Wednesday, September 3, 2025

WANANCHI WINDE BAGAMOYO, WASHANGAZWA NA KUPANDWA MAWE MAPYA KWENYE ENEO LAO.

 

Wananchi wazawa wa eneo la Winde lililopo kitongoji cha Mkwajuni kata ya Makurunge wilayani Bagamoyo wameshangazwa na uwepo wa mawe yanayoashiria mipaka mipya ndani ya eneo lao.


Wakiongea siku ya tarehe 30 Septemba 2025 katika mkutano ulioitishwa na wananchi hao ili kujadili mambo mbalimbali yanayohusu eneo lao wamesema wao ndio wenye eneo hilo na tayari baadhi ya familia wamefuata taratibu za kupima eneo hilo kisheria lakini chakushangaza yanaonekana mawe katika eneo hilo.


Mwenyekiti wa Wananchi hao, Muharami Seleman amesema kuwa eneo hilo ni mji wa Kale ambao una historia kubwa hivyo kuna haja ya kuuenzi kwa kuurasimisha na kuweka huduma za kijamii.


Seleman amesema kuwa moja ya vitu vya kihistoria ni uwepo wa kaburi lililopo hapo tangu mwaka 1,532 la mtu mweusi, visima vya maji ambayo yanatumika hadi hivi sasa.


Amesema kuwa pia eneo hilo maarufu kama namba 56 kuna mji ambao umezama baharini kwani unapakana na bahari, magofu ya kale, vyungu vya kupikia na kuna maeneo kwa ajili ya mila na tamaduni.


Aidha amesema kuwa Mji huo ulitambuliwa na Waingereza hata kwenye ramani ya maeneo waliyoyatawala unaonekana mji huo ambapo wao wamerithi kutoka kwa wazee wao ambao ni kaya 45 ndizo zinazomiliki ambapo ni jumla ya watu 4,500 kutoka vizazi vilivyotokana na wazee wa eneo hilo lenye ukubwa wa hekta 6,000.


Miraji Miraji ambae ni miomgoni mwa viongozi wa wananchi hao  wa eneo la Winde alisema kuwa amefuatilia sakata hilo kwa muda mrefu huku akieleza kuwa wakati linafikia hatua nzuri wanashangaa kuona maeneo hayo yamepandwa mawe.


"Cha kushangaza mawe yamepandwa na hata Mwenyekiti wa Kitongoji hana taarifa ya kupandwa kwa mawe hayo," alieleza Miraji.


Kwa upande wake mwana Winde,  Mussa Iddi amesema kuwa yeye alikuwepo eneo hilo mwaka 1953 akiwa anasoma hivyo historia ya hapo anaijua vizuri na kupitia wazazi wao walidai uhuru wa Tanzania.


Mussa amesema wanaomba eneo hilo lipimwe ili kuwe na huduma za kijami ili kuwe na makazi ya watu kwa kufuata utaratibu wa urasimishaji ardhi ili watu wamiliki kisheria.


Naye Wasaka Mnane mwenyekiti wa Kitongoji cha Mkwajuni lilipo eneo hilo amesema kuwa wanatambua eneo na kwamba  kinachotakiwa ni kufuata taratibu za urasimishaji ardhi  zilishaanza ambapo pia kuna baadhi ya watu wameingia kinyume cha utaratibu.


Mnane amesema kuwa wana Winde wanapaswa kuwa wamoja na kushirikiana ili waweze kuleta maendeleo yao na familia zao.


Katika kikao hicho walifanya uchaguzi wa kusimamia mambo yao ambapo Muharam Selemani amechaguliwa, kuwa Mwenyekiti mpya wa wana Winde.




Monday, September 1, 2025

DUA MAALUM KWA TAIFA NA RAIS SAMIA YAFANA DAR

 


Na Rashid Mtagaluka


Tukio la Dua ya kuiombea Taifa na Rais Samia Suluhu Hassan lililofanyika Tarehe 31 Agosti 2025 katika ukumbi wa DRIMP, Ilala Boma, ni kielelezo cha namna Watanzania wanavyotambua dhamana kubwa aliyoibeba Rais katika kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025. 


Dua hiyo iliyoongozwa na Sheikh Adam Mwinyipingu wa BAKWATA Ilala, imekusanya makundi mbalimbali ya kijamii wanawake, wanaume, vijana kwa wazee, ikiwa ni alama ya mshikimano wa kitaifa.


Kinachovutia zaidi ni kwamba tukio hili limeandaliwa na mwanadada jasiri na mwandishi wa habari anayeheshimika, Fatma Jalala, kupitia taasisi yake ya Seed of Changes. 


Hii ni ishara kwamba vijana, hususan wanawake, wanajitokeza mbele sio tu kama wachambuzi wa habari, bali pia kama wabunifu wa matukio yenye tija kubwa kwa taifa. 


Licha ya changamoto za kiutekelezaji, Fatma hakusita kuchukua jukumu la kuandaa tukio kubwa la kuliombea taifa na kiongozi wake mkuu jambo linaloonyesha uthubutu, uzalendo na imani ya dhati katika uongozi wa Rais Samia.


 Katika kuliombea taifa, Dkt. Samia na viongozi wengine wote  wa vyama 18 vyenye wagombea waliotia nia. 


Aidha dua hiyo iliyojulikana kwa jina la Munajjat ya Samia na Taifa ilibeba Kauli mbiu inayosema, " Bila Amani hakuna ndoto inayotimia"


 ujumbe ambao umebeba dhamira ya dhati ya kuwasisitiza Watanzania kuwa na wivu mkubwa na amani waliyonayo, hivyo wailinde na kuzidi kumuomba Mungu ajaalie amani na utulivu uliopo nchini udumu.


Kwa upande wa Rais Samia, dua hii ni ujumbe mzito kwamba wananchi wanamuona kama dira ya matumaini, kiongozi anayebeba maono ya mshikamo na maendeleo ya Watanzania wote. 


Ni heshima na upendo wa wananchi kwa kiongozi wao, wakimuombea apate nguvu, ulinzi na ujasiri wa kukabiliana na vikwazo vinavyoweza kuibuka katika safari ya kuelekea uchaguzi.


Kwa hakika, tukio hili linapaswa kuwa somo kwa vijana wengine nchini: kwamba mabadiliko na mafanikio makubwa hayahitaji kusubiri misaada ya nje, bali uthubutu, dhamira na moyo wa kujitolea kwa ajili ya taifa.




 

Sunday, August 31, 2025

MLIPUKO WAUA WAWILI BAGAMOYO

 


Watu wawili wamefariki dunia na mmoja kujeruhiwa baada ya kutokea mlipuko ambao bado haujafahamika ni wa kitu gani.


Akitoa Taarifa kwa vyombo vya habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Salim Morcase, amesema tukio hilo limetokea leo tarehe 31 Agosti 2025 Mtaa wa kichemchem kata ya Nianjema wilayani Bagamoyo majira ya saa moja na dakika ishirini asubui.


Amesema chanzo cha vifo hivyo ni mlipuko wa chuma ambacho Doto Mrisho (Marehemu) alikuwa anakikata kwenye karakana yake ya kuchomelea mageti.


Waliofariki katika tukio hilo ni Doto Mrisho mwenye umri wa miaka 24 fundi wa kuchomelea mageti mkazi wa kichemchem kata ya Nianjema na Saidi Ramadhani mwenye umri wa miaka 53 mkazi wa Sanzale Bagamoyo, na aliyejeruhuwa katika tukio hilo ni  Hassan Omari, mkazi wa Sanzale Bagamoyo.


Kamanda Morcase amesema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea kufanyika na jeshi la polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama ili kubaini chanzo cha mlipuko huo na ni wa kitu gani.



Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linatoa wito kwa baadhi ya wananchi wenye tabia ya kuokota vyuma ambavyo hawavijui na pia waache tabia ya kukata vyuma ambavyo ni aina ya mitungi ya gesi, au chochote chenye duara au mfano wa kibuyu kidogo kilichozibwa ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza.

Thursday, August 14, 2025

MARIAN SCHOOLS MARATHON NI KESHO

 



Na Albert Thomas Kawogo.

TAASISI ya Marian Schools Bagamoyo imeandaa mbio za marathon MARIAN SCHOOLS MARATHON 2025 zitakazofanyika Bagamoyo Ijumaa ya tarehe 15  Agosti.


Msemaji wa Marian Schools, Ohsana Mnalunde amesema mbio hizo zitaanzia kwenye kijiji cha Zinga Samakisamaki na kumalizikia kwenye hoteli ya Stella Maris Bagamoyo mjini.


Mnalunde amesema tayari zaidi ya washiriki 5,000 wamethibitisha ushiriki wao huku idadi kubwa ya watu wa Bagamoyo ikionyesha nia ya kushirki mbio hizo.



Msemaji huyo amesema mgawanyo wa mbio hizo ni wa km 21, km 10 na km 5 ambapo idadi ya washiriki watarajiwa ni wanafunzi, wazazi,  wafanyakazi, walimu na wakuu wa mashrika ya serikali na binafsi pamoja na wafanyakazi wao.


Naye Meneja wa Taasisi za Marian Schools Padre Valentine Bayo amewataka watu wengi kujitokeza kujisajili ili waweze kushiriki kwani kukimbia ni afya na  kunasaidia kupunguza kasi ya magonjwa yasiyoambukiza (NCDs) kama shinikizo la damu sukari na moyo ambayo huchangia zaidi ya asilimia 30 ya vifo vyote hapa nchini.


Padre Bayo ambaye pia ni mwanzilishi wa shule za Marian amesema watu wanaingia gharama kubwa kutibu magonjwa yatokanayo na uzito wa kupindukia lakini kama wangejenga utamaduni wa kufanya mazoezi hasa kukimbia wangeepuka magonjwa hayo.


Mbio hizo ambazo kwa mwaka huu zinatimiza miaka mitatu sasa zimedhaminiwa na Benki ya KCB.

Tuesday, August 12, 2025

TBN YAKEMEA 'MANABII' WA MITANDAONI, KWA UTABIRI WAO UNAOLETA TAHARUKI KWA JAMII.

 

Mkuu wa Mawasiliano Serikalini, Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, (PDPC) Innocent Mungy, akizungumza katika mafunzo hayo.


Na Mwandishi wetu, Dar es salaam.


Mtandao wa Bloga Tanzania (TBN) umekemea vikali tabia inayoshamiri ya watu kujinadi kufanya utabiri kwa watu na taifa kupitia mitandao ya kijamii, ukisema vitendo hivyo vinakiuka Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi.


Kauli hiyo imetolewa kama azimio katika kikao kazi cha mafunzo ya mabloga kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.


Mabloga hao wameitaka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) kushirikiana kuwasaka na kuwachukulia hatua kali wale wote wanaohusika na vitendo hivyo.


Katika kikao hicho, mabloga walibainisha kuwa kumeibuka kundi la watu wanaodai kuwa ni manabii na kutoa kauli zinazokiuka sheria za nchi na kuleta taharuki kuelekea uchaguzi mkuu.


Wakitolea mfano wa kauli hizo ni kama vile kusema kutatokea kifo cha kiongozi mkubwa siku za hivi karibuni, au kutatokea machafuko fulani, na kusema kuwa kauli hizo ni za kuleta taharuki kwa wananchi na kukiuka sheria ya ulinzi wa taarifa binafsi.


Walisisitiza kuwa baada ya kuchambua Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (Personal Data Protection Act), walibaini kwamba 'utabiri' wa namna hiyo unavuruga haki ya msingi ya faragha ya wahusika.


Akizungumza katika mafunzo hayo, Mkuu wa Mawasiliani Serikalini, Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, (PDPC) Innocent Mungy, amesema sheria  inakataza kutoa Taarifa za mtu binafsi bila ya ridhaa yake.


Aliongeza kwa kusema kuwa, katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wapo watu watatoa taarifa za Afya ya mtu kwa lengo la kumharibia ili asichaguliwe jambo ambalo ni kosa kisheria.


Mungy alisisitiza kuwa sheria hiyo ina adhabu kali na lazima ifuatwe na kila mtu, si tu mabloga na waandishi wa habari.


Mafunzo hayo yaliyoratibiwa na TCRA, yalilenga kuwaandaa mabloga kuripoti habari za uchaguzi kwa weledi na uadilifu. 


Pamoja na mada ya ulinzi wa taarifa binafsi, mada nyingine muhimu zilizotolewa ni pamoja na Mwongozo wa Waandishi wa Habari katika Uchaguzi na Matumizi ya Akili Mnemba (AI) katika uandishi wa habari.


Lengo kuu la mafunzo haya ni kuongeza uwezo wa mabloga kuhakikisha wanafuata sheria na maadili ya uandishi, jambo linalotazamiwa kuchangia mazingira ya uchaguzi yenye amani na utulivu.

Meneja wa Huduma za Utangazaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mhandisi Andrew Kisaka, akiwasilisha mada katika mafunzo maalumu kuelekea uchaguzi mkuu mahususi kwa bloga yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Agosti 11, 2025 Jijini Dar es Salaam








Monday, August 4, 2025

TCRA YAWAFUNDA BLOGA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025

 

Na Mwandishi Wetu

Wazalishaji wa Maudhui Mtandaoni, wameaswa kutotoa taarifa ambazo zitaleta taharuki na machafuko ndani ya nchi hasa katika kuelekea kipindi cha Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge  na Madiwani  utakao fanyika baadaye mwaka huu (2025).


Yamesemwa hayo jana tarehe 3, Agosti 2025 na Meneja Kitengo cha Huduma za Utangazaji,TCRA, Injinia Andrew Kisaka wakati  akiwasilisha makala (mada) katika mkutano ulioandaliwa na  wa  Tume Huru ya Uchaguzi nchini (INEC) kwa  watoa maudhui mtandaoni, amesema kuwa wakati wa uchaguzi kuna mazingira ya migawanyiko, mivutano ya kijamii, na upotoshaji wa hali ya juu hivyo ni muhimu  Mabloga waepuke  kuepuka kusambaza uvumi, kuripoti kwa umakini, kutopendelea upande wowote  na kukemea lugha za chuki.


Kisaka amewataka  bloga nchini kote  kuimarisha maadili yao na kuchukua jukumu muhimu katika kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani kwa kupandisha maudhui yenye tija na kama unaona maudhui yataleta taharuki  ni bora kuachana nayo.


Aidha Kisaka ametoa mfano wa  Historia ya machafuko ya uchaguzi yaliyotea katika nchi Kenya  Nigeria (2007) na Kenya (2011), amesema kuwa, katika machafuko hayo zaidi ya watu 800 walipoteza uhai nchini Nigeria mwaka 2011 wakati nchini Kenya zaidi ya watu 1,000 walipoteza uhai na wengine 600,000 kupoteza makazi.


Aidha amesema kuwa  katika mazingira magumu yenye shinikizo la juu la uchaguzi, vyombo vya habari vinaweza kujikuta vikichangia machafuko kwa kueneza uvumi au kuchochea upendeleo wa kisiasa.


Amesema ili kukabiliana na maafa wakati wa uchaguzi na baada kuna miongozo ya kuripoti ambayo inatatua changamoto hizo.


"Uvumi ndiyo chanzo kikuu cha vurugu hivyo  Vyombo vya habari vinapaswa kuchunguza kwa kina uvumi na kutoa taarifa sahihi haraka iwezekanavyo ili kuzuia mzunguko wa vurugu za kulipiza kisasi." amesema Mhandisi Kisaka.


Pia amehimiza Mabloga  kukataa lugha na vichwa vya Habari vya Kichochezi.


"Msiripoti kila kauli ya uchochezi kutoka kwa wanasiasa ,hata kama kauli hizo zinaonekana kuwa habari kwenu na zenye kuvutia msomaji acha kabisa ni muhimu kutokuzirudia kwenye vichwa vya habari, " amesema Mhandisi Kisaka na kuongeza kuwa lugha inayodhalilisha inaweza kuchochea wananchi kutenda vitendo vya kikatili.


Aidha amesema kuwa  katika kipindi hiki cha uchaguzi, ni  vyema Bloga kuchukua tahadhari binafsi  kutoa  matangazo ya moja kwa moja 'live'   ya mikutano ya kampeni za wagombea kwa sababu yanaweza leta  machafuko.


"Matangazo ya moja kwa moja 'live'  ya machafuko ya uchaguzi yanatakiwa kufanywa na Waandishi Waandamizi na  wenye  uzoefu na siyo 'One Man Show' kama ilivyo kwa Bloga .
Wanaohamasisha chuki na vurugu hawapaswi kupewa nafasi hewani," amesema Mhandisi Kisaka.

Aidha amesema kuwa  vyombo vya habari vinapaswa kuzuia kuonesha picha zinazochochea vurugu  na ikiwa  ni lazima, kusimamisha matangazo ya moja kwa moja ili kuzuia hali kuwa mbaya zaidi.


Maafa na miongozo ya kuripoti
katika hali ambapo uchaguzi unafanyika wakati wa maafa, ni sehemu ya elimu zinazotolewa kwa   Mabloga katika kuhakikisha taifa linavuka salama katika uchaguzi wa mwaka 2025 kama ilivyokuwa katika chaguzi nyingine.


WAZALISHAJI WA MAUDHUI MTANDAONI WAHIMIZWA KUHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2025

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutanio wa Tume na Wazalishaji Maudhui Mtandaoni kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 03 , 2025.

 

Baadhi ya wawakilishi wa serikali waliohudhuria mkutano huo.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg.Kailima Ramadhani akitoa mada wakati wa ufunguzim wa mkutanio wa Tume na Wazalishaji Maudhui Mtandaoni kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 03 , 2025.

Picha ya pamoja ya washiriki 


NA WAANDISHI WETU, DAR ES SALAAM.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele, amewahimiza wazalishaji wa maudhui mtandaoni kutumia majukwaa yao ya kidijitali kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.


Akizungumza leo tarehe 03 Agosti, 2025, jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kitaifa kati ya Tume na Wazalishaji wa Maudhui Mtandaoni, Mhe. Mwambegele amewapongeza wazalishaji hao kwa ushirikiano walioutoa kwa Tume katika hatua mbalimbali za maandalizi ya uchaguzi.


Mhe. Mwambegele amewasihi wazalishaji hao wa maudhui kuendelea kuwa daraja muhimu kati ya Tume na wananchi kwa kutoa taarifa sahihi na kwa wakati.


“Tuna imani kuwa tutazidi kushirikiana nanyi kwa karibu zaidi, na mtatumia nafasi zenu kuwapatia wananchi taarifa sahihi kuhusu maendeleo ya maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa 2025 na kuwahamasisha kushiriki kikamilifu kwa kupiga kura,” amesema Mhe. Mwambegele.


Amebainisha kuwa Tume inatambua mchango wa wazalishaji wa maudhui mtandaoni katika njia mbili kuu. Kwanza, kama daraja la mawasiliano kati ya Tume na wadau, na pili, kama wadau wa moja kwa moja wa mchakato wa uchaguzi.


“Tume inathamini kazi yenu ya kuandaa, kuchapisha na kusambaza taarifa kupitia majukwaa mbalimbali ya kidijitali kama mitandao ya kijamii, blogu, tovuti na majukwaa ya video kama YouTube,” ameongeza.


Akizungumzia nafasi ya vijana katika uchaguzi, Mhe. Mwambegele amesisitiza umuhimu wa mawasiliano ya kidijitali kwa kundi hilo, akiwahimiza wazalishaji hao wa maudhui kutumia ubunifu wao kwa kutumia michoro, video na ujumbe wenye mvuto ili kuwafikia wapiga kura kwa njia rahisi na ya kuvutia.


Amesema lengo kuu la mkutano huo ni kujadili hatua zilizofikiwa katika maandalizi ya uchaguzi, kubadilishana mawazo, na kusikiliza changamoto zinazowakabili wazalishaji wa maudhui mtandaoni ili kutafuta suluhisho kwa wakati.


“Mkutano huu si wa upande mmoja; ni jukwaa la mawasiliano ya pande mbili ambalo linawapa fursa ya kueleza changamoto zenu na kusaidia kuboresha utekelezaji wa shughuli za uchaguzi,” ameeleza Mhe. Mwambegele.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani, amehimiza waandaaji wa maudhui mtandaoni kutumia majukwaa yao kutoa habari sahihi, na zilizothibitishwa na kufanyiwa utafiti.


Ameongeza kuwa majukwaa hayo ya kidijitali yanasaidia kurahisisha upokeaji wa taarifa za Tume na kuwafikia wananchi kwa haraka.


Aidha, Bw. Kailima amewahimiza wazalishaji wa maudhui mtandaoni kutoa taarifa za mara kwa mara kuhusu mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa 2025, ikiwa ni pamoja na kuitumia kauli mbiu ya uchaguzi “Kura Yako Haki Yako, Jitokeze Kupiga Kura” ili kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi tarehe 29 Oktoba, 2025.


Mkutano kati ya Tume na Wazalishaji wa Maudhui Mtandaoni ni mfululizo wa mikutano ya Tume na wadau wa uchaguzi ambayo ilianza tarehe 27 Julai, 2025. Mikutano hiyo inatarajiwa kuhitimishwa tarehe 04 Agosti, 2025 kwa wahariri na waandishi wa vyombo vya habari kupatiwa mafunzo.







Picha mbalimbali za washiriki wa Mkutano huo.


Tuesday, July 8, 2025

DIRA 2050 INA KINGA YA BUNGE -PROF MKUMBO

 

Na Mwandishi wetu 


SERIKALI imewatoa hofu Watanzania kuhusu hoja ya kuwa utekelezaji Dira 2050 unaweza kukumbwa na changamoto ya uhalali wa kisheria na hivyo mpango huo muhimu kwa taifa ukawa na ombwe la kiufanisi hapo baadae 


Akiongea katika kikao maalum na Wahariri kutoka jukwaa la Wahariri Tanzania TEF Waziri wa nchi ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaii Profesa Kitila Mkumbo amesema Dira ya taifa 2050 imewekewa ulinzi kwa kupelekwa bungeni na kwamba hakuna Rais atakayeweza kwenda kinyume na uamuzi huo


Profesa Mkumbo amesema Dira 2050 itatekelezwa na Marais watatu,na kwa atakaetaka kuibadilisha atatakiwa kupeleka bungeni na kwamba Dira hii imekuwa tofauti kwa kuwa ya 2025 iliishia hatua ya kuidhinishwa na Baraza la Mawaziri tu.


Waziri huyo amesema mchakato wa kutengeneza Dira 2050 umepitia hatua 13 ambazo ni kuandaa na kuidhinisha miongozo ya Dira.


Mkakati wa kuandika Dira ulianza Aprili mwaka 2023, kwa kuunda vyombo vya kutathimini mchakato wa Dira na kufanya tathimini ya utekelezaji wa Dira 2025.


Pia kukusanya maoni ya wananchi na wadau juu ya maudhui gani yaingie kwenye Dira, kujifunza kutoka nchi mbalimbali za Afrika, Asia na Marekani kwa hatua zilizopigwa.


Alizitaja baadhi ya nchi walizojifunza ni Botswana, Moroco, Mauritius, Afrika Kusini na Kenya.


Kwa Asia wamejifunza Kusini mwa Asia za China, Indonesia, Korea Kusini, Singapore na India, na kwamba kwa Ulaya wamejifunza kidogo kutokana na kwamba historia yao si ya muda mrefu kama nchi zenye historia 1,000.


Hatua nyingine ni uchambuzi, uandishi na uhariri wa taarifa na kutoa Rasimu ya kwanza ya Dira 2050.


Pia kulinda rasmu ya kwanza ya Dira 2050 iliyozinduliwa Desemba 2024,na kuchukua Rasimu kupeleka tena kwa wadau ili kupata maoni ya kihariri.


"Tulikutana na wadau mbalimbali kama waandishi wa habari na vyama vya siasa ili kupata makubaliano ya pamoja.


Tulivyokutana na vyama vya siasa tulikubaliana tusibishane juu ya tunakwenda wapi ila tukubaliane tuende huku, Ilani zetu ziakisi tunaenda wapi, "amesema.


Hatua nyingine, ni kutoa rasimu ya pili ya Dira ya Taifa na kukabidhiwa kwa Waziri Mkuu, Juni 2025 iliidhinishwa na Baraza la Mawaziri na kufuatiwa na Bunge.


Aidha, amesema hatua ya mwisho ni kuutaarifu umma kuwa mchakato wa Dira umekamilika na itajulikana kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza Dira  2050 Tanzania Tuitakayo, na hatua ya mwisho ni Rais Samia Suluhu Hassan kuizindua Julai 17, mwaka huu.

Friday, June 13, 2025

ANUSURIKA KIFO BAADA YA KUPIGWA NA WAFUGAJI.

 

Na Omary Mngindo,u


ELIAS Madinga mkazi wa Kitongoji cha Mlelani, Kijiji cha Visezi Kata ya Vigwaza Halmashauri ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani, amenusurika kifo baada ya kushambuliwa na Wafugaji.


Mkazi huyo akiwa na mkewe katika nyumba ya bosi wake Kitongojini hapo, siku ya tukio akipulizia dawa mazao aliona makundi ya ng'ombe yaliyogawanyika mara tatu yakiingia ndani ya shamba hilo.


Alisema kuwa alipoona hivyo alianza kuiswaga ili itoke shambani, wakati huo akiwepo kijana mdogo jamii ya Wafugaji na kwamba wakati akiendelea na zoezi ilo ghafla yule kijana alitoweka.


"Kwakuwa nilikuwa na zoezi la kupulizia dawa, nikachukua baskeli nikaenda kisimani kuchota maji, wakati narudi nikamuona mke wangu amembeba mtoto wetu wa miezi mitatu wamemzingirwa na Wafugaji hao", alisema Madinga.


Aliongeza kuwa"Nikiwa nakaribia aliniambia nisifike kwani ameshashambuliwa na Wafugaji hao, sikumuelewa wakati nikaribia nikajikuta mimezingrwa na kundi la Wafugaji wakaanza kunishambuliwa kwa silaha mbalimbali za jadi," alisema.


Alieleza kuwa wakati wanamshambulia mke wake aliwaomba wamwachie akamvalishe mtoto nguo, akatumia nafasi hiyo kukimbilia kijijini kutoa taarifa kwa Mwenyekiti, ambapo alifika Askari Mgambo akamchukua wakamkimbiza Zahanati.


"Nilipoteza fahamu niliposhtuka nikajikuta niko Zahanati natibiwa, nilipochukuliwa pale nyumbani sikujitambua, pamoja na kwamba nilikimbilia ndani lakini waliingia wakaendeleza mashambulizi," aliongeza Mhanga huyo.


Aliongeza kwamba "Baada ya kupelekwa kesi Polisi Chalinze walimfuata wakataka kumpatia kiasi cha shilingi laki tatu nikakataa, nafuatilia ili suala ili niende Mahakamani," alimalizia mkazi hiyo.


Swala la wafugaji kudharau mashamba ya wakulima wilayani Bagamoyo limekuwa ni jambo la kawaida hali inayotishia usalama wa wakulima.


Wananchi walioongoe na BAGAMOYO KWANZA BLOG wameiomba Serikali kuchukua hatua dhidi ya wafugaji ili kukomesha vitenda vya dharau na unyanyasaji wanavyofanyiwa wakulima.


Thursday, March 20, 2025

TCRA KUSHIRIKIANA NA TBN KUSADIA KUZALISHA MAUDHUI YENYE TIJA

 


Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeahidi kufanyakazi na Mtandao wa Wana Blogu Tanzania (TBN), pamoja na vyama vingine vya waandishi wa habari ambavyo vinawakilisha mahitaji na matakwa ya wanachama wao.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe  19.Machi 2025 Jijini Dar es Salaam na Meneja wa Huduma za Utangazaji wa TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka, alipokutana na ujumbe wa TBN ofisini kwake, katika kikao cha kujadiliana changamoto mbalimbali zinazowakabili Bloga nchini.

“Sisi huwa tunapenda kufanya kazi na vyama ambavyo vinawakilisha mahitaji na matakwa ya wanachama wao, badala ya kufanyakazi na mwaandishi mmoja mmoja…tunafurahi sana kufanyakazi na waandishi kupitia vyama vyao,” amesema Mhandisi Kisaka.

Mhandisi Kisaka amesema kuwa TCRA imefurahi kukutana na TBN kwa kuwa wanafahamu kuwa Bloga wanasehemu kubwa sana kwenye maudhui ya ndani, na hata kwenye usajili wa TCRA Bloga wanachukua nafasi kubwa sana katika maudhui ya mtandaoni.

“Kwa hiyo TBN mtakuwa silaha moja wapo nzuri sana yakutuwezesha sisi kama Mamlaka ya Mawasiliano nchini, tunao simamia utangazaji pamoja na maudhui ya mtandaoni kuwa karibu na nyinyi na kuhakikisha maudhui ya mtandaoni yanaleta tija na maendeleo kwa wananchi,” amesema Mhandisi Kisaka.

Monday, March 17, 2025

MFUMO WA USAJILI WAANDISHI WA HABARI KIDIJITALI UPO MBIONI KUKAMILIKA- MSIGWA

 


Na Mwandishi Wetu, 

Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA) inaendelea na hatua za mwisho za ukamilishaji wa ujenzi wa mfumo wa Usajili na utoaji wa vitambulisho vya kidigitali kwa Waandishi wa Habari nchi nzima - Journalists Accreditation & Registrations System (JARS).


Mfumo huo unaotengenezwa na chini ya Idara ya Habari (Maelezo) na Wataalamu wa Mifumo wa e- GA, unalenga kurahisisha, kuongeza uwazi na kuimarisha utendaji kazi wa waandishi wa Habari kwa kuwapatia huduma ya usajili na utoaji wa vitambulisho vya kazi katika maeneo yao bila kulazimika kusafiri kwenda Dodoma au Dar es salaam kupata huduma hiyo.


Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa wakati akitoa taarifa kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo miradi iliyotekelezwa na serikali ya awamu ya sita wakati wa mkutano na waandishi wa habari tarehe 16 Machi, 2025 katika Bandari Kavu ya Kwala, mkoani Pwani.


Amebainisha kuwa Mfumo huo pamoja na mambo mengine utakuwa na uwezo wa kusajili, kuhakiki na kuhifadhi taarifa za waandishi wa habari wote nchini


"Mwandishi wa habari atakuwa na uwezo wa kujaza taarifa na kuweka mambo muhimu kama vile picha, mahali anapofanya kazi, taarifa za uraia wake n.k, na Mfumo utatoa alama za usalama ambazo mtu hawezi kughushi," amesema Bw. Msigwa na kuongeza;


"Kupitia mfumo huu Mwandishi wa Habari atakua na uwezo wa kuomba na kupata kitambulisho chake (physical ID). Mfumo una uwezo wa kuonesha taarifa kwenye ukurasa wa nyuma back-end ambazo zitahakikiwa na kutumiwa na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari-JAB kutoa kitambulisho (Press Card) kwa njia ya mtandao".


Amesisitiza kuwa Mfumo utakuwa na uwezo wa kumpatia mwandishi wa habari taarifa kabla ya muda wa kuisha matumizi ya kitambulisho chake (alert when the ID is about to expire) pia utamtumia ujumbe mfupi kupitia simu ya mkononi


Bw. Msigwa amesema kupitia mfumo huo Mwandishi anapoomba kitambulisho atapatiwa namba ya malipo “control Number” ya kulipia mtandaoni na akishalipia malipo yake yataonekana na kupitishwa na mamlaka husika (approved) na kwamba utakuwa na mwonekano wa aina mbili (madirisha) kwa ajili ya waandishi wa ndani na wa nje (International). 


"Mfumo utamwezesha Mwandishi wa Habari kupakia nyaraka muhimu kama vile vyeti vya taaluma kwa ajili ya uhakiki (VERIFICATION) na pia mfumo utapokea maombi ya waandishi wa nje ya nchi na wao kama ilivyo kwa wale wa ndani utawataka kupakia (Requirements) wakiwa wamekidhi vigezo ndipo hatua nyingine itafuata," amesema.


Mfumo utakuwa na uwezo wa kuhakiki taarifa za waandishi kwa kuunganishwa na mifumo mingine ya serikali kama GePG, NIDA, NECTA, Uhamiaji n.k kwa ajili ya malipo, uhakiki wa vyeti na taarifa (Verification).


Aidha, Bw. Msigwa amesema mfumo utakuwa na uwezo wa kuondoa wale wote waliokosa sifa/wasiohuisha taarifa zao pale wanapotakiwa kufanya hivyo, utamwezesha mtumiaji kuweka saini mahali panapohusika (Digital signature) pamoja na kuruhusu taarifa za kitaaluma na eneo la kazi kupatikana kwa njia ya msimbo papo (QR CODE).


"Huduma hii ya kupata vitambulisho vya kidigitali itapatikana kwa Waandishi wa habari wote watakaokuwa wamekidhi vigezo vya kitaaluma (Taaluma ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano kwa Umma),"










Monday, February 24, 2025

WAZIRI KIKWETE KUFANYA ZIARA YA SIKU TATU MKOANI SONGWE.

 

Anatarajiwa kukagua na Kuzindua Miradi ya Maendeleo  


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu -Mhe. Ridhiwani Kikwete Februari 23, 2025 amewasili mkoani Songwe kwa lengo la ziara ya  kukagua miradi ya Maendeleo ikiwemo ya sekta  ya Elimu, Afya na Miundombinu   kwa ajili ya ustawi wa maendeleo ya wananchi .


Mhe. Waziri Kikwete anatarajiwa kukagua na kuweka Mawe ya msingi katika miradi hiyo ambayo inakadiriwa kugharimu zaidi ya shilingi Bilioni 700 katika Halmashauri zote za mkoa huo.


Mara baada ya kuwasili katika  mkoa huo , Waziri Kikwete alipokelewa na Mkuu wa Mkoa huo Ndg. Daniel Chongolo ambaye alimpa hali ya maendeleo ya Mkoa huo na maandalizi ambayo yameshafikiwa kwa ajili ya ziara hiyo.


Vile vile Mhe.  Kikwete anatarajiwa pia kukagua Maendeleo ya Kituo cha Vijana cha Sasanda wilayani   Songwe ambapo atakagua  mradi wa Shamba la vijana lililopo kituo hicho.


 Mhe Waziri Kikwete ameambatana  na watendaji mbalimbali ambapo amemhakikishia Mkuu wa mkoa huo  kuwa timu yake ipo tayari kwa ajili ya kazi iliyowaleta.