Tuesday, September 19, 2017

DC BAGAMOYO AKIWA SHAMBANI KWAKE AHIMIZA KILIMO CHA UBUNIFU.



Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Alhaj, Majid Mwanga, amewahimiza wananchi wa wilaya  hiyo, kulima kilimo cha ubunifu ili kujiongezea kipato.

Mkuu huyo wa Wilaya ya Bagamoyo, aliyasema hayo hivi karibuni baada ya bagamoyokwanza blog kutembelea shambani kwake lililopo kata ya Kiromo wilayani humo.

Alisema, kilimo bora kitakachomuongezea kipato mtu ni kile kinachoendana na soko la zao husika.

Aliongeza kwa kusema kuwa, katika Wilaya ya Bagamoyo kuna viwanda kadhaa vya kusindika matunda, mbogamboga na viungo mbalimbali ambavyo vyote ni mazao yanayotokana na kilimo.

Majid alisema sio mwananchi ataweza kuajiriwa katika viwanda hivyo, bali kila mwananchi atafaidika kwa namna yake ikiwemo wale watakaoshughulika na kilimo cha mazao yanayohitajika kwenye viwanda hivyo.

Akitolea mfano wa Kiwanda cha viungo cha VEGETA kilichopo kata ya Kisutu wilayani Bagamoyo, mkuu huyo wa wilaya alisema kiwanda cha VEGETA kinatumia mazao ya kilimo ikiwemo, Pilipili, Nyanya NK. hivyo ni vyema wakulima wa Bagamoyo wakafanya utafiti kuhusu mazao yanayohitajika kwenye viwanda vilivypo ili walime mazao ambayo yakivunwa yanaenda sokoni moja kwa moja.

Mbali na kiwanda cha VEGETA Mkuu huyo wa wilaya amekitaja Kiwanda kingine cha Elvin kilichopo Kata ya Mapinga katika Halmashauri ya Bagamoyo, ambacho ni maalum kwa kukausha matunda ambayo yatasafirishwa nje ya nchi.

Alisema kuwa, kiwanda hicho cha Elvin ni kiwanda pia kitakachohitaji matunda ya aina mbalimbali kwa wingi ili kuweza kuzalisha bidhaa za matunda yaliyokaushwa na hivyo ni fursa kwa wakulima kutumia ubunifu wa kulima mazao ambayo tayari masoko yake yapo.

Aidha, alisema, mbali na hivyo kipo kiwanda cha Sayona Kata ya Msoga Halmashauri ya Chalinze ndani ya Wilaya ya Bagamoyo ambacho hicho ni kwaajili ya kutengeneza juisi za matunda na kwamba katika kiwanda hicho soko kubwa la matunda litapatikana hivyo ni vyema wananchi wa wilaya ya Bagamoyo wakachangamkia fursa hizo kilimo cha ubunifu kulingana na soko la zao husika ili kujiongezea kipato.

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Alhaj, Majid Mwanga, pamoja na majukumu yake aliyonayo ya kuingoza wilaya, hutmia muda wake wa ziada shambani, ikiwa ni sehemu ya kuonesha mfano wa kile anachokisema ambapo ameweza kupanda Migomba, Mipapai Pilipili, Ufugaji wa Samaki na Kuku wa Kienyeji.

Harakati hizi za shamba za mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, licha ya kuwa anaweza kujiongezea kipato kutokana na mazao yaliyopo shambani kwake, lakini pia ameweza kutoa ajira kwa vijana wanaofanya kazi za kuhudumia mazao hayo hapo shambani.

Ni Mfano wa Kuigwa kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Alhaj, majid Hemed Mwanga, mimi na wewe tufuate njia.

    Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Alhaj, majid mwanga akionesha zao la pilipili ambazo amepanda shambani kwake eneo la Kiromo.

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Alhaj, majid mwanga akiwa kwenye shamba lake la Migomba Kiromo wilayani humo.

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Alhaj, majid mwanga akionesha aina ya Mpapai ambao huzaa kwa muda mfupi katika shamba lake huko Kiromo ndani ya Wilaya yake.
Mkurugenzi wa bagamoyokwanza blog. Brother, Athumani Shomari (kulia) alipotembele shambani kwa Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, (kushoto) Alhaj Majid mwanga.

MAGAZETI YA LEO TAREHE 19 SEPTEMBA 2017.

Monday, September 18, 2017

RC NDIKILO AWATAKA VIONGOZI WA DINI KUKEMEA MADAWA YA KULEVYA.

Mkuu wa mkoa wa pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo amewataka viongozi wa dini mkoani humo kushirikiana na viongozi wa Serikali katika kupambana na Madawa ya kulevya.

Mkuu huyo wa mkoa wa Pwani ameyasema hayo katika hutuba iliyosomwa kwa niaba yake na mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Ahaj, Majid Mwanga wakati wa Kongamano la mahusiano ya kibinadamu liliandaliwa na Kituo cha kiislamu cha Kimisri -Dar es salaam.

Amesema Madawa ya kulevya yanapoteza kuvu kazi ya Taifa na hivyo mmoja anapaswa kupiga vita biashara hiyo haramu ili mkoa uwe na watu wenye nguvu watakaoweza kusaidia uzalishaji kwenye viwanda vinavyoendelea kujengwa mkoani humo ili kufanikisha malengo ya Rais Magufuli ya kuwa na Tanzania ya Viwanda.

Aidha, alitumia nafasi hiyo kuwahimiza wazazi kuwapeleka sekondari watoto waote watakaofaulu elimu ya msingi ili kila mtoto apate haki yake ya Elimu katika kipindi hiki ambapo Elimu inatolewa bure hapa nchini.

Akizungumzia swala usalama katika mkoa wa Pwani, mkuu huyo wa mkoa wa Pwani alisema Mkoa huo kwa sasa umekuwa tulivu baada ya vikosi vya ulinzi na usalama kuimarisha ulinzi mkoani humo na kuwataka Viongozi wa dini kuendelea kuhubiri amani ili kuwavutia wawekezaji kufika katika Mkoa wa Pwani kuwekeza zaidi.

Alisema Kwa sasa mkoa wa Pwani una viwanda vingi na ni mkoa wa Mfano kwa Viwanda hapa nchini, hivyo ni vyema Amani ikaendelea kudumishwa ili wawekezaji hao waliojenga na wanaoendelea kujenga Viwanda waweze kufanya shughuli zao kwa utulivu na nchi ifaidike na kodi huku wananchi nao wafaidike kwa kupata ajira na bidhaa zinazozalishwa katika viwanda hivyo.

Nae Mkurugenzi wa kituo cha Kiislamu cha Kimisri ,Sheikh Muhsin Sayyed Majid alisema uislamu ni dini inayoendana na maumbile ya binadamu na hivyo mafundisho ya uislamu yanahimiza kuwa na mahusiano mema na watu wa dini zote bila ya kubaguana kwa rangi, kabila wala kwa lugha.

Alisema mafundisho ya mtume muhammadi Swalallaahu Alayhi wasalama yanafundisho mahusiano mema kwa watu wote na kwamba si vyema watu fulani wakajiona bora dhidi ya wengine ispokuwa mbora ni yule anae mcha mungu tu.

Kwa upande wake Sheikha mkuu wa mkoa wa pwani, Sheikh  Khamisi Abasi Mtupa amesema uislamu haumzuii mtu kushiriki katika shughuli mbalimbali ili mradi shughuli hizo hazimtoi kwenye uislamu kwa mujibu wa sheria.  


Washiriki wa kongamano hilo.
  Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Ahaj, Majid Mwanga akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi wa kituo cha Kiislamu cha kimisri,Dar es Salaam Sheikh Muhsin Sayyed Majid, kushoto ni Qadhi wa Mkoa wa Pwani, Sheikh Khamisi Abasi Mtupa

Saturday, September 16, 2017

RTO PWANI APATA AJALI.



Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Pwani Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP. Abdi Isango amepata Ajali katika eneo la Kibiki, Msolwa Wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Jonathan Shana amethibisha tukio hilo  na kusema kuwa Ajali hiyo imegusisha Gari Dogo aina ya Noah T.424 iliyokuwa likiendeshwa na Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Pwani (RTO) na Roli lenye Namba za Usajili T.410 BEE.

Amesema Ajali hiyo imetokea alfajiri ya leo  Tarehe 16 mwezi huu wa Tisa 2017.

 Kamada Shana amesema katika Ajali hiyo mtu  mmoja amefariki ambae ni  baba mzazi  wa RTO huyo wa Pwani.
Na majeruhi wanne.

Kamanda Shana amemtaja Marehemu kuwa ni  Hamisi Isango ambae ni  baba mzazi wa Mkuu wa usalama barabarani Mkoa wa Pwani na majeruhi ni Mkuu huyo wa Usalama barabarani Mkoa wa Pwani, Abdi Isango na mama yake  mzazi Zena Juma.

Wengine ni  wadogo zake Mkuu huyo wa Usalama barabarani Mkoa wa Pwani ambao ni  Haji Hamisi Isango na Shabani Hamisi Isango.

Majeruhi wote  wamelazwa katika hospitali  ya Tumbi kwaajili ya matibabu.

Kamanda Shana amesema chanzo cha Ajali hiyo ni uzembe wa Dereva wa roli ambae ameegesha Gari bila ya Tahadhari.

Friday, September 8, 2017

RC. NDIKILO AMUAGA BALOZI WA CHINA.

Image may contain: 2 people
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Eng. Evarist Ndikilo kushoto akimkabidhi zawadi Balozi wa China hapa nchini, Dr Lu Youqing alipokweda kumuaga kufuatia Balozi huyo kumaliza muda wake.
Image may contain: 6 people, people smiling, people standingImage may contain: 2 people, people sitting