Sunday, October 28, 2018

PANGANI WAJIWEKA TAYARI KWA ZIARA YA WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA

MWENYEKITI wa Halmashauri ya wilaya ya Pangani Seif Ally akizungumza katika kikao hicho kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah kulia ni Katibu wa CCM wilaya ya Pangani
.................................


MKUU wa wilaya ya Pangani mkoani Tanga Zainabu Abdallah amewataka viongozi na wananchi wa wilaya hiyo kujitokeza kwa wingi kwenye mapokezi ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anayetarajiwa kuanza ziara wilayani humo Octoba 29 mwaka huu.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya Habari Mkuu wa wilaya hiyo mara baada ya kumalizika kikao cha maandalizi ya ziara hiyo aliwataka wananchi hao wakiwemo viongozi kujitokeza kwa wingi eneo la Mkwaja kwenye mapokezi hayo.

Alisema baada ya mapokezi hayo Waziri Mkuu anatarajiwa kuzungumza na wananchi kwenye maeneo ya Sakura,Mwera na Bomani Pangani mjini huku wananchi wakitakiwa kujumuika kwenye mikutano hiyo kwa wingi.


Hata hivyo aliwataka wananchio  kutumia fursa hiyo kwenda kumsikiliza Waziri Mkuu na kuwasihi wale watakaopata nafasi endapo itatolewa kuitumia kusema kwa niaba ya wana Pangani wengi na kueleza changamoto zao na kuzungumza na kiongozi wao aliekuja kwa ajili yao.


Katika hatua nyengine Mkuu wa Wilaya ya Pangani Zainab Abdallah kwenye muendelezo wa tamaduni ya ushirikiano na mshikamano wa viongozi katika wilaya ya Pangani amekutanisha  pamoja viongozi wote kwa kushirikisha Kamati ya ulinzi na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya,Halmashauri ya Wilaya ikiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Seif Ally,Mkurugenzi na wakuu wote wa Idara,Taasisi zote,Ofisi ya Mbunge,Kamati ya siasa ya chama Tawala(CCM),Madiwani wote,NGO’s,Viongozi wa Dini na viongozi wengine wote.

Lengo ni kuunganisha nguvu ya pamoja na kujiweka tayari kupokea ugeni mkubwa na wa heshima unaotarajiwa kutua wilayani hapa October 29 mwaka huu siku ya Jumatatu.

 

Katibu Tawala wa wilaya ya Pangani (DAS) Hassani Nyange akizungumza katika kikao hicho

Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gibson George akizungumza katika kikao hicho

MAGAZETI YA LEO OKTOBA 28 2018

 

Saturday, October 27, 2018

MAKAMU WA RAIS AENDELEA NA ZIARA WILAYANI KISARAWE

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Kisarawe ,Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais  TAMISEMI Mhe. Selemeni Jafo mara baada ya kukagua ujenzi wa mradi wa tenki la maji litakalokuwa na uwezo wa kubeba lita milioni 6 katika eneo la Mnarani Kisarawe. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasalimu wananchi mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara za lami Kisarawe mjini, Makamu wa Rais yupo wilayani Kisarawe ikiwa sehemu ya ziara yake ya siku sita ya kukagua na kuhamasisha shughuli za kimaendeleo mkoani Pwani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasalimu wananchi mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara za lami Kisarawe mjini, Makamu wa Rais yupo wilayani Kisarawe ikiwa sehemu ya ziara yake ya siku sita ya kukagua na kuhamasisha shughuli za kimaendeleo mkoani Pwani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA PWANI.