Thursday, December 13, 2018

RAIS DKT. MAGUFULI PAMOJA NA WAZIRI MKUU WA MISRI DKT. MOSTAFA MADBOULY WASHUHUDIA UTIAJI SAINI WA MKATABA WA UJENZI WA MRADI WA KUZALISHA UMEME MEGAWATI 2100 KATIKA MTO RUFIJI, IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly wakishuhudia utiaji saini wa Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme megawati 2100 katika mto Rufiji kati ya Waakilishi wa Kampuni ya J.V Arab Contractors/El Sewedy Electric pamoja na Waakilishi wa Shirika la Umeme nchini Tanesco.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly wakishuhudia utiaji saini wa Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme megawati 2100 katika mto Rufiji kati ya Waakilishi wa Kampuni ya J.V Arab Contractors/El Sewedy Electric kushoto pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Waakilishi wa Shirika la Umeme nchini Tanesco Dkt. Tito Mwinuka wapili kutoka kulia akifatiwa na Mwanasheria wa Shirika hilo Isdori Nkindi
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya Mazungumzo na kushuhudia utiaji saini wa Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme megawati 2100 katika mto Rufiji.
B
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly, Waziri wa Nishati Medard Kalemani wakipiga makofi wakati waakilishi wa Kampuni ya J.V Arab Contractors/El Sewedy Electric kushoto pamoja na Waakilishi wa Shirika la Umeme nchini Tanesco wakionesha vitabu vya mikataba hiyo Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly akizungumza na wageni mbalimbali Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya kushuhudia utiaji saini Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme megawati 2100 katika mto Rufiji.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi mara baada ya kushuhudia tukio la kihistoria la utiaji saini Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme megawati 2100 katika mto Rufiji ambao utagharimu zaidi ya kiasi cha Shilingi za kitanzania Trilioni 6.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly kabla ya tukio la la kihistoria la utiaji saini Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme megawati 2100 katika mto Rufiji ambao utagharimu zaidi ya kiasi cha Shilingi za kitanzania Trilioni 6.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma, Spika wa Bunge Job Ndugai pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Bashiru Ally.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuonesha picha ya mlima Kilimanjaro Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly kabla ya kumkabidhi zawadi ya picha hio.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati wakielekea kwenye Ukumbi wa Kikwete Hall kwa ajili ya hafla ya utiaji saini Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme megawati 2100 katika mto Rufiji ambao utagharimu zaidi ya kiasi cha Shilingi za kitanzania Trilioni 6.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na  mgeni wake Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly wakati wakielekea kwenye Ukumbi wa Kikwete Hall kwa ajili ya hafla ya utiaji saini Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme megawati 2100 katika mto Rufiji ambao utagharimu zaidi ya kiasi cha Shilingi za kitanzania Trilioni 6.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma, Spika wa Bunge Job Ndugai pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Bashiru Ally. Wengine katika picha mstari wa nyuma ni Mawaziri kutoka Tanzania na Misri.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakary Zubeiry mara baada ya hafla ya utiaji saini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Waziri Mkuu wa Misri Mostafa Madbouly katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma, Spika wa Bunge Job Ndugai pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Bashiru Ally pamoja na Viongozi mbalimbali wa Dini.
 
Askofu Josephat Gwajima akisali kabla ya hafla hio kuanza. PICHA NA IKULU

WAISLAMU MWANZA WAADHIMISHA MIAKA 50 YA BAKWATA KWA KUCHANGIA DAMU

 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya BAKWATA Mkoa wa Mwanza Nurdin Mbaji akishiriki kuchagia damu kwenye maaadhimish ya miaka 50 ya baraza hilo.
 Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Mwanza Alhaji Sheikh Hasani Musa Kabeke akizungumza na waumini wa dini ya Kiislamu wakati wa kuchangia damu kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya BAKWATA  yaliyofanyika kimkoa jijini Mwanza juzi.
.................................................


NA BALTAZAR MASHAKA, MWANZA.

WAUMINI wa Dini ya Kiislamu wameadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kwa kuchangia damu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza, Sekou Toure.

Akizungumza kwenye maadhimisho hayo na wakati wa uchangiaji damu Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Mwanza Alhaji Hassan Musa Kabeke alisema Waislamu waone fahari kujitolea kuchangia damu ili kuokoa maisha ya watu wenye mahitaji ya damu.

Alisema takwimu zinaonyesha waathirika na wahitaji wakubwa ni watoto chini ya miaka mitano,akina mama wajawazito wanaojifungua na majeruhi wa ajali mbalimbali zikiwemo za pikipiki maarufu bodaboda.

Alieleza kuwa ajali zina mchango mkubwa wa mahitaji ya damu na kuwataka watumiaji wa vyombo vya moto hasa pikipiki kutii sheria ili kupunguza ajali, vifo na majeruhi kwani jamii inataka kuona Mwanza na Tanzania salama isiyo na ajali.

“Tuliamua kuadhimisha siku hii kwa kuangalia wenye mahitaji na jambo linalotuunganisha ni damu.Wenye mahitaji makubwa wa damu ni akina mama wanaojifungua , watoto wadogo na majeruhi na tunasaidiana katika kumcha Mungu kwa kufanya mema badala ya dhambi,” alisema
Kaimu sheikhe huyo aliwataka waislamu wa taasisi zote kujipanga na kufanya kazi ya kuhudumia jamii na waone umuhimu wa kujitolea kwa Mungu na umma wa waislamu wenyewe na  hivyo kushiriki  kujitolea damu ni kutoa nafsi na mwili kuwasaidia wengine wenye mahitaji ya damu.

Aidha, Sheikh Kabeke alimpongeza Mufti wa Tanzania Abubakar  Zuberi Bin Ali kwa kuasisi maadhimisho ya kuzaliwa kwa BAKWATA ili kujitathmini na kujipima kama malengo yake yametimia au la, ingawa pia watangulizi wake walifanya mambo mazuri.

Alieleza zaidi  kuwa wapo watu wanapotosha kwa kueneza maneno yasiyo sahihi kuwa BAKWATA ilinzishwa na Mwl Nyerere kwa maslahi ya Ukristo na kuonya wanaofanya hivyo wanawavunjia heshima masheikh waliokiasisi chombo hicho cha Waislamu.

“Jambo hili linapoachwa kuzungumzwa linapotea.Masheikh hao walikutana Iringa kujadili na kuanzishwa kwa BAKWATA lakini leo watu wanapotosha ukweli huo.Sheikh Amin Abdallah aliombwa awe Mufti wa kwanza, lakini alikuwa mtu wa kujishusha na sababu ya uzee na busara alimpendekeza Hemed Bin Jumaa Bin Hemed awe Mufti wa Tanzania,”alifafanua sheikh Kabeke.

Pia alitumia fursa hiyo kumpongeza Rais John Magufuli kwa kuadhimisha miaka 57 ya Uhuru na kwamba uamuzi wake wa kuzuia fedha za sherehe za Uhuru na kuelekeza zitumike kwa shughuli za maendeleo kwa manufaa na maslahi ya Watanzani wote ni jambo la fahari.

 “Rais Magufuli kazi yake inaonekana na jinsi anavyosimamia rasilimali za nchi na nidhamu serikalini hakuna Mtanzania asiyejua maana nchi ilifikia pabaya.Fedha za sherehe za Uhuru hapa Mwanza zimejenga barabara hivyo hatuna budi kumpongeza,lakini pia wazee wetu wa Kiislamu,”alisema

Naye mgeni rasmi Mratibu wa Mabalozi wa Usalama Barabarani Kanda ya Ziwa Abel Ntahorutoba aliziasa taasisi za dini mbalimbali kujenga utamaduni wa kuchangia damu ili kuokoa maisha ya  watua huku akikemea tabia ya waendesha pikipiki kuvunja sheria badala utii bila shuruti.

Alisema mabalozi wa usalama barabarani wataendelea kuwaelimisha watumiaji wa barabara, abiria na madereva wa vyombo vya moto ili kuwafanya Watanzania kuziishi sheria na kuzitii ili kuwa na Tanzania salama isiyo na ajali.

“Tuwe na akiba ya damu na ni muhimu tukajenga tabia ya kuchangia damu, hivyoa kwenye nyumba za ibada tuwaeleze waumini wetu kuwa damu hainunuliwi na hakuna anayefahamu thamani yake.Lakini pia tuziogope ajali ambazo zinauawa kuliko UKIMWI,”alisema Ntahorutoba.

Kwa upande wake Katibu wa Hospitali ya Sekou Toure Leah Lint aliwapongeza waumini hao wa dini ya Kiislamu kwa mchango wao wa damu kwani wameokoa maisha ya watu wengi na kushauri taasisi zingine ziige kitendo hicho ambacho kinawafairiji pia wagonjwa.

“Wagonjwa wamefarijika kwa damu hiyo,hivyo kitendo hiki kikasambae kwa Watanzania wengine ili nao waige mazuri mnayofanya kwa kuwa uchangiaji huu una maslahi mapana kwa jamii,”alisema Lint.
 Afisa Eimu wa Dini ya Kiislamu Abdi Musa pamoja na waumini wa dini hiyo wakichangia damu kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou Toure juzi.
 Katibu Muhtasi wa BAKWATA Mkoa wa Mwanza aliyehamika kwa jina moja la Sikitu akichangia damu siku ya maadhimisho ya miaka 50 ya BAKWATA mkoani hapa. Wa kwanza kulia ni Katibu wa JUWAKITA Dotto Mangu.
 Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Mwanza na Mratibu wa Mabalozi wa Usalama Barabarani Abel Ntahorutoba (kushoto) wakichangia damu kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza, Sekou Toure.
 Mgeni rasmi wa zoezi la kuchangia damu kwa waumini wa dini ya kiislamu jijini Mwanza, Mratibu wa Mabalozi wa Usalama Barabarani Kanda ya Ziwa Abel Ntahorutoba akizungumza kwenye zoezi hilo wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya BAKWATA.

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII,MHE.KANYASU ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA KISIWA CHA LUBONDO

 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu (kulia) akipewa maelezo kutoka kwa Mkuu wa Hifadhi ya Kisiwa cha Rubondo, Ignas Gara (katikati) mara baada ya kuwasili katika hifadhi ya kisiwa hicho ambapo  ambapo aliweza kuzungumza na watumishi wa Hifadhi hiyo iliyopo wilayani Chato mkoani Geita. Kushoto ni Afisa wanyamapori wa Hifadhi hiyo, Emmanuel Kaaya.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akiwa pamoja na Mkuu wa Hifadhi hiyo, John Gara (kulia) wakiangalia baadhi ya picha kwenye simu ya Sokwe wakati Naibu Waziri huyo alipofanya ziara katika hifadhi ya Taifa  ya kisiwa cha Rubondo, Kushoto ni Katibu wa Naibu Waziri huyo,Bw. Zulu Ng’ondya.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu (katikati) akiwa pamoja na Mkuu wa Hifadhi hiyo, John Gara (kulia) wakiwa kwenye boti wakivuka  wakati Naibu Waziri huyo alipofanya ziara katika hifadhi ya Taifa ya kisiwa cha Rubondo, Kushoto ni Katibu wa Naibu Waziri huyo,Bw. Zulu Ng’ondya
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akisalimiana na baadhi ya watumishi   wakati Naibu Waziri huyo alipofanya ziara katika hifadhi ya Taifa ya kisiwa cha Rubondo.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akisaini kitabu cha wageni wakati Naibu Waziri huyo alipofanya ziara katika hifadhi ya Taifa  ya kisiwa cha Rubondo.

(PICHA ZOTE NA LUSUNGU HELELA-WMU)