Friday, February 4, 2022

MGANGA WA JADI ATUHUMIWA KUWAUA MKE NA MME NJOMBE

 No description available.

Mganga wa jadi anayejulikana kwa jina Joseph Paulos Mgunda na mtu mmoja anayedaiwa kuwa ni ndugu wa mtaalamu huyo bwana Endrew Varuhoki wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Njombe kwa tuhuma za kutekeleza mauaji ya mkwe na mume waliyofahamika kwa jina la Suzan Mtitu na Kasim Kitamkanga ambao walikuwa wakazi wa mji wa Makambako.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkuu wa jeshi la polisi mkoani humo Hamis Issa inasema watuhumiwa waliamua kutekeleza mauaji haya baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wanafamilia hao kuwa dawa ya biashara waliyopewa na mganga huyo haijafanya kazi.

Aidha jeshi linamshikiliwa Israel Msigwa maarufu mtoa roho ambaye anadaiwa kuwa ni mpiga debe Makambako kwa tuhuma za kumchapa mwanae anaefahamika kwa jina Haskari Israel Msigwa(7)kwa fimbo na waya za umeme kwa kosa la kukojoa kitandani.

Katika hatua nyingine jeshi la polisi linamshikilia mwanaume mmoja anaefahamika kwa jina la Ambwene Sanga(34) ambaye ni baba wa kambo na Michael Mbilinyi(32) kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya mwanae anaejulikana kwa jina la Mesia Kaduma(5) huku chuki zikidaiwa kuhusika.

Katika kukabiliana na changamoto ya mauaji jeshi limetoa rai kwa wananchi kuacha kujichukulia hatua mikononi huku onyo lingine likitolewa kujiepusha na imani za kishirikina .

 

Thursday, February 3, 2022

WAZIRI MASAUNI, NAIBU WAZIRI SAGINI WALA VIAPO KUIONGOZA TUME YA UTUMISHI YA JESHI LA POLISI, MAGEREZA, ZIMAMOTO NA UOKOAJI NA UHAMIAJI, JIJINI DODOMA

No description available.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akila kiapo cha kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu, Mheshimiwa Gerson Mdemu, jijini Dodoma.

No description available.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akila kiapo cha kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu, Mheshimiwa Gerson Mdemu (hayupo pichani), jijini Dodoma.

No description available.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini akila kiapo cha kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu, Mheshimiwa Gerson Mdemu (hayupo pichani), jijini Dodoma.

No description available.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini akila kiapo cha kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu, Mheshimiwa Gerson Mdemu, jijini Dodoma

No description available.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akimshukuru Jaji wa Mahakama Kuu, Mheshimiwa Gerson Mdemu (kulia), baada ya kumwapisha kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji, pamoja na wajumbe wengine walioapishwa akiwemo Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Jumanne Sagini (kulia kwa Waziri), jijini Dodoma leo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.