Thursday, September 28, 2017

MAADHIMISHO YA 87 YA SIKU YA TAIFA LA SAUDI ARABIA JIJINI DAR ES SALAAM

Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) akizungumza kwa niaba ya Serikali ya Tanzania wakati wa maadhimisho ya siku ya 87 ya Taifa la Kifalme la Saudi Arabia yaliyofanyika jana Jijini Dar es Salaam. Prof. Maghembe alikuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo. Kulia ni Balozi wa taifa hilo nchini Tanzania, Balozi Mohammed Bin Mansour Al Malik.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (katikati), Balozi wa Saudi Arabia nchini, Mohammed Bin Mansour Al Malik (wa pili kulia) na viongozi wengine wa ubalozi huo wakijiandaa kukata keki ya maadhimisho hayo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (wa tatu kushoto), Balozi wa Saudi Arabia nchini, Mohammed Bin Mansour Al Malik (katikati) na viongozi wengine wa ubalozi huo wakikata keki ya maadhimisho hayo.
Baadhi ya watoto wa Taifa la Kifalme la Saudi Arabia wakiinua bendera ya nchi hiyo kuashiria maadhimisho ya siku ya 87 ya Taifa hilo yaliyofanyika jana Jijini Dar es Salaam.


Tuesday, September 26, 2017

WAZIRI WA AFYA ATOA MIEZI 8 KILA HOSPITALI YA MKOA NA WILAYA KUJENGA JENGO LA HUDUMA ZA DHARULA.



Waziri wa Afya, Jinsia, Wazee na Watoto Umy Mwalimu ametoa miezi nane  kwa hospitali za mikoa na wilaya nchi nzima kuhakikisha wananjenga majengo ya kulea huduma za dharula katika hospitali hizo.

Waziri ummy Mwalimu ametoa agizo hilo mjini Bagamoyo, tarehe 25 Septemba 2017, alipokuwa akiweka jiwe la msingi jengo la huduma za dharula na jengo la wodi ya wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo.

Alisema wananchi wengi wanafariki kabla ya kufika kwa Daktari kutokana na kutokuwepo kwa majengo yanayotoa huduma za dharula katika Hospitali hizo.
alisema anatoa agizo hilo kuhakikisha kila Hospitali ya mkoa na Wilaya inaanza ujenzi wa majengo hayo na mwisho ni tarehe 30 juni 2018 kila Hospitali iwe imekamilisha ujenzi huo.

Ujenzi wa majengo ya huduma za dharula na wodi ya wazazi katika hospitali ya wilaya ya Bagamoyo umefadhiliwa na Taasisi ya Dhi nureyn na kwa kushirikiana na wahisani kutoka saudi Arabia 

Aidha, ujenzi huo ambao utagharimu shilingi milioni mia tani unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba mwaka huu.

Wakati huohuo Waziri Ummy Mwalimu alisema amekipandish hadhi kituo cha Afya cha msoga na kuwa Hospitali na kwamba kilichobaki ni kukabidhi rasmi Barua ya kupandisha hadhi kituo cha Msoga.

Awali Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Alhaj, majid Mwanga alimuomba Waziri wa Afya, kukipandisha hadhi kituo cha afya ili iwe Hospitali kutokana na kukuwa kwa mji wa Chalinze.

Mkuu wa wilaya pia alitumia nafasi hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungno wa Tanzania Dkt. john Magufuli kwa kukabidhi majengo yaliyokuwa yanatumika na Tan Roads huko msata ili yatumike kwa Halmashauri ya Chalinze.
Alisema kutokana na kufunguliwa kwa Barabara ya Msata Bagamoyo majengo ayo wanakusudia kufanya kituo cha Afya ambacho kitawahudumia wananchi wa Msata na wapita njia.

Waziri Ummy Mwalimu pia amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo kwa kutafuta wafadhili waliofanikisha ujenzi wa majengo ya huduma za dharula na wodi ya wazazi.
Watendaji kutoka Dhi nureyn, Kamati ya ulinzi na Usalama wilaya ya Bagamoyo pamoja na viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Bagamoyo wakifuatilia shughuli ya uwekaji jiwe la msingi katika majengo ya wodi ya wazazi na jengo la huduma za dharula katika Hospitali ya Wilaya bagamoyo.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Alhaj, majid Mwanga akizungumza katika shughuli hiyo iliyofanyika viwanja vya Hospitali ya wilaya ya Bagamoyo.

DKT.KIGWANGALLA AKABIDHI GARI LA WAGONJWA MKURANGA



Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla mapema jana Mei 28.2017 amekabidhi gari maalum la kubebea wagonjwa (Ambulance) na vifaa vya Hospitali ikiwmo vitanda na Magodoro katika Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga, Mkoani Pwani.

Dkt. Kigwangalla ambaye alikuwa mgeni rasmi katika tukio hilo, mbali na kukabidhi gari hilo la wagonjwa na vifaa hivyo vya Hospitali kwa uongozi wa Hospitali na Wilaya akiwemo Mkuu wa Wilaya na Mbunge wa Jimbo hilo, aliweza kufanya ukaguzi wa ghafla kujionea mazingira ya Hospitali hiyo na kubaini mapungufu mbalimbali ambayoo ametoa maagizo kupatiwa ufumbuzi kabla ya kuchukuliwa hatua kwa uongozi wa Hospitali hiyo.

Miongoni mwa changamoto hizo alizobaini katika Hospitali hiyo ni pamoja na kuwa na mfumo mbovu wa uhifadhi wa taka, pamoja na uchafu katika wodi ya wazazi jambo ambalo linaweza kusababisha hatari ya maambukizi kwa Wagonjwa na wahudumu wenyewe wa Afya.

Awali wakati wa kukabidhi gari hilo ambalo limenunuliwa kwa nguvu ya Madiwani kwa kushirikiana na wadau mbalimbali pamoja na Mbunge wa jimbo hilo la Mkuranga, Abdallah Ulega aliwataka kulitumia kwa uangalifu wa hali juu huku likitakiwa kufanya shughuli zilizokusudiwa katika kusaidia wananchi wake.

“Nimesikia kileo chenu ambacho ni kupatiwa mashine ya X-Ray na na vifaa vingine muhimu. Wizara yetu inalishughulikia hilo na tunawaomba muwe na imani na Mbunge wenu ambaye amekuwa akinisisitiza juu ya jambo hilo. 

Hospitali ya Mkuranga ni moja wapo ambayo itafaidika na msaada wa vifaa ikiwemo mashine hiyo ya X-Ray” alisema Dkt. Kigwangalla wakati akizungumza na wananchi mbalimbali ambao pia walipata fursa ya kuuliza maswali katika tukio hilo.