Na Omary Mngindo,u
ELIAS Madinga mkazi wa Kitongoji cha Mlelani, Kijiji cha Visezi Kata ya Vigwaza Halmashauri ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani, amenusurika kifo baada ya kushambuliwa na Wafugaji.
Mkazi huyo akiwa na mkewe katika nyumba ya bosi wake Kitongojini hapo, siku ya tukio akipulizia dawa mazao aliona makundi ya ng'ombe yaliyogawanyika mara tatu yakiingia ndani ya shamba hilo.
Alisema kuwa alipoona hivyo alianza kuiswaga ili itoke shambani, wakati huo akiwepo kijana mdogo jamii ya Wafugaji na kwamba wakati akiendelea na zoezi ilo ghafla yule kijana alitoweka.
"Kwakuwa nilikuwa na zoezi la kupulizia dawa, nikachukua baskeli nikaenda kisimani kuchota maji, wakati narudi nikamuona mke wangu amembeba mtoto wetu wa miezi mitatu wamemzingirwa na Wafugaji hao", alisema Madinga.
Aliongeza kuwa"Nikiwa nakaribia aliniambia nisifike kwani ameshashambuliwa na Wafugaji hao, sikumuelewa wakati nikaribia nikajikuta mimezingrwa na kundi la Wafugaji wakaanza kunishambuliwa kwa silaha mbalimbali za jadi," alisema.
Alieleza kuwa wakati wanamshambulia mke wake aliwaomba wamwachie akamvalishe mtoto nguo, akatumia nafasi hiyo kukimbilia kijijini kutoa taarifa kwa Mwenyekiti, ambapo alifika Askari Mgambo akamchukua wakamkimbiza Zahanati.
"Nilipoteza fahamu niliposhtuka nikajikuta niko Zahanati natibiwa, nilipochukuliwa pale nyumbani sikujitambua, pamoja na kwamba nilikimbilia ndani lakini waliingia wakaendeleza mashambulizi," aliongeza Mhanga huyo.
Aliongeza kwamba "Baada ya kupelekwa kesi Polisi Chalinze walimfuata wakataka kumpatia kiasi cha shilingi laki tatu nikakataa, nafuatilia ili suala ili niende Mahakamani," alimalizia mkazi hiyo.
Swala la wafugaji kudharau mashamba ya wakulima wilayani Bagamoyo limekuwa ni jambo la kawaida hali inayotishia usalama wa wakulima.
Wananchi walioongoe na BAGAMOYO KWANZA BLOG wameiomba Serikali kuchukua hatua dhidi ya wafugaji ili kukomesha vitenda vya dharau na unyanyasaji wanavyofanyiwa wakulima.