Tuesday, February 12, 2019

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA

Mnamo tarehe 11.02.2019 majira ya saa 23:45 usiku huko eneo la Soweto, Kata ya Ruanda, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya. Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lilikamata gari lenye namba za usajili T.937 CKD aina Toyota Saloon likiwa na vipodozi vya aina mbalimbali vilivyopigwa marufuku nchini. Vipodozi vilivyokamatwa ni:-

1.   Extra Clair katoni nane [08].
2.   Perfect White katoni mbili [02].
3.   Epiderm Cream dazani arobaini na saba [47]
4.   Diproson dazani ishirini na moja [21]
5.   Coco Pulp katoni mbili [02]
6.   Carolight katoni sita [06]
7.   Citro Light katoni tatu [03]
8.   Teint Clair katoni mbili [02]
9.   Top Lemon katoni nne [04]
10.                Clair Men katoni mbili [02]
11.                Princes Clair katoni nne [04]
12.                Movet boksi mbili [02]
13.                Miki Clair katoni mbili [02]
14.                Top Clair Plus katoni moja [01]
15.                Collagen formula boksi mbili [02]
16.                Mont Clair boksi mbili [02]
17.                Movet tube pcs mbili [02]
18.                Movet boksi mbili [02]
19.                Cocoderm boksi moja [01]

KUPATIKANA NA VIPODOZI VILIVYOPIGWA MARUFUKU NCHINI.

Mnamo tarehe 12.02.2019 majira ya saa 07:15 asubuhi huko eneo la Check Point Igurusi, Kata ya Igurusi, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali na Mkoa wa Mbeya, Polisi wakiwa doria walimkamata SAID IDDY @ MOHAMED [32] Dereva na Mkazi wa Mbadula Arusha akiendesha gari lenye namba za usajili T.298 DCH aina ya Scania Basi la abiria – HAJI’s akitokea Mbeya kuelekea Arusha akiwa na vipodozi vilivyopigwa marufuku nchini aina mbalimbali.

Vipodozi vilivyokamatwa ni:-

1.   Diana Boksi mbili [02].
2.   White Max Boksi tatu [03].
3.   Secret White Location Boksi moja [01]

Upelelezi unaendelea na mara baada ya kukamilika, mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani.

KUPATIKANA NA SILAHA [GOBORE] BILA KIBALI.

Mnamo tarehe 11.02.2019 majira ya saa 14:35 mchana huko eneo la Makasini – Uyole, Kata ya Uyole, Tarafa ya Iyunga, Jiji na Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi walimkamata PAUL ABRICK [66] Mkazi wa Mtaa wa Nyahoro – Uyole akiwa na silaha Gobore aina ya Tower yenye namba 1878 bila kibali. Upelelezi unaendelea.

Sunday, February 10, 2019

MKOA WA LINDI NA KAMPENI YA KUZUIA MIMBA KWA WANAFUNZI.

Na HADIJA HASSAN, LINDI.

Kutokana na tatizo la mimba kwa watoto wa kike wa Mkoa wa Lindi  kuwa kumbwa, Mkoa huo umezindua  kampeni maalumu ya kupinga mimba za utotoni   ambayo inajulikana kwa jina la “msaidie ,akue,asome Mimba Baadae


Uzinduzi huo ulifanyika February 9 mwaka katika Viwanja vya shule ya Msingi Mpilipili katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi uliambatana na maandamano ya wanafunzi kutoka katika shule mbali mbali za msingi na sekondari za manispaa hiyo yaliyongozwa na wanawake viongozi  waliofanikiwa wa Mkoa huo,


Katika Maandamano hayo  baadhi ya wanafunzi hao walionekana wakibeba mabango yenye ujumbe unaosomeka  “niache nisome mimba baadae,  mzazi /mlezi nitunze  nitimize ndoto zangu nataka shule sio mimba , miba baadae.


Mambango mengine yalikuwa yakisomeka “Vyukuvyuku hata kwetu vipo, nifanye kama mwanao nami nina ndoto, huoni hata aibu tafuta saizi yako, kuitwa nanunu mimi bado  pamoja  na niite dada hayo yote yakiwalenga wanaume wenye tabia ya kuwaraghai mabiti wadogo kimapenzi na hatimae kuwapa ujauzito


Akitoa  Taarifa ya kampeni hiyo  Katibu Tawala wa Mkoa Huo Bi, Rehema Madenge  alisema  kuwa Lengo  kuu la Kampeni hiyo ni kuimarisha mifumo ya ulinzi kwa Watoto kuanzia ngazi ya kaya hadi mkoa kwa kuwajengea uwezo wataalamu wanaoshughulikia masuala ya ulinzi na usalama wa watoto


Kutoa  Huduma kwa wahanga  wa mimba za Utotoni  ambapo huduma endelevu kwa watoto waliopata mimba na kuhakikisha Afya bora kwa watoto watakao zaliwa ikiwa ni pamoja na ufuatiliaji wa mashauri ya watoto na kuwapatia msaada wa kisaikolojia watoto waliopata mimba


Alitaja lengo linguine la kampeni hiyo kuwa ni kusimamia na kuchukuwa hatua za makusudi katika kuzuia mimba za utotoni kwa kufanya mikutano ya kutoa elimu na kuwajengea uwezo watoto, wazazi, walezi na wadau juu ya madhara ya mimba za utotoni kwa kuhusisha vyombo vya habari na kutumia elimu ya sanaa


 Madenge alisema katika Mkoa huo ongezeko la mimba za utotoni linauhusiano mkuwa na malezi duni ya wazazi ama walezi ambapo wazazi wengi wa maeneo hayo hawako makini katika kufuatilia malezi na makuzi ya watoto wao.


Hata hivyo madenge alisema kuwa jambo hilo uwafanya watoto hao kuwa huru, kufanya wanachokitaka, kucheza katika mazingira hatarishi ambako wanakuwa wanajifunza mambo mengi yasiyostahili kwa umri wao.


“ukiangalia kwa kiasi kikubwa jambo hili upelekea kumomonyoka kwa maadili, na mwisho wake watoto hawa upata mimba wakiwa katika umri mdogo” alifafanua Madenge


Akizindua kampeni hiyo Mkuu wa Mkoa Lindi, Godfrey Zambi ameziagiza shule zote za Msingi na Sekondari za Mkoa huo kujiwekea utaratibu wa kuwapima mimba wanafunzi mara tatu kwa mwaka , pamoja na kumtaka Mganga Mkuu wa Mkoa huo kuhakikisha anakuwa na vifaa vya kutosha kwa ajili ya kutekeleza agizo hilo


Hata hivyo Zambi aliagiza kuchukuliwa kwa hatua kali ikiwa pamoja na kuwaweka ndani wazazi wa watoto wa alieweka na aliewekwa mimba pamoja na kijana wa kiume ili kutoa fundisho kwa wazazi wasiowalea vyema watoto wao pamoja na vijana wenyetabia ya kuwataka kimapenzi watoto wadogo


Nae katibu tawala msaidizi utawala rasilimali watu wa mkoa huo DKT, Bora Haule aliyataja baadhi ya matarajio ya kampeni hiyo kuwa ni kuisha kabisa kwa tatizo hilo la mimba kutokana na kuimarika kwa mifumo ya ulinzi na usalama wa mtoto,kuongezeka kwa uwezo wa jamii katika kusimamia na kuchukua hatua kuzuia mimba za utotoni.


Mengine ni wadau wote kushiriki katika vita juu ya kutokomeza mimba za utotoni , kuwepo na ufahamu juu ya athari za mimba za utotoni kwa wanajamii wa lindi pamoja na huduma za Afya kutolewabila kikwazo kwa watoto wote walopata mimba na watoto waliowazaa


Hayo ni baadhi ya mabango yaliyobebwa na wanafunzi kama yanavyoonekana yakiwa na ujumbe wa aina mbalimbali unaopinga mimba katika umri mdogo kwa wanafunzi.
 
 Hayo ni baadhi ya mabango yaliyobebwa na wanafunzi kama yanavyoonekana yakiwa na ujumbe wa aina mbalimbali unaopinga mimba katika umri mdogo kwa wanafunzi.