Wednesday, February 2, 2022

WAWEKEZAJI KUTOKA SAUDI ARABIA KUWEKEZA TANZANIA.

 No description available.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (katikati) akizungumza na ujumbe wa wawekezaji kutoka Kiwanda cha Pioneers Chemical Factory cha nchini Saudi Arabia wanaotembelea Tanzania kuangalia fursa za biashara na uwekezaji.Kikao hicho kilifanyika ofisini kwa Mhe. Waziri Mtumba jijini Dodoma.

....................................................

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa wawekezaji kutoka Kiwanda cha Pioneers Chemical Factory cha nchini Saudi Arabia wanaotembelea Tanzania kuangalia fursa za biashara na uwekezaji.

 

Mhe. Waziri Mulamula amekutana na Ujumbe wa wawekezaji hao ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma leo tarehe 02 February 2022. Ujumbe wa wawekezaji hao umeongozwa na Balozi wa Tanzania nchini Saudia Arabia Mhe. Ali Mwadini umeelezea utayari wao wa kuja kuwekeza nchini.

Akizungumza katika kikao hicho Balozi Mulamula amewakaribisha wawekezaji hao na kuwahakikishia mazingira rafiki ya uwekezaji nchini na kwamba Tanzania iko tayari kuwapokea.

Amesema Tanzania na Saudia zina uhusiano wa muda mrefu ambao una historia ya aina yake na kwamba uwekezaji kutoka kwa kampuni hiyo ni sehemu ya kuimarisha mahusiano kati ya Tanzania na Saudi Arabia.

Kampuni hiyo inayomiliki viwanda mbalimbali nchini Saudi Arabia inajishughulisha na uzalishaji wa pembejeo za Killimo hususan, mbolea za kupandia na kukuzia mimea pamoja na dawa (pesticides) aina ya ‘phosphorus, nitrogen, potassium na sulfur’.

Mbali na uzalishaji wa mbolea na dawa, Kampuni hiyo pia inazalisha vifaa vya kilimo vya plastiki ikiwa ni pamoja na khusambaza bidhaa katika nchini za Saudi Arabia, ukanda wa Mashariki ya Kati na duniani kote.

 

Wawekezaji hao waliwasili nchini Januari 28, 2022  wametembelea Mikoa ya Mtwara, Lindi na Dodoma na kukutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Mikoa hiyo, wadau wa sekta binafsi na wakulima wa korosho kuzungumzia biashara na uwekezaji katika nyanja hizo. 

Wawekezaji hao wamemuhakikishia Mhe. Waziri Mulamula juu ya nia yao ya kuja kuwekeza Tanzania na kutaja maeneo ambayo ni kipaumbele chao kuwa ni madini, biashara, kilimo na mifugo.

No description available.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (katikati) akizungumza na ujumbe wa wawekezaji kutoka Kiwanda cha Pioneers Chemical Factory cha nchini Saudi Arabia (walioko kushoto) wanaotembelea Tanzania kuangalia fursa za biashara na uwekezaji.

No description available.

Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini (katikati) katika kikao na Wawekezaji kutoka nchini Saudi Arabia(hawapo pichani) kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Hemedi Mgaza na kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasia ya Uchumi Balozi Edwin Rutageruka wakati wa kikao na wawkezaji hao.

No description available.

Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini akiwa nje ya jengo la Wizara katika Mji wa Serikali Mtumba akizungumza na wawekezaji kutoka Kiwanda cha Pioneers Chemical Factory cha nchini Saudi Arabia aliokuja nao Tanzania kuangalia fursa za biashara na uwekezaji baada ya kumalizika kwa kikao chao na Mhe Waziri Mulamulajijini Dodoma

 

 

MBARONI KWA KUUZA JEZI BANDIA ZA YANGA

 No description available.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam ACP  Muliro Muliro akiwaonyesha waandishi wa habari jezi bandia za timu ya Yanga Afrika 1208 ambazo wamezibaini zinazotengenezwa na kusambazwa na kampuni ya GSM.

……………………

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam limewakamata watu 17 kwa tuhuma za kuuza jezi bandia za timu ya Yanga Afrika 1208 zinazotengenezwa na kusambazwa na kampuni ya GSM.

Kazi hiyo ilifanyika katika maeneo mbali mbali ya Jiji Dar es salaam,lakini pia kwa kushirikiana na baadhi ya mikoa nchini kwa kipindi cha kuanzia tarehe 02.01.2022 hadi tarehe 28.01.2022.

Katika Jiji la Dar es salaam Jeshi la Polisi limewakamata watuhumiwa watano, akiwemo Zahiri Hassan (17) Mmwera aliyekutwa huko Uwanja Benjamin William Mkapa akiwa na Jezi bandia za Timu ya Yanga 52, Kariakoo mtaa wa Agrey alikamatwa Majiba Ndahya (50) Msukuma akiwa na Jezi 124, Mohamed Ramadhani (26) Mchaga alikutwa na Jezi 86, John Staslaus (19) Mchaga alikamatwa na Jezi 39 Watuhumiwa hao waliwataja wenzao wa Zanzibar, ambapo Uwanja wa Amani watuhumiwa watatu walikutwa na Jezi bandia 36.

Jezi zingine bandia 134 zilipatikana kwa kushirikiana na Polisi Mkoa wa Tanga na Mwanza ambapo watuhumiwa tisa walikutwa na Jezi 811.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam linawatahadharishawananchi wote wanaojihusisha na vitendo vya kutengeneza, kuuza na kusambaza, bidhaa kwa kuiga au kufananisha nembo za biashara au huduma za watu wengine iliyosajiliwa kisheria, kufanya hivyo ni kosa nakinyume na sheria za nchi.

Jeshi la Polisi litashirikiana na mamlaka nyingine za kisheria ili kuona watuhumiwa wamechukuliwa hatua kali za kisheria

MULIRO J. MULIRO– ACP

KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM

DAR ES SALAM.

 

Saturday, December 11, 2021

SUBIRA MGALU AKABIDHI MATOFALI NIANJEMA NA MAPINGA

 No description available. 

MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa pwani, Subira Hamisi Mgalu (kulia) akimkabidhi Diwani wa kata ya Nianjema, Abdul Mzee Pyalla matofali kwaajili ya ujenzi wa choo katika shule ya mpya ya sekondari inayojengwa katika kata ya Nianjema Halamshauri ya Bagamoyo.

.........................................................

 

MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa pwani, Subira Hamisi Mgalu, ametoa Tofali 350 kusaidia ujenzi wa vyoo katika shule mpya za kata zinazojengwa Kata ya Nianjema na Mapinga zilizopo Halmashauri ya Bagamoyo  Mkoani humo.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi Tofali hizo akiwa kata ya Nianjema Halmashauri ya Bagamoyo, Mgalu alisema anamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassani kwa kutenga fedha kwa kila Halimashauri ili zitumike kujenga vyumba vya madarasa ambapo kwa kata za Nianjema na Napinga zimetumika kujenga shule mpya za kata ambazo hapo awali hazikuwepo.

Aliongeza kwa kusema kuwa licha ya fedha hizo zilizotolewa kwaajili ya ujenzi wa shule hiyo ya sekondari, bado baadhi ya kazi zinahitaaji kutekelezwa na Halmashauri,  wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo ili kufanikisha malengo hayo ambapo yeye Mbunge wa viti maalum, mkoa wa Pwani ambae pia ni mdau wa maendeleo alitoa ahadi ya kuchangia tofali na sasa ametekeleza.

Akielezea baadhi ya kazi ambazo zinahitaji kutekelezwa na Halmashauri,  wananchi na wadau mbalimbali ni pamoja ujenzi wa vyoo,

‘’ Nilipokuja Tarehe 21 mwezi wa 11 nilitoa ahadi ya kuchangia tofali 250 katika shule hii mpya ya Nianjema na Mwenyezimungu amenijaalia leo kutekeleza ahadi yangu’’ Alisema Mgalu.

Alisema mpaka sasa ameshatembelea shule 25 katika Halmashauri za Bagamoyo, Chalinze, Kibaha Mji, Kibaha Vijijini, Kisarawe, na Mkuranga ili kukagua miradi ya maendeleo na kuchangia kwa nafasi yake kama Mbunge anewakilisha Mkoa wa Pwani.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Nianjema Abdul Pyalla, amemshukuru Mbunge huyo kwa namna anavyoonyesha ushirikiano wa karibu katika mambo mbalimbali ya maendeleo.

Alisema Mh. Subira Mgalu ni mfano wa kuigwa kwani kwa hatua hii ya ujenzi ilipofikia tayari ameshatembelea mara tatu na hasa ikizingatiwa kuwa ana majukumu ya kutembea mkoa wote wa Pwani na hilo analifanya bila ya kuchoka.

 

Aidha, amewapongeza wananchi wa kata ya Nianjema kwa kujitolea mambo mbalimbali yanayohusu ujenzi huo wa shule mpya ya sekondari katika kata hiyo.

Alisema wananchi wa kata ya Nianjema ni waelewa na wpo tayari kwa kila wanachoshirikishwa kuhusu maendeleo ya kata yao.

Wakati huohuo amewashukuru wadau mbalimbali ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa ni wenye kujitolea hali na mali katika kufanikisha ujenzi huo

Ujenzi huo wa shule Kata za Nianjema na Mapinga unatekelezwa kupitia fedha zilizotolewa na Shirika la fedha la Kimataifa (IMF) kwaajili ya mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19, ambapo Halmashauri ya Bagamoyo imepokea shilingi Bilioni 1.4

No description available. 

MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa pwani, Subira Hamisi Mgalu akizungumza mara baada ya kukabidhi matofali kwaajili ya ujenzi wa choo  katika shule ya mpya ya sekondari inayojengwa katika kata ya Nianjema Halamshauri ya Bagamoyo.

No description available. 

MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa pwani, Subira Hamisi Mgalu, (kushoto) akipita eneo la ujenzi wa shule ya sekondari Nianjema kukagua kazi inavyoendelea, kulia ni Diwani wa kata ya Nianjema, Abdul Pyalla pamoja na Diwani wa kata ya Kisutu, Awesu Ramadhani.

No description available. No description available. 

MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa pwani, Subira Hamisi Mgalu, (kushoto) akipita eneo la ujenzi wa shule ya sekondari Nianjema kukagua kazi inavyoendelea, nyuma yake ni Diwani wa kata ya Nianjema, Abdul Pyalla pamoja na Diwani wa kata ya Kisutu, Awesu Ramadhani.

No description available.No description available.

MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa pwani, Subira Hamisi Mgalu, akiwa anachapia udongo kwenye moja ya chumba cha darasa katika ujenzi wa shule ya sekondari unaojengwa kata ya Nianjema Halmashauri ya Bagamoyo, Mgalu alifika eneo hilo la ujenzi kukaabidhi matofali yatakayotumika kujenga choo.