Tuesday, August 15, 2023

WATUMISHI MADINI WATEMBELEA MGODI WA BULYANHULU

 


Katibu Mkuu Madini aanza Utekelezaji Maazimio

Kahama.


Timu ya Watumishi wapatao 13 kutoka kada mbalimbali za Wizara ya Madini ikihusisha Makatibu Mahususi, Watunza Kumbukumbu na Wahudumu wametembelea Mgodi wa Barrick - Bulyanhulu uliopo Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga.


Ziara hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa maazimio na ahadi alizotoa Katibu Mkuu Wizara ya Madini Kheri Mahimbali wakati wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Wizara hiyo lililofanyika mwezi Mei, 2023, jijini Dodoma.


Aidha, ziara hiyo inalenga kuwajengea uelewa wa pamoja watumishi wote wa Wizara kuhusu shughuli zinazofanywa katika Sekta ya Madini hususan shughuli za uchimbaji wa madini katika migodi mikubwa, ya kati na midogo ili kuwezesha malengo mahususi ya wizara kutekelezwa kwa pamoja kama familia moja ya Madini.


Watumishi hao wamepata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali katika mgodi huo ikiwemo mgodi wa chini (underground mining), sehemu ya uchenjuaji (processing plant) bwawa la huifadhi tope sumu ( TSF) , sehemu ya upokeaji na utunzanji wa vifaa vinavyotumika katika mgodi pamoja na kutembelea miradi ya jamii inayotekelezwa na migodi hiyo kupitia Mpango wa Uwajibikaji wa Migodi kwa Jamii (CSR).


Hili ni kundi la kwanza la watumishi wa kada hizo kutembelea maeneo ya migodi ili kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa. Kundi lingine la watumishi kutoka kada hizo linatarajiwa kutembelea migodi mbalimbali mapema mwezi Septemba.








TUNATAKA KUWA NA MIFUMO MICHACHE YA TAARIFA ZA AFYA INAYOWASILIANA; DKT. SHEKALAGHE


 Na WAF, Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe amewataka wataalam wa TEHAMA kufanyia kazi mifumo ya taarifa ya Wizara ili iweze kuwasiliana na kuwa na mifumo michache yenye kuleta tija na kurahisisha utoaji wa huduma.

Dkt. Shekalaghe amesema hayo alipokuwa akifungua kituo cha umahiri katika masuala ya afya kidigitali Jijini Dodoma.

“Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliagiza kuanza kwa matumizi ya tiba mtandao lakini pia ameelekeza kwamba lazima mifumo yetu ipungue, ninafurahi siku ya leo ni moja ya hatua ya utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Rais. Wataalam wetu wakikaa hapa wataweza kuja na suluhisho la changamoto za mifumo iliyopo na kuwa na mifumo michache yenye tija” amesema Dkt. Shekalaghe

Amesema, kituo hicho cha umahiri katika masuala ya kidigitali (CDH) kitasaidia kuunganisha mifumo ya Sekta ya Afya pamoja na kupunguza mifumo iliyopo katika Wizara ya Afya.

“Kituo hiki kitasaidia kupungua kwa mifumo mingi ambayo haitazidi mifumo Minne au Mitano lakini pia kuwezesha kuunganisha mifumo iliyopo kwa kuweza kusomana ndani ya Wizara ya Afya”, amesema Dkt. Shekalaghe

Vile vile, Dkt. Shekalaghe amesema kuwa taarifa zinazotolewa na kituo hicho ziweze kutumika kwa ajili ya tafiti zitakazotuwezesha kufanya maamuzi mazuri zaidi.

“Tunataka kuwa na taarifa zote kamilifu na muhimu zinazosaidia utoaji wa huduma za matibabu, mtu ukifika hospitalini taarifa zako kuanzia mapokezi, vipimo na matibabu ziweze kuingizwa na kutunzwa kwenye mifumo yetu hii na iweze kuzungumza na kwa kuanzia tayari tunayo AFYA CARE, ambayo ipo tayari kwenye hospitali ngazi ya Mikoa kwenda juu, na GOTHOMIS ambayo inatumika kweney vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi” amesema Dkt. Shekalaghe.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la PATH Bw. Amos Mugisha amesema wamewezesha kukarabati wa kituo hicho, kuweka samani pamoja na vifaa vya kiteknolojia.

Amesema, moja ya umuhimu wa kituo hicho ni kuweza kutengeneza mifumo ambayo inazungumza na kupunguza mifumo mingi iliyopo katika Sekta ya Afya kwa sasa.

Naye, Kaimu Mkurugenzi wa TEHAMA Wizara ya Afya Bw. Silvanus Ilomo amesema kuwa kituo hicho kitatumiwa siyo tu na Wizara ya Afya bali wataalam wengine wa Sekta ya Afya kwa ajili ya kukutana na kuja na mifumo yenye tija katika uboreshaji wa huduma za afya nchini.

“Kituo hiki ni mali ya Serikali, wataalam wote wa Sekta mnakaribishwa kuja kufanya kazi hapa kwa kuwa hii ni Serikali moja na haya ni mafanikio ya Serikali hii”, amesema Bw. Ilimo.






SERIKALI YAWEKA KATAZO LA UWEKAJI WA MIFUKO LAINI KWENYE CHUPA ZA VINYWAJI

Mwandishi Wetu.

Serikali imepiga marufuku matumizi ya mirija ya plastiki na kuweka plastiki laini katika chupa za vinywaji vinavyozalishwa nchini na zinazoingizwa kutoka nje ya nchi,

Akizungumza na Waandishi wa habari katika Ofisi za Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Jijini Dar es Salaam, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais,( Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo amesema Serikali inaelekeza wazalishaji na wasambazaji wa bidhaa hizo kwa kuzingatia umuhimu wa utunzaji wa mazingira.

*"Tunatoa muda baada ya muda huo basi hatutarajii kuona bidhaa zinazalishwa zikiwa na ile karatasi laini kwenye kifuniko". Amesema Waziri Jafo.*

Amesema baada ya miezi sita kumalizika wazalishaji na wasambazaji wa bidhaa wanaelekezwa kuzalisha bidhaa zao bila kuweka plastiki laini nje ya chupa za vinywaji.

*"Bidhaa zinazozalishwa na kuingia sokoni kabla ya katazo hili ambazo muda wake wa mwisho wa matumizi haujafika zitaendelea kubaki sokoni hadi pale muda wake wa matumizi utakapokamilika". Amesema.*

Aidha amesema bidhaa zitakazozalishwa baada ya miezi sita kuanzia tarehe ya katazo hazitaruhusiwa kuingia sokoni.

Pamoja na hayo ameelekeza hoteli, migawaha na maduka ya vinywaji kutotumia mirija ya plastiki kwa kunywea vinywaji baada ya miezi sita kwani mirija hiyo imekuwa inaleta uchafuzi wa mazingira.

"Tunatarajia baada ya miezi sita watu watumie mirija mbadala kuliko kutumia mirija ya plastiki ambayo inafanya uchafuzi mkubwa wa mazingira".Amesema Waziri Jafo.





 

MAGAZETI YA LEO TAREHE 15 AGOSTI 2023.


 











Monday, August 14, 2023

MHE. MAJALIWA : TUUZE KOROSHO ZILIZOBANGULIWA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na wananchi stendi kuu wilayani Newala, akiwa kwenye ziara ya siku mbili mkoani Mtwara Agosti 14, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

............................

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wakulima zao la korosho wafanye kilimo cha kibiashara kwa kuacha kuuza korosho ghafi na badala yake wauze zilizobanguliwa ili kujiongeza tija zaidi.

“Wakati wa kubadilika umefika, tutumie fursa hii kujenga viwanda vya kubangulia korosho na kuwawezesha wakulima kubangua na kuuza katika masoko ya nje na ndani.”

Amesema bei ya kilo moja ya korosho iliyobanguliwa ni takribani shilingi 13,000 na ghafi ni takribani shilingi 2,000, ukibangua kilo nne za korosho ghafi unapata kilo moja ya ya korosho iliyobanguliwa.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatatu, Agosti 14, 2023) wakati akiongea na wananchi wa halmashauri ya Mji wa Newala akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Mtwara.

Amesema kitendo cha kusafirisha korosho ghafi nje ya nchi kinawakosesha baadhi ya mapato yatokanayo na maganda ya korosho ambayo yanatumika kutengeneza mafuta.

Aidha, Waziri Mkuu ametoa wito kwa wamiliki wa viwanda vya kubangua korosho watoe nafasi kwa wakulima kwenda kubangua korosho zao na kuwatoza gharama za ubanguaji.

“Wenye viwanda igeni mfano wa kiwanda cha kubangua korosho cha Organic Growth Limited (OGL) kilichopo Tandahimba ambacho kinaruhusu wakulima kwenda kubangua.”

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, kusimamia utekelezaji wa Mkataba wa Usambazaji wa umeme katika wilaya ya Newala unaotekelezwa na kampuni ya Central Electric International.

Kwa upande wake, Meneja wa TANESCO mkoa wa Mtwara Mhandisi, Tawakal Rwahila Alisema mkandarasi huyo alipaswa kukamilisha kazi hiyo mwezi Apriri 2023.

Mhandisi Rwahila amesema mkandarasi huyo alipewa kazi ya kusambaza umeme katika vijiji 70 vya wilaya ya Newala mwezi Agosti 2021 na amekuwa na utendaji usioridhisha.

Kadhalika, Waziri Mkuu amekukagua maendeleo ya ujenzi wa majengo ya uboreshaji wa utoaji wa huduma za afya katika hospitali ya Mji Newala uliogharimu shilingi milioni 800.










 

MAHAKIMU WATAKIWA KUSHUGHULIKIA MRUNDIKANO WA MASHAURI.


Msajili mkuu wa Mahakama ya Tanzania afungua Mafunzo Elekezi ya Mahakimu Wakazi wapya 37, awataka kushughulikia mrundikano wa mashauri


Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbert Chuma amefungua Mafunzo Elekezi kwa Mahakimu wakazi wapya 37 wa Mahakama za Mwanzo leo tarehe 14/08/2023.


Mafunzo hayo ambayo yameandaliwa na Mahakama ya Tanzania na kuendeshwa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) yanafanyika hapa Chuoni IJA na yatadumu kwa siku tano hadi taehe 18/08/2023.


Katika hotuba yake ya Ufunguzi Mhe. Chuma ambaye alikuwa mgeni Rasmi, amewataka Mahakimu hao kwenda kusaidia kuondoa mrundikano wa mashauri katika Mahakama za mwanzo kama inavyotaka Sera ya Mahakama ya Tanzania. 


“Mpaka sasa bado Mahakama za Mwanzo zinaendelea kuongoza katika umalizaji wa Mashauri na kutokuwa na mrundikano wa mashauri, kwa hiyo tunategemea ongezeko lenu litaendelea kupunguza mzigo kazi wa kila hakimu na hatimaye kuendeleza sera ya Mahakama ya Tanzania inayotaka kutaka kusiwe na mashauri yanayozidi miezi sita,” amesema Mhe. Chuma.


Pia Mhe. Chuma amewataka mahakimu wakazi hao wapya kujifunza matumizi ya Teknolojia ya habari na Mawasiliano(TEHAMA) ili waweze kutekeleza vema majukumu yao hasa wakati huu Mahakama ya Tanzania ikiwa imejielekeza katika eneo hilo la Teknolojia.


“Karne hii ya 21 imetawaliwa na matumizi ya Teknolojia katika kuwahudumia wananchi, jifunzeni matumizi ya mifumo ya TEHAMA inayoendeshwa na Mahakama ili msipate ugumu mnapotekeleza majukumu yenu,” amesisitiza Mhe. Chuma.


Vile vile, Mhe. Chuma amewasisitiza washiriki hao kuwa wanapotekeleza majukumu yao, basi hawana budi kuzingatia misingi ya haki za binadamu, maisha ya watu na ustawi wa usalama wa nchi.


Kwa upande wake Hakimu Mkazi Mkuu na Mkurugenzi wa Mafunzo ya Kimahakama IJA, Mhe. Dkt. Patricia Kisinda amezungumzia umuhimu wa mafunzo hayo kwa kubainisha kwamba yanalenga kuwapatia Mahakimu hao miongozo itakayowasaidia katika utekelezaji wa majukumu yao.


“Kimsingi umuhimu wa mafunzo haya ni kwa ajili ya kuwapatia muongozo Mahakimu wapya ambao wanaenda kuanza majukumu yao katika Mahakama za mwanzo, ukiwemo utoaji wa haki ambao ndio jukumu kubwa la Mahakimu hawa,” amesema Mhe. Dkt. Kisinda.








 

DC NYANGASA ATOA USHAURI WA MAENDELEO YA KISARAWE KATIKA DCC

 


KISARAWE PWANI


Mkuu wa Wilaya kisarawe Bi Fatma Nyagasa ameongoza watalaamu mbalimbali katika kikao Cha Kamati ya ushauri wa Wilaya (DCC) Leo 14.08.2023 


Akizungumza wakati wa kikao kilichoendeshwa kwa Mfumo wa taalamu wa Halmashauri ya Wilaya kisarawe Kutoa ushauri Wao kwa mkuu wa Wilaya jinsi ya kuifikisha Wilaya katika Maendeleo yanayotakiwa kwa Mujibu wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM alisema Imani alonayo ni Kubwa sana kwa jamii hii ya Kisarawe kupata Maendeleo kutokana na ushauri wanaopata kutoka kwao,


*"Hapa kisarawe kuna watalaamu katika fani Nyingi basi tumieni taluma zenu kuwatumikia wananchi ambao mmetumwa kwenu katika kufanya Kazi ikiwemo Elimu,Afya, umeme, Ardhi, Habari nk*"


*"Kupitia taluuma mbalimbali mlizonazo basi zinufaisheni Halmashauri katika kufanya Kazi kwa uzalendo na kujituma kwa weledi alisisitiza Mhe DC Nyangasa*"


Hata Hivyo kwa Upande wake Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Wilaya kisarawe Bi Beatrice Dominic alimhakikishia mkuu wa Wilaya kisarawe kuwa watumishi wote waliopo kisarawe wanafanya Kazi kwa umakini na Ufanisi kwa kuzingatia sheria na kanuni na Kuahidi kuleta matunda Mazuri ya Utumishi,


*"Mhe Mkuu wa Wilaya kwa niaba Yao tukuhakikishie kuwa tunaenda kufanya Kazi kwa umakini na Ufanisi Mkubwa kwa maslahi ya watu wa kisarawe na taifa kwa Ujumla kama ambavyo alimalizia Bi Beatrice*"


Aidha kikao hicho pia kilihudhuriwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya kisarawe Mhe Zuberi kizwezwe, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Komred Halfani Sika, Watalaamu na Wawakilishi wa Tasisi ya Tarura,Ruwasa,Tanesco, TFS, Ardhi,TRA, Nk







 


RAIS SAMIA, CCM, RAI YAO KUONA CHUO HIKI KINAENDA KUFUNDISHA MASOMO YANAOENDANA NA MAZINGIRA YA PWANI -QS KIPANGA

 


NA MWANDISHI WETU


Katika kuelekea hatu za mwisho kwa Mandalizi ya kuanza kwa Masomo katika Chuo Cha Ufundi Veta ndagoni Mkoa wa Pwani Wilaya Mafia, 


Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknologia Mhe Qs Omar Kipanga ametoa ufafanuzi kuwa chuo hicho kinaenda kuwa mkobozi kwa taifa kutokana kwa Vijana wambao watajiunga Kusoma Veta ndagoni,


*"Rai ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa Veta zote nchini ikiwemo hii ya ndagoni ni kuona Wingi wa Vijana wanaenda kupata maarifa yenye faida kwa taifa ikiwemo Kusoma fani zenye masilahi na zinazoendana na wakati huku zikiakisi Mazingira waliopo kwa ufanisi zaidi ikiwemo Kusoma mambo ya Tehama, Mazingira,pamoja na Mambo ya Uvuvi na bahari alisisitiza Mhe Qs Kipanga*"


*"Maudhui ya Chuo hiki ni pamoja na Kutoa Vijana wenye uwezo wa ambao wakitoka hapa hawatasubiri ajira Bali wanajiajiri wenyewe kupitia maarifa waliyoyapata kuendana na uhitaji Wao muda wote wawapo chuoni alisisitiza Mhe Qs Kipanga*"


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mafia Komred Mohamed Faki alifafanua kuwa Wao kama CCM Furaha Yao ni kuona chuo hicho kinaenda kuwa na Fani mbalimbali ambazo zinaenda kumapatia Kijana Uwanda Mpana Sana wa kuchagua Kusoma kulingana na anachokipenda na kinachomfaa,


*"Hiki chuo ni kikubwa kuliko chuo chochote hapa Mafia na kwa Mkoa wa Pwani ni chuo Cha Veta Cha Kwanza kwa ukubwa wa majengo na Fani zinazoenda kufundishwa basi kiendane na ukubwa wake alimalizia Komred Faki*" 


Mkoa wa Pwani una Veta mpaka Sasa katika Wilaya ya Kisarawe, Rufiji,Mafia nk ambazo zinaategemewa kwenda kusomesha Vijana katika Fani mbalimbali ili kuhakikisha Vijana wanatumia 99%ya vipaji na elimu za Ufundi na ubunifu walio nao katika Mazingira na Fani wanazitaka. 






MLIMA KITONGA KUFUNGWA CAMERA.

Jeshi la Polisi Mkoani Iringa kwa kushirikiana na Kamati ya Usalama Barabarani ya Mkoa huo, wapo mbioni kuanza utekelezaji wa mpango kabambe wa kuweka camera za kisasa kwenye maeneo korofi kwenye barabara kuu inayounganisha Mkoa huo na Mikoa mingine na kwa kuanzia camera hizo zitafungwa eneo la Majinja Wilayani Mufindi na Mlima Kitonga Wilayani Kilolo ili kupunguza ajali za barabarani.


Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Barabarani Mkoa wa Iringa, Salim Abri Asas @salimasas amesema hayo wakati kamati yake ikiongozwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa ilipotembelea maeneo kadhaa ambayo ni korofi na yanayoongoza kwa kusababisha ajali nyingi Iringa.


Asas amesema uwekwaji wa camera hizo utasaidia kupunguza ajali barabarani kwasababu zitakuwa zinafanya saa 24 na zikifungwa Polisi katika Ofisi ya RPC, RTO na OCD watakuwa wanaona LIVE kila kinachoendelea Kitonga na kote zilikofungwa, pia amesema Madereva wakijua eneo lina camera watazingatia sheria za usalama barabarani.


Katika ziara hiyo ya siku mbili Kamati hiyo imetembelea Nyang’oro, Mlima Kitonga na eneo la Majinja ambalo lilipewa jina hilo kufuatia ajali ya barabarani iliyohusisha basi la Kampuni ya Majinja Express lililogongana na lori la mizigo na kusababisha vifo vya Watu 50 na wengine 23 kujeruhiwa March 11, 2015