Wednesday, November 8, 2023

SERIKALI YAWATAKA WAWEKEZAJI KUJENGA VIWANDA VYA KUONGEZA THAMANI MADINI MKAKATI

 

Mahenge kunufaika na mradi wa madini ya Kinywe

Kuboresha sekta ya Maji, Afya na Miundombinu

Korea Kusini yaridhishwa na miundombinu ya Reli nchini

Na.Samwel Mtuwa- Dodoma.

Tanzania imefungua milango ya uwekezaji katika Sekta ya Madini kwa nchi ya Korea ya Kusini ikiwemo kuendeleza ushirikiano wa kikazi katika kufanikisha utekelezaji wa mikakati ya Vision 2030:MadinI Maisha na Utajiri.

Hayo yamesemwa leo Novemba 8, 2023 na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde wakati wa mazungumzo ya ushirikiano wa kisekta baina ya Tanzania na Jamhuri ya Watu wa Korea Kusini yaliyofanyika jijini Dodoma.

Wakati akizungumza na ujumbe huo kuhusu uwepo wa madini , Waziri Mavunde amesema kuwa Tanzania imebarikiwa kuwa na madini ya aina mbalimbali yakiwemo madini mkakati kama vile madini ya kinywe, lithium , Nibioum na Makaa ya mawe ambayo kwasasa mataifa mengi yanatafuta kuwekeza huko kutokana na mabadiliko ya tabia nchi na maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Waziri Mavunde amezikaribisha kampuni mbalimbali kutoka Korea ya Kusini kuja kuwekeza Tanzani na kuwaeleza kuwa kwasasa sekta ya madini nchini Tanzania ipo na vision2030 ambayo lengo lake ni kupata taarifa za utafiti ambazo zitatoa dira ya uwekezaji na uendelezaji kwa kufungamanisha sekta za kiuchumi.

Akielezea kuhusu kufungua kiwanda cha uchakataji madini ya kinywe na uongezaji thamani madini nchini Tanzania , Mkurugenzi wa Kampuni ya POSCO ya nchini Korea Ji Ki Chun amesema , baada ya kukamilisha uchimbaji wa madini ya kinywe wilayani Mahenge watafungua kiwanda cha kuchakata madini ghafi ya Kinywe na uingezaji thamani kabla ya kusafirisha nje ya nchi.

Chun amefafanua kuwa menejimenti ya POSCO imeridhika na hali ya miundombinu nchini ikiwemo reli ya kati pamoja ujenzi wa SGR.

Naye , Balozi wa Korea ya Kusini nchini Tanzania Kim Sumpyo ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuimarisha uhusiano mzuri wa kiuchumi na serikali ya Korea Kusini amebainisha kuwa Korea Kusini ina mkataba wa hiyari katika ushirikiano wa kikazi ndani ya sekta ya madini hivyo itaendelea kutoa ushirikiano katika uwekezaji.

Balozi Sumpyo ameongeza kuwa mazingira salama na Sera nzuri zinavutia wawekezaji wetu na kuahidi kuendelea kuwaleta wawekezaji wengi kutoka nchini korea kusini kuja kuwekeza Tanzania.

Awali , akifungua mazungumzo hayo ya ushirikiano Katibu Mkuu Wizara ya Madini Kheri Mahimbali ameimshukuru Balozi wa Korea kusini nchini Tanzania kwa uwekezaji mzuri katika sekta ya madini akitolea mfano uwekezaji katika madini ya Kinywe wilayani Mahenge.

Mahimbali amemuomba Balozi Sumpyo kuendeleza ushirikiana na kubadilishana uzoefu wa kisekta baina ya wataalam wa Korea kusini na wataalam wa sekta ya madini Tanzania.

VISION2030: MADINI NI MAISHA NA UTAJIRI










EWURA ZINGATIENI MASLAHI YA NCHI KATIKA SHUGHULI ZA UDHIBITI WA MAFUTA NA MAJI -DKT. BITEKO

 

Awapongeza kwa kushusha gharama za uagizaji mafuta.


Asisitiza EWURA kudhibiti vitendo vya urasimu na rushwa mahali pa kazi.


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka Watendaji na Watumishi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kuzingatia maslahi ya Watanzania na maslahi ya nchi katika kazi zao za Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji ili Watanzania wapate huduma bora na kwa unafuu mkubwa.


Dkt. Biteko amesema hayo wakati akifungua Kikao cha Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Mamlaka hiyo kilichofanyika tarehe 8 Novemba, 2023 jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali akiwemo Naibu Katibu Mkuu wa TUGHE Taifa, Rugemalira Rutatinwa na Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Bi. Ziana Mlawa.


“Tambueni kuwa Taifa lina mategemeno makubwa na ninyi, hivyo fanyeni kazi zenu kwa weledi na ubunifu mkubwa unaoendana na kasi ya teknolojia na maendeleo ya dunia; kanuni na miongozo yenu mnayotumia katika utekelezaji wa majukumu iundwe katika mifumo rafiki kulingana na hali iliyopo ili ilenge kuleta matokeo chanya kwa ustawi wa Taifa na hivyo Watanzania waendelee kupata huduma bora na kwa gharama stahiki.” Amesema Dkt. Biteko.


Pia amewataka Watumishi wa EWURA kuweka mkazo kwenye kudhibiti vitendo vya urasimu na rushwa mahali pa kazi, kutoangalia maslahi binafsi wakati wa kutenda kazi ili kuepusha kuwaumiza Watanzania walio wengi, na ametoa wito kwa wafanyakazi hao kumkemea mtu yeyote anayeonekana kuwa na vitendo vya rushwa na ubinafsi katika eneo la kazi.


Vilevile, amewasisitiza Wafanyakazi wa EWURA kuwajibika ipasavyo katika kutekeleza majukumu yao kwa kuhakikisha kuwa Watoa Huduma wanafanya ushindani wenye tija na ufanisi wa kiuchumi, kulinda maslahi ya Walaji na mitaji ya kifedha ya Watoa Huduma pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa huduma kwa makundi yote ikiwemo ya watu wanaoishi vijijini.


Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Mkuu ameipongeza EWURA kwa kupitia upya gharama za uagizaji wa mafuta ambazo amesema kuwa, awali zilikuwa kubwa na zilikuwa zikipelekea athari mbalimbali ikiwemo kuongezeka kwa gharama katika Sekta ya Usafirishaji na Uzalishaji.


“Gharama hizi za uagizaji mafuta zilikuwa kubwa mno huku kukiwa hakuna sababu ya kuwa kubwa kwa kiasi hicho, niliwapa maelekezo mkazitazame upya, nashukuru mmeziangalia na ninafurahi kwamba zimeshuka na hivyo kupunguza makali kwa watumiaji." Amesema Dkt. Biteko.


Vilevile Naibu Waziri Mkuu ameiagiza TUGHE- Taifa kueleza juhudi zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita kuhusu masuala ya Wafanyakazi akitolea mfano upandishwaji madaraja wa mseleleko kwa watumishi ambao hawajapanda madaraja kwa muda mrefu. Amewataka pia kuwashirikisha wanachama wao ili kuisaidia Serikali katika kupeleka maendeleo kwa wananchi na pia kuikumbusha Serikali kutimiza wajibu wake kwa Wafanyakazi.


Awali, Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile alisema kuwa, Taasisi hiyo imeendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi lengo likiwa ni kuhakikisha Huduma za Nishati na Maji zinapatikana kwa uhakika, kwa kutosha, kwa uendelevu na kwa gharama ambazo wananchi wanazidumu.


Alimshukuru, Dkt. Biteko kwa kutoa ushirikiano mkubwa kwa Taasisi hiyo na miongozo anayotoa ambayo inafanya EWURA iendelee kuboresha utendaji wake katika kuhudumia Watanzania.


Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa EWURA kinachoendelea jijini Dodoma kimelenga kujadili masuala mbalimbali ikiwemo utekelezaji wa Bajeti ya EWURA kwa mwaka 2022/2023 na Taarifa ya Ukaguzi wa Hesabu za EWURA za mwaka 2022/23.










Tuesday, November 7, 2023

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 08 NOVEMBA 2023.

 















TANZANIA, EU KUSHIRIKIANA KUENDELEZA UCHUMI WA BLUU NCHINI

 

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amekutana na Mkurugenzi Mtendaji anayeshughulikia Sera za Uvuvi na Sheria za Masuala ya Bahari kutoka Umoja wa Ulaya (EU), Bi. Charlina Vitcheva kujadiliana namna wanavyoweza kuendelea kushirikiana katika kukuza uchumi wa buluu hapa nchini.


Waziri Ulega amekutana na Mkurugenzi huyo jijini Dar es Salaam leo Novemba 7, 2023.


Katika majadiliano yao wamezungumza namna ya kuendelea kufungua fursa za ajira na kukuza uchumi wa jamii hususan wanaoishi katika Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi kwa kuwawezesha zana za kisasa za uvuvi, ufugaji wa Samaki, Kilimo cha Mwani, ufugaji wa majongoo bahari na kaa.


Pia, majadiliano yao yalilenga katika utunzaji endelevu wa mazingira ya bahari wakati wote wa utekelezaji wa miradi ya ukuzaji uchumi wa buluu.


Aidha, Waziri Ulega alimueleza Mkurugenzi huyo kuhusu mradi wa kielelezo wa Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wa BBT- LIFE na kwamba waone namna wanavyoweza kuunga mkono jitihada hizo za kuendeleza vijana kupitia uchumi wa buluu.






WAFANYABIASHARA KISARAWE WALIA NA TRA.

 

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara (JWT),Hamis Livembe akizungumza na wafanyabiashara wilayani Kisarawe.

.....................................

Wafanyabiashara Kisarawe walia na TRA wasisitiza elimu ya mlipa kodi


Na Mwandishi Wetu, Kisarawe 


WAFANYABISHARA wilayani Kisarawe mkoani Pwani, wameiomba Mamlaka ya Mapato (TRA) kuwapa elimu ya kutosha kuhusu ulipaji kodi wa hiari na matumizi ya mashine za EFD.


Ombi hilo lilitolewa na baadhi ya wafanyabishara wilayani humo, wakati wa mkutano wao na viongozi wa Jumuiya ya Wafanyabishara (JWT) wakiongozwa na Mwenyekiti wake Hamis Livembe, wakiwa kwenye ziara ya kikazi ya kusikiliza kero mkoani humo.


Mfanyabishara Christina Mulu, amesema TRA wanatakiwa kuwapa elimu ya kutosha kuhusu ulipaji kodi badala ya kukazania kukusanya bila kuwasikiliza wafanyabishara kwanza.


"Wafanyabiashara wengi hatuna elimu ya kodi, matumizi ya EFD hatujui wakati mwingine risiti zinagoma kutoka na mashine kusumbua sasa TRA wakija wao ni kutaka tu kutoza faini badala ya kutupa elimu kwanza," amesema Mulu.


Mfanyabishara John Masine, amewataka TRA kuwasaidia wafanyabishara urahisi wa kupata kodi na kuwalinda kwa kuondoa wamachinga mbele ya fremu za biashara.


"Mfanyabishara amekodi nyumba analipa kodi TRA, lakini anakuja mmachinga anaweka kibanda mbele yake na anauza bidhaa zinazofanana kwa bei ya chini zaidi na wala halipi kodi yoyote TRA zaidi ya ushuru wa serikali ya mtaa na hakuna anayejali zaidi ya kutaka kukamua kodi bila kujua tunauza au laa," amesema Masine.


Naye Mfanyabishara Ester Moshi, ametaka wafanyabishara kutofunga biashara siku ya Jumamosi ya mwisho wa mwezi ambayo ni siku ya usafi kwasababu wanakwamisha shughuli za kiuchumi.


"Siyo kwamba siku hiyo biashara hazifanyiki hapana, zinafanyika lakini kwa kujificha na kukimbizana wakati serikali inaweza kupunguza muda ikawa muda wa kufungua ni saa 2 badala ya 4 asubuhi," amesema Moshi.


Naye Ofisa wa TRA wilayani humo, Mohamed Chifu, ameushukuru uongozi wa JWT, kwa kazi kubwa wanayofanya ya kusikiliza kero za wafanyabishara lakini pia kutoa majibu ya kina kuhusu mambo mbalimbali yanayowahusu.


Amesema changamoto kubwa wanayokutana nayo TRA wilayani humo ni wafanyabishara wengi kuwa wa hali ya kati ambapo wanalipa kodi ndogo.


"Wengi wao wanalipa kodi ya ndogo kwa sababu ya halihalisi ya biashara, haujawa mji wa biashara kubwa. Kero ambazo zinatuhusu nimezibeba na naahidi nitaziwasilisha na kuzifanyia kazi," amesema.




Baadhi ya wafanyabiashara wilayani Kisarawe 



 

UJENZI WA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA LA HOIMA UNASHIRIKISHA WAZAWA MKOANI KAGERA

 

Wakandarasi na wa watoa huduma 42 wapatiwa kazi


Dodoma


Imeelezwa kuwa ujenzi wa Mradi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani mkoani Tanga unashirikisha wakandarasi wazawa kutoka mkoani Kagera.


Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga, kwa niaba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko wakati alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu kutoka mkoani Kagera Mhe. Neema Kichiki Lugangira aliyetaka kujua je ni wakandarasi wangapi kutoka mkoani Kagera wamepata kazi katika mnyororo wa ujenzi wa bomba la mafuta la Hoima mkoani Tanga. 


Mhe. Kapinga amesema kuwa wakandarasi wakuu wa Mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani mkoani Tanga wanaendelea kushirikiana na wakandarasi wadogo, wajenzi na na wanna huduma mbalimbali katika mikoa yote inayopitiwa na Mradi. 


Mhe. kapinga aliongeza kuwa jumla ya wakandarasi na watoa huduma 42 wamepata kazi mbalimbali katika mnyororo wa thamani wa ujenzi wa Mradi huu ikiwemo uuzaji wa vifaa vya ujenzi, huduma za usambazaji wa mafuta, huduma za umeme na hoteli. 

MAGAZETI YA TANZANIA LEO TAREHE 07 NOVEMBA 2023