Friday, March 1, 2019

Prof. Mohamed Janabi atoa tathimi ya undendaji kazi wa Taasisi ya moyo Nchini, Bodi yasifu


Kuongezeka wa idadi ya wagonjwa wanaofanyiwa vipimo na uzibuaji wa mishipa ya damu ya moyo ambayo imeziba kupitia  mtambo wa Cathlab ni ishara kuwa watu wengi wanahitaji kupata huduma hiyo.
Hayo yamesemwa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi wakati akisoma ripoti ya utendaji kazi wa Taasisi hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu ya Oktoba hadi Desemba kwa bodi ya Wadhamini.
Prof. Janabi alisema tangu kuanzishwa kwa Taasisi hiyo mwaka 2016 hadi 2018 katika mtambo wa Cathlab wameona zaidi  ya wagonjwa 2389 ambao waliwafanyiwa vipimo na kuwazibua  mishipa ya damu ya moyo iliyokuwa  imeziba.
“Kupitia mtambo huu tunafanya upasuaji wa moyo wa  bila kufungua kifua kupitia tundu dogo linalotobolewa kwenye paja.  Kwa mwaka jana pekee tulifanya upasuaji kwa wagonjwa 1056 na kuvunja rekodi katika nchi za Afrika Mashariki na Kati”, alisema Prof. Janabi.
Alisema hivi sasa madaktari wa magonjwa ya moyo kwa watoto kupitia mtambo huo wa Cathlab  wameanza  kuziba matundu na kuzibua mishipa ya damu iliyoziba.
“Kipindi cha nyuma watoto walikuwa wanafanyiwa upasuaji huu na madaktari wageni hii ilitokana na kutokuwa na daktari wa kutoa huduma hiyo katika Taasisi yetu. Mwaka jana daktari wetu mmoja aliyekuwa anasoma Afrika ya Kusini amerudi baada ya kumaliza masomo yake na anafanya upasuaji siku ya Jumatano”,.
“Tumetenga siku moja kwa wiki ambayo ni jumatano watoto wanafanyiwa upasuaji wa kuziba matundu na kuzibua mishipa ya damu iliyoziba, uhitaji ni mkubwa na mtambo uliopo ni mmoja. Kuna haja ya kuwa na mtambo mwingine wa Cathlab ili wagonjwa wengi wenye uhitaji wa huduma hii waweze kuipata”, alisema Prof. Janabi.
Katika hatua nyingine Prof. Janabi alisema mwezi wa sita mwaka huu Madaktari Afrika kutoka nchini Marekani watakuja nchini kupanda  mlima Kilimanjaro kwa ajili ya kuchangia fedha za matibabu ya magonjwa ya moyo kwa watoto.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Prof. William Mahalu aliipongeza menejimenti na wafanyakazi wote wa Taasisi hiyo kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kutoa huduma ya matibabu ya magonjwa ya moyo.
Prof. Mahalu ambaye pia ni daktari bingwa wa upasuaji wa  moyo na mishipa ya damu alisema kufanya vizuri kwa mtambo wa Cathlab kunaonesha kuwa watu wengi  wanahitaji huduma hiyo na wao  kama bodi wameona  kunahaja ya kuongeza mtambo wa pili wa Cathlab ili wagonjwa wengi wapate huduma hiyo.
“Mmetuambia hivi karibuni mmesaini mkataba wa makubaliano ya  kuletwa kwa wagonjwa kutoka nchi ya Malawi na Visiwa vya Zanzibar kwa ajili ya matibabu, hongereni sana. Endeleeni kufanya kazi kwa bidii na kujituma ili watu wengi zaidi wafaidike na huduma mnayoitoa”, alisema Prof. Mahalu.
Alisema miaka minne au mitano ijayo wataalamu kutoka nje ya nchi  wanaokuja  kufanya kambi maalum za matibabu ya moyo watakuja nchini kujifunza  kutoka kwa watanzania  baada ya wao kuja kutoa msaada.
Prof. Mahalu alimalizia kwa kuwataka wataalamu wa magonjwa ya moyo kufuatilia maendeleo ya  wagonjwa wanaotibiwa katika Taasisi hiyo pindi wanaporuhusiwa kurudi nyumbani.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. William Mahalu akizungumza jambo na wafanyakazi wa maabara alipotembelea maabara hiyo kwa ajili ya kuangalia mashine mpya za uchunguzi wa vipimo vya magonjwa ya moyo zilizofungwa. Watatu kulia kutoka kwa Prof. Mahalu ni mjumbe wa bodi Dkt. Donan Mbando.
Watoto wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa wanacheza gemu kama walivyokutwa  na mpiga picha wetu. Watoto wawili kati yao wamefanyiwa upasuaji wa bila kufungua kifua  na wawili wanasubiri kufanyiwa upasuaji wa moyo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. William Mahalu na mjumbe wa bodi hiyo Dkt. Donan Mbando wakitoka kuangalia wodi mpya ya watoto wenye magonjwa ya moyo ambayo imejengwa na kufanyiwa ukarabati.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. William Mahalu na mjumbe wa bodi hiyo Dkt. Donan Mbando wakiangalia chumba cha wagonjwa walioko katika uangalizi maalum (ICU) kilichopo katika wodi  mpya ya watoto wenye magonjwa ya moyo ambayo imejengwa na kufanyiwa ukarabati. Chumba hicho kikianza kufanya kazi kitakuwa na vitanda nane na kuweza kurahisisha kutoa huduma kwa watoto wanaohitaji matibabu  ya dharula.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. William Mahalu akiangalia (medical gas bed head panel) mahali pa kuchomeka mashine ya kutolewa hewa ya matibabu  kwenda kwa mgonjwa  katika wodi mpya ya kulipia ya watoto wenye magonjwa ya moyo ambayo imejengwa na kufanyiwa ukarabati. 
Picha na JKCI

Ratiba rasmi ya kuaga mwili wa Ruge, Dar es salaam Kesho Jumamosi March 2

Mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba umewasili nchini leo mchana, 1, Machi, 2019.

Mwili wake unatarajia kuagwa Jumamosi, 2 Machi, 2019 katika ukumbi wa Karimjee, Jijini Dar es salaam kabla ya kusafirishwa mkoani Kagera kwaajili ya mazishi yatakayofanyika Jumatatu, 3 Machi, kijijini kwao Kiziru wilayani Bukoba.

Hii hapa ni ratiba rasmi ya kuuaga mwili wake.


Advertisemen

MWILI WA RUGE WAWASILI DAR ES SALAAM.

Mwili wa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group, Ndugu Ruge Mutahaba umewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ukitokea Afrika Kusini alikokuwa akipatiwa matibabu.
Aliyeongoza mapokezi ya Mwili wa Ruge Mutahaba ni Waziri January Makamba akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es aalaam Paul Makonda pamoja na Mkurugenzi wa Clouds Media Group Bw. Joseph Kusaga.

LOWASA AREJEA CCM RASMI

Image may contain: 9 people, people smiling, people standing
Waziri Mkuu mstaafu Edwardi Lowasa leo tarehe 1 Machi amerejea CCM rasmi na kupkelewa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa Dkt. John Magufuli katika ofisi ndog za chama hicho zilizopo Lumumba jijini Dar es Salaam.


Akizungumza wakati wa kumpokea Dkt. Magufuli alisema CCM imepokea mawazo ya Lowasa ya kurejea CCM kwakuwa ndio nyumbani.


Alisema Lowasa ni mkongwe kwenye CCM na anajua mambo na kwamba alijamia CHADEMA kutokana na mambo ambayo hayakuweza kuzuilika.


Katika hafla hiyo fupi ya kumpkea Lowasa ilihudhuriwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Dkt. John Magufuli, Makamo Mwenyekiti CCM Mzee Philipo Mangula, Katibu Mkuu Dkt. Bashiru Ally Katibu Mwenezi na uenezi Hamphrey Polepole na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kasim Majaliwa.

Vodacom, TPB kuwawezesha wanachama wa Vicoba kutunza fedha kidijitali


  • Wamezindua huduma ya  mtandaoni ya M-Koba iliyounganishwa na M-Pesa inayotoa fursa ya kuhifadhi fedha kwa usalama na uwazi.
  • Inatarajia kuondoa changamoto za upotevu wa fedha na kuimarisha mitaji ya vikundi hivyo.
Dar es Salaam. Wanachama wa vikundi vya kifedha vya kijamii (Vicoba), vikundi rasmi na visivyo rasmi maarufu kama ‘upatu’ sasa wamepata suluhu ya kuhifadhi fedha zao baada ya kampuni ya mawasiliano ya simu ya Vodacom kwa kushirikiana na benki ya Posta Tanzania (TPB) kuzindua huduma ya mtandaoni inalotoa suluhisho la utunzaji fedha kidijitali.
Huduma hiyo, iliyopewa jina la M-Koba, iko chini mfumo wa huduma za kifedha kwa njia ya simu wa M-Pesa, itawezesha vikundi hivyo kutunza fedha kidijitali kwa usalama na uwazi zaidi.
Kaimu Mkurugezi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Hisham Hendi aliyekuwa akizungumza katika uzinduzi huo leo (Februari 28, 2019) jijini Dar es Salaam, amesema huduma hiyo itakuwa endelevu na kukidhi mahitaji ya vikundi vya kifedha kupata eneo salama la kutunza fedha na kuimarisha mitaji yao.
"Huduma hii ya kidijitali inalenga kutoa huduma endelevu ambayo itatumiwa na kufikia vikundi vilivyopo maeneo mbalimbali nchini kwa njia ya mtandao mkubwa wa Vodacom, "amesema Hendi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Vodacom, inakadiriwa kuwa asilimia 16 ya watanzania (zaidi ya watu milioni 4.4) wengi wao wakiwa wanawake, ni wanachama wa vikundi zaidi ya 50,000 vya kuweka akiba na mikopo (Vicoba) ambao huhifadhi akiba zaidi ya Sh100 bilioni kwa mwaka.
Pia kuna vikundi visivyo rasmi zaidi ya 50,000 visivyo rasmi vya wahitimu wa vyuo, wafanyakazi na wanafamilia ambao wanatumia mitandao ya kijamii kuweka akiba na kukopa.  
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom Tanzania, Hisham Hendi wa kwanza kulia akishirikiana na viongozi wengine kuonesha jarida la M-Koba wakati wa hafla ya kuzindua huduma ya M-Koba, huduma ya kwanza na ya kipekee nchini kwa ajili ya vikundi vya kuweka akiba nchini Tanzania.Picha|Vodacom.
Afisa Mtendaji mkuu wa TPB,  Sabasaba Moshingi amesema huduma hiyo inalenga kuongeza theluthi moja ya idadi ya watu waliosajiliwa katika mifumo rasmi ya kifedha na zaidi kuwafikia wanawake wa vijijini ambao wanajihusisha na shughuli hizo. 
“Kama taasisi ya kifedha, tunatambua umuhimu wa vikundi hivi na ndiyo sababu tumeshirikiana na vinara hawa wa sekta ya simu kuleta suluhisho hili la kidijitali ambalo litarahisisha kutunza akiba na kuwezesha watu kufikia malengo yao," amesema Moshingi


Naye Mwenyekiti wa mojawapo wa Vicoba aliyehudhuria uzinduzi huo, Abdallah Mkenga amesema huduma hiyo limekuja wakati mwafaka kwa sababu itawasaidia kutatua changamoto za utunzaji fedha. 
“Sasa tuna mfumo salama zaidi wa vikundi vyetu na tunachanga kwa uwazi kwani mfumo huu unaruhusu kuonekana kwa shughuli za kikundi," amesema Mkenga.
Kutokana na umuhimu wake katika jamii, Vicoba vimejumuishwa katika Sheria mpya ya Huduma Ndogo za Fedha ya Mwaka 2018 ambapo sheria hiyo imeweka utaratibu wa kuiwezesha Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kutoa elimu kwa watumiaji wa huduma ndogo za fedha hususan vikundi vya kijamii kwa lengo la kunufaika na fursa zilizopo.
Vicoba,wakopeshaji binafsi na asasi za kijamii vinaingia katika daraja la nne la sheria hiyo ambapo Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango wakati wa kupitisha sheria hiyo bungeni mwaka jana alisema vikundi hivyo viitaandaliwa kanuni na miongozo mahsusi kwa ajili ya kusimamia daraja hilo.

IGP SIRRO APANGUA PANGUA MAKAMANDA WA POLISI...RPC SHINYANGA ASUKUMWA MAKAO




Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro amefanya mabadiliko ya kiuongozi kwa maofisa wa jeshi hilo baada ya Rais John Magufuli kufanya uteuzi wa makamishna wapya.


Akizungumza na vyombo vya habari leo Machi Mosi, IGP Sirro amewataja makamishna walioteuliwa na Rais Magufuli kuwa ni Charles Mkumbo ambaye anakwenda kuongoza kamisheni ya intelijensia na Liberatus Sabas ambaye anakuwa mkuu wa operesheni na mafunzo.
Wengine ni Leonard Lwabuzala ambaye ataongoza kamisheni ya fedha na logistics na Benedicto Wakulyamba ambaye anakuwa mkuu wa kamisheni ya utawala na menejimenti ya utumishi na Shaaban Mlai ambaye ataongoza kamisheni ya maabara ya uchunguzi wa kisayansi.
Mbali na makamishna hao, Sirro amefanya mabadiliko ya kiutawala kwa maofisa wa jeshi hilo; James Mushi ambaye alikuwa kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma anakuwa Mkuu wa Chuo cha Polisi (CCP) Moshi wakati RPC wa Njombe, Renata Mzinga akirudishwa Makao Makuu.
Sirro amewataja makamanda wapya wa mikoa kuwa ni Amon Kakwale (RPC wa Temeke), Jonathan Shana (RPC Arusha), Marwa Mahiga (RPC Ruvuma), Salum Hamduni (RPC Njombe) na Zuberi Chembela (RPC Ilala).
Viongozi wengine waliohamishwa vituo vya kazi ni Mihayo Nsekela (ofisi ya operesheni na mafunzo), Simon Haule ambaye alikuwa RPC wa Shinyanga anarudishwa Makao Makuu na Yusuph Sarungi ambaye alikuwa RPC Songwe anakuwa mkuu wa kitengo cha kushughulikia wizi wa mifugo (SPU).
Benedict Mapugila ameteuliwa kuongoza kikosi cha bandari wakati Michael Marwa anapelekwa makao makuu Zanzibar. Sirro amesema Albert Nyamhanga na Nsato Marijani wanakwenda Idara ya Wakimbizi ambayo iko chini ya Idara ya Uhamiaji.