Sunday, December 31, 2017

CGP. DKT. JUMA MALEWA AHUTUBIA BARAZA LA KUFUNGA MWAKA 2017.



Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akiongoza Baraza Maalum la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018. Baraza hilo limehudhuriwa na Maafisa na Askari kutoka vituo mbalimbali vya Magereza Mkoani Mbeya, Chuo cha Magereza Kiwira na Chuo cha Ufundi Mbeya ambapo Baraza hilo limefanyika leo Desemba 31, 2017 katika Viwanja  vya Magereza Mkoani Mbeya.


Baadhi ya Askari wa kike wa Jeshi la Magereza kutoka vituo mbalimbali vya Magereza ya Mkoa wa Mbeya wakisikiliza hotuba ya Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(hayupo pichani) katika Baraza Maalum la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018.

Wakuu wa Magereza yaliyopo Mkoani Mbeya wakifuatilia kwa umakini mkubwa maelekezo ya Kamishna Jenerali wa Magereza aliyoyatoa katika Baraza Maalum la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018.

Mkuu wa Magereza Mkoani Mbeya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Kijida Mwakingi akitoa taarifa fupi ya Mkoa wake katika Baraza Maalum la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018.

Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila akitoa ufafanuzi wa masuala yahusuyo Divisheni ya Huduma za Urekebishaji mbele ya  Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa pili kulia) katika Baraza la kufunga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018 (wa kwanza kushoto) ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mbaraka Semwanza. Baraza hilo limefanyika katika Viwanja  vya Magereza Mkoani Mbeya.

Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu katika Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Chacha Binna akitolea ufafanuzi kuhusiana na masuala ya madeni ya watumishi yaliyoulizwa na Maafisa na Askari wa Jeshi hilo Mkoani Mbeya(hawapo pichani) katika Baraza hilo.

Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akikagua gwaride la Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza kabla ya kuhutubia Baraza Maalum la Maafisa na Askari wa Jeshi hilo lililofanyika katika Viwanja vya Magereza Mkoani Mbeya leo Desemba 31, 2017

Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza



SUBIRA MGALU ATOA AGIZO KWA TANESCO.



 Naibu  Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza na wananchi wilayani Bagamoyo kwa nyakati tofauti katika ziara yake ya siku mbili aliyoianza jana Tarehe 30 Desemba 2017 na leo Tarehe 31 Desemba 2017.
...........................
Naibu  Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amewataka mameneja wa Tanesco mikoa na wilaya kote nchini kuwaunganishia umeme wananchi wakaokuwa wameomba na kukamilisha malipo yao ndani ya siku saba tu.

Agzo hilo amelitoa wilayani Bagamoyo alipokuwa katika ziara ya kukagua mradi wa kusambaza umeme vijijini REA awamu ya tatu unaotekelezwa nchi nzima.

Alisema kila meneja wa TANESCO anatakiwa kuhakikisha kuwa, wateja wote waliojaza fomu na kukamilisha malipo yao wanatakiwa kuunganishwa umeme ndani ya siku saba tu ili kuondoa usumbufu kwa wananchi wa kusubiri kuunganishiwa umeme kwa muda mrefu.

Aidha, alisema kufuatia agizo hilo atafanya ziara kwenye ofisi za TANESCO nchi nzima ili kuona idadi ya wananchi walioomba na kulipia huduma ya umeme na idadi ya waliounganishwa na kwamba meneja atakaeshindwa kutekeleza hilo anapaswa kutoa maelezo juu ya kwanini mteja hakuunganishiwa umeme ndani ya siku saba toka kulipia kwakwe.

Naibu waziri huyo wa Nishati amewataka Wananchi waliopo kwenye vijiji vinavyopitiwa na mradi wa kusambaza umeme vijijini REA wametakiwa kutumia fursa ya mradi huo kuchukua fomu na kulipia gharama ya shilingi elfu ishirini na saba tu ili waunganishiwe umeme kupitia REA awamu ya tatu.

Alisema Serikali imewathamini wananchi wake kwa kuwepelekea mradi wa kusambaza umeme vijijini REA ili kila mwananchi apate huduma hivyo ni matarajio ya serikali kuona fursa hiyo inatumika vizuri.

 Kwa upande wao wabunge wa jimbo la Bagamoyo na Chalinze wamempongeza Naibu waziri huyo wa kwanza mwanamke katika wizara ya nishati kwa kujali wananchi na kuwatembelea vijijini.

Dkt. Shukuru Kawambwa Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo amesema kufika kwa naibu waziri huyo vijijini kutampunguzia maswali anayoulizwa na wananchi kuhusu vijiji ambavyo havijafikiwa na umeme.

Nae mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete amesema wananchi wanajenga imani na serikali yao ya awamu ya tano hasa pale wanpoona kiongozi kama Naibu waziri anawatembelea na kusikiliza vilio vya wananchi
Alisema mfumo huo unawafanya wananchi kuimanini serikali yao hasa pale ilani ya chama Cha mapinduzi inatekelezwa kwa vitendo.

Wakati huo huo Naibu waziri wa Nishati huyo amewahakikishaia wananchi wa Kijiji cha Kongo kata ya Yombo wilayani Bagamoyo, kuwa watapata umeme katikati ya januari 2018 ili kuwaondolea kero ya kukosa umeme katika kijiji hicho kwa zaidi ya miaka 40 sasa.

Katika hatua nyingine Naibu waziri wa nishati ambae ni Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Pwani amechangia shilingi laki mbili kwaajili ujenzi wa ofisi ya CCM katika kijiji cha Kongo kata ya Yombo wilayani Bagamoyo.

Mradi wa kusambaza umeme vijijini REA awamu ya tatu mzunguuko wa kwanza unatarajiwa kukamilika ifikapo Juni 2019 kwa kufikisha umeme katika vijiji 3559 ambapo REA awamu ya tatu mzunguuko wa pili unatarajiwa kuanza kutekelezwa 2019-2021 ili kutekeleza lengo la serikali la kuvipatia umeme vijiji vyote 7873 vilivyobaki ifkapo mwaka 2021.


 Naibu  Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza na wananchi wilayani Bagamoyo kwa nyakati tofauti katika ziara yake ya siku mbili aliyoianza jana Tarehe 30 Desemba 2017 na leo Tarehe 31 Desemba 2017.
Naibu  Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akitoa maelekezo kuhusu nguzo za umeme zilizokaa kwa muda mrefu katika kijiji cha Kongo kata ya Yombo wilayani Bagamoyo.
Naibu  Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akipokea na kusoma mabango yaliyowasilishwa kwake na wananchi wa kijiji cha Kongo kata ya Yombo Halmashauri ya Bagamoyo wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani wakilalamikia kukosa umeme kwa zaidi ya miaka 40 sasa licha ya kuwa kijiji hicho ndicho chenye mtambo maji wa Ruvu chini.

Naibu  Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (katikati) akisikiliza maelezo ya kitaalamu kutoka kwa Msimamizi wa Miradi ya umeme vijijini REA Mkoa wa Pwani Mhandisi Mohamed Sauko (Kushoto) kushoto mwa Naibu waziri ni Meneja wa TANESCO wilaya ya Bagamoyo Daniel Michael Kyando, na kulia ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Dkt. Shukuru Kawambwa.

Monday, December 25, 2017

RC PWANI ATEMBELEA KIWANDA CHA BETRI KIBAHA.


Mkuu wa Mkoa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo  jana Jumapili Tarehe 24 Desemba 2017. amekgua kazi ya ujenzi wa kiwanda cha kampuni ya China Boda Technical Group Ltd inayojenga kiwanda cha kutengeneza betri za magari katika Plot No 21 TAMCO Industrial Estate, Kibaha, Mkoa wa Pwani. 

Mkuu huyo wa Mkoa wa Pwani amefanya ziara hiyo ili kukagua kasi ya ujenzi na kupokea changamoto zozote wanazokabiliana nazo ili kuona namna ya kushirikiana nao katika kuzitatua ili kufikia malengo.

Katika ziara hiyo amefurahishwa na kasi ya ujenzi inavyoendelea na kusema kuwa ni ya kuridhisha.

Aidha alipata fursa ya kuwasiliana kwa simu na Kandarasi wa Ujenzi huo ambaye amemuhakikishia kwamba ndani ya kipindi cha wiki mbili zijazo atakuwa amekamilisha kazi ya ujenzi kama mkataba wake unvyoonesha. 

Alisema licha ya kazi nzuri inayoendelea katika kiwanda hicho bado kuna kazi kubwa ya ujenzi wa barabara kuingia kwenye kiwanda yenye upana wa meta 15 ambayo inatakiwa kujengwa na NDC kulingana na makubaliano ya Mkataba. 

Aliongeza kuwa, ili kukamilisha ujenzi Kiwanda hicho, kuna michoro ya ujenzi wa majengo mbalimbali inayotakiwa kuidhinishwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha ili ujenzi wa miundombinu hiyo ianze mara moja.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo ameahidi kushughulikia changamoto hizo mapema iwezekanavyo ili kazi hiyo ikamilike kwa wakati.

Kazi hiyo ya ujenzi inatakiwa ikamilike kabla ya mvua za masika zinazotarajiwa kuanza kunyesha mwezi Machi, 2018 ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza kipindi cha mvua.