Saturday, November 3, 2018

KATIBU MKUU MEJA JENERALI KINGU AONGOZA KIKAO CHA WATENDAJI WAKUU WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI, KUJADILI HOJA ZA KAMATI ZA BUNGE ZA PAC NA NUU, JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu (katikati) akiongoza kikao cha Watendaji Wakuu wa Wizara yake, cha kujadili hoja zilizotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) na Kamati ya Kudumu ya Bunge Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), katika Ukumbi wa Mikutano wa ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar es Salaam leo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu (kulia) akiongoza kikao cha Watendaji Wakuu wa Wizara yake, cha kujadili hoja zilizotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) na Kamati ya Kudumu ya Bunge Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), katika Ukumbi wa Mikutano wa ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar es Salaam leo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu (kushoto) akitaka ufafanuzi kutoka kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, (CGP), Phaustine Kasike, katika kikao cha Watendaji Wakuu wa Wizara yake, cha kujadili hoja zilizotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) na Kamati ya Kudumu ya Bunge Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), katika Ukumbi wa Mikutano wa ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar es Salaam leo.


Picha zote na Wizara ya Mambo ya ndani ya Nchi.

ARUSHA KUJA NA VITUO 4 MAALUMU VYA POLISI VILIVYOGHARIMU ZAIDI YA MIL. 80

Mkuu wa mkoa Mrisho Gambo
  
Kikao cha Sekta ya wadau wa Utalii kimefanyika Mkoani Arusha kikiwa na lengo la kuona namna wanatekeleza azimio la kusimika vituo vinne Maalum vya Polisi kwa ajili ya Ukaguzi wa magari yanayosafirisha watalii.

Kikao hicho kilichohudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta ya utalii ambapo Mkuu wa mkoa Mrisho Gambo amesisitiza azma yake katika kuhakikisha utalii unatengenezewa mazingira mazuri ya ukuaji.

Hakuna kitu kinatupa sifa mbaya kwa wageni kama kusimamishwa na askari kila baada ya kilomita moja”alisema Gambo


Amesema Vituo hivyo maalum vya ukaguzi  vitasaidia kuondokana na changamoto hiyo kwakuwa sekta ya utalii inategemewa sana katika kuliingizia taifa pato

“Magari yote yatakua na vituo maalum vya ukaguzi, tunafanya yote haya kwakua sekta ya utalii tunaitegemea sana kama taifa kwa kutuingizia pato la taifa.” Alisema Gambo.

Vituo hivyo vinne vinavyogharimu zaidi ya shilingi Milioni 80 vimetengenezwa kwa michango ya wafanyabiashara ya Utalii TATO na vinatarajiwa kuwekwa katika maeneo ya Kikatiti, Ngaramtoni, Makuyuni na Karatu.

Kwa upande wa serikali kupitia mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro na TANAPA, Mkurugenzi mkuu wa hifadhi za Taifa Dr. Kijazi amesema wao kama wadau wa mkubwa wa sekta hii wanaunga mkono wazo hili na wako tayari kuhakikisha taasisi zao zinajenga vyoo katika vituo hivi.

Sisi kama hifadhi za Taifa ni wanufaika namba moja endapo sekta hii inaboreshewa mazingira, na kwa kuunga mkono jitihada hizi mimi na wenzangu wa mamlaka ya Ngorongoro tunaahidi kujenga vyoo katika vituo vyote vinne kwa kushirikiana na ofisi za wakuu wa wilaya” alisema Kijazi.

Kwa niaba ya wafanyabiashara ya utalii Bwana Sirili Nko ambaye ni Katibu wa TATO, ametoa pongezi kwa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha kwa kuonyesha juhudi za kUkuzaji na kUboresha sekta ya Utalii Mkoani Arusha.

Toka kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha Gambo amefanya jitihada nyingi za kuboresha sekta ya utalii kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

Kutoka kushoto ni mhifadhi mkuu wa mamlaka ya  Ngorongoro Dkt. Fredy Manongi akifuatiwa na Mkurugenzi wa TANAPA Dr. Alan Kijaz

NAIBU WAZIRI WA AFYA AWAPA SOMO WANANCHI KUHUSU UGONJWA WA U.T.I

Wananchi wametakiwa kuwa na tabia ya kuhoji wahudumu wa afya kabla ya kuanza kutumia madawa wanayopatiwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Aidha wahudumu wa afya wametakiwa kuwauliza maswali wagonjwa kabla ya kuwapatia vipimo ili kujua historia ya tatizo linalomsumbua na kutoa dawa sahihi.

Agizo hilo limetolewa na Naibu waziri wa afya Jinsia Wazee na Watoto Dr.Faustine Ndugulile akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Manyara ambapo amesema, wananchi wananyweshwa madawa mengi ambayo hayana msingi hali inayowasababishia kupata matatizo mengine ya  kiafya.

Amesema kitaalamu asilimia zaidi ya themanini 80% ya Homa ambazo watanzania wanaugua si malaria,Typhod wala U.T.I, bali homa nyingi zinasababishwa na virusi ambayo havina tiba isipokuwa ni ugonjwa ataokaupata baada ya siku tatu hadi wiki moja mgonjwa anapata nafuu.

Naibu Waziri Dr. Ndugulie alisema Vipimo vya magonjwa ya  UTI na Typhod havipimwi kwa dakika 10 au saa kama inavyofanyika kwa sasa bali ni mchakato wa zaidi ya masaa 48 hadi 72 ndipo vimelea vya ugonjwa huo viweze kuonekana.

“Mwananchi ukienda kwenye kituo cha kutolea huduma ya afya na ndani ya dakika 15  ukaambiwa unagua UTI au Typhod muulize daktari maswali ya msingi,wewe umweza kumebaini ugonjwa huu kwa kutumia njia gani?”alisisitiza Dr.Ndugulile

Dr.Ndugulile amesema kinachofanywa katika vituo vya kutolea huduma ya afya ni Biashara na sio kumtibu mgonjwa kwa dawa inayoendana na ugonjwa  unaosibu.

Naibu waziri wa Afya,Maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dr. Faustine Ndugulile ametembelea hospitali ya rufaa ya mkoa wa Manyara kukagua  shughuli mbali mbali  ambazo zinatekelezwa chini ya wizara ya afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia wazee na watoto kupitia idara zake kuu mbili za Afya pamoja na Maendeleo ya jamii.

Amesema wizara ya Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia wazee na watoto inaendelea kujipanga kuhakikisha huduma katika hospitali za rufaa za mkoa zinaboreshwa na kuendelezwa ambapo katika bajeti ya mwaka 2018/2019 serikali imetenga shilingi Bilioni 30 kwa ajili ya kuimarisha hospitali za rufaa zilizopo na kujenga nyingine mbili mpya katika mkoa wa Simiyu na Njombe ambapo  maeneo yatakayopewa kipa umbele katika hospitali hizo ni huduma ya magonjwa ya dharura,chumba cha wagonjwa mahututi kwa watoto na watu wazima,kuimarisha huduma ya mama na mtoto.

Pamoja na yote hayo Dr.Ndugulile amwaleza watanzania kuwa serikali imeendelea kupambana na ugonjwa Malaria mabo hadi kufikia sasas mwaka 2018  ugonjwa huo umepungua toka asilimia 14% Miaka miwili iliyopita hadi kufikia asilimia 7%