Halmashauri ya mji wa Bagamoyo, imekabidhi vifaa vya TEHAMA kwa walimu wakuu wa shule za kata za Zinga, Dunda na Kata ya Yombo.
Makabidhiano hayo yameongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo Mhe Mohamedi Usinga Desemba 17,2025.
Katika makabidhiano hayo Mhe Mwenyekiti amekabidhi jumla ya komputa (Desktop)44 katika Shule ya Msingi Yombo wamepata Komputa 20,shule ya Msingi Kizuiani 12 na Shule ya Zinga 12 pamoja na Komputa Mpakato moja kwa kila shule na vifaa vyake kwa ujumla.
Mhe Usinga ametoa wito kwa walimu hao kuhakikisha wanavitunza na kuvilinda vifaaa hivyo kwa ajili ya kujifunzia kwa wanafunzi mashuleni ili kuendana na kasi ya teknologia.
Vilevile Mhe Mwenyekiti ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha anawezesha upatikanaji wa vifaa vya Tehama mashuleni lakini pia na kuwezesha miundombinu bora mashuleni.
Nae Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo Ndg Shauri Selenda amewasisitiza walimu hao kuhakikisha wanavitunza vifaa hivyo Pamoja na kuhakikisha wanatoa elimu iliyobora kwa wanafunzi ili kujenga msingi bora wa elimu katika Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo.
Aidha Ndg Selenda ametoa shukrani kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassani kwa kuhakikisha kila shule inakuwa na miundombinu bora lakini pia inapata vifaa vya kujifunzia mashuleni.
Kadhalika Afisa Elimu awali na Msingi Bi Wema Kajigili akitoa shukrani kwa niaba ya Walimu hao wote amesema kuwa “naendelea kutoa shukrani kwa Rais Samia Suluhu Hassani Pamoja na wadau wote wa elimu nchini vifaa hivi tutahakikisha tunavitunza na kuvilinda na kuhakikisha mwanafunzi ananufaika na vifaa hivi kwa kuwapatia elimu bora”.Bi Wema Kajigili.

































