Tuesday, August 8, 2023

DKT. MPANGO ASHIRIKI MKUTANO WA PILI WA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI WA NCHI 25 ZA AFRIKA, WANACHAMA WAZALISHAJI WA ZAO LA KAHAWA

 


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi 25 za Afrika Wanachama Wazalishaji wa Zao la Kahawa unaofanyika Kampala nchini Uganda leo tarehe 08 Agosti 2023.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiongozana na viongozi mbalimbali wa Afrika kuelekea katika Ukumbi wa Mikutano wa Speke Munyonyo uliopo Kampala nchini Uganda kushiriki Mkutano wa Pili wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi 25 za Afrika Wanachama Wazalishaji wa Zao la Kahawa leo tarehe 08 Agosti 2023.




Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiungana na viongozi wengine pamoja na wadau wa zao la kahawa katika kuimba wimbo wa Taif awa Uganda wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi 25 za Afrika Wanachama Wazalishaji wa Zao la Kahawa unaofanyika Kampala nchini Uganda leo tarehe 08 Agosti 2023.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango na Rais wa Uganda Yoweri Museveni wakifuatilia mawasilisho mbalimbali wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi 25 za Afrika Wanachama Wazalishaji wa Zao la Kahawa unaofanyika Kampala nchini Uganda leo tarehe 08 Agosti 2023.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Afrika mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi 25 za Afrika Wanachama Wazalishaji wa Zao la Kahawa unaofanyika Kampala nchini Uganda leo tarehe 08 Agosti 2023.


VIJANA 70 WAFUNGISHWA NDOA NA AL-HIKMA

Jumla ya vijana 70 wasiokuwa na uwezo wa kutoa mahari wamefungishwa ndoa kwa pamoja jijini Dar es Salaam kwa msaada wa Taasisi ya Al hikma Foundation.


Ndoa hizo zimefungwa kwenye ukumbi wa DYCCC, Chang'ombe na kushuhudiwa na maelfu ya watu pamoja na viongozi mbalimbali akiwemo Naibu Spika wa bunge la Tanzania, Mussa Azan Zungu, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu- Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi na Sheikh Mkuu na Mufti wa Tanzania, Sheikh Dkt. Abubakar Zubeir Bin Ally


Mkurugenzi wa Taasisi iliyoratibu ndoa hizo, Al Hikma Foundation, Sheikh Nurdin Kishki amesema kilichowasukuma kuwasaidia vijana hao kwa kuwatolea mahali ni kutokana na gharama za ndoa kuwa juu kulinganisha na uwezo wa maisha yao...


"Tulipokea ujumbe zaidi ya 1000 baada ya kutangaza jambo hili mwezi wa nne, waliojaza fomu za kutaka kusaidiwa kuoa walikua zaidi ya 200 lakini baada ya usaili tumepata 70 ambao leo wameoa", alisema Kishki.


Moja ya vigezo muhimu vilivyotumika kuwapata vijana hao ni nia yao ya kuoa, uwezo wa kumudu ndoa na wale ambao hawaongezi mke wa pili.


Mbali na kupewa nasaha za uvumilivu kwenye ndoa kutoka kwa viongozi karibu wote walioshiriki, mmoja wa vijana aliyeoa leo, Ally Ismail Mwaluka, mlemavu pekee katika kundi la waliooa anasema ni ndoto iliyotimia.


"Sikutarajia, wakati mwaka unaanza sikua hata na ndoto ya kuoa, leo nmeoa bure na nimepata vitu vingine juu kutoka kwa viongozi wa serikali, bajaji, mafuta ya bajaji kwa mwaka mzima na fedha mbalimbali, sina cha kusema namshukuru Mungu", alisema Ally.


Vijana hao wametoka mikoa 12 ya Tanzania bara na Visiwani na mahari waliozosaidia zimegharimu shilingi zaidi ya milioni 70 za kitanzania.



 

WAZIRI JAFO AWAASA WAKULIMA

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akizungumza wakati alipokuwa akitembelea mabanda ya Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Kati yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mjini Morogoro leo Agosti 08, 2023.

........................

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo ametoa wito kwa wakulima na wafugaji kuendelea kutunza mazingira ili shughuli ziwe endelevu.


Amesema hayo wakati akitembelea mabanda ya Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Kati yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mjini Morogoro leo Agosti 08, 2023.


Dkt. Jafo alisema kuwa endapo mazingira yataharibiwa ni dhahiri kuwa sekta za kilimo na ufugaji zitaathirika kutokana na ukame uliosababishwa na shughuli za kibinadamu.


“Ndugu zangu tunapokata miti ovyo na kufanya shughuli za kibinadanu kwenye vyanzo vya maji tunasababisha mito yetu kukauka na mito ikikauka kilimo chetu kinachotegemea mvua hakitakuwa na tija, nawaomba tutunze mazingira,” alisisitiza.


Aidha, Waziri Jafo alipongeza waandaaji wa maonesho hayo yanayojumuisha mikoa ya Morogoro, Dar es Salaam na Pwani maandalizi mazuri ambayo yanatumika kutoa elimu kwa makundi hayo na wananchi kwa ujumla.


Alibainisha kuwa ili kukabiliana na changamoto ya ukame Serikali ya Awamu ya Sita imejipambanua katika uwekezaji kwenye kilimo na mifugo kwa kuhakikusha sekta hizo mbili zinakuwa na tija na manufaa.


Hali kadhalika Waziri Jafo ametoa wito kwa Watanzania kuungana kwa pamoja na kuhakikisha wanalinda rasilimali zilizopo hapa nchini ili ziwe na manufaa kwa jamii nzima.


Kwa upande Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amesema changamoto ya ukosefu wa mvua inatokana na ukataji miti holela hasa katika maeneo ya milima.


Hivyo, amesisitiza kuwa kila mwananchi mkoani humo ashiriki kikamilifu katika zoezi la upandaji miti na huku akiwataka wakulima kuacha kulima kwa kuharibu mazingira.


“Miti imekatwa ndio maana kuna changamoto ya athari za mazingira mvua hazinyeshi kwa wakati au hazinyeshi kabisa na kusababisha mtu anashindwa kupanda na akipanda anapata hasara,“ alisema Malima.


Ili kukabiliana na hali hiyo alisema Kanda ya Mashariki wamekuja na mkakati wa kutengeneza ajenda ya kilimo itakayomsaidia mkulima katika kufanya kilimo endelevu na chenye mafanikio












MAGAZETI YA LEO TAREHE 08 AGOSTI 2023.

 














Monday, August 7, 2023

RAIS DKT SAMIA AWASILI MKOANI MBEYA KWAAJILI YA SIKUKUU YA NANENANE


 Rais wa Jamhuri ya Muungano *Dkt, Samia Suluhu Hassan* leo August 07, 2023 amewasili *Uwanja wa Ndege wa Songwe* kwaajili ya kushiriki maadhimisho ya Siku ya wakulima *(Nanenane)* yatakayofanyika Siku ya Kesho *August 08* Mkoani Mbeya.


Baada ya kuwasili *Mhe. Samia* amepokelewa na kusalimiana na *Viongozi* mbalimbali waliojitokeza Uwanjani hapo kwaajili ya kumpokea.


Maonyesho ya Siku ya Wakulima *Nanenane* kwa mwaka 2023 yameambatana na kauli mbiu isemayo *“Vijana na Wanawake ni msingi imara wa mfumo endelevu wa chakula”.*


Fuatilia mitandao yetu ya kijamii 

Instagram: @mamakajatz

Twitter @mamakajatz

Facebook: Mamakajatz

YouTube: Mama kaja tz 


#Mamakaja






 



HONGERA KISARAWE KWA KUHAKIKISHA HEWA SAFI NA SALAMA DAR ES SALAAM


 MWANDISHI WETU 

 *Morogoro* 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Dkt. Selemani Saidi Jafo amepongeza jitihada zinazofanywa na Halmashauri ya Wilaya kisarawe katika kuhakikisha inatunza Mazingira na kuhakikisha inafuga ngombe vizuri kanda Mashariki,

Mhe. Jafo, ametoa pongezi hizo leo Agosti 7,2023 alipotembelea Banda la Kisarawe kwenye maonesho ya Nanenane kanda ya Mashariki yanayoendelea katika viwanja vya Julius Kambarage Nyerere mkoa Morogoro Kanda Mashariki,

Aidha, ameitaka kisarawe kuendelea kutoa elimu ya utunzaji wa mazingira ikiwa ni pamoja na elimu ya kuzuia shughuli za kibinadamu zinazofanyika pembezoni mwa vyanzo vya maji ili kuepusha kujaa kwa uchafuzi katika msitu wa Kazimzumbwi ambalo ni chanzo mama cha hewa safi kwa wakazi wa Dare es Salaam na Pwani.

Sambamba na hilo amesisitiza juu ya utoaji wa elimu kuhusu athari ya vitendo vya uchomaji moto wa misitu iliyopo katika Milima ya Uluguru ili kuhifadhi mazingira na vyanzo maji Mkoa Morogoro,

Kisarawe inashiriki maonesho ya nanenane huku ikisogeza karibu huduma mbalimbali zinazotolewa na halmashauri hiyo pamoja na utoaji wa elimu ya umuhimu wa utunzaji wa Mazingira na vyanzo vya maji na utumzaji wa Mazingira,kulima Chikichi,kwa wananchi wanaojitokeza katika maonesho hayo pamoja na Kutoa elimu kuhusu ufugaji, Kilimo.


Aidha kwa upande wake mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe Adam malima alifurahishwa na Mdau wa Maendeleo wa Kilimo Cha Chikichi kutoka kampuni ya Ina mwanga na kumtaka abaki Morogoro baada ya Nanenane ili Kutoa elimu ya Kilimo hicho kwa Wakulima wa Morogoro,

Nae kwa upande wake pia Msimamizi wa Inamwanga alikubali Ombi la mkuu wa Mkoa kubaki Morogoro ili Kutoa elimu ya kulima zaidi Chikichi kisasa kwa mwalimu wa mkuu huyo. 

FEDHA ZA MIRADI ZIKAGUSE CHANGAMOTO ZA WANANCHI VIJIJINI

Na WAF- Kagera 

NAIBU Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel ametoa wito kwa Wadau na watendaji wote wa Serikali kuhakikisha fedha zote zinazoingia nchini na zinazotoka Serikalini kupitia ziara za nje za Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan zikatatue changamoto zilizokusudiwa za wananchi katika vijiji kuliko kwenye semina na warsha. 


Dkt. Mollel ametoa wito huo leo Agosti 07, 2023 wakati akizindua kampeni ya ugawaji wa vyandarua katika maeneo yote ya mikoa ya Kagera na Tabora inayoambatana na elimu itayosaidia katika mapambano dhidi ya maambukizi ya Ugonjwa wa Malaria katika mikoa hiyo.


"Niwaasa taasisi zote za Serikali na zisizo za Serikali, Rais wetu anapoenda kuzunguka kwenda kwenye makampuni makubwa na mashirika makubwa duniani ili kutafuta fedha, vipaumbele vyake ni kwenda kumfikia Mtanzania mnyonge kutatua changamoto katika vijiji". Amesema Dkt. Mollel. 


Sambamba na hilo, Dkt. Mollel amewataka Wadau kupunguza semina, warsha na mafunzo na fedha hizo ambazo zimetumika huko zielekezwe katika kuongeza nguvu kutatua changamoto zinazowagusa Watanzania wenye uhitaji ikiwemo changamoto za afya.


Aidha, Dkt. Mollel ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Kagera kutumia vyandarua vilivyo na dawa na kusikiliza vizuri maelekezo na ushauri kutoka kwa Wataalamu wa afya hasa kwenye afua mbalimbali za mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria ili kufanikisha dhamira ya Serikali ya kuutokemeza ugonjwa huo nchini. 


Kwa upande wake mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mhe. Erasto Sima ameomba Serikali kupitia Wizara ya Afya kuupa Mkoa wa Kagera kipaumbele kwenye eneo la rasilimali fedha na watu ili kuhakikisha wanatokomeza ugonjwa wa Malaria kwani Mkoa huo ni moja kati ya mikoa inayoongoza kuwa na maambukizi ya Ugonjwa wa Malaria. 


Pia, amewashauri wananchi kujenga tabia ya kupima ugonjwa wa Malaria kabla ya kutumia dawa ili kuondoa usugu wa dawa, huku akibainisha kama mkoa wataendelea kutekeleza juhudi za mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria ikiwemo kusafisha mazingira na kutoa elimu ya mapambano dhidi ya ugonjwa huo. 


Nae, Mkurugenzi wa afya ,Ustawi wa jamii na lishe OR-TAMISEMI Dkt. Ntuli Kapologwe amesema kama wasimamizi wa Sera watahakikisha Halmashauri zote zinatekeleza ununuzi wa viududu kupitia kiwanda cha Kibaha kwani tayari TAMISEMI imetenga bajeti kwaajili ya ununuzi wa viuadudu hivyo kwenye Halmashauri zote nchini.






 

MAKAMU WA RAIS AWATAKA VIJANA KUWA NA MAADIKI MEMA ILI KUJENGA UAMINIFU.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia viongozi, watoa mada pamoja na vijana mbalimbali wakati akifungua Kongamano la Vijana linalofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma. Tarehe 07 Agosti 2023.

....................................

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa wito kwa vijana hapa nchini kujiepusha na matendo yote yasioendana na maadili ya taifa ili waweze kuaminika katika taasisi za kifedha, katika uongozi pamoja na kuwa raia wema.

 

Makamu wa Rais ametoa wito huo leo Agosti 07 2023 wakati akifungua Kongamano la Vijana la Mkoa wa Dodoma linalofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma. Amesema maadili miongoni mwa vijana wengi yameporomoka ikiwemo kukosa uadilifu na hivyo kujiingiza katika vitendo visivyofaa kama vile matumizi ya madawa ya kulevya, unyang’anyi, mapenzi ya jinsia moja, rushwa na utapeli.

 

Amesisitiza vijana wanapaswa kutambua uadilifu ni mtaji wa kuaminiwa na kufanikiwa hivyo ametoa rai kwa kongamano hilo kujadili kwa kina nafasi na wajibu wa wazazi, walezi, viongozi wa dini, kimila, vyombo vya ulinzi na usalama, vyombo vya habari, mitandao ya kijamii na vijana wenyewe katika kujenga na kutunza maadili ya vijana wa Kitanzania.

 

Halikadhalika Makamu wa Rais ametoa maagizo mbalimbali kwa Halmashauri hapa nchini ili kuwasaidia vijana kujikwamua kiuchumi ikiwemo kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya uzalishaji mali kwa vijana ikiwemo kuanzisha kongani zinazoendana na fursa zilizopo kwenye maeneo, kuwaunganisha vijana na fursa za mitaji, kuhamasisha na kusimamia urasimishaji wa vikundi vya vijana ili viweze kutambulika. 


Maagizo mengine ni pamoja na kutengeneza kanzidata ya vijana na ujuzi au taaluma zao ili kuweza kuwaunganisha na fursa mbalimbali zinazojitokeza, kuhamasisha na kuwezesha vijana kuunda klabu za mazingira na kuunganisha vijana katika uzalishaji ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za kitaasisi zitakazosaidia kutoa ufumbuzi wa changamoto zao.

 

Makamu wa Rais amesema serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ina dhamira njema ya kuona vijana wa Tanzania wanaendelezwa na wanawezeshwa kushiriki katika ujenzi wa Taifa. Amesema Kutokana na dhamira hiyo serikali imeendelea kuwawezesha vijana ili kujiari, kushiriki kwenye shughuli za maendeleo na kuchangia katika pato la Taifa. 


Ameongeza kwamba katika mwaka 2022/2023, Mfuko wa Maendeleo ya Vijana ulitoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 1.88 kwa ajili ya kuwezesha miradi 85 ya vijana katika sekta za kilimo, viwanda na biashara katika halmashauri 28. 


Aidha amesema Serikali ilitoa mafunzo ya ujasiriamali, usimamizi, kurasimisha na kuendeleza biashara kwa vijana 2,497 pamoja na kukamilisha kazi ya kuboresha Mwongozo wa Utoaji mikopo kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana ambapo kwa sasa unatoa mikopo kwa vijana walio katika vikundi, mtu mmoja mmoja na Kampuni.

 

Makamu wa Rais ametoa rai kwa vijana kujitokeza na kushiriki katika juhudi za kukabiliana na uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi kwa ajili ya maendeleo endelevu. Pia amewataka kutumia fursa zitokanazo na uhifadhi wa mazingira kama vile kuanzisha na kuendesha kampuni za ukusanyaji na uzoaji taka, uzalishaji wa funza kutokana na taka kwa ajili ya chakula cha kuku na samaki, biashara ya kaboni, uanzishaji wa vitalu na kufanya biashara ya miche ya miti na ufugaji wa nyuki.

 

Makamu wa Rais amesema Kongamano hilo linapaswa kufanyika katika Mikoa yote nchini ili kuwawezesha vijana kutambua fursa na kutafuta namna ya kutatua changamoto zinazowakabili.

 

Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI Deogratius Ndejembi amesema mara baada ya kupitia upya utaratibu wa utoaji wa mikopo ya asilimia kumi kutoka katika Halmashauri nchini, serikali inatarajia kuanzisha mfumo wa kielekroniki wa uombaji wa mikopo hiyo ambapo itatoa nafasi pia kwa mtu mmoja mmoja mwenye wazo zuri na lenye tija kuweza kupata mkopo pasipo kuwa na kikundi.

 

Awali akitoa taarifa kuhusu Kongamano hilo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule amesema uwepo wa idadi kubwa ya vijana katika mkoa huo umepelekea kufanyika kwa kongamano hilo ili kuwakutanisha vijana hao na kuwaeleza mipango ya serikali na fursa zilizopo kwaajili ya kupata ajira na kujiajiri. 


Pia amesema kusanyiko hilo limelenga kutambua changamoto zinazowakabili vijana na kupata suluhu ya pamoja.

 

Mkuu wa Mkoa ameongeza kwamba baada ya kongamano hilo wanatarajia kupata maazimio ya namna ya kukabiliana na ukosefu wa ajira pamoja na maadili kwa vijana. Amesema kongamano hilo litasaidia katika kukamilisha mpango mkakati wa vijana kwa mkoa Dodoma unaotarajiwa kukamilika mwezi Novemba 2023. 

 

Imetolewa na

Ofisi ya Makamu wa Rais

07 Agosti 2023

Dodoma. 


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwasikiliza vijana waliojiajiri kupitia tehama wa Dodoma Data Tech walionufaika na mkopo wa asilimia 4 kwa vijana kupitia Halmashauri wakati akitembelea mabanda ya mbalimbali alipowasili kufungua Kongamano la Vijana linalofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma. Tarehe 07 Agosti 2023.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya vijana mara baada ya kufungua Kongamano la Vijana linalofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma. Wengine katika picha kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Bara Anamringi Macha, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule, Naibu Waziri Tamisemi Deogratius Ndejembi, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Patrobas Katambi, Mbunge wa Kilosa na mtoa mada wa Kongamano hilo Prof. Palamagamba Kabudi pamoja na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Ally Gugu.



MAGAZETI YA LEO TAREHE 07 AGOSTI 2023.

 

















Sunday, August 6, 2023

FURSA ZA MIFUGO NA UVUVI ZAZIDI KUPAA

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb), (wapili kutoka kushoto) akiangalia baadhi ya mifugo iliyopo kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima (Nanenane) yanayofanyika katika viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya). Wa kwanza kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Daniel Mushi. 

Na. Edward Kondela

Serikali imewaasa wadau wa sekta za mifugo na uvuvi kujisajili na kushiriki vyema katika Mkutano wa Jukwaa la Mifumo ya Chakula Barani Afrika 2023 (AGRF) ili waweze kufungua fursa za kibiashara ndani na nje ya nchi.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) amebainisha hayo (06.08.2023) katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima (Nanenane) yanayofanyika kwenye viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya, ambapo amesema tayari wizara imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali za kuhamasisha wadau wa sekta za mifugo na uvuvi kushiriki katika mkutano huo ambao utafanyika kuanzia tarehe 5 hadi 8 Mwezi Septemba mwaka huu na unatarajiwa kuhudhuriwa na washiriki zaidi ya 3,000 kutoka ndani na nje ya nchi.


Mhe. Ulega amesema mkutano huo wa Afrika utakaofanyika jijini Dar es Salaam unatarajia kufungua fursa mbalimbali za kiuchumi na kuongeza wigo wa mawasiliano ya kibiashara kwa wadau wa ndani na nje ya nchi.


Kuhusu Programu ya Kielelezo “Jenga Kesho Iliyo Bora” BBT – LIFE kwa ajili ya kuwezesha vijana kupata elimu ya vitendo katika unenepeshaji wa mifugo na viumbe vya kwenye maji, Waziri Ulega amebainisha kuwa programu hiyo inafanyika kutokana na maono na maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambapo hadi sasa takriban vijana 240 wapo kwenye mafunzo hayo.


Ameongeza kuwa vijana wanashirikishwa katika hatua zote ikiwemo ya kujenga mabanda na kwenda minadani na kuchagua ng’ombe wazuri ambao wanaweza kunenepeshwa na namna hatua za unenepeshaji zinavyofuatwa ambapo hadi sasa ng’ombe 500 wameuzwa.


Aidha, amesema programu hiyo ilivyo ni kwamba tangu siku ya kwanza kila kijana anajua idadi ya ng’ombe atakaowasimamia na kila anapowauza ule mzunguko faida inayobaki ndiyo atakayoondoka nayo kuanzisha biashara yake na upande wa uvuvi imetolewa elimu juu ya unenepeshaji wa kaa na jongoo bahari pamoja na ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba.


Pia, amesema matumaini ni kwamba Programu ya Kielelezo “Jenga Kesho Iliyo Bora” ni kupanua zaidi program hiyo na kuishusha katika ngazi ya mkoa na wilaya ili ziweze kujiendesha pamoja na kuongeza kundi la vijana kutoka Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ili wapate pia mafunzo hayo.


Kuelekea Uchumi wa Buluu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb), amesema serikali inaenda kuwezesha wavuvi wadogo wadogo kuingia kwenye maji marefu ili waweze kufanya huko shughuli za uvuvi.


Waziri Ulega amebainisha kuwa wavuvi hususan wadogo watawezeshwa boti kupitia mikopo isiyo na riba sambamba na kutumia fursa za uchumi wa buluu kwa kunenepesha jongoo bahari na kilimo cha mwani pamoja na uwepo wa vizimba vya kufugia samaki lengo ni kuongeza uzalishaji kupitia uchumi wa buluu kwa kuwa na ongezeko la samaki katika soko la ndani na nje ya nchi.