mbunge wa Jimbo la Buchosa, Mhe. Eric Shigongo, wa pili kulia ni Katibu mwenezi CCM Kata ya Nianjema Bagamoyo, Mzee Marijani (Minjori.) Waziri wa Maji na Mbunge wa Pangani, Mh. Juma Aweso, Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Mh. Muharami Mkenge,  na wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa CCM kata ya Nianjema ndugu Omar Makamba
..........................................

Na Athumani Shomari- Dodoma

Leo Tarehe 3 November 2023, Mbunge wa jimbo la Bagamoyo, Mheshimiwa Muharami Shaban Mkenge, amemkaribisha Bungeni Mdau wa Maendeleo Jimbo la Bagamoyo Mzee, Rajabu Selemani Mbagala, ikiwa ni nafasi ya kipekee kwa Mzee Mbagala kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo ya Bagamoyo.


Mzee Mbagala ni maarufu kwa wakazi wa Bagamoyo kutokana na kujitolea katika maendeleo ya huduma za jamii hasa ukizingatia ni mtu binafsi ambae hana cheo serikalini bali kinachomsukuma ni utu wake dhidi ya binadamu wenzie na kukereketwa kwake na Maendeleo ya mji wa Bagamoyo.


Miongoni mwa mambo aliyoyafanya katika kusaidia huduma za jamii, Mzee, Rajabu Selemani Mbagala ameweza kutoa eneo la kujenga Zahanati katika kitongoji cha Kimarang'ombe kata ya Nianjema, eneo la kuabudia (Msikiti) eneo la kuzikia (Makabuli) kwa waislamu na wakristo, eneo la kujenga ofisi ya Chama Cha Mapinduzi kata ya Nianjema ambapo maeneo yote hayo ameyapima pamoja na kugharamia michoro (survey plan), kwa fedha zake.


Mzee Mbagala aliweza kumiliki maeneo makubwa ya Ardhi ikiwa mji bado haujakua na baadae maeneo hayo kuyapima viwanja na kufanya maeneo kuwa na mitaa mizuri iliyopimwa kitaalamu jambo ambalo linaleta muonekano mzuri wa mji wa Bagamoyo.


Hali hiyo imepelekea Maeneo kadhaa ya Kitongoji cha Kimarang'ombe kuwa na viwanja vyenye muonekano mzuri wa mitaa ukilinginisha na maeneo ambayo hayajapimwa (unplanned areas).


Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge, amesema anamshukuru mzee Mbagala kwa kujitolea kwake katika mambo mbalimbali ya maendeleo hali inayoleta chachu ya maendeleo Kata ya Nianjema na Bagamoyo kwa ujumla.


Mbunge huyo Muharami Mkenge amewataka wadau mbalimbali wa maendeleo Bagamoyo kuiga mfano wa Mzee Mbagala ili kuisaidia Serikali katika huduma mbalimbali za kijamii.


Katika safari yake hiyo ya Bungemi Mzee Mbagala amesindikizwa na Mwenyekiti wa CCM kata ya Nianjema ndugu Omar Makamba na katibu mwenezi CCM Kata, Mzee Marijani (Minjori.)



ONDOENI WASI, NCHI IMEHIFADHIWA VIZURI-KIKWETE

 

Maneno hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofis ya Rais Utumishi na Utawala Bora baada ya ziara ya Kamati ya kudumu Bunge inayosimamia Utawala , Katiba na Sheria kutembelea idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa , Dodoma.



Akizungumza mbele ya kamati Mhe. Kikwete pamoja na kuishukuru kamati kwa kufanya ziara ameeleza kuwa ofisi yake itasimamia na kutekeleza maelekezo yote kwa kuwa tayari Serikali imeshatoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali katika Idara hiyo na mrejesho utatolewa kwa mujibu wa utaratibu mapema iwezekanavyo.


“Ujio wenu hapa umeambatana na maelekezo muhimu sana kwetu ili kuimarisha shughuli zinazofanywa na Idara hii kwa ustawi wa Serikali na Taifa kwa jumla, nasi tuko tayari kutekeleza maelekezo hayo kwa haraka na ufanisi” alisema Mhe. Kikwete.


Naye Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Bunge, Dkt. Mhagama amemsisitiza Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kuhakikisha ofisi yake inaisimamia vyema Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa katika zoezi la kuhifadhi nyaraka ambazo zimekusanywa hivi karibuni ili ziwe kwenye utaratibu mzuri kama zilivyo nyingine kwa lengo la kuepuka upotevu wowote wa nyaraka hizo.