Thursday, November 1, 2018

SAYONA FRUITS YAKABIDHI MAJENGO YA MILIONI 70 PAMOJA NA VIFAA TIBA KWA HALMASHAURI YA CHALINZE

Msaidizi wa Mkurugenzi  Mtendaji wa Sayona Bw Aboubakary Mlawa (kulia) akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze Bi Amina Kiwanuka, majengo pamoja vifaatiba vyenye thamani ya shilingi milioni 70 katika Zahanati ya Msoga.
...................................
 
Kampuni ya Sayona Fruits Limited ya  mboga Chalinze mkoani Pwani imekabidhi majengo na vifaa tiba yaliyogharimu shilingi milioni 70 kwa zahanati ya Kijiji cha Mboga.

Akikabidhi msaada huo,kwa Mkurungezi Mtendaji wa Halmashauri ya Bibi Amina  Kiwanuka, Msaidizi wa Mkurugenzi  Mtendaji wa Sayona Bw Aboubakary Mlawa alisema jumla ya shilingi milioni sabini zimetumika.

Alisema licha ya kusaidia sekta mbalimbali kijijini hapo ambapo ndipo kilipo kiwanda cha Sayona,wameamua kujenga nyumba ya mganga,jengo lenye maabara, mapumziko  na    duka la dawa.

Bw Mlawa alisema kutokana na ushirikiano mzuri baina ya kiwanda na jamii wameona ni muhimu kuboresha zahanati hiyo ambayo pia inasaidia kutoa huduma kwa wafanyakazi kwa kushirikiana na zahanati iliyopo ndani  ya kiwanda.

Aliongeza kuwa pamoja na kuboresha huduma pia kiwanda kitasaidia usafiri wa gari la wagonjwa pale itakapohitajika kupeleka hospitali kubwa kutokana na kuwepo gari la wagonjwa kiwandani.

Akishukuru kwa msaada huo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze Bibi Amina Kiwanuka alisema msaada huo wa Sayona umekuja wakati muafaka kwani mikakati ya Halmashauri ni kuboresha sekta ya afya katika Kijiji vyote.
Alisema Sayona ni moja ya kampuni ambayo ni mdau mkubwa wa maendeleo wilayani Bagamoyo,hivyo ushirikiano wake unampa faraja hata katika shughuli zake katika Halmashauri ya Chalinze.

Bibi Kiwanuka amewataka watumishi wa zahanati  hiyo kuhakikisha majengo na vifaa vinatunzwa na kulindwa.

Sayona Fruits Limited inamiliki kiwanda cha kusindika matunda na kuzalisha juisi za aina mbalimbali.
 
Msaidizi wa Mkurugenzi  Mtendaji wa Sayona Bw Aboubakary Mlawa akiwa na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Chalinze Dkt. Rahim Hangai pamoja watumishi wengine wakati wa kukabidhi majengo na vifaatiba vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 70 katika Zahanati ya Mboga.

Muonekano wa majengo hayo ya Zahanati ya Mboga ambayo yamejengwa na Kampuni ya Sayona Fruits yaliyogharimu shilingi milioni 70 pamoja na vifaatiba.

TCRA YAWACHUKULIA HATUA WANAOKIUKA SHERIA ZA MTANDAO.

Mkuu wa kanda ya Mashariki (TCRA) Lawi Odiero akizungumza.kwenye maonyesho hayo.
..........................................


NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeshawachukulia hatua za kisheria watu nane wanaodaiwa kukiuka sheria za mtandao, ikiwemo kusambaza picha za nusu uchi, video za ngono na kutupia matusi katika kipindi cha July -Septemba mwaka huu. 

Aidha wito umetolewa kwa jamii kuacha matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii ikiwa ni pamoja na video za ngono kwani kwa kufanya hivyo hawatamuangalia mtu kwa sura ama umaarufu bali sheria itachukua mkondo wake. 

Ofisa mkuu wa mawasiliano kwa umma (TCRA) Semu Mwakyanjala aliwatahadharisha ,watu wasisambaze picha ama video za ngono na kuanzisha tovuti hizo kwani ni kukiuka sheria.

Alieleza kuna faida unapotumia mtandao inarahisisha mawasiliano ,unapunguza gharama ,inaokoa muda ,inatoa elimu na kukuza biashara badala ya kutumia masuala yasiyo na tija.

“Kwasasa hatuna masihala, tunashirikiana na jeshi la polisi kubaini wale wanaokaidi kufuata sheria zilizopo “alieleza Mwakyanjala. 
Aliiomba jamii kutunza vifaa vya kielektronik ili watu waeiibe na kutymia vibaya .

Nae mkuu wa kanda ya Mashariki (TCRA) Lawi Odiero alisema, sheria ya kielektroniki iliyopo inakataza kusambaza ngono na baadhi ya watu wanachukuliwa hatua ya kulipa faini sh. mil tano ama miaka mitatu jela.

Aliwaasa wananchi kwenda kutembelea banda lao kujifunza ili kuelewa sheria zinazowabana ili kuepukana na adhabu. 

Odiero alieleza wazingatie wasiweke namba za siri kwenye simu ama internet miaka ya kuzaliwa bali watumie maneno mengine  kwani sio rahisi kughushi.

Akizungumzia ving’amuzi alisema ,serikali kupitia TCRA iliondoa baadhi ya channel kwenye baadhi ya visimbuzi. 

Odiero alifafanua, Azam, Dstv na Zuku huduma wanatoa kwa kulipisha hivyo hawaruhusiwi kubeba channel za ndani. 

Watumiaji wa internet hadi sasa nchini wapo milioni 22  ,luninga zipo 34 ,vituo vya redio zaidi ya 150 kutoka kituo kimoja kilichokuwepo mwaka 1961.

MAGAZETI YA LEO NOVEMBA 01, 2018.

Wednesday, October 31, 2018

DK. KALEMANI -TUTAHAKIKISHA TUNADHIBITI CHANGAMOTO YA KUKATIKA KWA UMEME VIWANDANI

WAZIRI wa Nishati Dk Merdad Kalemani ,wakati alipotembelea maonyesho ya bidhaa za viwandani yanayoendelea viwanja vya sabasaba, Pichandege Kibaha Pwani, ikiwemo banda la shirika la Maendeleo ya Petroli nchini ( TPDC), na kuelekeza kutangaza vituo vinavyosambaza gesi asilia. (picha na Mwamvua Mwinyi) 
.......................................................

NA MWAMVUA MWINYI, PICHANDEGE 

WAZIRI wa Nishati Dk Merdad Kalemani ,amesema umeme ni injini ya viwanda hivyo watahakikisha changamoto ya umeme kukatika kwenye viwanda nchini inadhibitiwa kwani hali hiyo haifai viwandani .

Aidha amewataka wawekezaji waendelee kujenga viwanda kwani umeme uko wa kutosha ambapo kwa sasa kuna akiba ya umeme wa ziada wa megawati 148.

Aliyasema hayo jana mjini Kibaha alipotembelea maonyesho ya viwanda kwenye viwanja vya Sabasaba vilivyopo Picha ya Ndege wilayani Kibaha .
Hata hivyo aliielekeza TPDC kuvitangaza vituo vya gesi asilia ili wananchi wapate uelewa juu ya gesi hiyo. 

“Sera yetu kwa sasa tunataka sisi tutangulie na viwanda ndiyo viufuate na siyo viwanda kuwafuata kwani kufanya hivyo tutakuwa tumewaondolea kero ya kufuatailia masuala ya umeme,” alisema Dk. Kalemani.

“Ndiyo maana tunajenga miradi mikubwa ya uzalishaji umeme kama ule wa Rufiji hydro power unaotokana na maji utakaozalisha megawati 2,100 na Rumakali utakaozalisha megawati 358 na ule wa gesi wa Kinyerezi kuhakikisha viwanda havikwami”

“Nimetembelea na kukagua mabanda na nimeona mahitaji na kati ya mabanda 17 ambayo ni ya viwanda  wana sema umeme siyo tatizo licha ya sehemu kama mbili wamelalamika kuwa umeme kwao ni changamoto”

Alibainisha  wameona kuna mahitaji makubwa ya umeme kwa ajili ya viwanda hasa katika maeneo ya Bagamoyo Kibaha na Chalinze viwanda vinajengwa kila siku hivyo wilaya na Tanesco waainisheni maeneo ambako vitajengwa viwanda ili miundombinu ipelekwe .

Aliwataka wataalamu wa Tanesco kuhakikisha wanaondoa changamoto ndogo ndogo zilizopo .

Nae mkuu wa wilaya ya Kibaha ,Assumpter Mshama alisema watayaanisha maeneo hayo ambayo yametengwa kwa ajili ya kuanzishwa viwanda ili huduma hiyo ipelekwe  kabla ya ujenzi wa viwanda kuanza.

Alisema wilaya yake ina viwanda vingi hivyo nishati ya umeme wa uhakika ni muhimu kuwepo ili kuondokana na changamoto hizo za ukosefu au kukatika kwa umeme.