Saturday, April 1, 2017

AREF NAHDI WA TIF APEWA TUZO MAALUM YA UTENDAJI KAZI.


Mwenyekiti wa The Islamic Foundation, Aref Nahdi, kulia akikabidhiwa Tuzo na Balozi wa  Pakistani, Amiri Muhammad Khan wapili kushoto, wa  pili kulia ni Meya wa Manispaa ya  ilala Charles  Kuyeko, na wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Alhuda Center of Islamic Banking and Economics, ya nchini Dubai Muhammad Zuberi ambao ndiyo waliotowa Tuzo hiyo.
....................................
Mwenyekiti wa Taasisi ya The Islamic Foundation Aref Nahdi amekabidhiwa Tuzo na Shirika la Kimataifa linalotoa mafunzo  kwa Benki za  kiislamu na kusimamia Uchumi wa  kiislamu  la  Alhuda Center  of Islamic Banking and Economics, (CIBE) ambalo Makao yake makuu  nchini Dubay.


Tukio hilo limefanyika katika Mkutano wa  kujadili Uchumi wa  Kiislamu  na Changamoto zake kwa nchi za Afrika ambao umeandaliwa na CIBE, mkutano uliofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regence jijini Dar es Salaam
Akizungumza  mara baada ya kupokea tuzo hiyo,  Mwenyekiti wa The  Islamic Foundation Aref Mubaarak Nahdi, amesema zawadi hiyo imetolewa kutokana na kutambua mchango wa The Islamic Foundation katika jamii na kusema kuwa hiyo inatoa fursa kwa  Taasisi ya The Islamic Foundation kuongeza juhudi.

Alisema The Islamic  Foundation  inatekeleza wajibu  wake  kwa kumuogopa Mwenyezimungu na wala  sio kwa kuwaangalia watu na  kwamba juhudi zinazofanywa na The  Islamic Foundation ni kielelezo tosha  kwenye uso  dunia kwamba  The Islamic Foundation inatekeleza wajibu  wake.

Aliongeza kwa kusema kwa kujiangalia  mwenyewe huwezi kujua ukubwa wa mambo unayofanya lakini  sifa na  pongezi zinazotolewa na  watu ndio  zinazopelekea kutambua kuwa TIF  inafanya  mambo makubwa hapa nchini.

Aidha,  aliwataka watendaji  wote  wa The  Islamic Foundation  kwenye  kila kitengo  kuongeza juhudi  ya utendaji kazi  ili  kufanikisha malengo ya  kuutumikia uislamu na kuongeza  kuwa malipo yake hayawezi  kupimwa kwa macho ya kawaida na kwamba faida ya kuitumikia TIF kwa maslahi ya uslamu ni yamilele.

Mwenyekitihuyo wa The Islamic Foundation  amepokea Tuzo  hiyo  kutokana  na kazi  zinazofanywa na Taasisi anayoingoza kutekeleza  majukumu  yake kwa juhudi kubwa ya  kueneza Elimu  kwa jamii  ya Kiislamu na wananchi kwa ujumla.

Akielezea wakati wa  kukabidhiTuzo hiyo mzungumzaji kutoka shirika  lakimataifa  la Alhuda alisema Tuzo  hiyo inakwenda kwa  Aref  Nahdi  kutokana na  mchango wake  mkubwa  katika  kuupeleka  mbele uislamu  ambao mpakasasa inamiliki  Hospitali, Shule za Msingi na  Sekondari, Gazeti,  Kituo cha Redio na  Tevisheni.

Aliongeza kuwa katika  idara zake za Elimu TIF pamoja na vyombo vyake vya Habari imekuwa  mstari  wa mbele katika kutoa Elimu inayopelekea watu  kujua  ubaya wa riba na kupelekea watu wengi  kuongeza ufahamu kuhusu madhara ya Riba  na kufahamu njia sahihi za kukuza Uchum  kwa mujibu wa uislamu.

Mkutano huo  wa siku mbili wa  kujadili Uchumi wa Kiislamu Afrika umehuduriwa  na  nchi  kumi zaidi ya kumi ambapo kwa  pamoja  wamekubaliana  kuongeza Elimu juu ya  matumizi ya  Benki za  kiislamu, Uharamu  wa Riba  na kuzitaka  Serikali  za nchi za Afrika kutunga Sheria zitakazosimamia uendeshaji  wa Benki  za  Kiislamu.

Miongoni  mwa Taasisi zilizopata Tuzo ni  Amana  Bank, Ibni Jazari, ZIC  Takaful, IFM, NBC ISLAMIC  WINDOW, ICCIU Uganda, Gulf African Bank, Nairobi, FSDT, Dar es Salaam.
Mezani ni tuzo aliyopewa Mwenyekiti wa The Islamic Foundation (TIF) Aref Nahdi.
 Mkurugenzi wa Amana Bank, Dkt. Muhsin Masoud kulia akikabidhiwa Tuzo na Balozi wa  Pakistani, Amiri Muhammad Khan wapili kushoto, wa  pili kulia ni Meya wa Manispaa ya  ilala Charles  Kuyeko, na wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Alhuda Center of Islamic Banking and Economics, ya nchini Dubai Muhammad Zuberi ambao ndiyo waliotowa Tuzo hiyo.
Mwenyekiti wa The Islamic Foundation, Aref Nahd kulia, akikabidhi cheti kwa Mwenyekiti wa ZIC Takaful, Dkt. Muhammad Hafidhi Khalifa.

MAGAZETI YA LEO TAREHE 01 APRIL 2017.

TANZANIA KUPATA MEGAWATI 400 ZA UMEME KUTOKA ETHIOPIA

A 4
Tanzania inategemea kupata Megawati 400 za umeme kutoka Ethiopia ikiwa ni moja ya makubaliano yaliyofikiwa baada ya ziara ya kikazi ya siku mbili ya Waziri Mkuu wa Ethiopia Mhe.Haile Mariam Desalegn.
 
Hayo yamesemwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari juu ya makubaliano na mikataba ambayo nchi za Tanzania na Ethiopia wametiliana saini leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.

“Tukitaka kujenga uchumi wa viwanda ni lazima tuwe na umeme wa kutosha,wenzetu Ethiopia wametuonyesha njia na mimi nimemuomba Mhe.Waziri atusaidie wataalamu kutoka nchini kwake ili  waje  tuwaonyeshe maeneo mbalimbali watusaidie katika kupata umeme wa uhakika kwa kujenga mabwawa ya umeme ambayo yamesaidia sana katika kupatikana kwa umeme wa kutosha nchini kwao.”Aliongeza Rais Magufuli.

Aidha amesema kuwa kupatikana kwa umeme huo kutasaidia kuleta changamoto kwa shirika la umeme nchini katika kuwapatia wananchi bei ya chini na hivyo kuleta ushindani katika upatikanaji wa umeme nchini.

Kwa upande wake Waziri Mkuu wa Ethiopia Mhe.Haile Mariam Desalegn amesema kuwa wana mengi ya kujifunza kutoka Tanzania kwani nchi hizi mbili zina historia inayofanana na kuongeza kuwa hakuna haja ya wao kwenda nje ya Afrika kupata uzoefu katika masuala mbalimbali.

Ameongeza kuwa lengo kuu la kuja nchini ni kwa sababu anahamini nchi hizi mbili zinaweza kuunganisha nguvu zake na kuwa nguzo kuu katika maendeleo katika eneo la ukanda wa Afrika Mashariki na kati.

“Tanzania na Ethiopia ni nchi ambazo zina ushirikiano mzuri sana,sisi sio washindani bali tunasaidiana katika masuala mbalimbali kwani tumekuwa katika hatua mbalimbali za kuwaondoa wananchi wetu katika umaskini katika hatua zinazofanana,na huu ni wakati muafaka katika kuimarisha ushirikiano wetu kwa faida ya watu wetu kwa ujumla”Alisisitiza Mhe.Desalegn.

Aidha amesema  kuwa  mabadiliko  ya  kilimo  katika  nchi  zetu ndio  msingi  wa  maendeleo  pamoja  na  utumiaji  wa  teknolojia  bora utasaidia katika maendeleo ya viwanda vidogo vidogo.

Viongozi hawa wamekubaliana kushirikiana kwa kubadilishana uzoefu juu ya namna sekta mbalimbali zitakavyoleta manufaa ya kiuchumi zikiwemo huduma za benki, madini na gesi, elimu na  mawasiliano.

Ziara ya Waziri Mkuu Mhe. Haile Mariam Dessalegn imekuwa ya manufaa makubwa kwa Tanzania na amesisitiza kuwa wakati umefika wa kukuza biashara kati ya nchi hizi ambazo kwa sasa thamani ya biashara kati yake ni Dola za Marekani milioni 2.24 tu.