Friday, September 29, 2023

TUSIKIMBIE KUFANYA KAZI VIJIJINI - KIKWETE

 

Watumishi wa Serikali wametakiwa kuacha tabia ya kukimbia kufanya kazi sehemu wanazopangiwa na kuchagua sehemu wanazotaka wao.



Maneno hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Ndg. Ridhiwani Kikwete alipokuwa anazungumza na watumishi wa Halmashauri ya Chalinze katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri hiyo.


Ndg. Kikwete alitumia mkutano huo kuwakumbusha watumishi umuhimu wa kufanya kazi kuzingatia misingi ya kazi ikiwemo kujitambua na kutambua tunaowahudumia. 


Katika kusistiza utumishi wenye tija na weledi, Naibu Waziri huyo aliwakumbusha watumishi kuendelea kuwahudumia wananchi wote sawa na hakuna sababu ya kuchagua na kuweka madaraja katika utoaji wa huduma. 


Katika mkutano huo , Ndg. Kikwete alitumia nafasi hiyo pia kuwakumbusha umuhimu wa kutochagua vituo vya kazi huku akiwakumbusha kuwa uchaguzi wa Vituo vya kazi unalenga sio tu kuwasaidia baadhi lakini unatengeneza madaraja katika utumishi wa umma. 


Aidha, Kikwete alitumia nafasi hiyo kuwaasa watumishi wa umma kutochagua vituo vya kazi na badala yake mtumishi kila mtumishi anapopangiwa sehemu fulani ya kazi anapaswa kutekeleza kwa mujibu wa maelekezo.


Popote ambapo utapelekwa pana hadhi ya mtumishi kufanya kazi na kuwakumbusha hasa wazazi kuacha utaratibu wa kupiga simu za kuwaombea watoto wao vibali vya kuhamishwa vituo wapelekwe mijini. 


Katika kikao hicho Ndg. Kikwete pia aliwapongeza watumishi wa halmashauri hiyo kwa kazi nzuri wanayoifanya. 



MAGAZETI YA LEO IJUMAA TAREHE 29 SEPTEMBA 2023.

 


























Thursday, September 28, 2023

MAJALIWA: VIONGOZI WA DINI TUSHIRIKIANE KUPIGA VITA DAWA ZA KULEVYA

 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasihi viongozi wa madhehebu ya mbalimbali ya dini nchini waendelee kushirikiana na Serikali katika kupiga vita biashara na matumizi ya dawa za kulevya . 


 


"Tushirikiane kupambana na biashara na matumizi ya dawa za kulevya ambayo yameathiri zaidi vijana ambao ndio nguvu kazi ya Taifa." 


 


Mheshimiwa Majaliwa ameyasema hayo leo (Alhamisi, Septemba 28, 2023), alipomuwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Baraza la Maulid lililofanyika Kitaifa jijini Dodoma kwenye kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete.


 


“Matumizi ya dawa za kulevya yana madhara mengi kwa Taifa yakiwemo ya kiuchumi, kiafya na kimazingira pamoja na kuathiri uwezo wa mtu kufikiri”


 


Pia, Waziri Mkuu ametoa rai kwa viongozi wa dini waendelee kukemea vitendo vya mmomonyoko wa maadili katika jamii na wawahamasishe waumini kushiriki katika shughuli zitakazowaongezea kipato. 


 


Kadhalika, Waziri Mkuu amewataka wananchi waendelee kudumisha amani nchini kwa kuwa amani ni jambo la msingi katika maendeleo ya Taifa. "Tuendelee kuishi kwa amani na upendo pamoja na kuliombea dua Taifa na viongozi wakuu. " 


 


Wakati huo huo, Mheshimiwa Majaliwa ametumia fursa hiyo kuwahakikishia wananchi kuwa Serikali itaendelea kuwachukulia hatua wale wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa pamoja na matumizi mabaya ya madaraka, hivyo waendelee kuiamini Serikali yao. 


 


Awali, Katibu Mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Alhaj Nuhu Jabir Mruma amesema kuwa Baraza hizo linaridhishwa na utendaji kazi wa Rais Dkt. Samia za kuwaletea watanzania maendeleo katika Sekta za Uchumi, Siasa, Kijamii pamoja na kuboresha mfumo wa demokrasia nchini.


 


Aidha, Alhaj Mruma ametumia fursa hiyo kuiomba Serikali iongeze wigo wa kutoa elimu ya uraia kwa kushirikiana na viongozi wa dini ili kuwawezesha wananchi kupata uelewa na washiriki katika chaguzi zijazo ukiwemo wa Serikali za Mitaa inayotarajiwa kufanyika 2024. 










MAGAZETI YA LEO TAREHE 28 SEPTEMBA 2023.