
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Bagamoyo, Shauri Selenda, akizungumza wakati wa
kuwatambulisha wajumbe wa Kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji
jamii, kuhusu magonjwa ya mlipuko uliofanyika leo Februari 15, 2023. katika Ukumbi wa Chuo cha unesi
Bagamoyo.
Afisa Mipango wa huduma za Afya ngazi ya Jamii kutoka Wizara ya afya,
Bahati Mwailafu, akizungumza na washiriki wakati wa Mkutano wa
kuwatambulisha wajumbe wa Kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji
jamii, kuhusu magonjwa ya mlipuko uliofanyika leo Februari 15, 2023. katika Ukumbi wa Chuo cha unesi
Bagamoyo.
Washiriki wa Mkutano wa
kuwatambulisha wajumbe wa Kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji
jamii, kuhusu magonjwa ya mlipuko uliofanyika leo Februari 15, 2023. katika Ukumbi wa Chuo cha unesi
Bagamoyo.
Mratibu
wa Elimu ya Afya kwa uma wilaya ya Bagamoyo, Jeni Mcharo, akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wa
kuwatambulisha wajumbe wa Kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji
jamii, kuhusu magonjwa ya mlipuko uliofanyika leo Februari 15, 2023. katika Ukumbi wa Chuo cha unesi
Bagamoyo.
Washiriki wa Mkutano wa
kuwatambulisha wajumbe wa Kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji
jamii, kuhusu magonjwa ya mlipuko uliofanyika leo Februari 15, 2023. katika Ukumbi wa Chuo cha unesi
Bagamoyo.
........................................................................
Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Bagamoyo, Shauri Selenda, amesema mafanikio ya utekelezaji wa Mipango
na mikakati mbalimbali ya serikali inatokana na jamaii kuelewa, kuhamasika na
kushirikishwa katika utekelezaji wa mikakati hiyo.
Mkurugenzi
huyo wa Halmashauri ya Bagamoyo, ameyasema hayo wakati wa kufunga Mkutano wa
kuwatambulisha wajumbe wa Kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji
jamii, kuhusu magonjwa ya mlipuko uliofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha unesi
Bagamoyo.
Alisema jamii
inahitaji kupata elimu juu ya jambo husika ili waweze kushiriki kikamilifu
katka mambo mbalimbali yanayoandaliwa na serikali na kwa kutambua hilo serikali
imeweza kuandaa namna ya kuwashirikisha, kuwaelimisha na kuwahamasisha kupitia
kamati hiyo.
Ameitaka
Kamati hiyo itakapopata elimu juu ya kile wanachotakiwa kwenda kukifanya
wakafanye kwa utaalamu waa hali ya juu kwa kuwafikia makundi mbalimbaali katika
jamii.
Aliwakumbusha
kuwa, kazi yao kubwa ni kwenda akutoa elimu, kuhamasisha na kuwashirikisha
kuhusu magonjwa ya mlipuko ili kila mmoja awe na uelewa ulio sahihi hali
itakayosaidia kwa serikali kutotumia nguvu katika kuhamasisha chanjo zaa
magonjwa ya mlipuko.
Kwa upande
wake Afisa Mipango wa huduma za Afya ngazi ya Jamii kutoka Wizara ya afya,
Bahati Mwailafu, amesema kamati ya
Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji jamii, imeundwa ili kukabiliana na
magonjwa ya mlipuko ambapo wananchi wanapaswa kupata elimu sahihi kuhusu
magonjwa hayo ili waweze kujilinda na kujitibu.
Alisema lengo
la mkutano huo ni kutambulisha kamati ambayo itashiriki katika kutoa elimu,
kuhamasisha, na kushirikisha jamii ili waweze kuelewa madhara ya magonjwa ya
mlipuko.
Nae Mratibu
wa Elimu ya Afya kwa uma wilaya ya Bagamoyo, Jeni Mcharo amesema wanatarajia
kupata mafanikio katika Kamati hiyo iliyotambulishwa kwakuwa imeshirikisha
makundi mbalimbali ya kijamii.
Alisema mara
kadhaa serikali inapotaka jambo la kijamii liwafikie wananchi hutumia makundi
mbalimbali ya kijamii ili kurahisisha ufikishaji wa taarifa kutokana na kamati
husika kukubalika katika jamii kwani miongoni mwao wapo viongozi wa ngazi
mbalimbali wakiwemo wa viongozi wa dini, serikali na asasi za kiraia.
Aliongeza kwa
kusema kuwa, mafanikio katika kutoa elimu kuhusu magonjwa ya mlipuko ni jambo
kwakuwa tutakuwa tumemsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt.
Samia Suluhu Hassan ambae amekuwa akihakikisha wananchi wake wanakuwa salama
dhidi ya magonjwa mbalimbali.
Alisema Rais
Samia ni mpenda maendeleo hivyo anapenda wananchi wake wawe na afya njema ili
waweze kushiriki katika kujiletea maendeleo wenyewe na taifa kwa ujumla.
Aidha,
amewashukuru Wizara ya Afya kitengo cha Elimu ya afya kwa uma kwa kuona umuhimu
wa jambo hilo na kuchagua mkoa wa Pwani kuwa miongoni mwa mikoa inayostahili
kupata kamati hiyo ili kuweza kupambana na magonjwa ya mlipuko.
Mkutano huo
wa kutambulisha wajumbe wa Kamati ya Uhamasishaji, Ushirikishaji na Uelimishaji
jamii, umeandaliwaa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais
TAMISEMI na Shirika la Afya duniani W.H.O.