Sunday, September 24, 2017

JESHI LA POLISI LAFUNGA MAFUNZO YA UTAYARI CHUO CHA POLISI KIDATU

2
Naibu Kamishna wa Polisi mstaafu (DCP) Venance Tossi (Kushoto), akizungumza jambo na Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Leonard Paulo (kulia),  muda mfupi kabla ya kufunga mafunzo ya Utayari ya kuwajengea uwezo askari wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kazi za Polisi.
 1
Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Leonard Paulo (katikati),  akiwa ameongozana na Naibu Kamishna wa Polisi mstaafu (DCP) Venance Tossi (Kushoto) na Mkuu wa chuo cha Polisi Kidatu kilichopo mkoani Morogoro, kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Zarau Mpangule, wakati alipowasili katika chuo hicho kwa ajili ya kufunga mafunzo ya Utayari ya kuwajengea uwezo askari wakati wanapotekeleza majukumu yao.
 3
Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Leonard Paulo, akifanya mazoezi ya viungo na baadhi ya askari wanaoshiriki Mafunzo ya Utayari na kujengewa uwezo wakati wanapotekeleza majukumu yao ya kazi za Polisi, mafunzo yanayofanyika katika Chuo cha Polisi Kidatu Kilichopo mkoani Morogoro. 

Picha na Jeshi la Polisi

MAHAFALI YEMEN ENGLISH MEDIUM WAZAZI WAASWA.



Wazazi na walezi wa kiislmu wametakiwa kuendelea kuwasomesha elimu ya dini ya kiislamu watoto wao hata baada ya kumaliza elimu ya msingi ili kuwajengea misingi ya kumjua Mwenyezimungu katika maisha yao yote.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Taasisi ya The Islamic Foundation (TIF) Aref Nahd alipokuwa akizungumza katika mahafali ya 06 ya kuwaaga wanafunzi wa darasa la saba 2017 wa shule ya msingi Yemeni English Medium Primary School iliyopo Chang'ombe jijini Dar es Salaam.

Aref, alisema imekuwa ni kawaida ya wazazi na walezi wengi kuwakatisha masomo ya elimu ya dini kiislamu watoto wao  mara watoto hao wanapomaliza Elimu ya msingi jambo ambalo linawafanya watoto kutoka kwenye misingi ya uislamu kwasababu hawakuendelezwa kwenye Elimu ya uislamu na badala yake wameendelezwa kwenye Elimu ya mazingira pekee.

Alisema uislamu ni dini iliyobeba maisha ya binadamu kuanzia kuzaliwa kwake mpaka kufa kwake hivyo muislamu hana nafasi ya kuishi nje ya mfumo ulioelekezwa na uislamu.

Aliongeza kwa kusema kuwa, mfumo huo wa maisha ya binadamu umefundishwa ndani ya uislamu kupitia Mtume Muhammad Swalallahu Alayhi Waslama, na kwamba huwezi kujua bila ya kusoma Elimu ya dini ya uislamu.

Alisema si vyema kwa mzazi au mlezi kumkatisha masomo ya elimu ya uislamu mtoto kwasababu mtoto huyo anaendelea kukua na bado anahitaji muongozo kutoka katika Qur'ani na sunnah ambavyo ndio dira ya maisha yake itakayompatia faida duniani na akhera.

Aidha, Aref Nahdi ambae ndiye aliyekuwa Mgeni rasmi katika Mahafali hayo aliwataka vijana walimaliza elimu ya msingi shuleni hapo kuendelea kuwa na tabia njema ya kiislamu kama walivyofundishwa wakiwa shuleni na kwamba wanapaswa kutambua kuwa, kumaliza elimu ya msingi sio mwisho wa kutafuta elimu katika maisha.

Wakati huo huo Aref aliwataka walimu kufanya kazi kwa moyo mmoja wakitambua kuwa kazi yao ni miongoni mwa sadaka licha ya kuwa wanalipwa mishahara.

Alisema pamoja na kufikiria kuongezwa posho na mishahara wanapaswa pia kufikiria mbinu mbalimbali za kuongeza taaluma ili watoto wanaoletwa katika shule hiyo wapate elimu bora kama ilivyokusudiwa.

Mwenyekiti huyo wa Taasisi ya The Islamic Foundation (TIF) inayomiliki vyombo vya habari vya  Tvimaan, Radio imaan, pamoja na Gazeti imaan, ametoa nafasi kwa uongozi wa shule hiyo ya Yemen English Midium Primary school kufika katika studio za Tvimaan zilizopo mjini Morogoro kuitangaza shule hiyo bure kwa kueleza namna wanavyoendesha shule hiyo ili watu wengi wajue Taaluma inayotolewa shuleni hapo.

Alisema  The Islamic Foundation inatoa nafasi hiyo ya muda wa hewani bure kupitia Tvimaan ikiwa kama ni mchango wake kwa shule hiyo ambapo kipindi hicho kama kingelipiwa kinagharimu shilingi milioni tatu.

Aidha, alisema pamoja na muda huo wa hewani kupitia Tvimaan, TIF itatoa nakala ishirini za gazeti imaan shuleni hapo kila wiki ili walimu  kupitia Gazeti hilo waweze kufaidika na taaluma inayotolewa ndani gazeti hilo na kuwajenga vijana wa kiislamu wanaosoma shule kuanza kupenda vyombo vyao vya habari kuanzia shuleni.
Nae Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo,  Hassan Akrabi, aliwataka wazazi wote wenye watoto waliomaliza elimu ya msingi shuleni hapo kuwarudisha tena katika shule hiyo kuendelea na masomo ya Sekondari ili waendelee kupat malezi yenye maadili pamoja na elimu bora inayotolewa katika shule hiyo.

Alisema watoto hao wamejengwa katika misingi ya kumjua Mwenyezimungu na kupata Elimu bora ya muongozo na mazingira hivyo uongozi wa shule unaomba ridhaa ya kubaki tena na watoto hao kuanzia kidato cha kwanza mpka cha nne.

Mwenyekiti huyo wa bodi ya shule alisema kumjenga mtoto kitabia inachukua muda mrefu na juhudi za ziada lakini kumbomoa inachukua muda mfupi na kwamba wazazi wasipokuwa makini kuchagua shule za kuwapeleka watoto wao watawabomoa kimaadili na kitaaluma.
 Mbunge wa viti maalum Da es salaam Zainabu Mndolwa Amiri akizungumza katika mahafali hayo katikati ni Mjumbe wa kamati ya shule Dkt. Tausi Mftaha na kushoto ni meneja wa shule hiyo Jamila Awadhi.
 Mbunge wa viti maalum Da es salaam Zainabu Mndolwa Amiri akimkabidhi mwanafunzi cheti pamoja na Dictionary, ambapo watoto wote mia moja na moja 101 kila mmoja alipata Dictionary moja katika mahafali hayo, katikati ni Mjumbe wa kamati ya shule Dkt. Tausi Mftaha na kushoto ni meneja wa shule hiyo Jamila Awadhi.

Kwa upande wake Mbunge wa viti maalum Da es salaam Zainabu Mndolwa Amiri  amejitolea Dictionary 102 ambapo kila muhitimu alipata Dictionary
Mbunge huyo alisema amejitolea Dictionary hizo ili kuunga mkono juhudi za kuwawezesha vijana kielimu na kuwataka vijana hao waongeze bidii katika safari yao ya masomo.

Dictionary hizo aina ya Oxford zimegharimu shilingi za kitanznia milion moja laki tatu elfu arubaini na sita na mia nne, 1,346,400/= ambapo kila moj ina thamani ya shilingi elfu kumi na tatu na mia mbili, 13,200/= 

Aidha, aliupongeza uongozi wa Yemeni English Medium Primary School kwa kuisimmia vizuri shule hiyo na kufanikiwa kutoa watoto wenye maadili ambao watakuwa na faida kwa wazazi wao na taifa kwa ujumla.
Kulia ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Rahim Burhan Abdallaah, wa pili kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya shule hza Yemen, Hassan Akrabi, na watatu ni Mgeni rasmi katika mahafali hayo, Mwenyekiti, wa the islamic Foundation, Aref Nahdi.

 Awali akisoma risala mbele ya mgeni rasmi Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Rahim Burhan Abdallaah alisem miongoni mwa mafanikio yalipatikana shuleni hapo ni pamoja na kukamilika kwa jengo la ghorofa tatu ambalo lina jumuisha Madarasa 36, Ofisi 18, Vyoo 52 Stoo 02, Maktaba 01, Chumba cha Mabara 01 Maabara ya Computer 01 na Ukumbi wa mikutano 01.

Aidha, alisema wanafunzi wameongezeka kutoka 35 Mwaka 1999 na kufikia 807 Mwaka 2017 na walimu kutoka walimu watatu mwaka 1999 mpaka walimu 48 mwaka 2017 huku shule ikiwa inamiliki mabasi manne kwaajili ya kusafirishia wanafunzi.

Alisema pamoja na mafanikio hayo, miongoni mwa Changamoto zinazoikabili shule hiyo ni pamoja na uhba wa mabasi ya kusafirisha wanafunzi na kuwataka wadau mbalimbali kujitokeza kutoa huduma ya usafiri shuleni hapo kwa gharama nafuu.

Aidha, alisema malengo ya shule hiyo ili kuendana na uwezo wa shule, ni kufikia wanafunzi elfu moja mia mbili na tano 1,205, kutoka wanafunzi mia nane na saba 807, waliopo sasa.

Jumla ya vijana  mia moja na moja 101, wamehitimu Elimu ya msingi shuleni hapo wakiwemo wavulana 44 na wasichana 57 .
Muonekano wa majengo katika shule hiyo ya Yemen English Medium Primary School iliyopo Chang'ombe jijini dar es Salaam.
 
Baadhi ya wahitimu wa elimu ya msingi wasichana 2017.
 Baadhi ya wahitimu wa elimu ya msingi wavulana 2017.
 Mgeni rasmi katika mahafali hayo, ambae ni mwenyekiti wa The Islamic Foundation, Aref Nahdi (katikati) Kulia ni mwenyekiti wa Bodi ya shule za yemen, Hassan Akrabi, na kushoto ni Mjumbe wa bodi ya shule za yemen Salmeen Aljabry.
Wa kwanza kulia ni Mbunge wa viti maalum Dar es Salaam, Mh. Zainab Mndolwa Amiri, katikati ni mjumbe wa kamati ya wazazi wa shule hiyo, Dkt. Tausi Maftah, na wa kwanza kushoto ni Meneja wa shule hiyo, Jamila Awadhi.




Friday, September 22, 2017

WAZIRI UMMY ALAANI MWANAFUNZI KUPEWA MIMBA.

IMG-20170921-WA0025
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy A. Mwalimu (Mb) amepokea kwa masikitiko makubwa kitendo cha mwalimu mmoja wa Shule ya Msingi Samanzi, iliyoko kijiji cha Samanzi, Kata ya Kisumba, wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa kumpa ujauzito mwanafunzi wa darasa la saba (jina limehifadhiwa), na kushindwa kufanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi. Mhe. Waziri amesema kitendo hicho ni ukatili na unyanyasaji dhidi ya mtoto wa kike na ni ukiukwaji wa Haki za Msingi za Mtoto ikiwemo haki ya Kuendelezwa na Kulindwa.

Waziri Ummy amewaasa walimu kuacha tabia ya kuwa na mahusiano ya kingono na wanafunzi maana shule kama taasisi, ni chombo madhubuti cha kujenga uelewa kwa jamii kuhusu ulinzi na usalama wa Mtoto katika jamii.

Aidha, amewataka walimu,  walezi na jamii kuhakikisha wajibu wa kuwalinda na kuwalea watoto bila uwanyanyasaji na ukatili wa aina yoyote. Ameongeza kuwa, inapotokea mwalimu amehusishwa na tuhuma ya kumpa mimba mtoto wa kike kitendo hicho kinatia doa dhamana ya mwalimu na nafasi ya shule katika malezi ya mtoto.

Waziri Ummy, ameitaka jamii kuboresha ushirikiano wa wazazi, walezi na walimu maana wanamchango mkubwa katika makuzi na maendeleo ya watoto. Kadhalika, amesisitiza kutambua kuwa madhara ya mwalimu kumpa mimba mwanafunzi anamfanya kuwa mwathirika wa vitendo vya ukatili katika maisha yake yote.

Aidha, Waziri Ummy ameelekeza vyombo vya dola mkoani Rukwa kuhakikisha suala hili linachunguzwa kikamilifu na kumfikisha mtuhumiwa mbele ya vyombo vya sheria ili haki iweze kutendeka. 
Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
22/09/2017