Thursday, October 18, 2018

WAANDISHI WA HABARI ZA KILIMO, SAYANSI, WATUNIKIWA VYETI.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Tekonolojia (COSTECH), Dkt. Amos Nungu, akimkabidhi cheti, Mwandishi wa habari Alex Mathias Sonna kutoka Mtandao wa Fullshangweblog baada ya kushiriki mafunzo ya Waandishi wa habari za Kilimo Sayansi yaliyofanyika Jijini Dodoma.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Tekonolojia (COSTECH), Dkt. Amos Nungu, akimkabidhi cheti, Mwandishi wa habari Suleiman Msuya, baada ya kushiriki mafunzo ya kuandika habari za Teknolojia ya Uhandisi Jeni (GMO), yaliyofanyika New Dodoma Hoteli mkoani Dodoma na kuibuka Mshindi wa Pili katika Mashindano ya uandishi wa habari  juu ya teknolojia hiyo kwa kundi la Waandishi wa habari za magazeti. Mafunzo hayo yaliandaliwa na Jukwaa la Wazi la Kilimo na Teknolojia Afrika (OFAB) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Cornell cha Marekani, Cornell Alliance For Science na African Agricutural Technology Foundation (AATF). 
Mshindi wa  Kwanza kwa upande wa Waandishi wa Habari za Magazetini Bw. Daniel Mkate kutoka Nipashe akipokea cheti.

 Mshindi wa kwanza wa kuandika habari hizo kwa njia ya redio katika mafunzo hayo, Kemsi Fadhil akipokea cheti.

 
Mshindi wa pili wa kuandika habari za GMO kwa njia ya Televisheni, Vumilia Kondo akipokea cheti.
 

Mshindi wa kwanza wa kuandika habari za GMO kwa njia ya Televisheni katika mafunzo hayo, Doreen Mlay kutoka TBC akipokea cheti.

 Mshindi wa jumla wa kuandika habari za GMO kwa njia ya magazeti katika mafunzo hayo, Rose Milondo akikabidhiwa cheti.
 

 Mwanahabari Dotto Mwaibale akipokea cheti cha ushiriki.

Meza kuu wakati wa utoaji wa vyeti hivyo.

 
Picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa mafunzo ya Semina kwa Wandishi wa habari za Kilimo Sayansi iliyofanyika Jijini Dodoma.



MWAMBISI SEKONDARI KIBAHA WALILIA UMEME

Na Omary Mngindo, Kongowe

SHULE ya sekondari ya Mwambisi Forest iliyoko Kata ya Kongowe Kibaha Mji Mkoa wa Pwani, haina huduma ya umeme kwa kipindi cha miaka sita sasa, tangu kuanzishwa kwa shule hiyo.

Shule hiyo ambayo inapakana na Hifadhi ya Msitu wa Kongowe mjini hapa (Kongowe Forest) ipo umbali wa mita 100, ambao ni sawa na urefu wa nguzo mbili za umeme ili ufike shuleni hapo.

Hayo yamebainika katika taarifa ya Wahitimu wa kidato cha nne shuleni hapo, iliyosomwa na wanafunzi Leah Samson na Fahad Salimu mbele ya mgeni rasmi Nabii Jofrey, Mwalimu Mkuu Josefu Simba na diwani wa Kata hiyo Idd Kanyalu.

Imeeleza kuwa kukosekana kwa nishati hiyo kunachangia kushindwa kutumika baadhi ya vifaa ambavyo vingesaidia kuboresha taaluma, pia ulinzi wa mali zilizopo shuleni hapo, na kwamba ulipoishia umeme kuna umbali wa mita 100 sawa na nguzo mbili.

"Mbali ya ukosefu wa umeme, changamoto nyingine ni uhaba wa vyumba vya madarasa, viti, meza, jengo la Utawala, ongezeko la wanafunzi, upingufu wa vifaa vya kujifunzia, uzio na idadi ndogo ya walimu wa somo la Baiolojia," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Akizungumza na wahitimu hao, Nabii Jofrey alisema kuwa amepokea changamoto hizo, huku baadhi yake akazitolea majibu hapahapo nyingine akiahidi kuzibeba kwa lengo la kwenda kuzitafutia ufumbuzi.

"Nitatengeneza meza 18 za walimu, nitanunua vitabu nitavyoelekezwa vya kiada pamoja na vifaa mbalimbali kwa ajili ya kufundishia," alisema Nabii Josefu.

Awali mwalimu Simba alisema kwamba shule hiyo pamoja na kuwa ya mfano katika utunzaji wa mazingira, wanaushukuru uongozi wa Hifadhi ya Misitu Kongowe kwa kuwapatia miti na wataalamu wa kutoa elimu ya utunzaji wa mazingira.

Kwa upande wake Diwani Kanyalu alianza kwa kumshukuru mgeni rasmi kwa kukubali mwaliko huo, huku akieleza kwamba anaimani kubwa kwamba changamoto alizoziahidi atazitekeleza mapema iwezekanavyo.